Nahitaji msaada wa haraka, hasira zitaniumbua mimi

Nahitaji msaada wa haraka, hasira zitaniumbua mimi

asante mkuu kwa ushauri ila loh
Nimekwambia ukachukulia masihara ila ingia google utafute uhusiano wa sex na hasira ni tiba moja matata..! Inatoa stress ambazo ndiyo chanzo kikuu cha hasira.

Naomba niotee, utakuwa hauna mpenzi au mwanaume wakwako unaye mmiliki wewe km wewe km unaye basi issue sex haujaipa nafasi yake, au huyo mtiaji ni joka la kidisa linang'ata ila hslina sumu.
 
Nimekwambia ukachukulia masihara ila ingia google utafute uhusiano wa sex na hasira ni tiba moja matata..! Inatoa stress ambazo ndiyo chanzo kikuu cha hasira.

Naomba niotee, utakuwa hauna mpenzi au mwanaume wakwako unaye mmiliki wewe km wewe km unaye basi issue sex haujaipa nafasi yake, au huyo mtiaji ni joka la kidisa linang'ata ila hslina sumu.
jamani nina mwanaume sema labda kuipa nafasi ya kutosha sex sina uhakika
 
Yaaani mimi hivi visa vinanikumbusha rafiki yangu mtei alioa Machame kipigo alichokuwa akikipata mkikutana asubuhi yaani utazan alikuwa kwenye ajali ya treni

WANAWAKE WA KICHAGA TULANE TU WAPITE IVI WANAVITABIA VYA KIPEPO
 
Yaaani mimi hivi visa vinanikumbusha rafiki yangu mtei alioa Machame kipigo alichokuwa akikipata mkikutana asubuhi yaani utazan alikuwa kwenye ajali ya treni

WANAWAKE WA KICHAGA TULANE TU WAPITE IVI WANAVITABIA VYA KIPEPO
We boy.a una generaliza mambo.

Afadhalia ukae kimya
 
sawa kaka
mkuu ulivyompole humu mtu hawezi dhani unahasira hivyo? kuna hii tovuti ya mashahidi wa Yehova inaitwa jw.org/sw. inaweza kukusaidia ushauri. nenda sehemu ya magazeti na download gazet la amkeni machi 2012. linasema,
upload_2016-10-18_16-9-47.jpeg
upload_2016-10-18_16-10-54.png


pia kuna mada zingine kuhusu hasira.

g_SW_201501_md.jpg

MSAADA KWA AJILI YA FAMILIA | VIJANA

Jinsi ya Kudhibiti Hasira

KIKWAZO
“Nilimfokea dada yangu na kuusukuma mlango kwa nguvu hivi kwamba chuma kilichokuwa nyuma ya mlango kikatoboa ukuta. Shimo hilo lilinikumbusha jinsi nilivyokuwa nimetenda kwa njia ya kitoto.”—Diane. *

“Niliinua sauti na kuropoka, ‘Sijui wewe ni baba wa aina gani!’ na kisha nikausukuma mlango kwa nguvu. Lakini kabla haujafungika, nilimtazama baba yangu usoni na kuona kwamba alikuwa amekasirika. Nilijuta sana kwa sababu ya kuropoka maneno hayo.”—Lauren.

Je, umewahi kufanya kama Diane na Lauren? Ikiwa ndivyo, makala hii itakusaidia.

MAMBO UNAYOPASWA KUJUA
Milipuko ya hasira inakuharibia sifa. “Mwanzoni nilifikiri kwamba watu wanapaswa kuelewa kwamba nina hasira,” anasema Briana, msichana mwenye umri wa miaka 21. “Lakini niligundua kwamba ni jambo lisilofaa kufoka ovyoovyo, na kwamba wengine waliniona kuwa mpumbavu!”

Biblia inasema hivi: “Yule anayekasirika upesi atatenda upumbavu.”—Methali 14:17.


Watu humwepuka mtu mwenye milipuko ya hasira kama wanavyokimbia volkano inayolipuka

Hasira inaweza kufanya watu wakuepuke. Kijana mwenye umri wa miaka 18 anayeitwa Daniel anasema hivi: “Unapokasirika unapoteza hadhi yako na heshima ambayo wengine wanayo kukuelekea.” Pia, Elaine msichana mwenye miaka 18 anakubaliana na jambo hilo. Anasema, “Watu hawapendi kushirikiana na watu wenye hasira. Badala yake wanawaepuka.”

Biblia inasema: “Usishirikiane na mtu yeyote mwenye mazoea ya kukasirika; wala usiende pamoja na mtu wa mifoko ya ghadhabu.”—Methali 22:24.

Unaweza kurekebisha hali. Sara, msichana mwenye miaka 15 anasema hivi: “Si rahisi nyakati zote kudhibiti hisia zako, lakini unaweza kudhibiti maneno na matendo yako. Hakuna haja ya kulipuka kwa hasira.”

Biblia inasema hivi: “Asiye mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwanamume mwenye nguvu, naye anayezuia roho yake ni bora kuliko mtu anayeteka jiji.”—Methali 16:32.

MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA
Uwe na lengo. Badala ya kusema, “Hivyo ndivyo nilivyo,” jitahidi kuboresha hali yako kwa kipindi fulani hususa—labda kipindi cha miezi sita. Katika kipindi hicho, andika maendeleo unayofanya. Kila mara unapokasirika, andika (1) jambo lililofanyika, (2) jinsi ulivyotenda, na (3) jinsi ambavyo ungetenda kwa njia bora zaidi na kwa nini ungetenda hivyo. Kisha azimia kutenda kwa njia hiyo bora zaidi wakati mwingine unapokasirishwa. Dokezo: Usisahau pia kuandika mambo mazuri unayotimiza! Vilevile andika jinsi unavyohisi baada ya kuonyesha sifa ya kujizuia.—Kanuni ya Biblia: Wakolosai 3:8.

Uwe na subira. Unapokasirishwa, usikimbilie kusema mara moja ulichokuwa ukitaka kusema. Badala yake, subiri. Shusha pumzi. Erik, mvulana mwenye miaka 15 anasema hivi: “Ninaposhusha pumzi ninapata wakati wa kufikiri kabla ya kusema au kufanya jambo nitakalojutia baadaye.”—Kanuni ya Biblia: Methali 21:23.

Panua maoni yako. Nyakati nyingine huenda umekasirika kwa sababu ya kufikiria upande mmoja tu wa jambo lililokupata, yaani, sehemu iliyokukasirisha wewe. Jitahidi pia kuelewa jinsi wengine wanavyohisi. Mwanamke mwenye miaka 24 anayeitwa Jessica anasema hivi: “Hata ikiwa watu ni wakaidi, kwa kawaida mimi hujitahidi kuelewa sababu inayowafanya watende hivyo.”—Kanuni ya Biblia: Methali 19:11.

Ondoka, ikihitajika. Biblia inasema hivi: “Kabla mabishano hayajalipuka, jiondokee.” (Methali 17:14) Kama andiko hili linavyoonyesha, nyakati nyingine jambo bora la kufanya hali inapokuwa mbaya ni kuondoka. Kisha, badala ya kuendelea kukazia fikira jambo hilo na hivyo kuzidi kukasirika, fanya jambo lingine. Mwanamke anayeitwa Danielle anasema hivi: “Nimeona kwamba kufanya mazoezi hunisaidia kupunguza mkazo na hilo limenisaidia nisilipuke kwa hasira.”

Jifunze kusamehe. Biblia inasema: “Fadhaikeni, lakini msitende dhambi. Semeni moyoni mwenu, . . . na kunyamaza.” (Zaburi 4:4) Kwa kweli si vibaya kukasirika. Lakini, utachukua hatua gani baada ya kukasirishwa? Kijana anayeitwa Richard anasema hivi: “Ukiruhusu matendo ya wengine yakukasirishe, hiyo itamaanisha kwamba wao ndio wanaokuamulia jinsi utakavyohisi. Kwa nini usijitahidi kuonyesha kwamba wewe ni mkomavu kwa kumsamehe aliyekukosea? ” Ukifanya hivyo, utakuwa umefaulu kudhibiti hasira yako badala ya kuiruhusu hasira ikudhibiti.
 

Attachments

  • upload_2016-10-18_16-9-46.png
    upload_2016-10-18_16-9-46.png
    125.3 KB · Views: 48
  • upload_2016-10-18_16-10-54.jpeg
    upload_2016-10-18_16-10-54.jpeg
    48.1 KB · Views: 54
Duh!
Hasira hadi za kupiga mtu??
Mi pia nina hasira ila sio kwa level hiyo

Ushauri Mimi nikiwa na hasira huwa zinaishia kwa kulia weee adi napitiwa na usingizi
Nikiamka hasira hakuna tena

Ama kama una mchumba ako mpigie, kua karibu nae akupet pet hasira zinapungua

Jaribu hayo
Hata yeye hajui inatokeaje
 
Back
Top Bottom