Mwaka mmoja ndani ya Merigos Fleury Prison

Mwaka mmoja ndani ya Merigos Fleury Prison

Mkuu naandika uzi huu nikiwa nipo huru,,nimeshamaliza kifungo,,
Ukikusanya simulizi yangu utajiona ulipo.
Nimendika Nina mwezi mmoja ktkt miezi 18 niliyofungwa.
Hapo nimeanza simulizi nipo jela,,nikakupeleka jinsi nilivyokamatwa..

Na sasa nakurudisha nimeshafungwa nipo celo,,
Hapo utakuja kujuwa kwann sikuweza kupata nafasi ya kupiga simu kwa muda wote?
endelea endelea mwamba
 
EPISODE 6.
Nipo cellule ground floor,,hii ni cellule ambazo ni maalum kwa new arrival prisoners...
Hizi cellule zinakuwa na tv tu,,bila fridge.
Lakini inakuwa ni nzr na Safi Sana.

wakati nipo ndani natafakari,,
anafungua mlinzi wa gereza ananijulisha kwamba sasa ni muda wa kwenda promenade (matembezi nje)
Hii promenade ni hiyari kutoka na kutembea..(ni uwanjani ambapo watu hutembea na kufanya mazoezi )
Ila prominade ni hatari sn,,
Watu wale wasiopenda matatizo hukaa ndani mwa cellule zao bila kwenda promenade kuhofia vurugu.

Promenade inakuwa ni muda maalum uliowekwa kwa ajili ya wafungwa wote kupata nafasi ya kwenda promenade.

Promenade ni masaa 2 na ikifika nusu saa kabla ya masaa 2 kuisha huwa kuna tangazo mnatangaziwa kujiandaa kurudi kwenye cellule zetu.
"La promenade est terminee"
utasikia sauti za walinzi wakitujulisha kuisha kwa promenade kupitia speaker iliyopo pale uwanjani.

Hii promenade masaa 2 kila floor,
Watu wa floor Mfano 2nd,,au 1st ,3rd ,au 4th..
Kila baada ya masaa mawili floor moja wanaingia ndani,,wanatoka floor ingine.
Hawa ni wale ambao hawana kazi pale prison.


Ila kwa wale wanaofanya kazi mbali mbali hapa prison,,
wao wanakuwa na muda maalum wa saa nzima kukutana kwenye promenade.
Na muda wao ni Kati ya saa 7 mchana na saa 8 wanarudi cellule..

Hawa wanakuwa ni mchanganyiko wa wafungwa wote wa jengo lile(batman)
Bila kujali floor wanazotoka.

Wafungwa hupangiwa floor kulingana na aina za kazi wanazofanya..
Mfano 1st floor 99 percent wanafanyakazi na ndani ya cellule wapo double.2 prisoners.
ni wafanyakazi either la cuisine(jikoni) or atelier.(kiwanda kidogo cha kutengeneza vitu humu humu prison).

2 nd floor hawa nao ni wafanyakazi either la cuisine(jikoni) or kazi za kusafisha gereza.(hawa huishi double person Dan la cellule).

3 rd floor hawa huishi double persons kwa cellule).wengi hawafanyi kazi Ila wachache ambao wanafanya kazi la cuisine.(jikoni)

4 th floor hawa huishi peke yao .
Mara nyingi ni watu wasiopenda sn vurugu na kupenda kuishi peke yao gerezani ..
Ukiwa 4th floor maana yake utaishi peke yako cellule.
Kila mfungwa ana hiyari ya kuishi na amtakae gerezani.
Kama hamuendani kitabia na cellule partner,, unaruhusiwa kuandika barua na kubadilishiwa cellule na rafiki umtakae.
Kwa wastani kila cellule ni 1 person au 2 Tu kama ukipenda kuishi double.

Huko new arrival promenade tulikuwa kama prisoners 10 tu ,
Nilipata taabu Sana kwenye mawasiliano,,
maana sijawahi kuongea wala kukisikia kifaransa zaidi ya bonjour,,ca va?

Kila ninaekutana nae English hajuwi,,
ilikuwa shida sn kwangu,,

Baada ya week nikahamishwa 2nd floor.

Hapo ndipo nilipokutana na jamaa wengi sn kutoka Nigeria,, England,,na baadhi ya English countries wanazoongea kingereza.

Hapo ndipo nilipojuwa habari na mambo mengi ya gerezani..
Hapa ndipo nilipogunduwa kumbe promenade ni sehemu ya wafungwa kuonyesha ufahari wa nguo na viatu.
watu huvaa nguo mpya na za thamani kubwa.

Wafungwa wanapata nafasi ya kuonana na jamaa zao kutoka nje na kuwanunulia chochote wanachotaka huko nje..

Mfungwa anampelekea mkewe nguo bag zima,,
Zinakwenda kufuliwa home na kuletewa nguo mpya zingine kila week.
Hiyo siku ya kukutana na wapenzi wao kila mfungwa amependeza vizuri na kunukia vzr.
Wenyewe wanaita( Palwa).

Hapo promenade nilikutana na jamaa kibao kutoka Africa,,
nilishangaa sn kwa nn nusu ya gereza ni blacks?

Senegalese,, Malians, Cameroonians, Congolese,na wengi wanazoongea french.

Nilikuja kugunduwa vitu vingi sn baadae.,,
Sisi watu weusi na hawa waarabu(Moroccoans, Algerians, Egyptians,libyans, Tunisians tumekuwa ni tatizo Sana ulaya.

Nusu ya watu weusi na waarabu hapa gerezani wapo kwa uhalifu wa mitandao,,na drugs,,au kupigana nk.

Hapa promenade ndy watu huongea biashara za magendo,,
Mfano ukitaka simu ,
Kupigana hapa ni kawaida Sana,,na mkipigana walinzi watawaacha hapo,,Ila baada ya kuingia ndani mtazuiwa kupelekwa chumba cha adhabu for 2 weeks.

Lakini kabla ya kuadhibiwa mnapewa nafasi ya kujieleza chanzo cha ugomvi na atakae bainika ndy tatizo basi hupelekwa kwenye adhabu.

Hapa ,ukitaka mwanamke,,watu wanaongea na demu nje anakuja kukutembelea na kugegeda pia kwa malipo..

Connecting kibao za maisha utazipata pale prominade maana huna nafasi ya kumwona mwenzako popote zaidi ya prominade au mkutane tena shule,,
au msikitini,,au kanisani,,au library.

Hapa prominade ndy watu hupata nafasi ya kupiga simu kwa jamaa zao.
Na namba zote ni lazima ziwe approval by utawala wa gereza.

Promenade ndy kuna mawakili wa kesi mbali mbali za humu jela huzungumzwa.

Mfano kama kuna mfungwa snitch amewaambia walinzi habari za mfungwa mwenye simu.,,basi hapa ukigundulika utahukumiwa kwa kipigo na wenzio.

Kama mfungwa amekopa vitu vya watu na hajalipa hapa prominade ndy atapata kipigo hadi arudishe pesa za watu.

Hapa prominade watu hupata nafasi ya kuri fresh akili na kufanya mazoezi mbali mbali..

Hapa ndipo sigara na hashishi huuzwa .
Jela hakuna matumizi ya pesa lakini biashara hufanyika kupitia sigara.
Unaweza kununuwa chochote Mfano simu,,jiko kutoka kwa mfungwa mwenzio kupitia pakti za sigara kwa kiasi kile cha pesa.
Mfano simu ni euros 250,
Utahitajika utoe sigara pakti 25 kulipia simu.

Kama iPhone 6 ni euros 500 utalazimika kulipa packet 50 za sigara.

Ukinunuwa chochote kwa mfungwa mwenzio ujuwe malipo ni sigara.
Na mtu huziuza humo kwa mfumo wa bitcom..au kuna namba fulani kama system fulani ya kupata pesa nje.
Sasa wapo watu hutoa bitcoin fake,,ukigundulika ndy hapo utakapokula kichapo.

Hapo ndipo watu huuza sigara kwa ulanguzi.
Dukani sigara huuzwa 8 euros kwa packet na kuuzwa euros 20 hapo promenade.


Hapa kuna ma group ya watu mbali mbali ambayo wana connection tokea huko nje walipotoka.

Hupigana pamoja na hutembea pamoja,
Ukipambana na mmoja basi umepambana na kundi zima.

Na pia kama kuna mfungwa ni snitch na hataki kuja prominade
,,anaadalia mtu wa kuishi nae cellule moja bila muhusika kujuwa.

Lengo ni kufuatwa huko huko cellule kwako ili upigwe na huyo mbabe..
Na malipo ya huyo mbabe ni kupitia sigara.

adhabu ya kupigana jela ni kuwekwa chumba cha peke yako bila tv,au fridge..kwa week 2,

then unapokonywa kazi unayofanya na kurudishwa floor ambayo hutofanya kazi tena.


Ukiwa new arrival unapewa karatasi maalum ya kuandika number zako za simu za watu wako.(phone numbers)
Unaituma kupitia box maalum la kutumia barua.

Then baada ya mwezi mmoja ndy namba zako zinaidhinishwa na uongozi wa gereza tayari kwa kupiga simu.
Utaweka pesa kiasi unachotaka ktk acc yako ya phone call box.
Utatumia namba zako za jela kama code ya kupiga simu ili uweze kuunganishwa.
Utalazimika kurecharge pesa kila zinapikwisha kwenye salio lako la simu.
Kila mfungwa ana namba zake alizosajiliwa kupiga simu.

Hakuna namba ambayo haijasahiliwa na uongozi wa jela itaweza kuunganishwa.
Ni lazima iwe approved.
Na maongezi ya simu ni recorded na yanasikilizwa na utawala..

Hairuhusiwi kuwa na simu Ila prisoners karibu 90 percentage wanasimu gerezani..

Nilitumia mwezi mmoja kusubiri namba zng za simu ziwe approved na utawala ili nipige simu nyumbani.
Muda wote karibu mwezi mzima hakuna aliyekuwa nilipo...

Itaendelea..
View attachment 2075464
 
EPISODE 5.
Nimeshahukumiwa miezi 18 jela for money smuggling.
Nipo cellule nasubiri kupelekwa gerezani.

Sheria za France sio ngumu Sana kwa wafungwa.
--Ukihukumiwa unaruhusiwa kukata rufaa ndani ya miezi 3.
Na procecutor ana nafasi ya kukata rufaa ya hukumu ndani ya muda huo kama hajaridhishwa na hukumu yako.
-- Ukihukumiwa unapata punguzo la miezi 5 kutoka kwa judge.
Hilo ni lazima.
-- kila mwezi wanapunguza siku 7 ktk kifungo chako.
-- kila mwaka mmoja wanapunguza miezi 3 ktk hukumu yako.
Ikifika 1/2 ya sentence yako yote unajadiliwa na judge kama Una sifa za kuachiwa huru na kupunguziwa tena miezi 3 ktk kifungo chako..

Mfano nimehukumiwa miezi 18 jela.
Nimepata miezi 5 ya punguzo la judge.
Itabaki miezi 13 .
Still napata punguzo la siku 7 kila mwezi wa hukumu yangu...
utapata miezi 3 mingine kwa mwaka.
nimepunguziwa,,itabaki miezi 9 ndy napaswa kukaa gerezani.

Katka miezi 9 hapo ndy nitajadiliwa na kupewa tarehe maalum ya kutoka gerezani.
Na kama ni raia wa inchi za kigeni kuna utaratibu wa kuwaachia kwa njia ya explusion.inakuwa kabla ya Ile miezi 9 kufika,,labda ningekaa miezi 6 Tu,, nikarudishwa home.(deportation)
Na uzuri wa France ukimaliza kesi yako hawana Mambo ya Pingu .
Ukiwa free basi wanakuacha free kuenda zako .
Kama ni kwenye ndege wanakata ticket unawekwa kwenye ndege, passport anapewa rubani na documents zako unapewa mwenyewe,, wanahakikisha ndege inaruka zako na wao wanaishia zao,

Hayo yote nilikuja kuyajuwa baadae nilipokuwa gerezani..

saa 0800 usiku,,walikuja walinzi wa gerezani,,tukabebwa wafungwa kama. 20 hivi kuelekea gerezani ambapo sikulijuwa hata jina lake kwa kipindi hicho.

Gari lilitembea kama umbali wa masaa 2 kutoka cello za mahakamani,, gari lilifungwa kila mahali lakini niliweza kuona kupitia sehem Nyembamba sn ya uwazi wa gari lile liliotubeba.

Mwisho tulijikuta tukiingia ndani ya majengo marefu yaliyokuwa yamezungukwa na waya wa senyenge pamoja na wire za umeme na cameras kila mahali..

Baada ya kushushwa nikagunduwa sasa nipo Merigos Fleury.
Baada ya kuona bango kubwa lililopo mbele ya uso wa jengo lile

Merigos Fleury prison,,ipo eneo linaitwa Fleury ambalo lipo ndani ya Paris.
Fleury ni jela kubwa kuliko zote ndani ya France.
Fleury ina majengo matano ambayo yote ni ya ghorofa 4 kila moja.
D 1
D2
D3
D4
D5
Na kila jengo linauwezo wa kubeba wafungwa 5000 kwa wakati mmoja.
Kila batman (jengo) Lina flour 1--4.
Na kila flour imegaiwa kwa maeneo 3.
Gauche(left)
Drote (right)
Milleu (middle)
Wafungwa watakaa humo,,ikitokea kuna chochote basi utatangaziwa taarifa kupitia radio ambayo IPO kwenye kila celo.
Kila celo ina TV 32 inches,, fully paid.
Fridge.kitanda double decker.
Na jiko kama ukihitaji kujipikia.
Choo self.
Dirisha kubwa lenye hewa nzr..
Jela ina maduka mle ndani,,na vitu vinauzwa Mfano lotions,,nguo,,vyakula,,radio,, home theatre ,,sigara,,majuice,,kuku,,nk.
Vyote hivyo ukivitaka wanakata ktkt pesa zako na wanakupa details kila mwezi.
Hii haikuwa jela bali ni 5 star hotel.

Nilipofika nikafanyiwa utaratibu wa kuchukuliwa alama za vidole.
Picha za upande zote tatu ya Sura yangu..
Uso upande wa mbele.
Uso kulia.
Uso kushoto.

Nikafunguliwa account ya jela,,kwamba ni utaratibu ili hata Kama ndugu na jamaa wakitaka kunitumia pesa popote walipo pesa zinaingia kwenye account yangu.
Kila mfungwa ana account ya jela hata Kama anafanya kazi basi pesa zake zinaingia kwnye account na wanakuletea bank detail kila mwezi kwamba Una umount kiasi gn,
Na kama haufanyikazi basi wanakuwekea euros 20 ktkt acc yako.

Baada ya kufunguliwa account,
,wale watu wa account ambao ni sehemu ya walinzi wa pale gerezani,, wakanambiya kwamba tumeweka euros 100 ktk account yako.
Dah,,nilinyong'onyea sn,,

Yaani ktkt pesa zng zote mmeweka 100 Tu?
Jamaa wakasema pesa zile zote ni chafu..zimetaifishwa,,
Nikasema hata zile zilizokuwa kwenye walett 1700 euros pia wametaifisha?
Nilihuzunika sn.

Baada ya kumaliza kuandikshwa kila kitu,,
tukachukuliwa na vitu vyetu tukapelekwa sehem ingine kwa ukaguzi zaidi tayari kwa kupelekwa cello..

Tuliitwa mmoja mmoja kulingana na tulivyoandikishwa,
Nilipoitwa jina langu,,nikakuta na mabag yangu yote yapo pale,,simu yng na kila kitu.

Wakanambiya nivue nguo zote,,moja baada ya ingine,,mwisho nikabali kama nilivyozaliwa..

Wakaanza kukaguwa nguo moja moja.
Mwishowe wakanambiya Unaweza kuvaa nguo zako.
Nilikuwa na kiatu changu fulani cha ngozi,,
Nikajaribu kukivaa,,Yule mlinzi akanikataza,,
This type of shoes is forbidden in prison..
Jamaa akanambiya..hairuhusiwi viatu vya ngozi hapa jela.
Shati au fulana ya blue pia marufuku,,
Maana zinafanana na Sare za walinzi wa jela.
Pia sweater la kuziba kichwa pia marufuku jela.

Nikapewa Raba mpya kabisa,,ambayo Africa unakwenda nayo disco.
Nikapewa na jeans 2,, track suits 2 pamoja na boxers kadhaa..
Nikapewa blanket moja ,,shuka nyeupe 2 ,taulo,na sandles za kuogea..
Jamaa wakanambiya ukihitaji nguo zingine kuna utaratibu wa kuomba nguo utapewa.

Nikakusanya nguo nilizoona ambazo naweza kuingia nazo celo,
Sasa naanza maisha mapya ya jela Merigos Fleury.

Itaendelea.
Jela unakuta Fridge tv na kingamuz kabisa,,, asee hawa watu wametuacha sana
 
Shida humu kuna watu wanajifanya wajuaji sana badala watulie mwamba atupe madini na kujifunza kitu wao wanaanza kurusha matusi.
It's bizzare wabongo tupunguze stress za maisha.
 
Back
Top Bottom