miss chagga
JF-Expert Member
- Jun 7, 2013
- 57,821
- 48,976
Habari zenu wakuu,
Nina tatizo kubwa la hasira nimejaribu kupitia thread za wengine walioomba msaada naona sijafanikiwa. Sasa naomba nijielezee mimi wanasema mficha maradhi kifo kiamuumbua.. Naelekea kufa sasa sababu jana nimekasirika nimefanya mambo ya ajabu hapa nilipo mwili unauma kila mahali, natetemeka kama teja sababu ya kunywa pombe sana.
Kwanza nachukua muda kukasirika ila huwa nalipuka kama bomu, unaweza niudhi leo jambo kubwa ila kesho ukaniudhi kidogo nikakufanyia jambo kwanza huwezi elewa na mara nyingi hutegemei reaction ile kwa hiyo huwa nakuwa mshindi nakupa ngumi mateke kukutafuna nikibahatika ndani ya dakika mbili nakuta nimefanya tukio la kutosha..
Wakati mwingine nalia sana na ukiniongelesha nalia kwa sauti kama napigwa aibu kwa mtoto wa kike.
Nakunywa pombe sana ili nilewe nizime nilale lakini hili nina miezi 10 sijafanya japo jana nimelifanya tena na mimi nilishafanikiwa katika hili naona linanirudia tena (japo akili yangu na nafsi yangu inaniambia bora kurudia kunywa pombe).
Naombeni msaada nifanye nini napokasirika?
NB: Nikikasirika huwa nashindwa kuongea na ukiona umeniboa naongea jua sijakasirika ila nikaa kimya kaa mbali na mimi... Mpaka nawaza au bado na utoto utoto japo ni mkubwa!
Asanteni..
===========
MADA HII IKIWA NA MAONI YA WANAJF IMESOMWA PIA KWENYE KIPINDI CHA JAMII LEO. TAZAMA VIDEO;
Nina tatizo kubwa la hasira nimejaribu kupitia thread za wengine walioomba msaada naona sijafanikiwa. Sasa naomba nijielezee mimi wanasema mficha maradhi kifo kiamuumbua.. Naelekea kufa sasa sababu jana nimekasirika nimefanya mambo ya ajabu hapa nilipo mwili unauma kila mahali, natetemeka kama teja sababu ya kunywa pombe sana.
Kwanza nachukua muda kukasirika ila huwa nalipuka kama bomu, unaweza niudhi leo jambo kubwa ila kesho ukaniudhi kidogo nikakufanyia jambo kwanza huwezi elewa na mara nyingi hutegemei reaction ile kwa hiyo huwa nakuwa mshindi nakupa ngumi mateke kukutafuna nikibahatika ndani ya dakika mbili nakuta nimefanya tukio la kutosha..
Wakati mwingine nalia sana na ukiniongelesha nalia kwa sauti kama napigwa aibu kwa mtoto wa kike.
Nakunywa pombe sana ili nilewe nizime nilale lakini hili nina miezi 10 sijafanya japo jana nimelifanya tena na mimi nilishafanikiwa katika hili naona linanirudia tena (japo akili yangu na nafsi yangu inaniambia bora kurudia kunywa pombe).
Naombeni msaada nifanye nini napokasirika?
NB: Nikikasirika huwa nashindwa kuongea na ukiona umeniboa naongea jua sijakasirika ila nikaa kimya kaa mbali na mimi... Mpaka nawaza au bado na utoto utoto japo ni mkubwa!
Asanteni..
===========
MADA HII IKIWA NA MAONI YA WANAJF IMESOMWA PIA KWENYE KIPINDI CHA JAMII LEO. TAZAMA VIDEO;