Nape: Lowassa ameanza kufanya kampeni, yuko hatarini kuenguliwa

Nape: Lowassa ameanza kufanya kampeni, yuko hatarini kuenguliwa

Hizo ni Lugha za wanasiasa na zote zina maana ile ile.

Labda mimi na wewe ndio hatujaelewana.
Tatizo sio kwamba mimi na wewe hatujaelewana bali tatizo ni kwamba wewe una mtu wako Lowassa kwahiyo unadhani kila mtu yupo against Lowassa... kwa upande mwingine, mimi sina mtu yeyote ninayempigia debe kwenye jamvi hili kwahiyo nipo huru kuelezea hisia zangu bila kuhofia chochote!
 
Habari wapendwa.

Akihojiwa kupitia kituo cha Radio cha Clouds FM Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi, Nape Moses Nnauye amesema kuwa kimsingi Lowasa amejiondoa mwenyewe kwenye kinyang'anyiro cha urais kwa Tiketi ya CCM.

My Take: Naamini kuwa Nape hakukurupuka kusema aliyosema na bila shaka amepata baraka za viongozi wake akiwemo Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana ambaye yupo naye sambamba kwenye ziara zake pamoja na Mwenyekiti, Jakaya Kikwete. Lowasa ujumbe ndio huo. Harakati zako ni sawa na mtu anayetwanga maji huku akitaraji kupata unga. Nakuhurumia sana
Mkuu Lizaboni, kwa tunaomjua Nape, hatutishwi na kubabaishwa na hizi vuvuzela zake na kupayuka payuka na kuweweseka kukumhusu Lowassa kwa sababu hakuanza leo.

  • Lowasa ndie Mwenyekiti wa Baraza la Udhani wa UVCCM, jee unakumbuka Nape alipayuka nini kumhusu Lowassa katika issue ya upangishaji jengo la UVCCM, nini kilimtokea?!.
  • Unakumbuka Nape alipopayuka na kupiga vuvuzela kwa kuzunguka nchi nzima kupigia chapuo kampeni ya kujivua gamba?, kwanza alitoa siku 30, kisha akatoa siku 60, kisha zikawa 90!, leo ni miaka 4 baadae, nini kimetokea?!, find out hiyo vua gamba imeishia wapi?!.
  • Kiukweli kwa vile Nape, ameziliwa CCM, amekulia CCM na sasa yuko CCM tena ndani ya CC, anajidhania anaijua CCM vilivyo!, kumbe masikini wa Mungu, hajui lolote!. Hata sisi tuu watu wa kawaida tumeishajua 'what is the name of the game!", masikini Nape hajui asemalo, wala atendalo, hivyo wakati wa kushuhudia kitakacho tokea, hata yeye atashangaa!.
  • Kwa kukusaidia tuu, Kinana ni mtu wa EL na JK hawakukutana barabarani!.
Pasco
 
ukweli ubaki kuwa ukweli,mimi sio shabiki wa EL wala sipo kwenye team yake,kwanza siwapendi wanasiasa,ila wanajamvi hebu tujiulize tu,hivi ni kweli EL anaratibu makundi yote haya na kuyapa pesa?hivi inakuja akilini kwa mtu kuacha kazi zake za kumuingizia kipato na kwenda kufanya maonyesho?kama kweli nyie mnaomnyooshea kidole EL mna uhakika na mnayosema na kuyasadiki,tusubiri siku si nyingi ukweli utadhihirika,sisi wengine yetu macho,ila namtahadharisha Nape,yasije yakatokea ya Kenya pale Moi alipompendekeza Uhuru kutaka kumuachia kiti hali iliyopelekea kuwapa wapinzani nchi kiulaini.
 
Hata Yesu alikataliwa na walimu wa dini wakati wake.

Walijua bado wataendelea kuongozwa na torati ya Mussa milele.
Hawakujua mwisho wa mambo yao umefika.

Mwalimu Nyerere alichukia matajiri,utajiri na nchi matajiri katika utawala wake wote.
Akaiongoza nchi maskini na watu maskini bila kupata misukosuko inayoletwa na nguvu ya umma.

Leo tumeona nchi zote tajiri duniani zinakimbilia Tanzania.
Watanzania wote wanapenda kushirikiana na nchi Tajiri.
Watanzania wote wanapenda kuwa matajiri.
Wazazi wote wanawapenda watoto matajiri.
Wanawake wote wanawapenda wanaume matajiri.
Misikiti yote inawapenda waumini matajiri.
Makanisa yote yanawapenda waumini matajiri.
Wanasoka wote wanapenda kuchezea club tajiri.
Wafanyabiashara wote wanapenda wateja matajiri.

Bila shaka huu ni wakati wa matajiri kwani matumaini ya kila mtu zama hizi ni kuwa tajiri.

Lowassa ndiye anayefaa kuongoza zama hizi za utajirisho.

_____
ACHA UHUNI, uongo wako kawapelekee michepuko yako huko.
 
Tangu mwaka 2005 CCM imekuwa kama company binafsi yaani kunavijamaa feki vimepata ulaji CCM vimejiwekea ukuta kabisa kila mtu avipigie magoti, eti vina haki ya kuonya mtu na kutukana mtu, hadi Mzee mkapa kuna kipindi aliguswaguswa sana, mwanaCCM Kiongozi kabisa anamtuka Kiongozi hadharani bila stahaa, baraza la maadili lipo tu. alitukanwa tinga tinga mzee wa watu kanyamaza sasa, Lowassa antukanwa hovyo, waryoba anapigwa, mafisadi hawagusiki. Mimi najua Nape, Makonda na wengineo ni watu ambao ni wasaka tumbo tu, hakuna mjenga chama. Uwepo wao CCM miaka 10 Upinzani umekuwa kwa kasi kutokana na uongozi mbovu kabisa na ufisadi. Eti Leo wanasema wanajenga CCM hawa kweli?? Wezi wakubwa mafisadi wazuri kabisa. Lowassa na mtu yoyote Yule anahaki ya kugombea urais kupita CCM na mmekikuta chama na mtakiacha. Mnaendekeza kujuanajuana tu huku chama kinadidimia tu. Nasema toeni UCHADEMA ndani ya CCM na ibakie Democracy tu, ndani ya nchi yetu tunataka Amani, Kama siasa haiwezekani basi biashara nayo inawashinda? Waachiwe wote wanaotaka urais wajinadi kivyao, kwani kujinadi ndio kuwa Rais??? Hebu Rais Kikwete ingilia hili swala linaudhi sana hii karne 21, science na technology tunataka mchuano sawia.
 
Habari wapendwa.

Akihojiwa kupitia kituo cha Radio cha Clouds FM kwenye kipindi cha Power Breakfast juu ya makundi mbalimbali ya kijamii kumtaka Lowasa kutangaza nia yamkugombea nafasi ya urais kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 2015, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi, Nape Moses Nnauye amesema kuwa kimsingi Lowasa ameonesha na ametangaza nia ya kugombea nafasi hiyo kwa muda mrefu na ndo maana chama kilimwadhibu kwa kuanza kampeni kabla ya wakati wake. Anasema kuwa kinachofanyika kwa sasa ni usanii na ulaghai wa kisiasa wa mwanasiasa huyo ambaye anausaka urais kwa udi na uvumba na kwamba kinachofanyika kwa sasa ni muendelezo wa kampeni za mapema zinazovunja kanuni na misingi ya chama.

Anasema kuwa si kweli kuwa makundi hayo ndiyo yanayomtaka Liwasa agombee bali watu hao wanaandaliwa na gharama zote zinalipwa na Lowasa ikiwa ni pamoja na nauli, malazi, chakula pamoja na fedha zinazotolewa kwa lengo la kugharamia uchukuaji wa fomu. Nape anaongeza kwa kusema kuwa wanazo taarifa kuwa makundi mbalimbali yanaendelea kuandaliwa ambayo yataenda Dodoma siku si nyingi. Anasema kuwa wakiwa Kilimanjaro, wamepata taarifa za baadhi ya watu walioombwa na Team Lowasa kwenda Dodoma. Ameyataka makundi hayo kuwa ni pamoja na Walemavu na Wafanya Biashara ndogo ndogo maarufu kama Wamachinga.

Akitoa ufafanuzi zaidi anasema kuwa nyumbani kwa Lowasa yamewekwa mahema na viti vya kutosha muda mrefu hata kabla ya kundi la kwanza kwenda. Anasema kuwa kama kweli wageni hao hawakutokana na jitihada zake Lowasa, maandalizi hayo ya nini? Kwa nini waitwe waandishi wa habari na pia maandalizi ya chakula cha wageni hao kufanyika hata kabla ya ujio wa wageni hao? Anahoji Nape Nnauye.

Kwa msingi huo, Nape anasema kuwa hatua ambayo amefikia Lowasa haivumiliki na kwamba mwanasiasa huyo amejiondoa mwenyewe kwenye kinyang'anyiro cha urais kwa Tiketi ya CCM labda kama jitihada zake zinalenga kugombea nafasi hiyo kupitia chama kingine ambacho Nape hakukibainisha.

My Take: Naamini kuwa Nape hakukurupuka kusema aliyosema na bila shaka amepata baraka za viongozi wake akiwemo Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana ambaye yupo naye sambamba kwenye ziara zake pamoja na Mwenyekiti, Jakaya Kikwete. Lowasa ujumbe ndio huo. Harakati zako ni sawa na mtu anayetwanga maji huku akitaraji kupata unga. Nakuhurumia sana

Sawa inawezekana Kinana naye yumo katika waliomtuma Nape maana jamaa huyu ni vuvuzela la kufa na kupona. lakini Kinana huyo alishamuumbua Nape mbele ya waandishi wa habari kwamba Nape aachane na kumsarandia Lowasa kwa kumuunganisha na upumbavu. Kwa hiyo Kinanakajitenga hapo na alimfagilia sana Lowasa alipoingia Monduli. Kwamba kule ccm ni kila kitu.
 
Pendekezo lako ni zuri sana. Nami naunga mkono. Ila Lowasa akae pembeni baada ya kukiuka maadili na miiko ya chama na taifa

Mkuu tumeshasikia Maoni yako juu ya Lowasa sasa Ngoja tuwasikilize Makamanda Mingoi na MUSSA ALLAN
 
Last edited by a moderator:
Vijana wengi humu wanaomshangilia Lowassa wana ufahamu mdogo sana kwenye masuala ya siasa mwaka 1995 wakati Mwalimu Nyerere alipomkataa Lowassa wengi wenu humu mlikuwa wadogo kiumri wengine mlikuwa shule za msingi kwahiyo hata ufahamu wenu kwa masuala ya siasa ulikua mdogo au kutojua kabisa kwa taarifa yenu Lowassa alishindwa kutolea maelezo utajir i aliokuwa nao ndani ya Muda mfupi aliotumikia ktk uongozi wa nchi hii ambapo ilipelekea kuondolewa kwenye kinyanganyiro cha urais
Jambo la pili lowasa ni fisadi papa ana biashara ambazo msingi wake upo kwenye uhujumu uchumi wa nchi hii na ilitangazwa hivyo hadharani na yeye lowasa aliahidi kwenda kuwa shitaki waliotangaza hivyo lakini mpaka leo haja fanya hivyo.
Mwisho nasema hivi Laiti kama Mwalimu Nyerere angekuwapo hai leo basi tusingeona upuuzi huo unao fanya na Lowassa
 
MAJIBU YA LOWASA KWA NAPE KUPiTIA HUSSEIN BASHE:

Akizungumza kwa niaba ya Lowassa, Bashe alisema kinachotokea nyumbani kwa Lowassa mjini Dodoma ni utekelezaji wa ushauri uliotolewa na Rais Kikwete wakati wa sherehe za CCM mjini Songea, mkoani Ruvuma alipowaruhusu watu wakashawishi wanaoona wanafaa kuwania urais.

"Rais hakusema kushawishi namna gani, hakusema kushawishi kwa barua wala kwa sms (ujumbe mfupi wa simu ya mkononi), bali alisema wawashawishi. Na huwezi kumshawishi mtu ndotoni, utamshawishi kwa kumfuata na kumwambia," alisema Bashe.

Aliongeza: "Ndiyo maana Nape yuko mikoani anashawishi Watanzania juu ya kukiamini Chama Cha Mapinduzi. Hajakaa chumbani kwake, amewafuata. Kuna watu wanamshawishi Mwandosya, kuna wanaomshawishi Muhongo na vyombo vya habari vinaripoti."

"Umefika wakati Nape atangaze mgombea wake wa urais hadharani, ambaye mimi Bashe namjua, badala ya kuwatisha wana-CCM wengine kwa kutumia kofia ya Ukatibu Mwenezi wa chama."

"Kwa hiyo, mimi kama Bashe, ambaye ni mwana-CCM nataka tu nimhakikishie Nape na wenzake kuwa hawana hatimiliki ya CCM. Wote wanaCCM tuna kadi moja ya rangi moja na tunalipia ada sawasawa. Hakuna mwanachama wa daraja la kwanza wala wa daraja la pili."

Bashe ambaye ni mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa, alisema kauli ya Nape ya kumtaka Lowassa kwenda nje ya CCM, haiwezekani, kwani hajawahi kufanya hivyo kama alivyowahi kufanya yeye (Nape).

Hivyo, akasema wana-CCM wanaomshawishi Lowassa na Watanzania wanatekeleza ushauri uliotolewa na Mwenekiti wa chama hicho, Rais KIkwete.

"Imefika wakati sasa Nape atazamwe kauli anazoongea. Na sisi tunaomfahamu Nape hii kawaida ya kuropoka, siyo maa yake ya kwanza. Aliwahi kusema Kikwete akishinda mwaka 2005 atahama nchi, lakini hajahama , akapewa na U-DC (ukuu wa wilaya) na Kikwete na hivi sasa ni katibu mwenezi wa CCM," alisema Bashe.

Aliongeza: "(Nape pia) aliwahi kusema mkataba wa jengo la Umoja wa Vijana (UVCCM) ni wa kifisadi na yeye (Nape) leo anaishi kwenye jengo hilo hilo na linakipa chama mapato."

Alisema mtu pekee, ambaye anaweza kutengua kauli ya Rais Kikwete aliyoitoa Songea mwezi uliopita, ni yeye mwenyewe (Rais Kikwete) kwa sababu ndiye aliyetoa maelekeo na sasa Watanzania wanayatekeleza.

Aliongeza: "Na mkumbuke mwaka 2011 kuelekea 2012, ni huyu huyu ndiye aliyekuwa anapita kwenye vyombo vya habari akiwaambia wanahabari kwamba, wanakwenda kumfukuza Lowassa Dodoma na leo anamhukumu kuwa anakosa sifa na kumwambia aende nje ya CCM.

"Nataka nimhakikishie kuwa Lowassa hawezi kuondoka CCM kwa sababu hajakutana na CCM barabarani.

Alisema wanaCCM wataendelea kuheshimu ushauri wa mwenyekiti wao na kwamba, Lowassa amekuwa akiheshimu kanuni na taratibu za chama.
"Na Nape na genge lake wakumbuke kwamba, Lowassa amevumilia mengi sana. Na asidhani yeye na wenzake wana hatimiliki ya chama hiki.

Aliongeza: "Hawa wanaosema haya leo, aliyasema mwaka 2009, 2010 na 2011 kwamba Lowassa hachaguliki, hakubaliki. Nyimbo yao ilipokosa soko, wakaja na nyimbo mpya ni fisadi, nayo ikakosa soko. Wakaja na nyimbo mpya ni mgonjwa, nayo ikakosa soko. walimtabiria hadi kifo, nayo ikakosa soko.
"Baada ya kuona kwamba, anaungwa mkono na makundi mengi ya kijamii mgombea wao wa kwenye brifkesi anakosa uhalali katika umma, sasa wanaanza kutoa kauli za vitisho na kusema watu wamenunuliwa.

Kuwadhalilisha Watanzania tuna bei. Kwamba, unanunulika. Na hiyo ni kudhalilisha utu wa Kitanzania na uwezo wa Watanzania wa kutafakari.

Alisema hakuna mtu anayenunuliwa na Lowassa, bali watu wote wanaongozwa na akili zao katika kutafakari na kuamua na kwamba, msingi wote wa chama chochote cha siasa, ni imani, demokrsia na haki.

"Nimtahadharishe Nape sehemu yoyote, ambayo haki na demokrasia kulazimishwa kufinywafinywa huathirika," alisema Bashe.

"Kwa hiyo, kama wanafikri njia zinazotumiwa na Watanzania kushawishi siyo sahihi, basi atoe maelekezo ya namna ya kushawishi. Hatutavumilia kuona haki haitendeki."

Karibu wiki mbili sasa, nyumbani kwa Lowassa, mjini Dodoma, makundi mbalimbali ya kijamii yamekuwa yakipishana na kupigana vikumbo yakimshawishi agombee urais baadaye mwaka huu.

Awali, walianza wajumbe wa Halmashauri Kuu (Nec) ya CCM Wilaya ya Arumeru, kisha marafiki wa Lowassa, Kanda ya Kaskazini na Uongozi wa Shirika la Umoja wa Machinga Tanzania (Shiuma).

Baadaye, walikwenda nyumbani kwake masheikh 50 kutoka wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani.

Masheikh hao walifuatiwa na wanafunzi wa vyuo vikuu sita mkoani Dodoma, wenyeviti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM, wamachinga na waendesha bodaboda zaidi 350 kabla wachungaji 110 wa makanisa ya Kipentekoste kutoka sehemu mbalimbali nchini kufuata nyayo hizo juzi.

CHANZO: NIPASHE
 
Sasa nina uhakika Lowasa hatateuliwa na CCM kugombea urais.
Asichojua Lowasa ni kwamba akina Nape wana vyanzo vingi sanavya kupata taarifa zake.Hata mlinzi wake binafsi Bwana Tendewa anaweza kutoataarifa za mipango ya Lowasa akitakiwa kufanya hivyo.
Na kuna baadhi ya wale wanaoenda kwa Lowasa wanaweza wakawawanaenda kupeleleza.Atashangaa atakapoonyeshwa ushahidi wa yote aliyokuwaanafanya.
Kwa hiyo,Lowasa akijidanganye kuwa watu hawajuianachokifanya kwa siri.

 
Nape hana tofauti na mjomba wake Tundu Lissu.
 
Mbowe analindwa na lowasa katka biashara zake hakuna mpnzani mwenye ubavu wa kumtukana lowasa na wmbo wa ufisadi watanzania walishauchoka sijui mtakuja na tape gani nakuhakkshia lowasa aksmama kuptia ccm si tu atashnda ila atasambaratsha upnzani nchini lowasa ni mzee mikakati na pia ni mzee wa plan b tym will tell alipo ana plan b hamtaamini na kna nape mtoseni lowasa muone kama ccm haijasambaratka asubuhi
 
Back
Top Bottom