Asante mkuu kwa kujali ila nimeshaanza kubadilikafanya tuonane nikushauri! najua unavyo pata tabu. hata mimi nilikuwa hivyo!
Habari zenu wakuu,
Nina tatizo kubwa la hasira nimejaribu kupitia thread za wengine walioomba msaada naona sijafanikiwa. Sasa naomba nijielezee mimi wanasema mficha maradhi kifo kiamuumbua.. Naelekea kufa sasa sababu jana nimekasirika nimefanya mambo ya ajabu hapa nilipo mwili unauma kila mahali, natetemeka kama teja sababu ya kunywa pombe sana.
Kwanza nachukua muda kukasirika ila huwa nalipuka kama bomu, unaweza niudhi leo jambo kubwa ila kesho ukaniudhi kidogo nikakufanyia jambo kwanza huwezi elewa na mara nyingi hutegemei reaction ile kwa hiyo huwa nakuwa mshindi nakupa ngumi mateke kukutafuna nikibahatika ndani ya dakika mbili nakuta nimefanya tukio la kutosha..
Wakati mwingine nalia sana na ukiniongelesha nalia kwa sauti kama napigwa aibu kwa mtoto wa kike.
Nakunywa pombe sana ili nilewe nizime nilale lakini hili nina miezi 10 sijafanya japo jana nimelifanya tena na mimi nilishafanikiwa katika hili naona linanirudia tena (japo akili yangu na nafsi yangu inaniambia bora kurudia kunywa pombe).
Naombeni msaada nifanye nini napokasirika?
NB: Nikikasirika huwa nashindwa kuongea na ukiona umeniboa naongea jua sijakasirika ila nikaa kimya kaa mbali na mimi... Mpaka nawaza au bado na utoto utoto japo ni mkubwa!
Asanteni..
===========
MADA HII IKIWA NA MAONI YA WANAJF IMESOMWA PIA KWENYE KIPINDI CHA JAMII LEO. TAZAMA VIDEO;
Asante mkuu nitafanyia kaziPata mtu wa kukushauri, penda kukaa na watu wachangamfu, tembelea sehemu za garden na miti mingi(Nature), listern to slow musics...jiaminishe kuwa utaishinda hii hali cause everthing comes from your brain an everthn gets SOLVED by your brain...
Note;
Usipende kukaa na watu wenye masihara, au utani na wale unaoamini at anytime atakutoa kwenye mood...kaa na watu wanaokufanya ucheke na kuwa na amani moyoni utaanza kuona changes as time goes by.
Hebu fafanua zaidi kiongoziTumia yeegnko ya kichina hasira zitapungua sana kitakachobaki ni gubu tu.
Mimi nakwambia kweli nikipitisha wiki moja sijachapa mzigo ilihali nahisi hamu kwa siku zote hizo, huwa nakuwa na hasira nisizoziimili, nikishachapa mzigo kila kitu kinakaa sawa. Vipi unapata makamuzi yakutosha?
Dah hongera mkuu,Hio hali ni hali ambayo unaweza kuibadilisha, hasira unaweza kuibadilisha wewe mwenyewe tena kwa kupuuzia tu, kuwa aah kwani kitu gani, najikumbuka mimi mwenyewe nilikuwa nina hasira sana, nyumbani balaa ni kila wakati sitaki kuonewa na rafiki wala kaka wala dada angu, lakini huwezi amini nimejicontrol mpk sasahivi nimekuwa raia wa kawaida kabisa, ata unifanye nini sina time kabisa, tabia hio ukiwa nayo inaendana na kukosa usingizi unakuwa mtu wa mawazo usiku kucha, nimeacha vyote ata unifanye nini sshivi nakoroma tuu yaani nasahau kabisa kama ulinifanya kitu, kwaiyo jicontrol tu, maana hio hali ni hatari kwa afya yako na kwa sifa ya mtoto wa kike
asante mkuu ,.. usipige utauaAisee hata mimi nina hasira sana tena za haraka mno ila kuleta impact ni nadra. Nadhani ni asili yetu kwetu ukoo wa Washana baba zangu wote ni short tempered. R.i.P Mama nae alikuwa mkali yani, hapendagi ujinga ingawa alikuwa na upendo sijawahi ona yani. Mshua nae mzungu wa roho balaa ila shida ni akimaindi anaeza kunyonga.
Kwangu mi hasira cjui nmechukua za nani kati ya hao wazazi ila najijua so napendaga kucheka na watu mara nyingi utani mwingi na kumaindi mara chache ni mpaka unikere sana. Tutacheka sana ila in real life kebehi na dharau ndio haswaa sifagili yani ukitaka ni blow into flames uniguse maeneo hayo. Sitaangalia we ni nani na wadhifa gani tutaharibiana tu.
Njia ninayotumia kama anger control ni kutukana kistaarabu tu bila kupayuka...Yani hata ukinudhi kiasi gani nikitukana tu on the spot hapo hasira zinaisha kabisa tunakuwa marafiki tena. Sinaga tabia ya kuweka vinyongo.
Kupigana niliacha utotoni, na utu uzima huu nimefanikiwa kumtia makofi demu wangu tu aliekuwa analeta dharau za kike nkamuonesha kilichomtoa kenge manyoya.
Vinginevyo miss chagga unaweza ukajaribu hii njia mi inanisaidia sana. Inaniepusha na mengi mabaya ya hasira.
Habari zenu wakuu,
Nina tatizo kubwa la hasira nimejaribu kupitia thread za wengine walioomba msaada naona sijafanikiwa. Sasa naomba nijielezee mimi wanasema mficha maradhi kifo kiamuumbua.. Naelekea kufa sasa sababu jana nimekasirika nimefanya mambo ya ajabu hapa nilipo mwili unauma kila mahali, natetemeka kama teja sababu ya kunywa pombe sana.
Kwanza nachukua muda kukasirika ila huwa nalipuka kama bomu, unaweza niudhi leo jambo kubwa ila kesho ukaniudhi kidogo nikakufanyia jambo kwanza huwezi elewa na mara nyingi hutegemei reaction ile kwa hiyo huwa nakuwa mshindi nakupa ngumi mateke kukutafuna nikibahatika ndani ya dakika mbili nakuta nimefanya tukio la kutosha..
Wakati mwingine nalia sana na ukiniongelesha nalia kwa sauti kama napigwa aibu kwa mtoto wa kike.
Nakunywa pombe sana ili nilewe nizime nilale lakini hili nina miezi 10 sijafanya japo jana nimelifanya tena na mimi nilishafanikiwa katika hili naona linanirudia tena (japo akili yangu na nafsi yangu inaniambia bora kurudia kunywa pombe).
Naombeni msaada nifanye nini napokasirika?
NB: Nikikasirika huwa nashindwa kuongea na ukiona umeniboa naongea jua sijakasirika ila nikaa kimya kaa mbali na mimi... Mpaka nawaza au bado na utoto utoto japo ni mkubwa!
Asanteni..
===========
MADA HII IKIWA NA MAONI YA WANAJF IMESOMWA PIA KWENYE KIPINDI CHA JAMII LEO. TAZAMA VIDEO;
Inategemea na aina ya mapenzi na unayempata kukupa penzi.mapenzi yana maudhi
asante mkuuInategemea na aina ya mapenzi na unayempata kukupa penzi.
Jitahidi sana kukumbuka maneno matatu yakiongozwa na
Wewe ninani?
1. umetoka wapi
2. Upo wapi na
3. Unakwenda wapi
Jitahidi sana kulala lakini si kunywa pombe.
kabisapole sana, nafikiri sasa hivi utakuwa umeanza kupona