Msaada Bei ya Tank la Maji la Kiboko (2000L au zaidi) kwa aliyewahi kununua tafadhali

Msaada Bei ya Tank la Maji la Kiboko (2000L au zaidi) kwa aliyewahi kununua tafadhali

Jumanne Mwita

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2014
Posts
557
Reaction score
1,544
Habari wana JF,

Naomba msaada kwa yeyote aliye wahi kununua au anayefahamu bei za tanks za Kiboko (Polytank) za kuhifadhia maji – hasa zile za ujazo wa 2000 L liters au zaidi.

Nimepitia kurasa zao za Instagram na Facebook (@kibokoplasticstz) lakini hawajaweka bei, na hata namba zao za simu kupokea ni changamoto.

Ningependa nijue bei kabla sijaenda kununua ili nijipange mapema – kama nitakuwa na pungufu niweze kuongeza fedha mapema badala ya kurudi rudi.

Kama kuna wakala, muuzaji wa jumla, au hata mtu aliyewahi kuagiza akiwa mikoani na anajua gharama ya usafiri au bei halisi aliyolipa, tafadhali naomba anisaidie.

Pia kama unajuana na wakala wao au sehemu ya karibu nisaidie nifahamu bei nashida nalo sana, nitashukuru sana.
 
Mnunuzi WA rejareja nae anataka Bei ya kiwandani, haya ndo tumewafukuzisha nayo wachina k'koo
Hapana ndugu! Unajua kuna bei mbili, kiwandani na wauzaji wa rejareja, maana naambiwa hizi zinauzwa bei kubwa sana huku mkoani milioni nasehemu au kasoro ndio maana nikataka nijue pia!
 
Hapana nimeuliza tu si-kwa ubaya unaweza kuta hiyo ni bei ya kiwandani siyo dukani, nikaondoka na point ya bei hiyo kumbe si sawa kwa rejareja. Ndio maana nikauliza hivyo. Samahani
Laki 4 unapata
Ukilia sana 380 unapata
 
Kiboko lita 5000 linauzwa laki nane na ushee.
 
Habari wana JF,

Naomba msaada kwa yeyote aliye wahi kununua au anayefahamu bei za tanks za Kiboko (Polytank) za kuhifadhia maji – hasa zile za ujazo wa 2000 L liters au zaidi.

Nimepitia kurasa zao za Instagram na Facebook (@kibokoplasticstz) lakini hawajaweka bei, na hata namba zao za simu kupokea ni changamoto.

Ningependa nijue bei kabla sijaenda kununua ili nijipange mapema – kama nitakuwa na pungufu niweze kuongeza fedha mapema badala ya kurudi rudi.

Kama kuna wakala, muuzaji wa jumla, au hata mtu aliyewahi kuagiza akiwa mikoani na anajua gharama ya usafiri au bei halisi aliyolipa, tafadhali naomba anisaidie.

Pia kama unajuana na wakala wao au sehemu ya karibu nisaidie nifahamu bei nashida nalo sana, nitashukuru sana.
Andaa laki 3 ila ni chini ya laki 3. Inacheza around 210,000 hadi 260,000 hapo mara ya mwisho nilipoulizia.
 
Mmmmhmn mimi nilinunua la lita 5000 laki saba na 80 hapo hadi usafiri kuniletea home. Nakumbuka niliulizia la lita 2000 nikaambiwa bei haikufika laki 3.
Hiyo 300k labda Lita 1000
 
Mnunuzi WA rejareja nae anataka Bei ya kiwandani, haya ndo tumewafukuzisha nayo wachina k'koo
Wabongo always hudhani kununua kitu dukani kwa mfanyabiashara wa rejareja wanapigwa hawajui huwa kuna bei elekezi viwanda huwa vinatoa kumlinda mteja na muuzaji.

Hii ya kusema nitaenda kununua kiwandani nina jamaa yangu alikuwa na pagala lake huko Msumi bati 135 akawapita wauza mabati pale Tazara akaingia Alaf kiwandani akatia order bati moja 39,500/= akidhani kaokota kumbe mtaani kwa authorized dealer bati moja ni 37,000/= nilimwambia hakuamini akarudi kiwandani kuhoji wakamwambia sisi tunauza bei ya jumla kuanzia bati 1,000 wewe hazikukidhi pia mitaani tunawauzia bei ya chini ili kukimbizana na soko mteja akija kiwandani na sisi tuna bei zetu jamaa alichoka.
 
Back
Top Bottom