minyoo
JF-Expert Member
- May 25, 2013
- 23,495
- 22,499
Vijana wengi humu wanaomshangilia Lowassa wana ufahamu mdogo sana kwenye masuala ya siasa mwaka 1995 wakati Mwalimu Nyerere alipomkataa Lowassa wengi wenu humu mlikuwa wadogo kiumri wengine mlikuwa shule za msingi kwahiyo hata ufahamu wenu kwa masuala ya siasa ulikua mdogo au kutojua kabisa kwa taarifa yenu Lowassa alishindwa kutolea maelezo utajir i aliokuwa nao ndani ya Muda mfupi aliotumikia ktk uongozi wa nchi hii ambapo ilipelekea kuondolewa kwenye kinyanganyiro cha urais
Jambo la pili lowasa ni fisadi papa ana biashara ambazo msingi wake upo kwenye uhujumu uchumi wa nchi hii na ilitangazwa hivyo hadharani na yeye lowasa aliahidi kwenda kuwa shitaki waliotangaza hivyo lakini mpaka leo haja fanya hivyo.
Mwisho nasema hivi Laiti kama Mwalimu Nyerere angekuwapo hai leo basi tusingeona upuuzi huo unao fanya na Lowassa
Marehemu baba wa Taifa hakumkataa Lowasa wala hakuna ushahidi wa wazi kabsa, isipokuwa kipindi kile Lowasa alikuwa na Ugonvi na mengi juu ya Viwanja vyake kule Mjini kati ndipo mengi na maadui wa Lowasa wakaenda kwa Nyerere kupiga Fitna na Majungu juu ya Lowasa kwa Lengo la kumharibia lakini baadae Nyerere alikuja kugundua kuwa zilikuwa Fitna na majungu tu, Hivyo kuendelea kukariri kuwa Nyerere alimkataa Lowasa ni kumsingizia Uongo marehemu baba wa Taifa, Lowasa anaweza akawa na mapungufu yake lkama Binadamu wengine lakini si kwa kiasi ambacho nyie wafuasi wa Membe mnataka aonekane, Nchi hakuna aliye Msafi kila Kiongozi ana Madhambi yake na Wakiletwa FBI hapa wawachunguze mmoja baada ya Mwingine hakuna ambaye atapona kwani wengi wanaishi kinyume na Vipato vyao Harisi