Muvi gani seriously ulijikuta unatoa machozi (wakati unaiangalia au baada ya kuiangalia) kutokana na uhalisia wake kukugusa sana moyoni...achana na ile umeingalia ikakugusa na kuikubali tu kwa kuwa ni nzuri...NO..ILIYOKUTOA CHOZI!!
Sina uhakika kama hii topic ilishawahi jadiliwa humu maana nimejaribu ku search ila sijapata ninachokitaka..
Kwa upande wangu mimi ni hizi..
1. Marley and me
...hii nilivyoangalia mara ya kwanza baada tu ya kuisha nikaingia zangu chooni kujifungia ili nifute machozi maana tulikuwa tunaangalia watu wengi..kila mtu alinyanyuka kivyake ofcoz so sijui wengine kama nao walilia au la..
2. Pursuit Of Happiness
...nilijikuta tu machozi yanandondoka mwenyewe wakati muvi inaendelea..
3. Hatchiko the Dog Story
...inatia huruma sana hii..
4. Armeggedon
...ni SCI-FI movie ila pale mwisho chozi lilitoka kimtindo..
5. JOHN Q
6. Rango (Animation)
...hii machozi kwa kucheka...very touching ila inachekesha balaa..
7. Black Hawk Down
8. Blood Diamond
...hizi ni baadhi ya nnazozikumbuka harakaharaka...ningependa kuonza na nyingine zaidi ya hizi kwa msaada wenu..