Msajili wa Vyama vya Siasa ahoji CHADEMA kuwafukuza Mdee na wenzake 18. CHADEMA wajibu kuwa hawawezi kutoa maelezo kwa Msajili

comte

JF-Expert Member
Dec 11, 2011
8,222
5,946
Wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo kikiwa kwenye maandalizi ya Baraza Kuu, Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi amekitaka kitoe maelezo ya kina kwa nini kiliwafukuza uanachama wanachama wake 19 ambao ni wabunge wa viti maalumu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 14, 2021, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Benson Kigaila amesema chama hicho kimepokea barua kutoka kwa Msajili huyo Julai 6 na wakaijibu Julai 9 mwaka huu.

Katika maelezo yake, Kigaila amesema barua ya Jaji Mutungi imewataka kutoa maelezo hayo kwake baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa waliokuwa wanachama wao 19.

"Tumemjibu kuwa hatuwezi kutoa maelezo hayo kwa sababu barua aliyotuandika hajaambatanisha malalamiko ya hawa waliomlalamikia.Tunakiona hapa ni kutaka kuvuruga mchakato wa Baraza la Kuu la Chama linalotakiwa kuketi mwaka huu.

"Huwezi kufungua kesi ya aina moja kwenye mahakama mbili tofauti, hawa watu 19 baada ya kufukuzwa uanachama mwaka jana kisha wakakata rufaa Baraza Kuu, ambalo bado halijakaa.Sasa bado rufaa yao haijasikilizwa wamekimbilia kwa msajili," amesema Kigaila

Kigaila amesema hawawezi kutoa maelezo kwa Jaji Mutungi kwakuwa ni kinyume cha utaratibu wa chama hicho.

"Sasa msajili akisema hakubaliani na maelezo yetu na kwamba hawa watu 19 ni wanachama halali, si amevuruga mchakato wa Baraza Kuu?

Wabunge hao 19, wakiongozwa na Halima Mdee aliyekuwa mwenyekiti wa baraza la wanawake la Chadema ( Bawacha), walifukuzwa uanachama mwaka jana na kamati kuu ya Chadema baada ya kwenda kinyume na msimamo wa chama hicho kwa hatua yao ya kuapa kuwa wabunge wa viti maalumu bila ridhaa ya chama.

Chanzo: Mwananchi
 
Chadema siyo chama Cha kwanza kufukuza wanachama wake. Bernard K. Membe alipofukuzwa CCM hatukusikia msajili wa vyama vya siasa akiitaka CCM itoe maelezo kwa Nini imemfukuza membe. Sheria zifuatwe bila upendeleo. Kwa Nini chadema leo?

Hata Magufuli alimpofukuza uanachama Sophia Simba na wenzake plus kumvua Ubunge msajili hawajawai kuwaambia CCM watoe maelezo ya kwanini waliwafukuza ndo maana tunasema tunataka Katiba Mpya ambayo haitaruhudu Msajili wa Vyama vya Siasa kuteuliwa na Rais.
 
Huyo huwa halei vyama
Bali huwa anachonganisha uongozi wa vyama na mwanachama.
Rejea CUF
Mwanachama ana udhamini na Msajili au Na chama kilichosajiliwa?
Unavilea vipi vyama vinavyokuja kuonekana nyakati za uchaguzi.
IPO SIKU TUTAINGIA AUTOMATIC KWENYE VURUGU KWA KUKIUKA SHERIA/KANUNI

Hasira za watu zikiwadhuru watu ambao wanawadharau wananchi Huyo Mlezi atajitokeza?

Kama mwananchi kamati kuu mkikaa muwe pia na agenda yakuwafungulia mashitaka hao Covid 19.
Watu walivyo na hasira nao nadhani watachangia kuwalipa mawakili.
Tafadhali muwe na azimio lakuwashitaki tujuwe moja
 
Wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo kikiwa kwenye maandalizi ya Baraza Kuu, Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi amekitaka kitoe maelezo ya kina kwa nini kiliwafukuza uanachama wanachama wake 19 ambao ni wabunge wa viti maalumu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 14, 2021, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Benson Kigaila amesema chama hicho kimepokea barua kutoka kwa Msajili huyo Julai 6 na wakaijibu Julai 9 mwaka huu.

Katika maelezo yake, Kigaila amesema barua ya Jaji Mutungi imewataka kutoa maelezo hayo kwake baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa waliokuwa wanachama wao 19.

"Tumemjibu kuwa hatuwezi kutoa maelezo hayo kwa sababu barua aliyotuandika hajaambatanisha malalamiko ya hawa waliomlalamikia.Tunakiona hapa ni kutaka kuvuruga mchakato wa Baraza la Kuu la Chama linalotakiwa kuketi mwaka huu.

"Huwezi kufungua kesi ya aina moja kwenye mahakama mbili tofauti, hawa watu 19 baada ya kufukuzwa uanachama mwaka jana kisha wakakata rufaa Baraza Kuu, ambalo bado halijakaa.Sasa bado rufaa yao haijasikilizwa wamekimbilia kwa msajili," amesema Kigaila

Kigaila amesema hawawezi kutoa maelezo kwa Jaji Mutungi kwakuwa ni kinyume cha utaratibu wa chama hicho.

"Sasa msajili akisema hakubaliani na maelezo yetu na kwamba hawa watu 19 ni wanachama halali, si amevuruga mchakato wa Baraza Kuu?

Wabunge hao 19, wakiongozwa na Halima Mdee aliyekuwa mwenyekiti wa baraza la wanawake la Chadema ( Bawacha), walifukuzwa uanachama mwaka jana na kamati kuu ya Chadema baada ya kwenda kinyume na msimamo wa chama hicho kwa hatua yao ya kuapa kuwa wabunge wa viti maalumu bila ridhaa ya chama.

MWANANCHI
 
ni ubabaishaji wa viongozi wa chadema kama kawaida yao hawanaga kitu wanachokianzisha wakakimaliza ni uhuni mtupu
 
Back
Top Bottom