mwakweya70
JF-Expert Member
- Feb 13, 2015
- 414
- 106
Suala hili linaweza kuwa na mshindo mkuu,ila bado naamini serikali ipo haijaenda likizo na itajua tu kumaliza harakati hizi za watu kwa misingi ya kisheria,hatupaswi kutoka povu sana
Nje ya lowasa mna mwingine wa kumuweka?
Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Nape Nnauye amesema kitendo cha mgombea mmoja anayepokea makundi ya watu ili wamshawishi kupiga kura huko Dodoma ni kuanza kampeni na yuko hatarini kuenguliwa.
Waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa ndiye anayepokea makundi ya watu wakiwemo masheikh, maaskofu na wanafunzi wakimshawishi kugombea.
Akizungumza na radio VOA, Nape alisema: "Labda niweke vizuri hili, mtu yoyote anayekiuka kanuni hatapitishwa labda kamaa anakwenda kugombea kwa chama kingine.
"Kinachofanyika Dodoma cha watu kuchukuliwa na magari huku wengine wakiwa hawajui, halafu wakifika wanakuta viti vimeshapangwa na vyakula;halafu eti wanamshawishi kugombea, ni kukiuka kanuni na anaweza kuondolewa," alisema Nape.
Haya yote yanaaeleweka vizuri kabisa.Ni uchovu tu wa wanasiasa.
Nape ni CCJ.
Livingstone Lusinde ni ni Chadema .
J.Makamba amebebwa kwa nguvu ya baba yake.
Samwel sita ni CCJ
Benard Membe ni CCJ
Makonda ni CCM madaraka.Bila madaraka atahama na kujiunga na ACT ili apate angalau udiwani.
Mwakyembe ni CCJ
Wasira ni NCCR Mageuzi.
Magufuli ni CCM asiye na histori ndefu ya kukitumikia chama katika shida na raha.
Sumaye ni CCM madaraka.Mana alishasema akienguliwa atatafuta chama kingine.
Hawa wote wanacheza ngoma na nyimbo za Chadema.
Tumeona Nape na hilo Kundi lake wakifurahia kifo cha marehemu capt Komba huku wakisahau mazuri yote aliyoyafanya kukijenga chama cha mapinduzi katika uhai wake wote. Hawa ndio watu wanaosema wanakipigania chama.
Kinana ni CCM halisi ndio maana anajua mbinu za kukijenga chama.
Lowassa ni kati ya makada wa kweli wa CCM waliobakia. Kumuengua Lowassa kwa sababu ya kusikiliza kelele za wapita njia litakua ni jambo la kipuuzi na lisilokubalika.
Eti wanasema kwa nini watu wanakuja na kukuta viti vimepangwa na chakula.Ni akili za ajabu kabisa. Kwa ulimwengu wa sasa hivi wageni waje bila kutoa taarifa.
Hata kwa mila zetu za kiafrika mtu akienda kuposa anatoa taarifa kwa wakwe ili wajiandae kupokea ujumbe unaoletwa wa posa.Na usipotoa taarifa basi linakua ni jambo lisilokubalika.
Simu na mitandao iko kila mahali halafu mtu aende kwa mtu bila taarifa.
Ndio maana viongozi wa dini kwa muda mrefu wamepima wakagundua kuwa Lowassa ana hekima kuliko hawa waruka njia ,Nape na kundi lake.Kwani hata hoja zao za kumshambulia Lowassa ni za kijinga na chuki tu.
Eti watu wanazolewa bila kujua kinachoendelea halafu wanapelekwa kwa Lowasa kupewa hela.Hivi kweli inaingia akilini Msomi wa Chuo kikuu azolewe bila kujua anakoenda?
Hivi kweli unaweza ukamzoa mchungaji au shehe ukampeleka asikokujua na akakubali kwenda.
Viongozi wa dini siku zote wanapenda viongozi wasikivu.Na wamegundua kuwa Lowassa hana makuu.
Nape muda Mrefu amekua akionekana dhahiri sio kutumia nafasi aliyo nayo kuhakikisha kuwa anatumia Muda mwingi kupambana na Lowasa ili alete Mtu wake anayemtaka.
Mnafiki na Joka la Mdimu siku zote hawana jema.
Ingetokea wale wachungaji ,mashehe na wanafunzi wa vyuo wakaenda kimya kimya kwa Lowassa bila taarifa na kufika bila hata mashahidi ikiwemo waandishi wa habari basi leo hii Lowasa angekua ameshaitwa kwenye kamati ya maadili na kuhojiwa kuwa anafanya kampeni na vikao vya siri.Ingekua ni ishu kubwa kweli kweli.
Hii ndio tabia ya wanafiki walovamia ndani ya CCM na sasa wanataka kuwaengua makada wa komavu wa chama na serikali ili wapitishe wanachama wenzao wa CCJ!!!
Ni mwendo wa KANU kule Kenya CCM itakuwa chama cha Upinzani kwa itagawanyika na kuwapa mwanya Chadema kuchukua Nchi kisha Lema atakuwa Waziri wa mambo ya ndani, sikilizia balaa lake kila mkutano wa CCM Polisi watatoa vipigo ile mbaya.Upepo wa kisiasa umeanza kumwendea vibaya Mh Lowassa hasa baada ya makundi mbalimbali kwenda kumshawishi agombee urais. Baadhi ya viongozi wa chama wanasema ameanza kampeni kabla ya kingenga kupulizwa. Je, ikitokea jina lake likaenguliwa na vikao vya chama na ilhali "anakubalika kwa wananchi", ni kitu gani kinaweza kutokea kwake binafsi na kwa CCM?
Membe si Chaguo la JK alishamtosa kitambo hawamtaki baada ya kugundua kuwa alimuua balozi wa Libya kisha akachukuchia mapesa ya marehemu Gadafi, hawataki Rais ajae awe Rais wa Mahakama ya The Hague kwa Uhalifu juu ya binadamu, wanamjua Membe ni mpenda Visasi atawafunga na kuwaua wapinzani wake, chagua la Jk ni pinda au kinana na akishindwa atakuwa kwa Lowasa au Wasira.Kikwete katika vita hii ya URAIS anasukumwa na jinsi gani anaweza kumpata mgombea ambae atamjenga mwanae Ridhwani na mkewe kisiasa baada ya yeye kung'atuka mwezi wa kumi; kigezo hicho ndio kinachonifanya niamini kuwa Kikwete atamtosa Edward na kumpigia debe Membe ambae katika MOU yao atamuachia mkewe ubunge huko Lindi na atamlea Ridhwani kisiasa ili baadae nae aje apate uongozi!! Dhaifu akumbuke tu kwamba hakuna sitting president aliyefanikiwa kuwachagulia wananchi mrithi wake na yeye is no exception!! I stand to be proven wrong!! Hata kama watamtosa Edward lakini kwa hakika magamba hawawezi kumpa Membe.!!!!
napekapewa kazi na membe ya kumchafuwa lowasa kwa makubaqliano kwamba nape ataachiwa jimbo na membe,ridhiwani mama yake naye wanampotosha baba jk,membe amekuwa akimtumia riz kupeleka majungu kwa baba yake
Lowassa asipogombea ccm,wemekwisha.
Hakuna Presidential candidate ccm anayemkaribia Lowassa hata kwa mbali."Quote my words"
anachokosea lowasa ni timing,,angesubiri mda mwafaka na afanye anachofanya sasa angefaulu.[/QUOTE
katika baadhi ya makundi ya What'sapp niliona pendekezo moja la Kiongozi wangu mmoja wa dini ambaye Baadaye niliamua kuwasiliana naye kwa UFAFANUZI.AMETOA USHAURI UFUATAO KWA VYAMA VYA SIASA
VIWE NA FOMU MAALUM YENYE MASWALI MUHIMU KWA WAGOMBEA WOTE. KILA CHAMA KITENGENEZE MASWALI YAKE.
WANANCHI TANGU MWANZO WAONE UMAKINI WA MASWALI YA KILA CHAMA NA JINSI KILIVYOJIRIDHISHA NA MAJIBU YA WAGOMBEA. Haya ni nje na sera, ilani NA mipango ya CHAMA. ( haya ni yale niliyoweza kuandika wakati wa mawasiliano. Kama nitakuwa nimepunguza natumaini atanielewa.
Mfano wa MASWALI
1. Ni kwa nini unagombea nafasi kubwa hii? Unafuata NINI ikulu ambacho huwezi kukifanya ukiwa nje ya Ikulu? Je ikitokea hatukukuteua kisha akateuliwa mwingine tutakayemuona Ana uwezo wa KAZI HII wewe utafanyaje?
2.Utafanya NINI kuinua Uchumi wa nchi yetu
3, Mahusiano yako na majirani zako yakoje?
4. Tafadhali eleza juu ya uadilifu wako na uaminifu wako kwa maisha ya na mahusiano ya NDOA
5. Je umewahi kuwa na tuhuma zozote za rushwa, udanganyifu, ubadhirifu au kuhojiwa juu ya uadilifu wako KWA mambo ya fedha?
6. Endapo watu wangeulizwa kuhusu mke/ mume wako au watoto unadhani wanasema NINI kukuhusu? Tunaomba uweke sahihi Hapa chini kuruhusu uchunguzi wa kina juu ya Maisha yako.
7. Utafanyaje kuondoa udini, ukabila unaonyemelea taifa letu , Je utafanya NINI kuzuia ubaguzi mwingine wowote KATIKA taifa?
8. TAIFA hili hupoteza mamilioni ya Fedha KWA njia mbalimbali umewahi kufanya NINI kuzuia upotevu wa FEDHA ? Utafanya NINI kubana matumizi ya Serikali ? Utafanya NINI kuhakikisha ufisadi unakoma Tanzania?
9. Ni NINI Tafsiri yako ya ucha Mungu? Je wewe waweza kuitwa mcha Mungu?
10. Utatumia mbinu gani kuhakikisha raslimali za taifa hili hazipotei na zinatumika sawa sawa-
11. TUPE MPANGO WAKO WA MIAKA MITANO
12. Tueleze mambo ambayo unadhani una udhaifu kwayo. ( UDHAIFU WAKO NI NINI?).
13. Una mpango wa KUTOA NINI KWA taifa lako. Una hakika kutoka moyoni mwako hakuna unachotafuta kupata Kutokana NA nafasi hiyo? Kama kipo unachotaka kupata tafadhali eleza.
KULINGANA NA MAONI YAKE HAPO TUTAONEKANA TUNAELEWA THAMANI YA KAZI YA URAIS KWAMBA SIO URAHISI.
Majibu ya wagombea yawekwe wazi kabla ya uteuzi.
Lowasa aligundulika ni mwizi tangu Baba wa taifa yupo hai na mwalimu mwenyewe aliacha wosia kuwa huyu mtu asipewe uongozi wa nchi atauza kila Kitu kwa hiyo tunafuata wosia wa baba wa taifa.Nani alipaswa kumweka Lowassa gerezani na kwa nini anamwacha mwizi anawakisha watu wa Monduli mpaka leo?
Kwa nini anapowakilisha watu wa Mondili anakua Jembe na mchapa kazi lakini anapoombwa kuchukua tu form anakua fisadi na mwizi?
Tuliogundua kuwa hii ni michezo ya wanasiasa tu kusaka madaraka basi tuna chambua pumba na mchele.
MBONA LOWASA NI KM MBUZI WA SIKUKUU. UPINZANI WALA HATUMSEMI VIBAYA ILI CCM WAMSIMAMISHE NA I SWEAR CCM HAWATOAMINI MACHO YAO KWA KICHAPO TUTAKACHOMPA FISADI Uyu..