Kwaiyo watz hawana ruhusa ya kwenda kumuomba mtu wanayehisi anafaa kugombea uraisi? Au wakienda kumuomba hawaruhusiwi kumpa taarifa kabla ili ajiandae kuwapokea mf. viti. Au ukiwa mgombea ukipata wageni nyumbani kwako utawaambia wakatafute sehemu ya kula maana ww ni mgombea? Wadau wekeni hapa hicho kifungu cha sheria ya ccm tukijadili.
Haya yote yanaaeleweka vizuri kabisa.Ni uchovu tu wa wanasiasa.
Nape ni CCJ.
Livingstone Lusinde ni ni Chadema .
J.Makamba amebebwa kwa nguvu ya baba yake.
Samwel sita ni CCJ
Benard Membe ni CCJ
Makonda ni CCM madaraka.Bila madaraka atahama na kujiunga na ACT ili apate angalau udiwani.
Mwakyembe ni CCJ
Wasira ni NCCR Mageuzi.
Magufuli ni CCM asiye na histori ndefu ya kukitumikia chama katika shida na raha.
Sumaye ni CCM madaraka.Mana alishasema akienguliwa atatafuta chama kingine.
Hawa wote wanacheza ngoma na nyimbo za Chadema.
Tumeona Nape na hilo Kundi lake wakifurahia kifo cha marehemu capt Komba huku wakisahau mazuri yote aliyoyafanya kukijenga chama cha mapinduzi katika uhai wake wote. Hawa ndio watu wanaosema wanakipigania chama.
Kinana ni CCM halisi ndio maana anajua mbinu za kukijenga chama.
Lowassa ni kati ya makada wa kweli wa CCM waliobakia. Kumuengua Lowassa kwa sababu ya kusikiliza kelele za wapita njia litakua ni jambo la kipuuzi na lisilokubalika.
Eti wanasema kwa nini watu wanakuja na kukuta viti vimepangwa na chakula.Ni akili za ajabu kabisa. Kwa ulimwengu wa sasa hivi wageni waje bila kutoa taarifa.
Hata kwa mila zetu za kiafrika mtu akienda kuposa anatoa taarifa kwa wakwe ili wajiandae kupokea ujumbe unaoletwa wa posa.Na usipotoa taarifa basi linakua ni jambo lisilokubalika.
Simu na mitandao iko kila mahali halafu mtu aende kwa mtu bila taarifa.
Ndio maana viongozi wa dini kwa muda mrefu wamepima wakagundua kuwa Lowassa ana hekima kuliko hawa waruka njia ,Nape na kundi lake.Kwani hata hoja zao za kumshambulia Lowassa ni za kijinga na chuki tu.
Eti watu wanazolewa bila kujua kinachoendelea halafu wanapelekwa kwa Lowasa kupewa hela.Hivi kweli inaingia akilini Msomi wa Chuo kikuu azolewe bila kujua anakoenda?
Hivi kweli unaweza ukamzoa mchungaji au shehe ukampeleka asikokujua na akakubali kwenda.
Viongozi wa dini siku zote wanapenda viongozi wasikivu.Na wamegundua kuwa Lowassa hana makuu.
Nape muda Mrefu amekua akionekana dhahiri sio kutumia nafasi aliyo nayo kuhakikisha kuwa anatumia Muda mwingi kupambana na Lowasa ili alete Mtu wake anayemtaka.
Mnafiki na Joka la Mdimu siku zote hawana jema.
Ingetokea wale wachungaji ,mashehe na wanafunzi wa vyuo wakaenda kimya kimya kwa Lowassa bila taarifa na kufika bila hata mashahidi ikiwemo waandishi wa habari basi leo hii Lowasa angekua ameshaitwa kwenye kamati ya maadili na kuhojiwa kuwa anafanya kampeni na vikao vya siri.Ingekua ni ishu kubwa kweli kweli.
Hii ndio tabia ya wanafiki walovamia ndani ya CCM na sasa wanataka kuwaengua makada wa komavu wa chama na serikali ili wapitishe wanachama wenzao wa CCJ!!!