Naomba msaada jinsi ya kusoma Mita ya maji (DUWASA)

donlucchese

JF-Expert Member
Mar 23, 2011
17,047
21,523
Salam wakuu,

Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu, naomba msaada jinsi ya kusoma hizi Mita maana muda mwingine nahisi wananibambika bili.

Matumizi ya kawaida tu ya maji na hapo ni familia ya watu wanne tu lakini jana wamenitumia bili elfu thelathini.

Ningesema pengine labda kwakuwa nilipanda migomba ila tangu mvua zianze December migomba hatumwagilii tena. Naomba msaada wakuu!

PXL_20240201_081337208.jpg
 
Salam wakuu,
Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu, naomba msaada jinsi ya kusoma hizi Mita maana muda mwingine nahisi wananibambika bili. Matumizi ya kawaida tu ya maji na hapo ni familia ya watu wanne tu lakini jana wamenitumia bili elfu thelathini. Ningesema pengine labda kwakua nilipanda migomba ila tangu mvua zianze December migomba hatumwagilii tena. Naomba msaada wakuu!View attachment 2890471
Issue siyo kusoma Mita, unapaswa kujuwa bei ya maji ya per unit.

Kila tarehe ya usomi mita unaambiwa ili uhakiki, na bili ikitumwa inaonesha ni kutoka unit Fulani mpaka unit Fulani, sasa hapo unaibiwa vipi?

Ukitaka kuthibitisha kama Una simtak jaza maji kwenye simtak soma meter yako andika pembeni, yakiisha jaza tena andika pembeni usimtumie direct Bombay linaleta maji then mwisho wa mwezi utajuwa meter yako ulitumia unit ngapi.
 
Issue siyo kusoma Mita, unapaswa kujuwa bei ya maji ya per unit.

Kila tarehe ya usomi mita unaambiwa ili uhakiki, na bili ikitumwa inaonesha ni kutoka unit Fulani mpaka unit Fulani, sasa hapo unaibiwa vipi?

Ukitaka kuthibitisha kama Una simtak jaza maji kwenye simtak soma meter yako andika pembeni, yakiisha jaza tena andika pembeni usimtumie direct Bombay linaleta maji then mwisho wa mwezi utajuwa meter yako ulitumia unit ngapi.
Nashukuru mkuu japo simtank bado sijajaliwa. Issue ni kwamba hata ile sms hua wanasema usomaji uliopita ni unit kadhaa, usomaji wa sasa NI kadhaa hamna, wanaleta tu bill
 
Issue siyo kusoma Mita, unapaswa kujuwa bei ya maji ya per unit.

Kila tarehe ya usomi mita unaambiwa ili uhakiki, na bili ikitumwa inaonesha ni kutoka unit Fulani mpaka unit Fulani, sasa hapo unaibiwa vipi?

Ukitaka kuthibitisha kama Una simtak jaza maji kwenye simtak soma meter yako andika pembeni, yakiisha jaza tena andika pembeni usimtumie direct Bombay linaleta maji then mwisho wa mwezi utajuwa meter yako ulitumia unit ngapi.
Pia Kuna kipindi maji yanakuwa hayatoki wanafungua Bomba wanaacha wazi Ili yakitoka wasikie ule upepo nao unazungusha mita.... Ama anafungua maji anayaona. Yanafoka zaidi kuliko kutoka lakini anaendelea tu kuacha yanafoka weee yanatoka kidogo yanafokaaaa yanatoka kidogo nayo hiyo inakimbiza mita.... Na pia matumizi ya maji kila saa bombani ni Bora kuwa na vifaa vya maji unajaza unatumia yakiisha unajaza Tena sio matumizi mazuri kutumia maji mara Kwa mara Moja Kwa Moja kutoka bombani ... Kingine watoto na majirani kama anawarusu kutumia Bomba.....
 
Nashukuru mkuu japo simtank bado sijajaliwa. Issue ni kwamba hata ile sms hua wanasema usomaji uliopita ni unit kadhaa, usomaji wa sasa NI kadhaa hamna, wanaleta tu bill
Sasa soma hiyo bill lazima inaonesha unit ulizotumia, Anza kufuatilia mwenyewe.

Haiwezekani Mita yako inasoma upo kwenye unit 200 halafu bill isome upo unit 250 hapo unaweza hata kuwashtaki mahakamani.

Ila nyinyi ndio mtasababisha tuletewe Mita za Luku za maji sasa.

Kuna huduma post paid ina faida yake kuliko prepaid.
 
Pia Kuna kipindi maji yanakuwa hayatoki wanafungua Bomba wanaacha wazi Ili yakitoka wasikie ule upepo nao unazungusha mita.... Ama anafungua maji anayaona. Yanafoka zaidi kuliko kutoka lakini anaendelea tu kuacha yanafoka weee yanatoka kidogo yanafokaaaa yanatoka kidogo nayo hiyo inakimbiza mita.... Na pia matumizi ya maji kila saa bombani ni Bora kuwa na vifaa vya maji unajaza unatumia yakiisha unajaza Tena sio matumizi mazuri kutumia maji mara Kwa mara Moja Kwa Moja kutoka bombani ... Kingine watoto na majirani kama anawarusu kutumia Bomba.....
Pale kwenye meter usiache on Bila kulock, hizo meter hata ule upepo hakuna maji huwa zinarekodi.

Ukitaka kwenda sawa na watowa huduma za maji tumia tank, tank likijaa lock kwenye meter hakuna kuleta maji bombani.
 
Salam wakuu,
Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu, naomba msaada jinsi ya kusoma hizi Mita maana muda mwingine nahisi wananibambika bili. Matumizi ya kawaida tu ya maji na hapo ni familia ya watu wanne tu lakini jana wamenitumia bili elfu thelathini. Ningesema pengine labda kwakua nilipanda migomba ila tangu mvua zianze December migomba hatumwagilii tena. Naomba msaada wakuu!View attachment 2890471
Wewe soma hapo kwenye 00495 m3. Mfano mwezi ujao ikasoma 00500 m3 maana yake umetumia 5 m3. Kwa bei ya huku kwetu 1 m3 ni tshs 1772 au tshs 2000 kama utatumia 5 m3 au zaidi.
Sasa fanya hesabu Ile za kkk hazihitaji hata darasa.
 
Wewe soma hapo kwenye 00495 m3. Mfano mwezi ujao ikasoma 00500 m3 maana yake umetumia 5 m3. Kwa bei ya huku kwetu 1 m3 ni tshs 1772 au tshs 2000 kama utatumia 5 m3 au zaidi.
Sasa fanya hesabu Ile za kkk hazihitaji hata darasa.
Nashukuru mkuu!
 
Tarehe 08Jan24 walinitumia meseji kwamba bill iliyopita ni .00 (kumaanisha niliclear sidaiwi), Jana tarehe 31Jan24 sijaambiwa previous bill ni kiasi gani ila moja kwa moja kwamba nadaiwa shekeli 30,502/=
 
Nashukuru mkuu japo simtank bado sijajaliwa. Issue ni kwamba hata ile sms hua wanasema usomaji uliopita ni unit kadhaa, usomaji wa sasa NI kadhaa hamna, wanaleta tu bill
Lazima wakuambie usomaji uliopita na wa sasa kisha tofauti ule na huu ni uniti kadhaa sawa na shilingi kadhaa, hapo mmemaliziana.
 
Back
Top Bottom