Nafikiria kuachana na mke wangu

Nafikiria kuachana na mke wangu

Habari za muda humu ndani,nawaza kuachana na wife niliyekaa nae kwenye mahusiano miaka 5 kwa maana miaka mitatu tumeishi pamoja.
Sababu iliyofanya kufikiria maamuzi haya ni kukosa mtoto mpaka leo,sasa nafikiria kuanza maisha mapya tu.Naombeni ushauri wenu juu hili.
Hapo sasa unamwacha anaenda kupata mtoto
 
Unauhakika shida ni yeye na sio wewe? Usikute wewe ndio unatatizo yeye ndio anakuvumilia.Vp kama ukimwacha yeye akaenda huko akapata mtoto harafu wewe ukachukua mwanamke mwingine na usipate?
 
Umemchakaza dada wa watu sa unataka kumenya kitu kingne yeye umteme why ustafute mtoto nje ya ndoa tu halafu huyo abaki kuwa mkeo otherwise umemchoka tu hilo la kukosa mtoto ni kiungo tu
ntajaribu kumshirikisha hili nione atasemaje
 
Unauhakika shida ni yeye na sio wewe? Usikute wewe ndio unatatizo yeye ndio anakuvumilia.Vp kama ukimwacha yeye akaenda huko akapata mtoto harafu wewe ukachukua mwanamke mwingine na usipate?
mpaka napost tumeshaenda hospital kufanya check up
 
MTOTO NI ZAWADI YA NDOA
tatizo sio yeye tatizo ni nyie
Ndio maana wazungu wanaadapt watoto n.k sio sawa kumuacha mwanamke eti kisa kachewa kupata mtoto, yaani itakosea sana, badili mtazamo wako kaka, yaani umenunua shamba kila ukipanda mazao hayaoti soln ni kuuza na kununua shamba jipya? Huku unatumia mbegu zilezile ?

Hapana utachemka vibaya, watu hawaowani ili wapate watoto wanaoana ili waishi pamoja kwenye shida na raha kucheqakupata mtoto ni shida mojawapo
Kwann niadopt mtt na atujafunga ndoa
 
Umeshalipq mahali unahitaji ndoa gani? Kwa mkristo hufungi ndoa UNABARIKI ndugu huyo ni mkeo,
Kuna utofauti kati ya kukaa na binti kama 'demu' wako tu, na kuishi na mwanamke kama mke wako, wewe huyo ni mke wako serikali, mungu na wazazi wanajua hilo.
Kwahiyo huwezi kumuacha mke wako kisa hajakuzalia watoto, basi na yeye akuache kisa hujamzalisha mtoto? Nyote wawili inatakiwamfarijiane na kupata ushauri wa kitaalau au kiroho kwanza malizieni kufunga ndoa, ndipo baraka zitazidi kumiminika
 
Habari za muda humu ndani,nawaza kuachana na wife niliyekaa nae kwenye mahusiano miaka 5 kwa maana miaka mitatu tumeishi pamoja.
Sababu iliyofanya kufikiria maamuzi haya ni kukosa mtoto mpaka leo,sasa nafikiria kuanza maisha mapya tu.Naombeni ushauri wenu juu hili.

Pole sana.

Vipi mlienda hospital kuonana na daktari ili kubaini sababu za kukosa mtoto?

Kama hamjaenda hospital basi ni muhimu mkafanya hivyo.

Kila la kheri.
 
kama swala ni mtoto usijaribu.
hata hivyo miaka mitano ni michache sana.
zamani ningekujibu inbox lakini kwa faida ya wengi na kwakuwa sasa nimekuwa mtu mzima naomba nikujibu haphapa.
  • kwanza niktaarifu kuwa mimi ni mmoja ya watu waliokaa muda mrefu bila mtoto nikiwa na mke kwa ndoa halali ya kanisani kwa zaidi ya miaka ishirini ukiongeza uchumba sugu wa miaka 4 unaweza ona nimekaa naye kwa miaka 24.
  • faida za kuwa naye ni nyingi zaidi ya watoto kwakuwa naziona ndoa za rafiki zangu zilivyo.
  • ikumbukwe kwamba tunapooana kigezo cha kwanza ni kwasababu tumependana na watoto wanakuja kwa hatua nyingine lakini chakwanza huongozwa na upendo.
  • atakayekuja atakuja kwasababu unataka mtoto/watoto kiukweli hautampenda kwakuwa mwanadamu anapenda mtu mmoja tu anayefuata ni by the way.
    • utasikia hivi Gerome huyu ndio mke wake wa kwanza nao watajibu hapana waliachana na mkewe kisa hazai ndo akaoa huyu.
    • hata ukiwa mgane mke wa pili lazima atatambulika kuwa livyofariki yule ndo akamuoa fulani.
  • kiufupi hautapata satisfaction ya love
  • hatukufundishi dhambi kama unaona swala ni mtoto we tafuta mtoto kwingine halafu baki na ndoa yako wako manesi na waalimu kibao hawana pa kushika kubaliana naye terms kuwa utatunza mtoto kwa mwezi utapeleka kiasi fulani cha fedha kwa kutunza mtoto.
  • mwisho kabisa watoto sio muhimu kwakuwa watoto wote tulionao tunapewa na MWENYEZI MUNGU tuwatunze tu mwisho wa siku lazima waondoke kwenye himaya yetu unasomesha mtoto kuanzia chekechea mpaka chuo kwa average ya ada ya milioni tatu kwa mwaka ukihesabu chekechea miaka 2, primary 7, secondary 6 na chuo 3 master 2 jumla kama miaka 20 sawa na 60,000,000/- halafu unakuja kulipwa mahali milioni 3 send off unatumia milioni 10 na mikopo hiyari isiyopungua milioni 20 achilia mbali wazazi mnatoa zawadi ya kiwanja chenye thamani ya milioni 20 halafu jamaa anaondoka na mshahara wa binti yako usiopungua milioni tatu kwa mwezi kwa miasha yake yote. mwezi wa kwanza tu mahali isharudi.
nimekuelewa ushauri lakini hatujafunga ndoa.
 
Umeshalipq mahali unahitaji ndoa gani? Kwa mkristo hufungi ndoa UNABARIKI ndugu huyo ni mkeo,
Kuna utofauti kati ya kukaa na binti kama 'demu' wako tu, na kuishi na mwanamke kama mke wako, wewe huyo ni mke wako serikali, mungu na wazazi wanajua hilo.
Kwahiyo huwezi kumuacha mke wako kisa hajakuzalia watoto, basi na yeye akuache kisa hujamzalisha mtoto? Nyote wawili inatakiwamfarijiane na kupata ushauri wa kitaalau au kiroho kwanza malizieni kufunga ndoa, ndipo baraka zitazidi kumiminika
tumeshapita hospitali
 
Pole sana.

Vipi mlienda hospital kuonana na daktari ili kubaini sababu za kukosa mtoto?

Kama hamjaenda hospital basi ni muhimu mkafanya hivyo.

Kila la kheri.
Tumeshaenda hospital
 
Habari za muda humu ndani,nawaza kuachana na wife niliyekaa nae kwenye mahusiano miaka 5 kwa maana miaka mitatu tumeishi pamoja.
Sababu iliyofanya kufikiria maamuzi haya ni kukosa mtoto mpaka leo,sasa nafikiria kuanza maisha mapya tu.Naombeni ushauri wenu juu hili.
Muombe Mungu kama vile ulivyo omba upate mke kama ulifanya hivyo
 
Back
Top Bottom