Tunduru: Wafanyabiashara 28 washikwa na kuachiwa kwa dhamana kwa kuuza bei ya juu sukari

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
Mtatiro.jpg

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma, Julius Mtatiro

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma, Julius Mtatiro amesema mara baada ya Serikali kutoa muongozo wa bei elekezi ya sukari uongozi wa Wilaya ukafanya vikao kwa ajili ya kutoa mwelekeo.

Amesema “Kwanza ilikuwa kupata orodha ya watu wanaofanya biashara ya sukari ngazi ya Wilaya ili kuwapa maelekezo.

“Baada ya hapo tukatoa maelekezo kwa Wananchi kuhusu muongozo wa bei kuwa ni Tsh. 2,900 hadi Tsh. 3,200 pamoja na kuwapa namba za kutoa taarifa lakini tumewapa maelekezo Wafanyabiashara wote kuwa wanatakiwa kuweka vibao vinavyoonesha bei ya sukari ili kama muuzaji atauza bei tofauti iwe rahisi mteja kubaini hilo.”

Ameongeza “Kama hawataweka vibao ndio itakuwa mwanzo wa kufanya udanganyifu.

“Baada ya kutoa namba za mawasiliano Wananchi wakatoa mrejesho, tulipokea ripoti 17 awali kuhusu wananchi kuuziwa bei tofauti na zilizoelekezwa kesho yake tukapata ripoti nyingine 11 na waliotuhumiwa wote walifikishwa Kituo cha Polisi na kutoa maelezo.

“Wakati wanachukuliwa kwa ajili ya kwenda kutoa maelezo biashara zao hazikufungwa, walitakiwa kuwaachia watu mbadala wa kuuza kisha wao wakawa wanachukuliwa, baada ya hapo wote 17 na wale 11 wamepatiwa dhamana.

“Hawa Wafanyabiashara wetu wa vijijini sio busara kuwapelekea Mahakamani mwanzoni, ndio maana wanachukuliwa maelezo yao, na kutakiwa kurejea Polisi baada ya siku kadhaa.”

Tangazo la Serikali lililotolewa lilisema mtu yeyote anayeuza Sukari kinyume na Bei Elekezi zilizoainishwa atakuwa ametenda Kosa na akitiwa hatiani atawajibika kwa adhabu iliyoainishwa katika masharti ya Sheria ya Tasnia ya Sukari.

Bei Elekezi za Rejareja kwa Kilo 1 Sukari ziko kama ifuatavyo: Dar, Morogoro, Pwani Tsh. 2,700 - 3,000, Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe Tsh. 2,700 -3000, Dodoma, Singida, Tabora Tsh. 2,800 - 3,000, Lindi Mtwara, Ruvuma Tsh. 2,900 - 3,200.

Mikoa ya Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Mara Tsh. 2,800 - 3,000, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Manyara Tsh. 2,700 - 3,000 na Kagera, Kigoma, Katavi, Rukwa Tsh. 2,800 - 3,200.
 
Dunia ya serikali kupanga bei imeshapita.

Serikali iweke mazingira mazuri ya biashara wazalishaji waongezeke, mbinu za uzalishaji zikiwa nzuri, sukari ikizidi kwenye soko, bei itapungua kwa forces za demand and supply. Naturally.

Lakini haiwezi kushuka zaidi ya cost of production.
 
View attachment 2888839
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma, Julius Mtatiro

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma, Julius Mtatiro amesema mara baada ya Serikali kutoa muongozo wa bei elekezi ya sukari uongozi wa Wilaya ukafanya vikao kwa ajili ya kutoa mwelekeo.

Amesema “Kwanza ilikuwa kupata orodha ya watu wanaofanya biashara ya sukari ngazi ya Wilaya ili kuwapa maelekezo.

“Baada ya hapo tukatoa maelekezo kwa Wananchi kuhusu muongozo wa bei kuwa ni Tsh. 2,900 hadi Tsh. 3,200 pamoja na kuwapa namba za kutoa taarifa lakini tumewapa maelekezo Wafanyabiashara wote kuwa wanatakiwa kuweka vibao vinavyoonesha bei ya sukari ili kama muuzaji atauza bei tofauti iwe rahisi mteja kubaini hilo.”

Ameongeza “Kama hawataweka vibao ndio itakuwa mwanzo wa kufanya udanganyifu.

“Baada ya kutoa namba za mawasiliano Wananchi wakatoa mrejesho, tulipokea ripoti 17 awali kuhusu wananchi kuuziwa bei tofauti na zilizoelekezwa kesho yake tukapata ripoti nyingine 11 na waliotuhumiwa wote walifikishwa Kituo cha Polisi na kutoa maelezo.

“Wakati wanachukuliwa kwa ajili ya kwenda kutoa maelezo biashara zao hazikufungwa, walitakiwa kuwaachia watu mbadala wa kuuza kisha wao wakawa wanachukuliwa, baada ya hapo wote 17 na wale 11 wamepatiwa dhamana.

“Hawa Wafanyabiashara wetu wa vijijini sio busara kuwapelekea Mahakamani mwanzoni, ndio maana wanachukuliwa maelezo yao, na kutakiwa kurejea Polisi baada ya siku kadhaa.”

Tangazo la Serikali lililotolewa lilisema mtu yeyote anayeuza Sukari kinyume na Bei Elekezi zilizoainishwa atakuwa ametenda Kosa na akitiwa hatiani atawajibika kwa adhabu iliyoainishwa katika masharti ya Sheria ya Tasnia ya Sukari.

Bei Elekezi za Rejareja kwa Kilo 1 Sukari ziko kama ifuatavyo: Dar, Morogoro, Pwani Tsh. 2,700 - 3,000, Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe Tsh. 2,700 -3000, Dodoma, Singida, Tabora Tsh. 2,800 - 3,000, Lindi Mtwara, Ruvuma Tsh. 2,900 - 3,200.

Mikoa ya Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Mara Tsh. 2,800 - 3,000, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Manyara Tsh. 2,700 - 3,000 na Kagera, Kigoma, Katavi, Rukwa Tsh. 2,800 - 3,200.
Kwanini ofisi ya mkuu wa Wilaya wasifungue duka la sukari wauze kwa bei ya chini?
 
Sukari wanazopangiwa wafanya bei yakuuzia ziko wapi? Mf, mikoa ya pembezoni wanapata sukari Toka nchi za jirani utawapangieje bei hata hujui wananunu shilingi ngapi?
 
View attachment 2888839
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma, Julius Mtatiro

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma, Julius Mtatiro amesema mara baada ya Serikali kutoa muongozo wa bei elekezi ya sukari uongozi wa Wilaya ukafanya vikao kwa ajili ya kutoa mwelekeo.

Amesema “Kwanza ilikuwa kupata orodha ya watu wanaofanya biashara ya sukari ngazi ya Wilaya ili kuwapa maelekezo.

“Baada ya hapo tukatoa maelekezo kwa Wananchi kuhusu muongozo wa bei kuwa ni Tsh. 2,900 hadi Tsh. 3,200 pamoja na kuwapa namba za kutoa taarifa lakini tumewapa maelekezo Wafanyabiashara wote kuwa wanatakiwa kuweka vibao vinavyoonesha bei ya sukari ili kama muuzaji atauza bei tofauti iwe rahisi mteja kubaini hilo.”

Ameongeza “Kama hawataweka vibao ndio itakuwa mwanzo wa kufanya udanganyifu.

“Baada ya kutoa namba za mawasiliano Wananchi wakatoa mrejesho, tulipokea ripoti 17 awali kuhusu wananchi kuuziwa bei tofauti na zilizoelekezwa kesho yake tukapata ripoti nyingine 11 na waliotuhumiwa wote walifikishwa Kituo cha Polisi na kutoa maelezo.

“Wakati wanachukuliwa kwa ajili ya kwenda kutoa maelezo biashara zao hazikufungwa, walitakiwa kuwaachia watu mbadala wa kuuza kisha wao wakawa wanachukuliwa, baada ya hapo wote 17 na wale 11 wamepatiwa dhamana.

“Hawa Wafanyabiashara wetu wa vijijini sio busara kuwapelekea Mahakamani mwanzoni, ndio maana wanachukuliwa maelezo yao, na kutakiwa kurejea Polisi baada ya siku kadhaa.”

Tangazo la Serikali lililotolewa lilisema mtu yeyote anayeuza Sukari kinyume na Bei Elekezi zilizoainishwa atakuwa ametenda Kosa na akitiwa hatiani atawajibika kwa adhabu iliyoainishwa katika masharti ya Sheria ya Tasnia ya Sukari.

Bei Elekezi za Rejareja kwa Kilo 1 Sukari ziko kama ifuatavyo: Dar, Morogoro, Pwani Tsh. 2,700 - 3,000, Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe Tsh. 2,700 -3000, Dodoma, Singida, Tabora Tsh. 2,800 - 3,000, Lindi Mtwara, Ruvuma Tsh. 2,900 - 3,200.

Mikoa ya Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Mara Tsh. 2,800 - 3,000, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Manyara Tsh. 2,700 - 3,000 na Kagera, Kigoma, Katavi, Rukwa Tsh. 2,800 - 3,200.
soko huria liko wapi
hizo bei elekezi hazipo. hazifanyi kazi
 
Hawa wafanyabiashara wamevunja sheria gani?,bei elekezi ya serikali SIO sheria hii, wao mbona maduka ya ushirika yaliwashinda?,kick ccm government to the touch, wale maadui ujinga, umasikini, maradhi na binamu yao rushwa bado wametamalaki nchini, uzuzu wa kioga ndio unaoleta police state
 
Yaani serikali yetu ni ya kijinga sana, sasa mnaacha kuwakamata mapapa wa sukari wanaouza kwe bei za juu za jumla matani na matani mnakuja kukamata Hawa wanaouza kilo 1 au mbili, muuza duka kanunua Bei ya jumla 3700 aje auze 2900 si ndo mnataka hivo? Kwanini msiwakamate mliowapa vibali vya sukari ambao wanauza kwa Bei wanaojiskia
 
Back
Top Bottom