Naishauri Serikali kununua na kutunza chakula cha kutosha kwa ajili ya kutumika wakati wa upungufu wa chakula

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,310
9,737
Ndugu zangu Watanzania,

Nimeona nitumie jukwaa hili kwa upendo,Heshima na unyenyekevu mkubwa Sana kuishauri serikali yangu kuhakikisha kuwa katika mpango wake wa kila mwaka wa kununua chakula na kukitunza, ihakikishe kuwa mwaka huu inanunua Chakula cha kutosha na kukitunza kwa umakini mkubwa Sana hususani kwa watendaji watakao kuwa wamepewa dhamani hiyo.

Ifahamimike kuwa chakula hiki hutumika kusaidia maeneo yanayo kuwa na njaa Kali na Upungufu mkubwa wa chakula kwa kukiuza kwa Bei ambayo mwananchi anaweza kumudu Bei,chakula hiki huwa msaada mkubwa Sana kwa wananchi ukilinganisha na kile kinachokuwa kinauzwa sokoni na watu binafsi.

Pia serikali yetu kupitia viongozi wetu wakiwepo wale wa kisiasa wahakikishe kuwa wanatoa Elimu ya kutosha na kuwakumbusha wananchi kutunza chakula majumbani kulingana na ukubwa wa Wana Kaya au familia,kila mmoja wetu kwa kadri ya uwezo wake ahakikishe kuwa anatunza chakula.

Wananchi wakumbushwe ili wasiuze vyakula vyote na kubaki kuhenyeke na Bei kubwa ya vyakula miezi ya huko mbele, Ni wajibu na muhimu Sana kwa serikali yetu kuhakikisha kuwa inaweka msisitizo wa kutosha katika Jambo Hilo.

Ikumbukwe ya kuwa hakuna Jambo la hatari,baya na gumu katika kuongoza serikali kwa utulivu na Amani ikiwa njaa ya chakula imetamalaki katika mamilioni ya kaya au familia nchini.Ni ngumu Sana kumuongoza au kusikilizwa na mtu mwenye njaa tumboni mwake,huwezi ukasikilizwa Wala kueleweka mbele ya watu wenye njaa.

Ni Rahisi Sana mtu mwenye njaa kushawishika kufanya vurugu au uharifu au uasi dhidi ya nchi yake,Ni Rahisi kwa mtu mwenye njaa ya chakula kuingia katika mkumbo na mtego wa kuiboa nchi yake kwa mikono yake mwenyewe. Ni Rahisi kupandikizwa chuki au vinyongo kwa watu wenye njaa ya chakula ,Ni Rahisi kwa mtu mwenye njaa kujitoa ufahamu na kufanya tukio la Aina yoyote Ile kupata kitu Cha kuponya njaa yake.

Ndio maana kwa kulipenda Taifa langu,nchi yangu na serikali yangu nimeamua kutoa ushauri huu mapema wakati msimu wa mavuno ukiwa umewadia, Naiomba Sana serikali yangu kutunza chakula Cha kutosha.

Rais wangu Samia Suluhu Hassani nakushauri kwa unyenyekevu, upendo, hekima, busara na uzalendo mkubwa Sana kuhakikisha serikali yako inatunza chakula Cha kutosha. Tunza chakula Rais wangu. Tunza na hifadhi chakula Cha kutosha mama yangu ,weka na fuatilia fedha za kununua chakula kuhakikisha zinatimiza malengo ya serikali. Tumia hata vyombo vyako na wasaidizi wako waaminifu kuhakikisha chakula kinakuwepo Cha kutosha.

Rais wangu Tunza chakula kwa kuwa wapo wenye kipato Cha chini wasioweza kujitunzia chakula na njaa ikiingia wote watakutazama na kukulilia wewe na serikali yako ,kwa kuwa wewe ndiye Rais wao,mama Yao na kiongozi wao na mwenye serikali yao. Rais wangu watu wenye njaa hawatawaliki Wala kusikiliza ,Ni watu wenye maneno na malalamiko,watakulilia na kukulalamikia Sana. Wataona ni kama umewabeba mgongoni na kuwaacha jangwani pasipo na maji Wala chakula.

Rais wangu mh mama Samia suluhu Hassani naomba na kukuomba Sana upokee ushauri wangu na kuuzingatia Sana ,maana Naifahamu vyema Sana njaa na mawazo ya mwenye njaa,Napenda Uendeleee kuongoza Taifa letu kwa Hali ya utulivu na Amani kubwa Sana pasipo malalamiko Wala maneno kutoka kwa wananchi wako, ndio maana napenda kutoa ushauri wangu katika hili. Nakuomba Sana mh Rais utunze chakula Cha kutosha kwa kuwa chakula ndio usalama wa Taifa,ndio utulivu wa serikali,ndio amani ya nchi,ndio mshikamano wetu na ndio Matumaini ya wengi.

Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
 
Waambie wafungue njia zaidi kwa mavuno hafifu ya mwaka huu wakulima wakauze vizuri kisha wao wakatuletee vitu vya ajabu toka nje.
 
Umeanza lini kupingana na sera ya serikali yako ya kutojishughulisha kununua hicho chakula?

Unataka na wale wafanyabiashara wa Bashe nao wanunue nini kwa wakulima wetu, kwa ajili ya kupeleka kwenye nchi zao?
 
Umeanza lini kupingana na sera ya serikali yako ya kutojishughulisha kununua hicho chakula?

Unataka na wale wafanyabiashara wa Bashe nao wanunue nini kwa wakulima wetu, kwa ajili ya kupeleka kwenye nchi zao?
Serikali yetu ya CCM Ina utaratibu wa kununua na kutunza chakula kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wanapokuwa wamekumbwa na njaa katika maeneo yao, kwa hiyo nilichokifanya hapa Ni kuishauri inunue chakula cha kutosha mwaka huu na kukitunza vizuri
 
Serikali yetu ya CCM Ina utaratibu wa kununua na kutunza chakula kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wanapokuwa wamekumbwa na njaa katika maeneo yao, kwa hiyo nilichokifanya hapa Ni kuishauri inunue chakula cha kutosha mwaka huu na kukitunza vizuri
Mimi naona ungewekeza nguvu kubwa kwenye zile mada zako za kumsifia Rais Samia kukata kiu za watanzania wa aina yako. Huku utapotea.
 
Tanzania haina maghala ya kutosha. Maghala yaliyopo nchi nzima yana uwezo wa kuhufadhi tani laki 2 tu ambazo zinatosha kulisha watanzania kwa mwezi mmoja tu.

Nchi za wenzentu kuna maghala mengi na makubwa kiasi kwamba yanahifadhi chakula cha kutosheleza mahitaji ya nchi husika kwa miaka 10 - 15..

Ukiona nchi zilizoendelea zinatoa msaada maana yake ni kwamba zinafungua maghala ya mwaka 2000 kwasabb mazao hayo yamekaa muda mrefu.
 
Tanzania haina maghala ya kutosha. Maghala yaliyopo nchi nzima yana uwezo wa kuhufadhi tani laki 2 tu ambazo zinatosha kulisha watanzania kwa mwezi mmoja tu...
Ikitaka kuhifadhi chakula Cha kutosha Hilo halina shida maana inaweza hata kukodi ya watu binafsi ambayo huwa yanakuwepo na yanakodishwa kwa ajili ya kuhifadhiwa vitu au bidhaa
 
Ikitaka kuhifadhi chakula Cha kutosha Hilo halina shida maana inaweza hata kukodi ya watu binafsi ambayo huwa yanakuwepo na yanakodishwa kwa ajili ya kuhifadhiwa vitu au bidhaa
Mkuu maghala ya kuhifadhi chakula kwa miaka zaidi ya 10 yanapaswa kujengwa kwa muundo usiyo ruhusu hewa na wadudu kuingiza (airtight).

Kwahiyo haya mabanda ya watu binafsi yanaweza kuhifadhi kwa msimu mmoja tu
 
Unasubri serikali ikutunzie chakula kwan ww huwezi ukalima hata eka mbili za mahindi. Tz ni kubwa Sana tafuta eneo ulime, acha kutegemea ruzuku hata kwenye chakula Cha kula na familia. Achana na Mambo ya hati punguzo hayo🤣
 
Unasubri serikali ikutunzie chakula kwan ww huwezi ukalima hata eka mbili za mahindi. Tz ni kubwa Sana tafuta eneo ulime, acha kutegemea ruzuku hata kwenye chakula Cha kula na familia. Achana na Mambo ya hati punguzo hayo🤣
Mimi naweza kutunza lakini siyo wote wenye uwezo huo
 
Naunga mkono HOJA 100%.

In other words, unamshauri Sa100 amuondoe BASHE kwenye uwaziri maana ana msimamo tofauti na hataki kusikia habari hizo za kutunza chakula.
 
Unasubri serikali ikutunzie chakula kwan ww huwezi ukalima hata eka mbili za mahindi. Tz ni kubwa Sana tafuta eneo ulime, acha kutegemea ruzuku hata kwenye chakula Cha kula na familia. Achana na Mambo ya hati punguzo hayo🤣
Unajua maana ya serikali?? Majukumu yake?? Uneandika kitoto sana mkuu nahuhakika hujasoma
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nimeona nitumie jukwaa hili kwa upendo,Heshima na unyenyekevu mkubwa Sana kuishauri serikali yangu kuhakikisha kuwa katika mpango wake wa kila mwaka wa kununua chakula na kukitunza, ihakikishe kuwa mwaka huu inanunua Chakula cha kutosha na kukitunza kwa umakini mkubwa Sana hususani kwa watendaji watakao kuwa wamepewa dhamani hiyo.

Ifahamimike kuwa chakula hiki hutumika kusaidia maeneo yanayo kuwa na njaa Kali na Upungufu mkubwa wa chakula kwa kukiuza kwa Bei ambayo mwananchi anaweza kumudu Bei,chakula hiki huwa msaada mkubwa Sana kwa wananchi ukilinganisha na kile kinachokuwa kinauzwa sokoni na watu binafsi.

Pia serikali yetu kupitia viongozi wetu wakiwepo wale wa kisiasa wahakikishe kuwa wanatoa Elimu ya kutosha na kuwakumbusha wananchi kutunza chakula majumbani kulingana na ukubwa wa Wana Kaya au familia,kila mmoja wetu kwa kadri ya uwezo wake ahakikishe kuwa anatunza chakula.

Wananchi wakumbushwe ili wasiuze vyakula vyote na kubaki kuhenyeke na Bei kubwa ya vyakula miezi ya huko mbele, Ni wajibu na muhimu Sana kwa serikali yetu kuhakikisha kuwa inaweka msisitizo wa kutosha katika Jambo Hilo.

Ikumbukwe ya kuwa hakuna Jambo la hatari,baya na gumu katika kuongoza serikali kwa utulivu na Amani ikiwa njaa ya chakula imetamalaki katika mamilioni ya kaya au familia nchini.Ni ngumu Sana kumuongoza au kusikilizwa na mtu mwenye njaa tumboni mwake,huwezi ukasikilizwa Wala kueleweka mbele ya watu wenye njaa.

Ni Rahisi Sana mtu mwenye njaa kushawishika kufanya vurugu au uharifu au uasi dhidi ya nchi yake,Ni Rahisi kwa mtu mwenye njaa ya chakula kuingia katika mkumbo na mtego wa kuiboa nchi yake kwa mikono yake mwenyewe. Ni Rahisi kupandikizwa chuki au vinyongo kwa watu wenye njaa ya chakula ,Ni Rahisi kwa mtu mwenye njaa kujitoa ufahamu na kufanya tukio la Aina yoyote Ile kupata kitu Cha kuponya njaa yake.

Ndio maana kwa kulipenda Taifa langu,nchi yangu na serikali yangu nimeamua kutoa ushauri huu mapema wakati msimu wa mavuno ukiwa umewadia, Naiomba Sana serikali yangu kutunza chakula Cha kutosha.

Rais wangu Samia Suluhu Hassani nakushauri kwa unyenyekevu, upendo, hekima, busara na uzalendo mkubwa Sana kuhakikisha serikali yako inatunza chakula Cha kutosha. Tunza chakula Rais wangu. Tunza na hifadhi chakula Cha kutosha mama yangu ,weka na fuatilia fedha za kununua chakula kuhakikisha zinatimiza malengo ya serikali. Tumia hata vyombo vyako na wasaidizi wako waaminifu kuhakikisha chakula kinakuwepo Cha kutosha.

Rais wangu Tunza chakula kwa kuwa wapo wenye kipato Cha chini wasioweza kujitunzia chakula na njaa ikiingia wote watakutazama na kukulilia wewe na serikali yako ,kwa kuwa wewe ndiye Rais wao,mama Yao na kiongozi wao na mwenye serikali yao. Rais wangu watu wenye njaa hawatawaliki Wala kusikiliza ,Ni watu wenye maneno na malalamiko,watakulilia na kukulalamikia Sana. Wataona ni kama umewabeba mgongoni na kuwaacha jangwani pasipo na maji Wala chakula.

Rais wangu mh mama Samia suluhu Hassani naomba na kukuomba Sana upokee ushauri wangu na kuuzingatia Sana ,maana Naifahamu vyema Sana njaa na mawazo ya mwenye njaa,Napenda Uendeleee kuongoza Taifa letu kwa Hali ya utulivu na Amani kubwa Sana pasipo malalamiko Wala maneno kutoka kwa wananchi wako, ndio maana napenda kutoa ushauri wangu katika hili. Nakuomba Sana mh Rais utunze chakula Cha kutosha kwa kuwa chakula ndio usalama wa Taifa,ndio utulivu wa serikali,ndio amani ya nchi,ndio mshikamano wetu na ndio Matumaini ya wengi.

Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
Nyie si ndiyo mlikuwa mnamshangilia Bashe aliporuhusu Chakula kuuzwa ovyo nje ya nchi!
 
Back
Top Bottom