Ok,tukiacha faida binafsi, ndoa inafaida kubwa kijamii.
Ukiitazama ndoa kwa kuangalia faida binafsi ambazo zitakunufaisha wewe kama wewe basi huwezi kuona faida yake.
Kwa sababu mmomonyoko wa kimaadili uliopo kwenye jamii leo hii umemfanya mtu aweze kuzipata hata kama hana ndoa.
Mfano wa faida hizo ni kama, ngono na kupata watoto, na wakati mwingine kuhudumiwa kama anavyoweza kuhudumiwa mume.
Lakini katika upande wa kijamii, ili uweze kuzipata hizo faida binafsi hapo juu, ni lazima umpate mwanamke fulani, ambaye atakuwa ni binti wa mtu, dada wa mtu, shangazi wa mtu, mama wa mtu n.k
Hivi kuna mazazi anakubali umchukue binti yake kama tu chombo cha starehe?