Nafikiria kuachana na mke wangu

Nafikiria kuachana na mke wangu

sasa alokwambia hormone ni tatizo permanent la uzazi ni nani?
Hormone mbona zinarekebishika?
We mpk umri huo kuna mwanamke umeshampa ujauzito?
Umeshafanya kipimo cha uwezo wako wa kutungisha mimba?( zingatia sijakuuliza iwapo unadinda au la)mana ndo huwa mnajuaga mradi unasimamisha basi unaweza kutungisha mimba.
If hujawahi kufanya kipimo cha uwezo wa manii zako kuwa na mbegu za kutungisha mimba usimwambie mwanamke hazai!
mkuu mpaka nakuna hapa hizo taste za sperm nimefanya asee..usikariri
 
Ebu nenda kapige need miezi mitatu mfurulizo ukipata mtoto nje usimuache mkeo tafuta suruhisho mkeo azae usipopata mtoto nje wewe ndio tatizo kubali kulea damu siyo yako kitamda hakizai haramu
Tumeshafanya vipimo sio swala naongea nisichokijua
 
Mmeshajua shida ni nini? Piteni kwa wataalam mnaweza kupata solution,pia kuna Dr yupo pale Kairuki alimsaidia jamaa yangu,mkewe amejifungua last week.Pia nina Kaka yangu wa hiyari amezunguka mpaka India hakufanikiwa lakini amepata watoto watatu ndani ya miaka mitano ila wote wanazaliwa na miezi saba maana ikivuka hapo kiumbe kinakufa,kuna Dr yupo na clinic yake pale Buyuni njia ya kwenda Chanika,kama utahitaji mawasiliano yao nitakupa, ni rahisi kuchukua kwa hawa jamaa zangu.

Binafsi nakushauri usimwache kwasababu hiyo utampa shemeji psychological torture ya hali ya juu sana.Fanya jitihada ili mjue shida ni nini, kama hakuna solutions then mtafanya mutual agreement 🙏
nimepokea ushauri wako
 
Sasa unaachana nae umejua tatizo lipo wapi lipo kwako au kwake? Je Umefanya vipimo vyovyote
 
Habari za muda humu ndani,nawaza kuachana na wife niliyekaa nae kwenye mahusiano miaka 5 kwa maana miaka mitatu tumeishi pamoja.
Sababu iliyofanya kufikiria maamuzi haya ni kukosa mtoto mpaka leo,sasa nafikiria kuanza maisha mapya tu.Naombeni ushauri wenu juu hili.
Huoni hata aibu kusema unajikiria kiachana na mke wako!! Kaeni mzungumze, maana hakuna mkamilifu chini ya jua.
 
Habari za muda humu ndani,nawaza kuachana na wife niliyekaa nae kwenye mahusiano miaka 5 kwa maana miaka mitatu tumeishi pamoja.
Sababu iliyofanya kufikiria maamuzi haya ni kukosa mtoto mpaka leo,sasa nafikiria kuanza maisha mapya tu.Naombeni ushauri wenu juu hili.
Piga nje cup,ukipata mtoto.mlete home,acha dharau mkuu huenda damu haziendani na wewe je umehawahi kutest mitambo.
 
Hoja laini sana homoni sio ishu bn we sema kuna mengne lakin utaki kusema
 
Habari za muda humu ndani,nawaza kuachana na wife niliyekaa nae kwenye mahusiano miaka 5 kwa maana miaka mitatu tumeishi pamoja.
Sababu iliyofanya kufikiria maamuzi haya ni kukosa mtoto mpaka leo,sasa nafikiria kuanza maisha mapya tu.Naombeni ushauri wenu juu hili.
Katika mahusiano ya ndoa au ya kuishi pamoja, mtoto ni zawadi — siyo haki ya moja kwa moja wala kipimo cha thamani ya mke/mume. Mara nyingi jamii humlaumu mwanamke, lakini kimatibabu sababu za kutopata mtoto zinaweza kuwa kwa mwanaume, mwanamke au wote wawili.

Je, mmewahi kupima wote wawili kwa madaktari bingwa wa uzazi (fertility specialists)?
 
Habari za muda humu ndani,nawaza kuachana na wife niliyekaa nae kwenye mahusiano miaka 5 kwa maana miaka mitatu tumeishi pamoja.
Sababu iliyofanya kufikiria maamuzi haya ni kukosa mtoto mpaka leo,sasa nafikiria kuanza maisha mapya tu.Naombeni ushauri wenu juu hili.

Don't dare to do that!!!!!

Kamwe usijaribu kufanya hivyo.

utajiweka kwenye mazingira ya kujuta milele.
 
Back
Top Bottom