Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 397
- 993
Wakuu kwema?
Suala la mita za DAWASA limekuwa ni changamoto na kero kubwa kwetu watuamiaji, na si kwamba ni watu wachache, malalamiko ni mengi ikiwemo na kwangu mdau lakini DAWASA wanakaza shingo.
Nilishangazwa na mhudumu wa DAWASA kuona ni jambo la kawaida kwa familia ya watu watatu kuletewa bili ya unit 15-20, hawana biashara yoyote ya kuuza, muda mwingi wapo kazini, hakuna leakage na anaona ni kawaida tu kupokea bili hiyo, nikaacha hata kubishana nae, kama anaona hilo ni sawa.
Mimi bili yangu ilianza kushoot nikaletewa bili ya unit 12, mara ikaenda 15, iliyofuata ikaja unit 21! Hapo naishi mwenyewe, siku nzima inatumika kwenye shughuli za kujiingizia kipato, weekend kufua ni nguo hizo zilizovalia kwa wiki nzima, sijawahi kuacha bomba wazi hata siku moja, naweza sikae hapo kwa wiki au hata wiki mbili lakini bado nikaletewa bili hiyo!
Kuwatafuta DAWASA kwanza walinijibu kwa nyodo, nilipoendelea kuwasumbua waliniletea mtu wa kucheki mita, walipocheki wakasema hakuna leakage shida itakuwa kwenye matumuzi yangu au jirani yangu atakuwa anatumia maji upande wangu (mimi na jirani yangu tuna mita tofauti, jirani ni familia ya watu wanne na watoto wawili).
Nikamwambia hatushei maji, na hata tungekuwa tunashea bado bili hii ni kubwa kwetu wote kwa matumizi ya kawaida, ukizingatia hata wao wanaoshinda siku nzima ndani hawazidi wata watatu. Ndio huyo muhudumu akanipa majibu hayo kwamba jirani yake alikuwa anatumia maji yao baada ya kuwadhibiti sasa hibi wanatumia uniti 15-20 kwa mwezi, na anaona kupata bili hiyo ni sawa kabisa!
Nimesikia fununu kuwa DAWASA wanataka kubadili mita hizi kwasababu zina mtatizo na ndio chanzo cha kuleta bili hizi ambazo haziendani kabisa na matumizi ya watu na hivyo kuongeza mzigo kwa wananchi.
Kama ndivyo kwanini hawatoi taarifa kwa umma na bado wanaendelea kutuletea bili hizi za kipuuzi kwa makusudi? Sawa, mwenye uwezo anaweza kulipa huku akiwa na manung'uniko, lakini vipi kwa ambaye hana uwezo huo? Unampelekea bili hiyo mtu wakati unajua fika unamuonea na akishindwa kulipa unamuondolea hudumuma hiyo, hii ni haki?
Au mnataka wote tuanze kuwa wakorofi mkija kusoma mita tuwe tunashikana mashati?
Suala la mita za DAWASA limekuwa ni changamoto na kero kubwa kwetu watuamiaji, na si kwamba ni watu wachache, malalamiko ni mengi ikiwemo na kwangu mdau lakini DAWASA wanakaza shingo.
Nilishangazwa na mhudumu wa DAWASA kuona ni jambo la kawaida kwa familia ya watu watatu kuletewa bili ya unit 15-20, hawana biashara yoyote ya kuuza, muda mwingi wapo kazini, hakuna leakage na anaona ni kawaida tu kupokea bili hiyo, nikaacha hata kubishana nae, kama anaona hilo ni sawa.
Mimi bili yangu ilianza kushoot nikaletewa bili ya unit 12, mara ikaenda 15, iliyofuata ikaja unit 21! Hapo naishi mwenyewe, siku nzima inatumika kwenye shughuli za kujiingizia kipato, weekend kufua ni nguo hizo zilizovalia kwa wiki nzima, sijawahi kuacha bomba wazi hata siku moja, naweza sikae hapo kwa wiki au hata wiki mbili lakini bado nikaletewa bili hiyo!
Kuwatafuta DAWASA kwanza walinijibu kwa nyodo, nilipoendelea kuwasumbua waliniletea mtu wa kucheki mita, walipocheki wakasema hakuna leakage shida itakuwa kwenye matumuzi yangu au jirani yangu atakuwa anatumia maji upande wangu (mimi na jirani yangu tuna mita tofauti, jirani ni familia ya watu wanne na watoto wawili).
Nikamwambia hatushei maji, na hata tungekuwa tunashea bado bili hii ni kubwa kwetu wote kwa matumizi ya kawaida, ukizingatia hata wao wanaoshinda siku nzima ndani hawazidi wata watatu. Ndio huyo muhudumu akanipa majibu hayo kwamba jirani yake alikuwa anatumia maji yao baada ya kuwadhibiti sasa hibi wanatumia uniti 15-20 kwa mwezi, na anaona kupata bili hiyo ni sawa kabisa!
Nimesikia fununu kuwa DAWASA wanataka kubadili mita hizi kwasababu zina mtatizo na ndio chanzo cha kuleta bili hizi ambazo haziendani kabisa na matumizi ya watu na hivyo kuongeza mzigo kwa wananchi.
Kama ndivyo kwanini hawatoi taarifa kwa umma na bado wanaendelea kutuletea bili hizi za kipuuzi kwa makusudi? Sawa, mwenye uwezo anaweza kulipa huku akiwa na manung'uniko, lakini vipi kwa ambaye hana uwezo huo? Unampelekea bili hiyo mtu wakati unajua fika unamuonea na akishindwa kulipa unamuondolea hudumuma hiyo, hii ni haki?
Au mnataka wote tuanze kuwa wakorofi mkija kusoma mita tuwe tunashikana mashati?