Naombeni msaada nimetapeliwa

Naombeni msaada nimetapeliwa

Ungeleta 'hadithi' nzima hapa ili iwe fundisho hata kwa wengine kuchukua tahadhari.

Tukio kubwa namna hiyo unaishia kuleta picha tu bila hata kueleza tukio zima lilivyokwenda, pia kueleza ni location gani huko?
Story ya uwongo hii hujastuka tuu

Kuna kitu kinatafutwa hapa
 
Wakati mwingine unawaza hii Jamii Forums ina Watoto tupu wa LY waliomaliza juzi auuu...maana uwezi tegemea msaada wa mawazo kama mko hv
Mtu ametapeliwa mnaanza kumcheka na kumdhiaki kama hujawai tapeliwa basi uwezi jua Mtu anatapeliwa vipi?
Mjifunze kukaa kimya kama huna lenye msaada kwa mfikwa
La hasha! Basi labda ili jamvi ni sehemu ya mizaha na inda
Humu JF tunawatahadharisha kila mara, na sio watoto wa LY ni watu wazima lkn utapeli acha watu wafunguke huwezi wazuia
Wengine ndio maana tunaangalia km wewe na tupite tu tusiwadhrau wenzetu
Juzijuzi nimeambulia matusi humuhumu JF tumewakumbusha wizi wa magari uliotokea kule Mtoni kwa Aziz Ally jamaa akalipata gari lililotapeliwa na Askari wenyewe kituo cha K
Nikaeleza nilivyotaka kuibiwa Kunduchi kwa Warioba
Bado mtu anaweka Gari na zake na simu yake UNASHINDWAJE kusearch wakati ukiingia TRA, Bima, Traffic utaiona hiyo Gari cha mwisho ni namba zake za simu kwani ndio registered na NIDA sasa vinapishana kwa hiyo huyo lazima atakuwa DALALI, lkn bado watu hawaelewi
Na madalali waliomo humu JF wa Magari wanakutishia eti kuna mama alichomew nyumba kwa kuharibu biashara hakutoa ulaji.
Ndio maana katokea mrangi na baadhi ya member wameshawatambua na Mleta Mada angeendelea kutupa Feedback Matapeli wangekimbia kwani kuingia JF ni bure
 
Mbona comment zingine huzijibu?
ukisoma post 202 ya mrangi ni kwamba jamaa watapatikana na tayari POLISI wanafuatilia, hawa Matapeli wanaweza mtoroka bunazi kupitia JF kwani hata vitochi vinafungua mtandao wa JF
Msimcheke hapa tu najaribu kumpa tag
Kwa kifupi alipelekwa kwenye yard iliyoko Morocco.... Huko ndiko alipopigwa
Ila Mpaka dakika hii jamaa anapambana na polisi na mwenye yard
Jamaa ashapewa a, b, c za kufata ili awapate Hao matapeli
Ningekuwa dar ningeinunua kesi hiyo Yaani mpaka kesho saa nane kingeshaeleweka
 
#bunazi
Hebu eleza kwa kina,issie hii ili tujue pa kuanzia sasa wengine huku ni makachero wabaya sana. hapo ni eneo gani ? ndani ya Tanzania hii.
 
Kuwa makini unapotaka kuuza au kununua gari,nilikuwa nauza gari yangu kipindi flani,jamaa akatokea anaitaka hiyo gari,lakini sharti ili anunue ni lazima niipeleke kwenye yard yake ili akaikague,nikamwambia kwanini ni lazima nikuletee, kama unaihitaji njoo uione au tupange mahali pengine zaidi ya pale jamaa akaingia mitini,ila ikawa kila baada ya siku mbili au tatu ananipigia simu kutaka nimpelekee gari nikaachana naye.Mwingine alitaka kuniuzia gari nzuri sana lakini wakati naikagua ile gari nikaona pale kwenye engine namba ndani ya bonnet kile kibao kimen'golewa nilipomuuliza kaniambia njoo kesho,kuanzia kesho yake hakupokea tena simu yangu.Mwingine nilitaka kumuuzia gari akaja kuikagua akaniambia anataka kuiteset nikamuambia twende wote,tukiwa njiani jamaa alikuwa anaongea na watu wengine kwa lugha ambayo nilihisi ni Kikongo,tulipofika mahali ambapo alidai nimsubirie jamaa aliingia mitini na hakupokea simu yangu.Sasa ukiangalia utaona kuna sababau gani usiipokee simu kama gari ulikuwa hutaki kununua au hutaki kuuza? ni lazima tuwe waangalifu sana...
Ujumbe mzito sana huu kwa wanaokusudia kununua magari nchini
 
Pale panaitwa full stop kun bar pale madalali wengi wapigaji..... Kuna mshikaji mmja alitaka vanguard jamaa walienda kumpanga yard wakampanga jamaa kama mmiliki
Jamaa Ile anataka kudeposit Hela bank alipewa ac..... Huyo jamaa anayetaka kununua Gari alitokea rukwa Ile tu Nmpigia Sim asubirie tufike tuone mazingira ya biashara na Jina la ac anayo deposit je ni ya yard..... Kufika pale bahati nzr yule mmiliki wa yard pale mnyanya namjua tukamrukia hewani kutup ac yke Jina tofauti na akasema hajui khsu biashara hyo
Ahh Mara akaja jamaa mmja alijifanya mwenye yard tukamtmbua anaitwa kabila
Jamaa alipona upepo syo akasepaaa

Ova
Kino ni hatari mimi nanunua zebonga mana kuna mtu namjua miaka ndio humtumia,ila napo ukiingia kizembe unapigwa tu
 
Wanajf kwa kifupi nimetapeliwa na hawa watu hapo chini, wameniuzia gari hewa kwa yeyote anaewafahamu wahusika hapo chini naomba anifahamishe.


Pole sana.
Ila ningeshauri ungetupa habari hii kwa undani kidogo ilikuwaje kuwaje hadi ukatapeliwa gari ili pia kutusaidia na sisi tusije ingia mikononi mwao.

NB:
Inaelekea ulifahamu kuwa utatapeliwa ndiyo maana ukawapiga hizo picha. Ripoti polisi ukiwsilisha hizo picha na namba zao za simu unaweza pata msaada zaidi.
 
huyo mwenye miwani ukimcheki tuu usoni ana kesi ya kujibu..

Kitambi cha wizi,
anaangalia kiwizi,
kakaa kiwizi wizi,
hata miwani amevaa kihuni......

Hicho kitambi ni frexible.....
Akiwa kwenye meza ya makubaliano anakivimbishaa(huoni hata alivyokaa?)

Ukimshtua kina nyweaa

Ungemshtua tuu hapo hata kwa kupiga miguu chiniiii......
Ungeachiwa viti tuu hapo.......
Hata majii haachi.......

Usikute hata hayo maji kayatapeliii
 
Kino ni hatari mimi nanunua zebonga mana kuna mtu namjua miaka ndio humtumia,ila napo ukiingia kizembe unapigwa tu
Zebonga smart...
Unajua mm kna wakati nlikuwa nalenga sana magari kuuza nlikutana na kila Aina ya style
Kuanzia watu wa magomeni chipolopolo, lumumba, Biafra, Catalunya etc
Yaani ukijipindua unaweza uziwa Gari la moto

Ova
 
Aisee huu mji na matapeli kazi kweli juzi nimetoka kupata info za big mama mmoja nimeishi nae mtaani zaidi ya miaka mitatu kumbe issue zake za utapeli magari tena hao ndo balaa.

Wanakodi gari kwa Car rental wakiaminiwa wanafogi kila kitu kuhusu gari kisha wanauza msala unabaki kwa alieuziwa issue yao ya mwisho wamemuuzia mjeda gari za kukodi kama nne hivi na utapeli wa mitandaoni ndo yao anatafutwa kama pesa sasa hivi sjui katokomea wapi na hawa jamaa wana connection kubwa na polisi na waganga nguli unaowajua.

Utawapata tuu ila next time kuwa makini unapotaka kununua gari yard nenda ofisini jiridhishe kwa kila kitu
 
Back
Top Bottom