Manumbu
JF-Expert Member
- Oct 28, 2009
- 1,746
- 1,283
siamini kwamba dunia utakosa mtu unayefanana nae. hata humu jamvini wapo. na kuna wengi tu wangependa kuishi kama ww. so hilo sidhani kama ni la msingi sana.
kuhusu kufurahia maisha, kila mtu ana mtazamo wake kuhuku kipi kinamfurahisha. lkn kama nimekusoma vizuri uliyoandika na ambayo hukuyaandika ila yanaonekana ktkt ya mistari, nadhani umeanza kuchukua hatua ya kubadilika. unadhani maisha uliyoaishi imetosha na sasa unajaribu kuisukuma hulka yako kwenye aina ya maisha tofauti na hiyo. binafsi naona hii ni hatua nzuri. wengi wetu tumeishi maisha ya kujirusha na mwishoni hurudi 'kundini' na kuishi maisha ya 'kawaida' (wengine wanapenda kuyaita a more responsible life).
Naamini ukimpata mtu sahihi utagundua kuwa ni yeye uliyekuwa unamtafuta ili uanze nae familia. na muombe Mungu wako akuoneshe huyu mtu ili nawe ujaribu maisha ya familia. labda utakuja kuyafurahia zaidi kuliko maisha ya kujiachia ambayo tayari unayajua na umeyaishi kwa muda wa kutosha. Muda nao hauko upande wako, manake wanasema usiringie ujana, fainali uzeeni.
Lkn pia kama hapatikani mtu wa kuwa nae kwenye familia na kama unadhani unahitaji mtoto, for sure, kwa uzoefu wako unajua nini na nani atakuwa bora kwako kwa hili. unaweza pata mwanao na ukaendelea na maisha huku ukimtunza mwanao.
kuhusu kufurahia maisha, kila mtu ana mtazamo wake kuhuku kipi kinamfurahisha. lkn kama nimekusoma vizuri uliyoandika na ambayo hukuyaandika ila yanaonekana ktkt ya mistari, nadhani umeanza kuchukua hatua ya kubadilika. unadhani maisha uliyoaishi imetosha na sasa unajaribu kuisukuma hulka yako kwenye aina ya maisha tofauti na hiyo. binafsi naona hii ni hatua nzuri. wengi wetu tumeishi maisha ya kujirusha na mwishoni hurudi 'kundini' na kuishi maisha ya 'kawaida' (wengine wanapenda kuyaita a more responsible life).
Naamini ukimpata mtu sahihi utagundua kuwa ni yeye uliyekuwa unamtafuta ili uanze nae familia. na muombe Mungu wako akuoneshe huyu mtu ili nawe ujaribu maisha ya familia. labda utakuja kuyafurahia zaidi kuliko maisha ya kujiachia ambayo tayari unayajua na umeyaishi kwa muda wa kutosha. Muda nao hauko upande wako, manake wanasema usiringie ujana, fainali uzeeni.
Lkn pia kama hapatikani mtu wa kuwa nae kwenye familia na kama unadhani unahitaji mtoto, for sure, kwa uzoefu wako unajua nini na nani atakuwa bora kwako kwa hili. unaweza pata mwanao na ukaendelea na maisha huku ukimtunza mwanao.