News Alert: Mwandishi wa Habari, Kazimbaya Makwega ashikiliwa na Polisi, asafirishwa kutoka Mwanza hadi Dodoma

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Salama Wana JF, Nimeona andiko hili huko Mtandaoni, kuna mwenye taarifa ya kinachoendelea?
Makwega.png

===

Mwandishi Kazimbaya Makwega asafirishwa toka Mwanza kwenda Dodoma

Ndugu waaandishi wenzangu muda huu nimefika kituo kikuu cha polisi kati na mawakili wa wawili wa OJADACT kufuatilia kukamatwa kwa Mwandishi wa habari kazimbaya makwega.

Kwa bahati nzuri tumemkuta hapa kituoni na nimepata nafasi ya kuongea naye ana kwa ana kama dakika 5 hivi.

Wakati naongea naye wakaja maafisa waliojitambulisha kuwa wanatoka ofisi ya RCO Dodoma na wamekuja kumchukua ili waondoke naye.

Nao pia walikubali kuongea na mimi pia na sio mawakili nami nikafanya hivyo tukaongea na wakaniambia wanaondoka naye kwenda dodoma saa 7 mchana.

Pia wakasema kuna tuhuma huko Dodoma za kujibu hivyo tuwe na amani kwani hizo ni tuhuma.

Hapo nikawauliza kuwa kama.wanatoka Dodoma mbona tumeongea na ofisi ya RPC dodoma na ikathibitisha kuwa hakuna askari wake waliokuja Mwanza.

Wao wakajibu kuwa ofisi ya RPC ni kubwa ila wao wanatoka ofisi ya RCO Dodoma.

Maelezo toka kwa makwega mwenyewe ni kuwa alikamatwa jana kwao Malya na akanyang'anywa laptop na simu zake tatu na pia alipofika hapa kituoni akaandikishwa maelezo.

Gari yenye namba za usajili SU 45605 landCruiser imeondoka na Makwega hapa kituo cha polisi kati Mwanza.

Maelezo ya mwisho toka kwa watu wanaomshikilia walisema wataondoka saa 7 mchana ila kwa sasa wanaenda wapi ? Hatujajua na ilikuwa ngumu kuhojji.

Afya ya Makwega
Ipo salama kabisa nilipoomba tumpe kwanza chai anywe wakasema watampa wao na hiyo ni haki yake kama binadamu hivyo watamhudumia.

Naomba wemzetu mlioko Dodoma jipangeni kwa ajili ya kumpokea .

Ushirikiano na Jeshi la polisi.
Tangia nilipofika kituoni nimepata ushirikiano mzuri na nilipojitambulisha wakamruhusu niongee naye kwa kina.

Ahsanteni sana wote

Edwin Soko
Mwenyekiti
OJADACT
MPC .


================

MAELEZO YA MWENYEKITI WA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mwanza, Edwin Soko ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari wa kupinga Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uhalifu (OJADACT) anasimulia:

Taarifa nilizipata ni kuwa akiwa Chuo cha Mallya Wilayani Kwimba (Mwanza), jana Februari 22, 2024, alifuatwa na maafisa waliojitambulisha kuwa ni Askari Polisi wanatoka Ofisi ya RPC Dodoma.

Wakaenda naye hadi nyumbani kwake lakini walionana pia na Mwneyekiti wa Serikali za Mtaa, wakaanza ukaguzi, kutokana na ukaguzi huo wakachukua laptop yake moja na simu mbii.

Wakamwambia kesi yake ipo Dodoma, wakamwambia anatuhumiwa kuandika habari za uchochezi kuhusu Chuo Kikuu cha Dodoma.

Wakamsafirisha hadi Mwanza. Asubuhi ya leo (Februari 23, 2024) nilifika katika Kituo cha Polisi Mwanza, nikaomba kuonana naye, wakaniruhusu kuonana naye.

Nikazungumza na Makwega akaniambia wamemshikilia kwa madai ya kuandika habari ya uchochezi kuhusu UDOM.

Tukiwa tunaendelea na mazungumzo wakaja maafisa wengine ambao walijitambulisha kuwa wao ndio waliomchukua kutoka nyumbani kwake.

Nilipowauliza kuwa mnatoka Ofisi ya RPC lakini nimezungumza na RPC wa Dodoma kasema yeye hana taarifa, wakasema “Ofisi ni kubwa sana, wao wanatoka Kitengo cha RCO”.

Hivyo, wakasema wataondoka naye saa saba mchana (leo Februari 23, 2024) kwenda Dodoma, baada ya hapo hatujui nini kilichoendelea.


RPC DODOMA AKIRI KUKAMATWA KWA KAZIMBAYA MAKWEGA
Alipoulizwa kuhusu taarifa hizo: Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno amesema:

Amekamatiwa Mwanza, kuna tuhuma dhidi yake zinazomkabili, anamiliki blog inayoitwa ‘Mwanakwetu’, inasemekana ametumia mtandao vibaya, watu wa kitengo cha Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) wamemfungulia mashtaka ya kutumia mtandao vibaya.

Kuna vitu ambavyo aliandika akituhumu hicho chuo, hivyo amekamatwa ili aandike maelezo na taratibu nyingine za kipelelezi zitaendelea na ikithibitika kuna kitu ambacho amekutwa nacho taratibu nyingine zitaendelea.

Anasafirishwa kutoka Mwanza kuja Dodoma kwa ajili ya kutoa maelezo zaidi na taratibu nyingine za Kipolisi.

UTPC WASEMA WANAFUATILIA MCHAKATO
Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya anasema:

Ni kweli amekamatwa tumepata taarifa hizo, amekamatiwa Mwanza na anasafirishwa kwenda Dodoma, kuhusu tuhuma hasa hatujajua, tunasubiri afikishwe Dodoma kisha taratiu nyingine zitaendelea, kwa sasa ni hayo tu.
 
Mambo yameanza
Bado wewe na uzushi wako.Mzushe muachwe tu.Nchi ina utawala wa sheria hii.Ukituhumiwa kufanya kosa la jinai unahojiwa kama wananchi wengine.Freedom of speech ina mipaka yake.Na maana yake sio matusi,kejeli na uzushi.
 
CCM ni ileile, kuteka watu, kutesa watu, kuficha watu na kuuwa watu ndio kitu pekee wanachokiweza.
Hadi sasa wameshindwa kusambaza maji safi na salama kwenye majiji na miji mikubwa nchini.
Wameshindwa kuhakikisha nchi ina umeme wa uhakika.
Wameshindwa ku provide huduma bora za afya.
Wameshindwa kutoa elimu bora, wanatoa bora elimu ndio maana hamna mtoto wa mkubwa anasoma shule za kata.
 
Bado wewe na uzushi wako.Mzushe muachwe tu.Nchi ina utawala wa sheria hii.Ukituhumiwa kufanya kosa la jinai unahojiwa kama wananchi wengine.Freedom of speech ina mipaka yake.Na maana yake sio matusi,kejeli na uzushi.
We vipi?
 
Salama Wana JF, Nimeona andiko hili huko Mtandaoni, kuna mwenye taarifa ya kinachoendelea?
View attachment 2913618
===

Mwandishi Kazimbaya Makwega asafirishwa toka Mwanza kwenda Dodoma

Ndugu waaandishi wenzangu muda huu nimefika kituo kikuu cha polisi kati na mawakili wa wawili wa OJADACT kufuatilia kukamatwa kwa Mwandishi wa habari kazimbaya makwega.

Kwa bahati nzuri tumemkuta hapa kituoni na nimepata nafasi ya kuongea naye ana kwa ana kama dakika 5 hivi.

Wakati naongea naye wakaja maafisa waliojitambulisha kuwa wanatoka ofisi ya RCO Dodoma na wamekuja kumchukua ili waondoke naye.

Nao pia walikubali kuongea na mimi pia na sio mawakili nami nikafanya hivyo tukaongea na wakaniambia wanaondoka naye kwenda dodoma saa 7 mchana.

Pia wakasema kuna tuhuma huko Dodoma za kujibu hivyo tuwe na amani kwani hizo ni tuhuma.

Hapo nikawauliza kuwa kama.wanatoka Dodoma mbona tumeongea na ofisi ya RPC dodoma na ikathibitisha kuwa hakuna askari wake waliokuja Mwanza.

Wao wakajibu kuwa ofisi ya RPC ni kubwa ila wao wanatoka ofisi ya RCO Dodoma.

Maelezo toka kwa makwega mwenyewe ni kuwa alikamatwa jana kwao Malya na akanyang'anywa laptop na simu zake tatu na pia alipofika hapa kituoni akaandikishwa maelezo.

Gari yenye namba za usajili SU 45605 landCruiser imeondoka na Makwega hapa kituo cha polisi kati Mwanza.

Maelezo ya mwisho toka kwa watu wanaomshikilia walisema wataondoka saa 7 mchana ila kwa sasa wanaenda wapi ? Hatujajua na ilikuwa ngumu kuhojji.

Afya ya Makwega
Ipo salama kabisa nilipoomba tumpe kwanza chai anywe wakasema watampa wao na hiyo ni haki yake kama binadamu hivyo watamhudumia.

Naomba wemzetu mlioko Dodoma jipangeni kwa ajili ya kumpokea .

Ushirikiano na Jeshi la polisi.
Tangia nilipofika kituoni nimepata ushirikiano mzuri na nilipojitambulisha wakamruhusu niongee naye kwa kina.

Ahsanteni sana wote

Edwin Soko
Mwenyekiti
OJADACT
MPC .


================

MAELEZO YA MWENYEKITI WA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mwanza, Edwin Soko ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari wa kupinga Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uhalifu (OJADACT) anasimulia:

Taarifa nilizipata ni kuwa akiwa Chuo cha Mallya Wilayani Kwimba (Mwanza), jana Februari 22, 2024, alifuatwa na maafisa waliojitambulisha kuwa ni Askari Polisi wanatoka Ofisi ya RPC Dodoma.

Wakaenda naye hadi nyumbani kwake lakini walionana pia na Mwneyekiti wa Serikali za Mtaa, wakaanza ukaguzi, kutokana na ukaguzi huo wakachukua laptop yake moja na simu mbii.

Wakamwambia kesi yake ipo Dodoma, wakamwambia anatuhumiwa kuandika habari za uchochezi kuhusu Chuo Kikuu cha Dodoma.

Wakamsafirisha hadi Mwanza. Asubuhi ya leo (Februari 23, 2024) nilifika katika Kituo cha Polisi Mwanza, nikaomba kuonana naye, wakaniruhusu kuonana naye.

Nikazungumza na Makwega akaniambia wamemshikilia kwa madai ya kuandika habari ya uchochezi kuhusu UDOM.

Tukiwa tunaendelea na mazungumzo wakaja maafisa wengine ambao walijitambulisha kuwa wao ndio waliomchukua kutoka nyumbani kwake.

Nilipowauliza kuwa mnatoka Ofisi ya RPC lakini nimezungumza na RPC wa Dodoma kasema yeye hana taarifa, wakasema “Ofisi ni kubwa sana, wao wanatoka Kitengo cha RCO”.

Hivyo, wakasema wataondoka naye saa saba mchana (leo Februari 23, 2024) kwenda Dodoma, baada ya hapo hatujui nini kilichoendelea.


RPC DODOMA AKIRI KUKAMATWA KWA KAZIMBAYA MAKWEGA
Alipoulizwa kuhusu taarifa hizo: Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno amesema:

Amekamatiwa Mwanza, kuna tuhuma dhidi yake zinazomkabili, anamiliki blog inayoitwa ‘Mwanakwetu’, inasemekana ametumia mtandao vibaya, watu wa kitengo cha Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) wamemfungulia mashtaka ya kutumia mtandao vibaya.

Kuna vitu ambavyo aliandika akituhumu hicho chuo, hivyo amekamatwa ili aandike maelezo na taratibu nyingine za kipelelezi zitaendelea na ikithibitika kuna kitu ambacho amekutwa nacho taratibu nyingine zitaendelea.

Anasafirishwa kutoka Mwanza kuja Dodoma kwa ajili ya kutoa maelezo zaidi na taratibu nyingine za Kipolisi.

UTPC WASEMA WANAFUATILIA MCHAKATO
Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya anasema:

Ni kweli amekamatwa tumepata taarifa hizo, amekamatiwa Mwanza na anasafirishwa kwenda Dodoma, kuhusu tuhuma hasa hatujajua, tunasubiri afikishwe Dodoma kisha taratiu nyingine zitaendelea, kwa sasa ni hayo tu.
Aisee
Chuo Kikuu Dodoma ni nyeti kiasi kwamba nguvu kubwa inatumika kwa ishu ya maandishi tu?

Alipanga kupindua uongozi wa chuo?
 
Back
Top Bottom