Mkuu wakati nataka kureply pale ulipodai unataka CDM kisife ili kipate kutoa changamoto kwa CCM nikakutana na jibu lako juu kuwa hutaki kife kwa sababu utakuwa huna chama cha kukishambulia humu JF. Natumai hili jibu kwa Aweda should be taken as sense humour taking into consideration that you belong to the caliber that analyse issues with objective and unprejudiced mind. Lakini palepale mtu mwenye hizo virtues kwanini unampa kichwa na jeuri mtu ambaye ujengaji wake wa hoja haukisi level ya elimu aliyokuwa nayo? Kuhalalisha kufa kwa CDM kwa sababu ya kundi masalia na forged cum fabricated expulsion allegations za Shibuda na Zitto ni kushindwa mtu kuitendea taaluma yake haki na siasa kwa ujumla.
Kama kweli CDM itakufa kwa sababu Zitto na Shibuda watafukuzwa basi CDM hakipashwi kuwepo maana mnataka kutuaminisha kuwa toka Tanga mpaka Sumbawanga na Mutukula mpaka Mtwara ni watajwa wawili na kundi lao na masalia ndio CDM. Kwamba wanabaguliwa kwa sababu za kidini na ukanda na hivyo CDM kitakufa. Sijui labda Zitto ajiunge ili apate kufanya supplement kwa hiki kilichoandikwa. Halafu ili ukweli udhihiri kwanini ndugu Nape asiende awahoji au aongee nao waheshimiwa hawa ili waonyeshe kweli wanabaguliwa kwa sababu ya dini,kabila au sehemu wanakotoka? Wakisema hivyo basi atujuze through public communication channels at disposal ambazo zitaturuhusu kuwahoji na sisi pamoja na yeye. Na hapo tunakuwa na balanced story.
Lingine labda nimkumushe Nape kuwa ili utoe tuhuma nzito kama za ukabila, udini na ukanda lazima uwe umefanya tafiti za kutosha ili kukuwezesha kutoa conclusion ya namna hiyo. Lazima atuambie population ya utafiti wake, study areas na samples na sisi tukapime ili tuone kweli zinawakilisha wananchi wote wa Tanzania na hapo tuhuma zionekane zina ukweli ndani yake. Lakini pili tuhuma anazozitoa aangalie zisiwe zinapingana na tambo zetu kimataifa kwenye international fora. Tunajitambulisha kuwa kisiwa cha amani, hatuna ukabila, udini wala ukanda au tofauti zozote. Sasa kama CDM kina hayo yote je wanachama wa CDM sio sehemu ya Tanzania? Ni kweli wana CDM sio integral component ya peace and tranqulity constodians? Naomba anipe majibu haya kwa ufasaha bila jaziba na mimi na wengine tutasema mengine.
Jingine wanasema first put your house in order before turning to your neighbour's. Sijui kama ndani ya nyumba ya Nape kama hakuna moto unaowaka maana mengi yamesemwa kiasi watu wanatishiana pistols, mwenyekiti wake alisema wengine hawaachiani birauri mezani wakiogopa sumu na mengine mengi. Sasa kuna grand corruption kama za EPA, Meremeta, Buzwagi, Richmond/Dowans, Rada ya kuongpzea ndege, ndege ya rais, mikataba ya madini na ukaguzi wake na mengine mengi. Hivi nyumba yenye haya yote mwenye nayo anaweza kwenda kujaribu kusafisha nyumba ya jirani yake/ Kama affirmative basi inahitaji ujasiri wa hali ya juu
Mkuu
Bigaraone , big up for the analysis.
Mimi ni mmoja sitafurahi CDM ikifa, CDM inafanya kazi nzuri ni wale wajinga wajinga tu ambao huchukulia criticisms kama matusi na hivyo ku argue in kind.
Wana CDM kama wewe mkuu mpo wachache, wachache sana.
Kwanza kabisa tupo katika dunia ya multipartysm, dunia ya vyama vingi katika nchi karibu zote barani Africa.
Sasa leo vyama mbadala kwa chama tawala huwa inaleta a fresh breath of air in politics.
Kama kuna makosa katika vyama hivyo basi hayo ni makosa yao yanayoweza kutokea kwa kila chama.
Ni lazima tujipambanue kuwa chama kioja kinapofanya makosa, basi kingine kina capitalise makosa hayo na kuyashambulia vilivyo.
Huwa mimi ni mpezi wa kipindi cha PMQ(Prime Ministers Questions time), kipindi cha House of Commons Uingereza.
Jamaa wale wanavyoshambuliana utafikiri watashikana mashati punde!
Lakini mwisho wa siku wako pamoja kwa masuala ya mshikamano wa kitaifa.
Kama nilivyosema hapo nyuma makosa ya kisiasa hayako CDM tu, bali hata CCM, NCCR, CUF n.k.
Kwa upande mmoja bango lilishikwa na CDM wakati wa EPA,RICHMOND , Kagoda na kasha nyingine naweza kusema zilikuwa na taifa hili at heart.
Tuna kumbuka vizuri wengine ilibidi tuishambulie CCM wazi wazi kwa kushindwa kuchukua hatua kwa kashfa hizo, wale ambao watapinga fungueni archives za JF ili mjiridhishe-hakuna anayependa kuibiwa.
On the otherhand CDM imeanza kubweteka na umaarufu wake, imekuwa complacent, and complacency breeds laisszes faire, watu wameanza kujiona miungu watu, they cant do no bad.
Na hapo ndipo CCM inawa-nail!
Piga msumari haswa.
Kwamba kuna matumizi mabaya ya ruzuku
Kwamba kuna ubaguzi
Kwamba hakuna utawala bora ndani ya chama
Kwamba chama kilianza kuvuka hata mipaka ya madaraka yake na kujiona kinaweza kupambana na dola kutokana na wingi wa wapenzi
Sasa hayo ni makosa megine yanayotokana na hiyo complacency, na kujiona kujua.
Wenzenu ccm hatujalala, kuna kazi mbili tu.
Moja ni kujenga nchi na kuongoza
Pili ni kujibu mashambulizi ya vyama vingine kama CDM, CUF nk, na kwa maoni yangu yote yanafanyika vizuri sana tu.
Nakushukuru Bigaraone kwa kuonyesha jinsi ya kujenga hoja mtandaoni ili facts zionekane badal ya wale wenye matusi yanayotokana na utupu wa vichwa vyao.
Tutapingana katika hoja , lakini tutaijenga Tanzania yetu