Nape: Dhambi ya ubaguzi inaimaliza CHADEMA!

Nape: Dhambi ya ubaguzi inaimaliza CHADEMA!

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,621
Reaction score
14,577
Katibu wa NEC-CCM Nape NNauye ambaye vile vile ni Mkuu wa Itikadi na Uenezi, ametoboa siri ya kifo cha CHADEMA kuwa kitatokana na ubaguzi kati ya wananachama wake.

Ingalau magazeti mawili yamemnukuu akikomelea msumari katika tofauti zinazojitokeza hivi sasa ndani ya CHADEMA.Gazeti la Majira (21/1/2013) lenyewe limedai kwamba :

"Nape afichua siri za kifo cha CHADEMA, na kudai-hakuna dawa ya kutumia lazima kife-ameendelea kudai ni laana ya Nyerere, wasitafute mchawi"

Page 4 ya gazeti hili linaendelea

"Alisema(NAPE) ubaguzi ulioota mizizi kwa muda mrefundio unakimalizachama hichoambao umelelewa na waasisi pamoja na viongozi wa kitaifa hivyo kina haki ya kufa kutokana na dhambi hiyo"

Aliendelea...

"Hamuwezi kuwa na chama ambacho kinaendekeza ubaguzi..ili kiongozi wake adumu na kuheshimika lazima atoke ukanda fulani au ukoo fulani vinginevyo anasukiwa mizengwe na kutimiliwa. Walianza na marehemu Wangwe.... hivi sasa wameanza kumuandama Zitto Kabwe(Naibu Katibu Mkuu CHADEMA) na wanaoitwa vijana wake, nasikia wiki ijayo wamejipanga kumfukuza Shibuda(Bunge wa Maswa)"

Nnauye akamalizia kwa msumari mzito

"CHADEMA ni chama kidogo kinabaguana kiasi hicho, wakipewa dhamana ya kutawala nchi hali itakuwa mbaya zaidi"


My take

Wana CHADEMA huo ni msumari unaoweza kuwa mkuki moyoni.
Jisahihisheni kabla hamjafa kweli.
(NB wale wenye matusi chukueni likizo)
 
mwambie huyo Nape kwanza aorodheshe dhambi zinlizoifikisha CCM kuwa hapo ilipo makundi ya wachawi, majambazi wehu, magaidi nk halafu, akimaliza kuzitubu na kukiunganisha chama cha majangili aje akosoe CHADEMA.
 
Ukweli unauma huo ndio ukweli msipoukubali mpende msipende mta dead,tutawasau .ubaguzi na udini ni janga cdm ingawa mnajifanya hamuoni
 
ZITTO ameisha wajibu. Mradi wa gesi duniani kote ni 1.2mill/mile,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,Tanzania chini ya ccm ni 2.2mill/km
 
mwambie huyo nape kwanza aorodheshe dhambim zinlizoifikisha ccm kuwa hapo ilipo makundi ya wachawi,majambazi wehu,magaidi nk halafu,akimaliza kuzitubu na kukiunganisha cnama cha majangili aje akosoe cdm.

Ndo mnapukutika hivo , wakati gari kubwa linachnja mbuga.
Chama chenu kitajiua chenyewe.
 
CHADEMA ikifa sio ndiyo furaha ya CCM! Am I missing something?
 
CDM ikifa sio ndiyo furaha ya CCM! Am I missing something?

Yes, you are. CDM ni chama cha kufa na kuzikana kwa sisi wa kaskazini.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mwambie Nape Chadema sio CCJ alichokiasisi na kufa kikiwa kwenye mimba. Atasubiri sana!
 
CDM ikifa sio ndiyo furaha ya CCM! Am I missing something?
NO!
Definately NO!

Sasa ikifa CDM, CCM itapata wapi sparring partner wa uhakika.
Na sisi waswahili wa vichochoroni tunakihitaji chama hicho KUISAHIHISHA CCM ITAWALE VIZURI.
 
cdm mmekwisha nawaambia . na mrema aje na majibu jins mlivyotumia mil 500 za m4c au ndio mlikopesha baba junior
 
My take

Wana Chadema huo ni msumari unaoweza kuwa mkuki moyoni.
Jisahihisheni kabla hamjafa kweli.
(NB wale wenye matusi chukueni likizo)

Wana Chadema huo ni msumari unaoweza kuwa mkuki moyoni.

Huo msumari unang'olewa kwa taabu sana toka CCM, hautoki kwa sababu ukitoka utatoka na uhai. Hizo kauli za Nape aka Nepi hazina tija labda angezitolea chama chake cha CCJ.

Jisahihisheni kabla hamjafa kweli.

CDM ni mwendo mdundo kuna kusonga mbele wenye kujisahihisha ni CCM wenye makovu yanayoongezeka kila kukicha
 
ajiulize vzur huyu bwn ne.pi,ni kwa nini wananchi wajipange barabarani ni kuwazomea yeye na magamb.a wenziwe??
tutaizika sisiem kabla ya 2015 .
 
Back
Top Bottom