Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

kwi kwi kwi,

Kuanzia leo Mkapa atabadili ratiba baada ya kilichotokea! Nadhani the best way ni kufanya shtukizo hadi yeye na walinzi wake washangae. Unasubiria akiwa kwenye good moments zake (hasa kwenye ile hotel .....x..... anayotembelea ijumaa jioni kuchati na mafisadi wenzake) kisha unatokea na bonge la bango limeandikwa fisadi fisadi fisadi na kutumia vipaaaza sauti ukicheza muziki wa I work it out ... i work it out... i work it out....

Ahahahahahahaaaa......you are my favorite person!!
Did you know that...?
 
Nyani Ngabu,

Kwanini Wamrushie Mawe,Kwa kosa gani??hakuna aliye juu ya sheria,kama watanzania tunaona ana kosa basi ttumpeleke Mahakamai ili asurubiwe na sio kumuita Mtu fisadi.

Kweli ukishangaa ya musa, utaona ya..........
 
jamani Fisadi Mkapa Akionekana Katika Sherehe Za Kitaifa, Watanzania Wote Tumzomee Fisadi Fisadi Fisadi!!!! Tuone Watafunga Wangapi?
 
vijana wa kileo wamekuwa hawana adabu.

huo ndio ukweli na tukishindwa kukaza kamba kwenye malezi taifa litaelekea kubaya

Hawana adabu kwa sababu mama zao wanatembea kilomita zaidi ya 15 kufuata zahanati,

Hawana adabu kwa sababu wadogo zao wanasoma kwenye shule zenye walimu wawili tena wale wa crash program,

Hawana adabu kwa sababu wanajua wenzao walishindwa kupelekewa hela walipokuwa ukraine ili waendelee na masomo,wakati fedha za serikali zilitumika kumsafirisha mkwe wa kikwete kwenda makka kuhiji

Hawana adabu kwa sababu kiongozi wao mmoja anaita bilioni moja ni vijisenti,

Hawana adabu kwa sababu ajira hakuna,

Hawana adabu kwa sababu gharama za maisha zinapanda kila siku,

Hawana adabu kwa sababu waliotakiwa wawe na adabu hawana adabu!
 
Toka lini kuzomea ni kosa?
Kuna sheria inayokataza kuzomea? Kama ipo iweke hapa maana itakuwa ni moja ya unjust laws. Na kama ipo, application yake ikoje? Kwa mfano nikikuzomea wewe kwa kumtetea Mkapa polisi watanikamata au ina apply tu pale "wakubwa" wanapozomewa? Please tell me...

Ni ki gazeti feki hiki kilibidi kiseme. Tatizo Bongo hakuna Media. Hapa ilibidi mwandishi afuatilie Polisi kujua wamekamatwa kwa shuku ya kuvunja sheria gani, au atuambie juhudi zake za kufuatilia zilizaa matunda gani.

Tunajadili kwamba vijana wanaweza kwenda kuthibitisha Mahakamani kwamba Mkapa fisadi. Lakini kama sheria inasema huwezi kumwita unayemdhania mwizi mwizi kabla mahakama haija amua kwamba ni mwizi basi vijana watakuwa bado na hatia hata wakuthibitisha kwamba ni kweli waliye mdhania mwizi ni mwizi.

Tanzania hakuna Media.
 
Kuhani,,

Ninavyojua mimi ni kuwa sheria inawataka media wanaporipoti ndiyo waseme mtuhumiwa mpaka mahakama I rule.Mimi kama nakujua wewe fisadi naruhusiwa kukuita fisadi na kama hupendi nishtaki mahakamani nikutolee ushahidi zaidi.
 
jamani ufisadi si kosa la jinai!! Hakuna sheria inayotaja makosa ya kifisadi. Na kumuita mtu fisadi si kosa.
 
Pundit unaongelea misingi ya libel na defamation. Lakini unachanganya Civil na Criminal law. Kwenye Civil Law hutiwi ndani. Hawa jamaa kesi yao haihusiani kabisa na Civil Law.
 
Mwnkjj;

Inawezekana kosa ni kumzomea Kiongozi mstaafu.
 
Mwnkjj;

Inawezekana kosa ni kumzomea Kiongozi mstaafu.

hakuna kosa la kuzomea awe kiongozi mstaafu au kiongozi aliyeko madarakani. Kuna makosa ya kumdhalilisha (Libel), kutukana au kuchochea chuki dhidi ya serikali na makosa ya kumdaia mambo ya uongo. Hawana kesi, zaidi ya kutishia watu.
 
hakuna kosa la kuzomea awe kiongozi mstaafu au kiongozi aliyeko madarakani. Kuna makosa ya kumdhalilisha (Libel), kutukana au kuchochea chuki dhidi ya serikali na makosa ya kumdaia mambo ya uongo. Hawana kesi, zaidi ya kutishia watu.

Mwnkjj,

Kama nilivyo mwambia Pundit, makosa ya libel na kumsingizia mtu uongo hayaingii kwenye huu mjadala kwa sababu kwa sababu ni Civil wrongs ambazo huwa hukamatwi mtu hata siku moja.
 
Duu mambo ya yule mkuu wa wilaya (Dr. ..) Mahenge-Morogoro yanatokea hadi dar? wale jamaa wa mahenge walishikwa na kuwekwa rumande kwasababu ya kufurahi na kushangilia ilipotangazwa kwamba Mbunge wa Mhe. Ngasongwa amekosa Uwaziri. sasa hii ya watu kusema fisadi, fisadi ni haki yao jamani.
- mbona Mhe Kimaro hajapelekwa polisi?
- Kunauhakika gani kuwa vijana hao walikuwa wanamsema Mkapa?
- Je kuwakamata hao kutaondoa hisia za wananchi kumuona Mkapa fisadi?

Hii inaweza kuongeza chuki, eti uliowaibia unawakamata na kuwafunga kwasababu wanasema umewaibia! shit!
 
Heri hao vijana waaachiwe huru mapema maana magazeti ya kesho ndo yatakoleza vichwa vya habari ili kumchokonoa ajitetee kwa nini yeye si fisadi.

This is the best that can be expected to come out of the young folks` inconvenience, mega publicity. Mkapa himself would not wish for this happening, I am certain!
 
Vijana wapewe dhamana waje nje na watafute mawakili wakaunguruma .Kwani wanakamatwa malalamikaji ni nani ? Ni Jamhuri mbona wasiwakamate wale tunao walalamikia kila mara jamani >
 
Kitila,



Ni makosa makubwa, inaonekana walitaka hao vijana wasifie tu na kupiga vigelegele kuwa mkubwa kapita.

Pambaffff kabisa!
TATIZO LA UKUBWA NAO KAMA ULEVI HIVI KUNA KITU WANAITA NIGERIA KABIO OSSI MENTALITY AMBACHO NILIKIONA KIKIJIONYESHA SANA KWA MKAPA ILE KUWA RAISI AKAWA KAMA YEYE NDIYE MWENYE AKILI KULIKO WOTE,SASA ALITAKA ASHANGILIWE HUYO KABIO OSSI (MWENYEENZI MUNGU)
 
Mkapa Na Mahalu Ni Fisadi Sana Nakumbuka Kule India Tulisomeshwa Wanafunzi Zaidi Ya 5000 Kwa $10,000/ Kichwa/mwanafunzi Kwa Mwaka Lakini Wanafunzi Tukawa Tunapewa $1,200.00 Tu. Nyingine $8,800.00zikapelekwa Kwenye Account Zao Us, Uk, German Etc Through Edcl (wakala) Wa India.
 
kwi kwi kwi kwi koh koh koh duu yaani mpaka nimepaliwa koh koh aaaaagh...na bado na huu ni mwanzo, tunakoelekea tutakuwa hata tukikutana na watoto wao tunawashushia mkong'oto heavy ili kufidia ubani wetu kwa baba zao
 
Mkapa Na Mahalu Ni Fisadi Sana Nakumbuka Kule India Tulisomeshwa Wanafunzi Zaidi Ya 5000 Kwa $10,000/ Kichwa/mwanafunzi Kwa Mwaka Lakini Wanafunzi Tukawa Tunapewa $1,200.00 Tu. Nyingine $8,800.00zikapelekwa Kwenye Account Zao Us, Uk, German Etc Through Edcl (wakala) Wa India.

Mazee kwa hesabu za chap chap, kama unayosema yana uhakika, hizo ni $ 44,000,000!

Kwa nini Chenge asiseme "vijisenti"?
 
Mimi naomba wana blog wote mziweke habari hizi ktk mitandao ytenu iwe kwa kiingereza ama kiswahili maadam habari kama hizi zisambae hadi ktk vyombo vya haki za kibinadamu.
Tusiyazungumze humu tu na kuyaacha kama yalivyo ni wakati wa hata kupeleka hoja kama hii kwa wabunge wetu....
Ni matukio kama haya yanaweza badilisha kabisa vitendo vya watawala kama tutaweza kusimama imara...
 
Back
Top Bottom