Mwalimu Mkuu aliyepewa fedha za TAKUKURU Afariki Dunia, yadaiwa amekunywa kimiminika chenye sumu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Mnamo tarehe 14.09.2023 majira ya saa 1:30 asubuhi huko katika nyumba za Walimu wa Shule ya Sekondari Mtanila iliyopo Kijiji cha Igangwe Wilaya ya Chunya, Mkuu wa Shule hiyo aliyefahamika kwa jina la MAGWIRA NKUTA [41] alifariki dunia baada ya kunywa kimiminika kinachodhaniwa ni sumu.

Chanzo cha tukio hilo ni msongo wa mawazo kwani inadaiwa kuwa kabla ya ujio wa mbio za mwenge wa uhuru, marehemu alikabidhiwa fedha na ofisi ya TAKUKURU kwa ajili ya kufanya maandalizi ya kibao cha “KLABU YA TAKUKURU RAFIKI SHULENI” lakini pamoja na kutumiwa fedha hizo hakuweza kutengeneza kibao hicho hadi Mwenge wa Uhuru ulipofika shuleni hapo kwa ajili ya ufunguzi wa Klabu hiyo.

Aidha, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa wananchi walioibiwa mali mbalimbali kufika kituo cha Polisi Rujewa, Mbeya Mjini na Chunya kwa ajili ya utambuzi wa mali zao. Aidha, linatoa rai kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu ili wakamatwe na kuchukulia hatua za kisheria.
 
Mnamo tarehe 14.09.2023 majira ya saa 1:30 asubuhi huko katika nyumba za Walimu wa Shule ya Sekondari Mtanila iliyopo Kijiji cha Igangwe Wilaya ya Chunya, Mkuu wa Shule hiyo aliyefahamika kwa jina la MAGWIRA NKUTA [41] alifariki dunia baada ya kunywa kimiminika kinachodhaniwa ni sumu...
Kati ya vifo vya kizembe ni hiki.
 
Huyu mwalimu vipi huyu, watu tunadaiwa mamilioni na tunakomaa angejua. Tunadaiwa na serekali, upande mmoja TRA wametuma reminder miksa vitisho hadi wamekaa kimya achilia mbali madeni ya bank 2 tofauti ambapo inayodai kidogo ni milioni 67 na Riba zinapanda tu Kila siku lakini ndio kwanzaaaaaaaaa tunakaa bar Tena kaunta kwa raha zote
 
Huyu mwalimu vipi huyu, watu tunadaiwa mamilioni na tunakomaa angejua. Tunadaiwa na serekali, upande mmoja TRA wametuma reminder miksa vitisho hadi wamekaa kimya achilia mbali madeni ya bank 2 tofauti ambapo inayodai kidogo ni milioni 67 na Riba zinaoanda tu Kila siku lakini ndio kwanzaaaaaaaaa tu akaa bar Tena kaunta kwa raha zote
Mimi nadaiwa na Benk nne na hainistui
 
Kuna wakati maisha yanakupiga, usidharau mahangaiko ya wengine.
Huenda kiasi kilichopelekea yeye kujitoa uhai kwako wewe ni kidogo lakini kwake kwa wakati huo mpaka anachukua uamuzi wa kujitoa uhai sio jambo jepesi.
Mungu atupe mioyo ya ujasiri na imani tupitiapo magumu, na mwalimu apumzike kwa amani.
Note; Siungi mkono kujiua!
 
Mnamo tarehe 14.09.2023 majira ya saa 1:30 asubuhi huko katika nyumba za Walimu wa Shule ya Sekondari Mtanila iliyopo Kijiji cha Igangwe Wilaya ya Chunya, Mkuu wa Shule hiyo aliyefahamika kwa jina la MAGWIRA NKUTA [41] alifariki dunia baada ya kunywa kimiminika kinachodhaniwa ni sumu.

Chanzo cha tukio hilo ni msongo wa mawazo kwani inadaiwa kuwa kabla ya ujio wa mbio za mwenge wa uhuru, marehemu alikabidhiwa fedha na ofisi ya TAKUKURU kwa ajili ya kufanya maandalizi ya kibao cha “KLABU YA TAKUKURU RAFIKI SHULENI” lakini pamoja na kutumiwa fedha hizo hakuweza kutengeneza kibao hicho hadi Mwenge wa Uhuru ulipofika shuleni hapo kwa ajili ya ufunguzi wa Klabu hiyo.

Aidha, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa wananchi walioibiwa mali mbalimbali kufika kituo cha Polisi Rujewa, Mbeya Mjini na Chunya kwa ajili ya utambuzi wa mali zao. Aidha, linatoa rai kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu ili wakamatwe na kuchukulia hatua za kisheria.


Kuna watu wanaiba mamilioni ya serikali wapo na hawafanywi kitu, uoga ni mbaya sana.
 
Back
Top Bottom