Nafasi za kazi Jeshi la Polisi Tanzania

Unaweza kwenda nalo ila binafsi nakushauri kama ukichaguliwa kwenda huko nenda na kirasket tu, vingine utanunua huko huko.Tranka ni muhimu sana kwa usalama wa vitu vyako. Ila linaweza likawa mzigo mkubwa sana siku ya kwanza ukifika huko 😂😂😂
Oyaa jamani hivi depo Kiwira au Ccp wanaendaga na ma tranka? maana wizi sio mzuri kwakweli


Ila

Unaweza ukaenda na tranka kumbe hawaruhusiwi unaenda kuwa kichekesho kule kama wale first year wa UDOM walio ripoti na ma tranka walipigwa hadi na picha


Mpka leo sijapata jibu wanaenda nao wajuzi tafadhali
 
Unaweza kwenda nalo ila binafsi nakushauri kama ukichaguliwa kwenda huko nenda na kirasket tu, vingine utanunua huko huko.Tranka ni muhimu sana kwa usalama wa vitu vyako. Ila linaweza likawa mzigo mkubwa sana siku ya kwanza ukifika huko
Hapo ulipo bold unanitisha mkuu tafadhali fafanua
 
Hapo ulipo bold unanitisha mkuu tafadhali fafanua
Kama hupendi usumbufu tu siku ya kwanza kufika kambini basi nakushauri usiwe na mizigo mingi sana...maana itakulazimu kuibeba kwa umbali mkubwa kidogo kutoka getini mpaka sehemu ya kupumzikia...ni hilo tu. Hamna la kutisha hapo boss
 
Kama hupendi usumbufu tu siku ya kwanza kufika kambini basi nakushauri usiwe na mizigo mingi sana...maana itakulazimu kuibeba kwa umbali mkubwa kidogo kutoka getini mpaka sehemu ya kupumzikia...ni hilo tu. Hamna la kutisha hapo boss
Ahaa hilo halina shida hasa sisi wanaume hatuna vingi vya kubeba nakumbuka jkt nilibeba tranka lina trak basi na raba sabuni na dawa ya mswaki lilikua jepesi kama karatasi nikawa nalitumia kuvundikia maparachichi

Kwahyo hitimisho kuhusu tranka kwa hizi kambi za mafunzo mkuu we unaona ni vyema ? Maana nilijua kidogo zitakuwa na ustaarabu
 
Ahaa hilo halina shida hasa sisi wanaume hatuna vingi vya kubeba nakumbuka jkt nilibeba tranka lina trak basi na raba sabuni na dawa ya mswaki lilikua jepesi kama karatasi nikawa nalitumia kuvundikia maparachichi

Kwahyo hitimisho kuhusu tranka kwa hizi kambi za mafunzo mkuu we unaona ni vyema ? Maana nilijua kidogo zitakuwa na ustaarabu
Kwenye wengi, wezi hawakosekani.Kosa la wizi ni la kukufukuzisha mafunzo. Ingawa sheria ni kali ,ila hao watu wapo na watu wanaibiana.Ukikamatwa na ushahidi basi unafukuzwa.Tranka ni MUHIMU
 
Kwa mda gani kwenda huko jkt kujitolea mpaka watangazi nafasi au hata kama hawajatangaza??
Utakaa miaka miwili ya mkataba kambini ndani ya hyo miaka wanaweza kuja ukaomba ukapata mkataba ukiisha bado hawajaja unaomba kuongeza mkataba hapa wanakupa mmoja wa mwisho wasipokuja unarud zako home

Zikikutia home ata hivyo cheti utakuwa unacho utaomba tu

Na sio lazima uongeze mkataba ukiisha unaweza rudi home
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom