Kwanza kabisa
masopakyindi nikufahamishe kwamba ccm haijengi nchi na wala haiongozi hii nchi, kinachofanyika ni kwamba mnaitafuna na kuitawala. Katika hili mmeshapoteza legitimacy yenu kwa watanzania.
Pili usidanganye watu kwamba mnajibu mashambulizi ya vyama vingine kama Chadema na cuf. Hawa cuf mnashirikiana kuendesha serikali kule zenji na tangu wakati huo hatujawahi kuwasikia viongozi wenu wa ccm wakipanda kwenye majukwaa ama mashabiki wa ccm kwenye mitandao wakiishambulia cuf.
Tunachoshuhudia kila kukicha si kwa viongozi tu bali hata wapenzi, mashabiki pamoja na vibaraka wa ccm ni kuishambulia Chadema tu kila uchao. Kiongozi yeyote wa ccm akizungumza na wanaccm wenzake bila kuitaja Chadema anaweza kupondwa mawe. Hata mzee wassira alijipatia kura za kishindo akiwania ujumbe wa nec kwa ahadi kwamba yeye ndiye kiboko ya Chadema!! kwamba imefika mahali wanaccm wakiisikia Chadema wanaumwa matumbo ya kuhara!!
Kama haitoshi ccm mmeamua kutenga fungu maalum la kuendesha propaganda chafu dhidi ya Chadema kwa kuwalipa waandishi wa habari wa magazeti, televison na wamiliki wa mitandao ya kijamii ili wawasaidie kufanya propaganda chafu. Mmekwenda mbali kiasi cha kuajiri vijana na kuwapatia vitendea kazi (computer) ili wakeshe mitandaoni kuwatukana viongozi wa Chadema.
Kwanini hizo nguvu msizielekeze kwenye kutekeleza ilani yenu ya uchaguzi ili wananchi wenyewe wajionee maendeleo mliyowaletea badala ya kuzungusha mawaziri mikoani kuyatetea maendeleo yasiyoonekana? hivi kweli kiongozi mzima na akili yake anawaambia wananchi kwamba ccm imeleta maendeleo mwanza kwakuwa sasahivi kuna mabugando mengi tofauti na ilivyokuwa hapo awali!!??
Mkuu
Mwita Maranya , a.k.a "Murra", umechanganyikiwa.
Inaelekea toka umeingia DSM hujawahi kurudi kwenu kutambika.
Na ndio maana unashindwa kuona hata maendeleo yanayoonekana dhahiri hata kwenu.
Haijapita hata miaka kumi, na umesahau kuwa kufika Musoma mlikuwa mkipitia Sirari mkitokea Kenya.
Na hii ni kwa vile barabara zilikuwa mbovu kiasi cha kutopitika, meshaambiwa andamaneni tena sana katika barabara zilizojengwa na serikali ya CCM.
Mkuu look around you na utaona jinsi ilani ya CCM inavyotekelezwa.
Maendeleo utayaonaje na wewe ni kinara wa M4C?
Kutwa kuchwa kupanga mipango isiyoendelevu ya maandamano?
Tembelea miji ya Mwanza, Singida hata Arusha na uone jinsi unavyoweza kufika kwenu haraka kwenye ngoma za mababu huko Musoma.
Na hii si barabara tu, hata nauli ya 32,000 ya Fastjet inakushinda mkuu?
Na huduma hiyo ingekujaje kama si sera nzuri za maandalizi kuvutia wawekezaji?
Kama wewe na chama chako mkiamua kufumbia macho maendeleo ya wazi nchini, hatuna budi kuwahurumia tu, maana nyie mawazo yote yako kwenye maandamano.
Ni sehemu chache sana mlizoweza kuhumiza maendeleo, hata zile mlizo shinda katika viti vya ubunge.
,baya zaidi chama chenu kinakosa mvuto kwa kasi.Kelele na shutuma za uongozi mbaya ndani ya chama chenu hazikuasisiwa na CCM.
Ccm haikumtuma Dr Slaa kujichotea mapesa ya ruzuku kwenye hazina ya chama chenu, na sasa mnaanza kuona kuwa ni rahisi kulaumu tu na kutoa shutuma zisizo na mashiko.
Kuendesha chama noma!
Mnajifunza the harsway kuwa chama si cha waliokianzisha bali kinatakiwa kuwa chama cha wanachama.
No wonder watoto wadogo umri wa watoto wenu wanawavua nguo hadharani.
Narudia, hakuna mtu anayependa kuibiwa.
Hili la ubaguzi sitaliongelea sana maana limeshajadiliwa kwa kirefu sana hapa , kama mna masikio na msikie.
Sasa hivi upende usipende, CHADEMA is under a shadow cast of doubt.
Dr Slaa anjinafasi na fungu la chama
Mkewe anajinadi kisiasa mikoani kwa fungu la chama
Chama kinatimua wale wanohoji mwelekeo hasi
M4c yenyewe ilianza kuwa kiwanda cha mauaji
Mwenyekiti Mbowe , kimya utafikiri ana muogopa katibu wake
Mzee Mtei ndo kabisa amedozi, anaamshwa akiambiwa Zitto anataka kugombea uraid!
Mkuu hiyo limelight ya chama chenu ilishafika peak, na sasa inzidi kuporomoka kwa kasi.