Nape Nnauye kuongea na wanahabari

Nape Nnauye kuongea na wanahabari

Status
Not open for further replies.
NAPE UMEINGIA TAYARI KWENYE VITABU VYA MASHUJAA WA TAIFA HILI KWA KUISIMAMIA KWELI HADI MWISHO
Unamdanganya Nape wa watu. Hana ushujaa bali kajaa mihemko na viherehere visivyo na kifani. Nape kama nani aunde tume ya kumchunguza Mteule mwenzie wa Rais? Ushujaa ni kuvunja kiapo chake cha uwaziri kwa kumdharau Rais wa nchi hadharani? Jitafakarini. Ama hamna akili iliyo sawasawa ama nanyi ni kati ya mashabiki msiochunguza mambo kwa jicho la tatu. Ugomvi binafsi Nape augeuze vita ya serikali kwa serikali nani atamuacha?
 
  • Thanks
Reactions: e2n
NAPE UMEINGIA TAYARI KWENYE VITABU VYA MASHUJAA WA TAIFA HILI KWA KUISIMAMIA KWELI HADI MWISHO
Unamdanganya Nape wa watu. Hana ushujaa bali kajaa mihemko na viherehere visivyo na kifani. Nape kama nani aunde tume ya kumchunguza Mteule mwenzie wa Rais? Ushujaa ni kuvunja kiapo chake cha uwaziri kwa kumdharau Rais wa nchi hadharani? Jitafakarini. Ama hamna akili iliyo sawasawa ama nanyi ni kati ya mashabiki msiochunguza mambo kwa jicho la tatu. Ugomvi binafsi Nape augeuze vita ya serikali kwa serikali nani atamuacha?
 
  • Thanks
Reactions: e2n
Sikuwahi kuwaza kuna siku nitamuunga Nape mkono hasa kwa nafasi yake aliyokuwa nayo awali ...nimeamini kwenye siasa masaa 24 ni mengi

Kama wamekuondoa kwa kusimamia ukweli basi elewa una sapoti kubwa sana ya wananchi nyuma yako

Omba msamaha pale ulipo kosea songa mbele
 


Mheshimiwa Nape Moses Nnauye anaatarajia kuongea na wanahabari leo, stay tuned Movie bado inaendelea.

Kutoka vita ya ufisadi hadi vita ya wanaompinga Daud.Sasa hakuna vyeti fake, hakuna ufisadi kilichobaki ni timua timua.Watanzania tujilaumu wenyewe, haiwezekani rais anapiga push-ups jukwaani halafu bado tukamchagua aongoze kidiplomasia.Mabadiliko yanahitajika maana historia mpya inaandikwa as we comment
 
Kweli mkuu, unapopata msuko suko ni muhimu sana kutulia na kutafakari kwa kina kuliko kukimbilia kwenye public, huwezi jua may be boss wake ameona hatoshi hapo anatosha sehemu nyingine ambayo atakuja kumuweka baadae.....anaweza kujifunza kwa mamaetu Kilango, alitumbuliwa akakaa kimya kwa kanuni ya sikio halizidi kichwa na sasa anapeta,anachotaka kukifanya ni sawa na nazi kujipigiza kwenye jiwe.SIKU ZOTE MUNGU YU PAMOJA NA WENYE KUSUBIRI.
Kwani mshajua anataka kuongelea nini??? Je kama anataka kumshukuru raisi???
 
Nape ni Baba wa Taifa ktk tasnia ya habari. Naomba media houses wamjengee mnara huyu kijana ktk maeneo ya ofisi zao. Hata jina la newsroom kwa heshima yake itakuwa poa.

Hili jambo ni kubwa. Ukiona kwenye PhD anajipendekeza kama Mwakyembe lakini kijana na masters yake anakomaa kiume inabidi utoe salute. Imagine pamoja na kujipendekeza mtu unahamishwa Sheria unakokujua vizuri na kupelekwa michezo wakati hata jogging huwa hufanyi.
 


Mheshimiwa Nape Moses Nnauye anaatarajia kuongea na wanahabari leo, stay tuned Movie bado inaendelea.

Ingawa sijajua atazungumzia nini, huyu mwanasiasa angeshauriwa kukaa kimya. kukaa kimya kuna faida nyingi, yeye bado ni mwanasiasa kijana na ana safari ndefu. ajiangalie vizuri kabla ya kuongea na waandishi wa habari.
 
  • strongly opposed to your comment, ukitaka kujua mambo we sikiliza, he is mature enough to know what/not to say. utashangaa unajua mambo ambayo usingeyajua kama asingeongea. tuliza ball young boy
Kubishana na mbabe hadharani kuna hatari
 
Nape angekaa tu kimya lakini kama anaona analazimika kuzungumza, basi aeleze tu kwamba:

1. Nili tender resignation, sijatumbuliwa na aeleze kwanini.

2. Ashukuru wadau wa habari kwa kumpa ushirikiano akiwa waziri.

3. Ashukuru watumishi wa wizara ya habari kwa hilo pia.

4. Ashukuru wananchi kwa utulivu katika kipindi chote kuanzia tukio lilipotokea hadi ripoti ya kamati yake ilipokamilika.

5. Aeleze kwamba nimeifikisha ripoti ya kamati niliyounda kwa Rais ikiwa ni mchango wangu kwa tasnia ya habari na kwa taifa kwa ujumla kusimamia kile ambacho nimekuwa nikikisema tangia sakata hili lianze.

6. Aombe radhi kwa wananchi kwa kushiriki katika utungaji wa sheria kandamizi akiwa Waziri mwenye dhamana husika. Aombe radhi pia kwa kuwa sehemu ya uongozi wa chama ambao siasa zake ndio zimetufikisha hapa kama Taifa. Haya ni muhimu sana kama anatafuta future ndani au nje ya CCM.

7. Aseme anaelekea bungeni kutumikia wananchi wa Mtama na taifa kwa ujumla.

8. Aseme mimi kama Nape nimeufunga rasmi mjadala, na namtakia kila la kheri waziri Mwakyembe.

Na asikubali maswali kutoka kwa waandishi wa habari.

#6 ni ngumu sana lakini ndio itakayo define his future kama anataka kuwa kiongozi baadae. Nje ya hapo, wananchi watamshukuru kwa kusimamia ukweli katika hili, lakini hawatamwamini kwa mengineyo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom