kama hizi habari ni za kweli,basi kweli JK anahitaji pongezi za hali ya juu! Kuuzwa kwa hizi kulikuwa kwa kifupi ni kichekesho, hasa ukizingatia bei ya hizo nyumba walivyouziana. Nyumba iko Oysterbay inauzwa milioni 18 au 20 mpaka 30,wakati mashirika kama TTCL waliuza nyumba hukohuko O/bay shs milioni 400!
Ukiangalia kwa upande mwingine,wale wazee waliokuwa wa kwanza kukaa kwenye hizo nyumba,baada ya uhuru,wao pia walifikiriwa?
Maana mtu kama Balozi Sharif,aliyekuwa waziri mdogo wa mambo ya Nje,amekaa nje ya nchi hii miaka yote,na inasemekana ana passport ya uingereza pia,anarudi hapa na kuuziwa nyumba kwa bei ya kutupa,matokeo yake kaitengeneza na kuupangisha ubalozi wa UAE pale Kaunda Drive,kwanza walivyouza si walisema zile nyumba wanauziwa ili wakae wenyewe na hawaruhusiwi kupangisha...sasa mtu ananunua nyumba milioni 20,anapangisha kwa dola 5,000 kwa mwezi,hapo haki iko wapi?Miezi 4 pesa yake imerudi!
Hao wazee waliogombea uhuru mpaka nchi hii ikawa huru si ndio angalau wangestahili kupewa hizo nyumba kwa kuuziwa na kuwekewa utaratibu mzuri ambao ungewafanya waweze kuzilipia hizo nyumba...wengi wao wako hoi tu maskini,na hio sio lazima wapewe za O/bay. Bila ya wao hizo nyumba za kuuzwa zingetoka wapi?
Sasa logic iko wapi,unamtoa waziri O/bay unampeleka Kijitonyama,kwa kuuza nyumba ambayo angekaa,na kutumia pesa zaidi kumjengea nyumba kwenye sehemu ambayo kihistoria haikutengwa kukaa viongozi?
Mawaziri wengi wamegoma kuhamia nyumba hizo mpya kwa sababu wanasema hakuna privacy,maana wote wamewekwa kwenye kijiji!Hivi Mwalimu alivyosema 'i wont let my country go to the dogs..' reading between the lines u get a different perspective!
Pongezi sana JK na hao waliotoa hio stori kwenye gazeti,maana sisi Watanzania have been taken for a ride for too long.Na kwa sababu kawaida yetu,tutanung'unika,then yatapita.Tuna sifa hizo,hata sasa hivi issue ya umeme,hio Kiwira Coal Mine has been there miaka nenda rudi,leo ndio wanasema wanauwezo huo na Serikali finally imekubali,lakini hakuna mtu anayehoji,jamani mpaka IPTL inaingia nchi hii, (hakuna lolote wanalofanya),kumbe kulikuwa hakuna haja ya wao kuja kama hawa Kiwira wanasema wana uwezo wa kuzalisha megawatt 200! Na ni kwamba wana uwezo wa kuzalisha zaidi ila serikali imewapa kibali cha kuzalisha umeme huo tu!
Hili la nyumba watu walinung'unika na likapita.Nchi nyingine hata hizo nyumba zingepigwa mawe! Leo Mtanzania wa kawaida kupata mkopo wa kununua nyumba ni mbinde,na yeye analipa kodi,NSSF na vurugu nyingine nyingi tu,lakini huko juu,watu wanakopeshana majumba,tena they have the luxury of choosing where they want to live.Sasa most of those are no longer in the government,they are now ordinary citizens with mansions in Oysterbay,not in their wildest dreams did most of them ever think they would own property in such a prime location...
Maana ule ulikuwa ni mradi wa Tajirika na Serikali ya Awamu ya Tatu! Ila sasa huo utaratibu wa kuzinunua upya hizo nyumba nao usiwe tena mradi wa Tajirika
Mh........