Naombeni msaada nimetapeliwa

Naombeni msaada nimetapeliwa

Kuwa makini unapotaka kuuza au kununua gari,nilikuwa nauza gari yangu kipindi flani,jamaa akatokea anaitaka hiyo gari,lakini sharti ili anunue ni lazima niipeleke kwenye yard yake ili akaikague,nikamwambia kwanini ni lazima nikuletee, kama unaihitaji njoo uione au tupange mahali pengine zaidi ya pale,jamaa akaingia mitini,ila ikawa kila baada ya siku mbili au tatu ananipigia simu kutaka nimpelekee gari,nikaachana naye.Mwingine alitaka kuniuzia gari nzuri sana lakini wakati naikagua ile gari nikaona pale kwenye engine namba ndani ya bonnet kile kibao kimen'golewa nilipomuuliza kaniambia njoo kesho,kuanzia kesho yake hakupokea tena simu yangu.Mwingine nilitaka kumuuzia gari akaja kuikagua akaniambia anataka kuiteset nikamuambia twende wote,tukiwa njiani jamaa alikuwa anaongea na watu wengine kwa lugha ambayo nilihisi ni Kikongo,tulipofika mahali ambapo alidai nimsubirie jamaa aliingia mitini na hakupokea simu yangu.Sasa ukiangalia utaona kuna sababau gani usiipokee simu kama gari ulikuwa hutaki kununua au hutaki kuuza? ni lazima tuwe waangalifu sana...
 
Kutapeliwa umependa mwenyewe, we dunia hii ya digit unaibiwa kizembe hivyo, ulishindwa kushirikisha wakili? Inaonekana wewe uliingizwa kwenye kitu cha tamaa cha bei rahisi ukaingia mkenge ukidhani we ndo umepata pole dogo ndo unajifunza hivyo.
Nitaandika yote hayo kwa kirefu ni story ndefu kidogo
 
Najua mpaka sasa unafahamu fika kuwa uliingia tamaa na kudanganyika kizembe ndo maana hutaki kuelezea story ilivokuwa. Hapa JF kuna experts watano tu nnaowanyooshea mikono, kwa kesi yako mshtue mrangi akupe mwongozo
 
Watanzania ni watu ovyo sana, jamaa kaomba msaada, kwa yule ambae anaweza kumsaidia, sasa utakuta watu wengine wamemjibu kwa KUMKEJELI na kumuona mjinga muomba msaada..

Sasa kama mtu hawezi kutoa msaada, kwanini asikae kimya tu, kwanini aje na comments za kijinga??
Ndio maana waafrika tunaongoza kwa uchawi duniani.
Hao wote ni wanga
 
Yaani kwa picha na maelezo hayo ingekuwa wenzetu tayari jamaa wameishadakwa zamani kwa wasamaria wema kuwatambua na kuwaanika
Wananchi ndio hufanya wahalifu wakamatwe haraka zaidi duniani kote kwa kuwauliza watu

Sasa naona jamaa badala ya kusaidiwa watu wanamkejeli
Kweli tuko nyuma sana kwa masuala ya misaada ya utapeli na wizi kwani wengi ni matapeli na ushirikiano ni mdogo sana
 
Mtoa mada na wewe kama hutoa full stori ulivyotapeliwa ili tujifunze na kujua pakuanzia kukusaidia wewe ni mzushi.
 
Na wewe umezidi. Unanunuaje gari na kufanya makubaliano bar ya chimpumu! Hujui bar kuna jini ulevi!?
 
Back
Top Bottom