Katibu wa NEC-CCM Nape NNauye ambaye vile vile ni Mkuu wa Itikadi na Uenezi, ametoboa siri ya kifo cha CHADEMA kuwa kitatokana na ubaguzi kati ya wananachama wake.
Ingalau magazeti mawili yamemnukuu akikomelea msumari katika tofauti zinazojitokeza hivi sasa ndani ya CHADEMA.Gazeti la Majira (21/1/2013) lenyewe limedai kwamba :
"Nape afichua siri za kifo cha CHADEMA, na kudai-hakuna dawa ya kutumia lazima kife-ameendelea kudai ni laana ya Nyerere, wasitafute mchawi"
Page 4 ya gazeti hili linaendelea
"Alisema(NAPE) ubaguzi ulioota mizizi kwa muda mrefundio unakimalizachama hichoambao umelelewa na waasisi pamoja na viongozi wa kitaifa hivyo kina haki ya kufa kutokana na dhambi hiyo"
Aliendelea...
"Hamuwezi kuwa na chama ambacho kinaendekeza ubaguzi..ili kiongozi wake adumu na kuheshimika lazima atoke ukanda fulani au ukoo fulani vinginevyo anasukiwa mizengwe na kutimiliwa. Walianza na marehemu Wangwe.... hivi sasa wameanza kumuandama Zitto Kabwe(Naibu Katibu Mkuu CHADEMA) na wanaoitwa vijana wake, nasikia wiki ijayo wamejipanga kumfukuza Shibuda(Bunge wa Maswa)"
Nnauye akamalizia kwa msumari mzito
"CHADEMA ni chama kidogo kinabaguana kiasi hicho, wakipewa dhamana ya kutawala nchi hali itakuwa mbaya zaidi"
My take
Wana CHADEMA huo ni msumari unaoweza kuwa mkuki moyoni.
Jisahihisheni kabla hamjafa kweli.
(NB wale wenye matusi chukueni likizo)
Pambaf!
Magamba acheni fikra mfu na potovu za kutaka kujenga mazingira ya hofu kwa wana-CHADEMA. Hizi ni propaganda mfu za miaka ya 47 za kuleta hoja mfu kuwa kuna dhambi ya Ubaguzi ndani ya CDM wakti si kweli!!Tunajua huu ni mkakakti wa CCM na serikali yake kutaka kuimaliza CDM. Tunajua kuna mipango imeandaliwa kwa kuwatumia UWT-Usalama wa Taifa na Jeshi la Polisi-CCM! Tumesikia mwishoni mwa wiki Katibu Mkuu-CDM Dr.Slaa akisema ana habari za kutoka ndani ya UWT kuwa kuna Bilions za Fedha ya walipa Kodi zimetengwa kuimaliza CDM!!!
Alichosema Nepi Naye kuwa dhambi ya Ubaguzi ndani ya CDM ni uongo wa mchana kweupe.Kama hayo aliyoyasema Nepi ni ya kweli basi hata CCM ni Wabaguzi na ndiyo watakufa kwanza kabla ya CDM. Mwalimu Nyerere ndiye alianzisha CCM kama Mwenyekiti na Mkuu wa nchi. Tuangalie safu aliyokuwa nayo kwenye uongozi: Waziri Mkuu alikuwa Joseph Warioba- anatoka Mkoa wa Mara,Mkuu wa JWTZ alikuwa Msuguri baadaye Mwita Kiaro wote kutoka Mkoa wa Mara, kulikuwa na Katibu mkuu Ofisi ya Rais Bwana Timothy Apiyo toka Mkoa wa Mara,alikuwepo Waziri Steven Wassira na yupo mpaka leo kutoka Mkoa wa Mara na wengine wengi! Je,huu ni Ubaguzi wa Kikanda kwa madai ya Nepi Naye!!!
Naamini Mwalimu alikuwa kiweka watu kulingana na uwezo wao kiutendaji na mpaka leo CCM ipo tangu enzi za TANU. Mfano mwingine rahisi kuhusu Ubaguzi, nenda pale BOT au TRA utakuta Wachagga na Wapare wamejaa kwenye ofisi hizo! Je, tuseme basi kuwa BOT na TRA zinaendeshwa kikanda kwa Ubaguzi??? Mbona hazijafa pamoja na Ufisadi ulnaoendelea huko????
Mimi naona CCM ndiyo wanaoenda kufa maana msemo wa MFA MAJI HAACHI KUTAPATAPA kwa sasa unajidhihirisha wazi kwa CCM. Haiwezekani hata kidogo kila siku kila kiongozi wa CCM akiamuka hana jambo jingine la kuzungumzia kuhusu maendeleo ya Watanzania isipokuwa kifo cha CDM. Huu ni upuuzi na ujinga. Kwa watu wenye akili wanaelewa nini kinachotengenezwa na CCM. Mbinu zilezile zilizotumiwa kuua CUF,NCCR-Mageuzi,TLP,UDP na sasa CDM ndizo zinazotumika.
Lakini napenda kuwatahadharisha Nepi,Mchembe,Wassira na timu yao kuwa kabla CDM haijafa CCM itakuwa tayari imeshaoza na kubakia mifupa!!!Kama ni LAANA YA MWALIMU NYERERE KUHUSU UBAGUZI BASI CCM WAMESHAKUFA TAYARI BADO MAZISHI TU! MAANA UBAGUZI UNAOFANYWA NA CCM KUBAGUA VYAMA VYA UPINZANI UNATISHA NA UNASIKITISHA NA UNATOSHA KUIMALIZA CCM!!MAKABURU WA SOUTH AFRIKA WALIKUWA WAKIWABAGUA WAAFRIKA WENZETU KINA MANDELA NA VYAMA VYAO VYA ANC ILI WASICHUKUE NCHI LAKINI MWISHO WA SIKU LEO ANC INATAWALA S.AFRICA.!!!
IT WILL BE THE SAME FOR CHADEMA IN TANZANIA. CCM BAGUENI SANA,PIGENI SANA RISASI ZA MOTO NA MABOMU WAFUASI WA UPINZANI HASA CHADEMA,TUMIENI SANA HELA YA WALIPA KODI KUHUJUMU UPINZANI LAKINI MWISHO WA SIKU MTAWEKWA PEMBENI TU WHAT MAY!!!HIVI BADO MNAFIKIRI TANZANIA YA SASA NI ILE YA ENZI ZA MWALIMU MIAKA YA 19 KWEUSI???YOU MUST BE CHEATING THYSELF! MAANDAMANO YA KUPINGA UJENZI WA BOMBA LA GESI ASILIA FROM MTWARA TO DAR IS JUST A TIP OF AN ICEBERG. WATANZANIA WAMEAMKA SASA.JUENI TU KWAMBA UPINZANI SI UADUI!!!
Tatizo lenyu CCM mnafikiri kwamba UPINZANI ni uadui na serikali which is not! Kwa nchi zenye true Democracy upinzani ni changamoto kwa serikali iliyoko madarakani, ni kioo cha serikali iliyoko madarakani kujitazama na kujisahihisha pale inapoboronga. Lakini hapa Tanzania things are just opposite. CCM na serikali yake mko tayari kuua vyama vya upinzani ili tu muendelee kubaki madarakani!!Mko tayari kumwaga damu ya viongozi na wafuasi wa upinzani kwa kutumia mamluki,mashushu na UWT!. Mie siyo mpiga ramli wala matabiri lakini kwa mazingira tu(circumstancial evidence) nia uhakika Wangwe hakuuawa na CDM baali aliuawa na mbinu chafu za CCM nyuma za pazia ili kutaka kukipaka CDM matope hatimaye kichukiwe na Watanzania.
Namaliza kwa kusema hivi; this time Watanzania hatudanganyiki. Hakuna Mtanzania anayekubali kuitwa Mdanganyika(Tanganyika). Tunajua mnawatumia watu kama Zitto Kabwe, John Madale Shibuda na mapandikizi mengine hasa ndani ya BAVICHA ili kufanikisha uovu wenu. Kama yie CCM mna sera safi,uongozi bora na hakuna Ufisadi kwanini mlazimishe kufa kwa chama????Uchaguzi ni mwaka 2015, why don't you appeal to wananchi through the Ballot BOX???Mna hofu ya nini kama Watanzania wana imani na serikali yenu si watawapigia kura???
Lakini cha ajabu badala ya kusubiri uamzi wa Ballot Box hapo 2015 sasa mmeanza kutumia live BULLET!!! Hii inadhihirisha kuwa maji yako shingoni so that you are just fighting for your survival! Time will tell. Poleni sana!