Mkuu
Bigaraone , big up for the analysis.
Mimi ni mmoja sitafurahi CDM ikifa, CDM inafanya kazi nzuri ni wale wajinga wajinga tu ambao huchukulia criticisms kama matusi na hivyo ku argue in kind.
Wana CDM kama wewe mkuu mpo wachache, wachache sana.
Kwanza kabisa tupo katika dunia ya multipartysm, dunia ya vyama vingi katika nchi karibu zote barani Africa.
Sasa leo vyama mbadala kwa chama tawala huwa inaleta a fresh breath of air in politics.
Kama kuna makosa katika vyama hivyo basi hayo ni makosa yao yanayoweza kutokea kwa kila chama.
Ni lazima tujipambanue kuwa chama kioja kinapofanya makosa, basi kingine kina capitalise makosa hayo na kuyashambulia vilivyo.
Huwa mimi ni mpezi wa kipindi cha PMQ(Prime Ministers Questions time), kipindi cha House of Commons Uingereza.
Jamaa wale wanavyoshambuliana utafikiri watashikana mashati punde!
Lakini mwisho wa siku wako pamoja kwa masuala ya mshikamano wa kitaifa.
Kama nilivyosema hapo nyuma makosa ya kisiasa hayako CDM tu, bali hata CCM, NCCR, CUF n.k.
Kwa upande mmoja bango lilishikwa na CDM wakati wa EPA,RICHMOND , Kagoda na kasha nyingine naweza kusema zilikuwa na taifa hili at heart.
Tuna kumbuka vizuri wengine ilibidi tuishambulie CCM wazi wazi kwa kushindwa kuchukua hatua kwa kashfa hizo, wale ambao watapinga fungueni archives za JF ili mjiridhishe-hakuna anayependa kuibiwa.
On the otherhand CDM imeanza kubweteka na umaarufu wake, imekuwa complacent, and complacency breeds laisszes faire, watu wameanza kujiona miungu watu, they cant do no bad.
Na hapo ndipo CCM inawa-nail!
Piga msumari haswa.
Kwamba kuna matumizi mabaya ya ruzuku
Kwamba kuna ubaguzi
Kwamba hakuna utawala bora ndani ya chama
Kwamba chama kilianza kuvuka hata mipaka ya madaraka yake na kujiona kinaweza kupambana na dola kutokana na wingi wa wapenzi
Sasa hayo ni makosa megine yanayotokana na hiyo complacency, na kujiona kujua.
Wenzenu ccm hatujalala, kuna kazi mbili tu.
Moja ni kujenga nchi na kuongoza
Pili ni kujibu mashambulizi ya vyama vingine kama CDM, CUF nk, na kwa maoni yangu yote yanafanyika vizuri sana tu.
Nakushukuru Bigaraone kwa kuonyesha jinsi ya kujenga hoja mtandaoni ili facts zionekane badal ya wale wenye matusi yanayotokana na utupu wa vichwa vyao.
Tutapingana katika hoja , lakini tutaijenga Tanzania yetu