Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Mwanahabari Kazimbaya Makwega ambaye alikamatwa na Askari Polisi akiwa Chuo cha Mallya, Kwimba (Mwanza), Februari 22, 2024 kisha kusafirishwa hadi Dodoma kwa tuhuma za kuandika maneno ya uchechezo dhidi ya Chuo Kukuu cha Dodoma (UDOM) kupitia tovuti yake ya ‘Mwanakwetu’, ameachiwa kwa dhamana.
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mwanza, Edwin Soko amesema “Makwega ameachiwa kwa dhamana na suala lake linatarajiwa kufikishwa Mahakamani Jumanne ya wiki ijayo (Machi 5, 2024), kwa sasa hapatikani hewani kwa kuwa wakati wanamshikilia Askari walichukua simu zake mbili pamoja na laptop.”
Alipotafutwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno amesema “Nipo njiani muda huu, bado sijapata ripoti ya mwendelezo wa Shauri lake (Makwega) lakini ninavyojua suala lake kina dhaminika, nikifika ofisini nitapata ripoti kisha nitakujulisha.”
Pia soma - Mwandishi wa Habari, Kazimbaya Makwega ashikiliwa na Polisi, asafirishwa kutoka Mwanza hadi Dodoma
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mwanza, Edwin Soko amesema “Makwega ameachiwa kwa dhamana na suala lake linatarajiwa kufikishwa Mahakamani Jumanne ya wiki ijayo (Machi 5, 2024), kwa sasa hapatikani hewani kwa kuwa wakati wanamshikilia Askari walichukua simu zake mbili pamoja na laptop.”
Alipotafutwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno amesema “Nipo njiani muda huu, bado sijapata ripoti ya mwendelezo wa Shauri lake (Makwega) lakini ninavyojua suala lake kina dhaminika, nikifika ofisini nitapata ripoti kisha nitakujulisha.”
Pia soma - Mwandishi wa Habari, Kazimbaya Makwega ashikiliwa na Polisi, asafirishwa kutoka Mwanza hadi Dodoma