Mwaka mmoja ndani ya Merigos Fleury Prison

Mkuu nipe connection nikafungwe uko France na Mimi nipigie izo euro 100 kwa mwezi ..mwaka tu narud bongo na mtsji wa kutosha
Hakuna kitu kama hicho... utapatiwa account na pesa utaipata kwa kufanya kazi(mshahara) na ukikaa bila kufanya kazi utalipwa vilevile ila ni kiwango kidogo sana!

Njia nyingine ni kuhamisha pesa yako toka kwenye account yako kwenda account ya jela, ili uweze kuitumia kwenye maduka hapo jela.....
 
Mkuu kuna kitu umekisema hapo kuwa unapewa simu unaongea na ndugu zako ila unachoongea wanakuwa wanasikiliza sasa mfano kama mtu anaongea kilugha cha kwao labda kihaya kigogo kisukuma wakikusikia nn kinatokea
Kwanza unatakiwa uandike namba zako ambazo utahitaji kuzitumia,

Halafu unaziwakilisha hizo namba kwa chief wa prison.
Wanazisajili.

Baada ya mwezi utapata majibu ya kuanza kutumia hizo namba.

Unapewa na tahadhari kwamba simu zote ni recorded na zinasikilizwa..

Na kama itatokea watashindwa kuelewa unachoongea basi wanaweza kusitisha mawasiliano yako.,
Au wakablock namba unazozungumza kwa lugha tata.

Mfano ,
week moja baada ya kukamatwa kuna barua moja niliiandika kwa Kiswahili kuituma nyumbani Tanzania.
Lakini ilijaa maneno ya kiswahili cha mitaani,

Ile barua haikufika hadi leo ,

Means waliishindwa kutafsiri baadhi ya maneno na kuamua kuitupa.
Barua zinazomwa kabla ya kuzituma,au zinazomwa kabla ya kuzipokea.
Simu pia zinasikilizwa.
 
Jela za wenzetu je upewa haki ya kuwa na simu?
Maana hizi zetu ni jehanamu sijui kwann awataki mfungwa amiliki simu apate mawasiliano na ndugu zake. Ukiweza ishi jela za bongo kuzimu ni supermarket huwezi shindwa ishi.
 
Jela za wenzetu je upewa haki ya kuwa na simu?
Maana hizi zetu ni jehanamu sijui kwann awataki mfungwa amiliki simu apate mawasiliano na ndugu zake. Ukiweza ishi jela za bongo kuzimu ni supermarket huwezi shindwa ishi.
Hapa kwetu jela ni kukomoana.
Na sio kurekebishwa tabia.
 
Back
Top Bottom