Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Nyani Ngabu,

Kwanini Wamrushie Mawe,Kwa kosa gani??hakuna aliye juu ya sheria,kama watanzania tunaona ana kosa basi ttumpeleke Mahakamai ili asurubiwe na sio kumuita Mtu fisadi.

Kosa la kuhatarisha Amani.Mathalani kama wangempiga Risasi Rais mstaafu unaju Madhara yake ni yapi.


Mtuhumiwa wa wizi Jijini apigwa hadi kufa

2008-05-03 16:17:34
Emmanuel Lengwa said:

Wananchi wenye hasira wamemshambulia kwa mawe na marungu na kumuua kijana mmoja Jijini Dar es Salaam kwa tuhuma kuwa ni kibaka. Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Jamal Rwambow amesema tukio hilo limetokea jana mishale ya saa 3:00 asubuhi pale katika eneo la Mburahati Motomoto Jijini.

Akamtaja kijana aliyeuawa kwa kupigwa na wananchi hao kwa tuhuma za wizi kuwa ni Eliya Kilyafoo, anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 20 na 25. Akasema mpaka sasa hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa na Polisi kuhusiana na tukio hilo, na kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Mwananyamala.

Hata hivyo, Kamanda Rwambow hakusema kijana huyo amepatwa na umauti kwa kutuhumiwa na tukio gani la wizi. Badala yake Kamanda Rwambow ametoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mikononi mwao na wajenge mazoea ya kuwafikisha wahalifu kwenye vyombo vinavyohusika.

Je, polisi waliwashika waliomuua huyo kijana au hawana kazi za kufanya?


From Arusha

DEOGRATIAS MUSHI in Arusha said:
Daily News; Monday,May 05, 2008 @00:03


Mob lynches man in Arusha

A MAN was on Saturday lynched by an angry mob at Moivaro village near Tengeru town, as he tried to break into a retail shop with an intention to steal. Arusha Regional Police Commander Mr Basilio Matei told ‘Daily News’ here yesterday that Richard Tobias Mollel (24), who also resides at the same area was killed, as he tried to forcefully gain entry into the shop owned by a person who could only be identified by one name as Muwas.

Mr Matei said that Mollel had a history of being associated with various burglary incidents at the area, and the public had closely started monitoring his movements. The RPC further said that Mollel has a pending robbery case in court, which was first mentioned in January this year, and he had been released on bail. Before being killed, Mollel and other four people who managed to escape had already stolen some items from homes of Denison Ngoseki, Erasto Steven and Obeid Chifuwa.

“The man is one of the few suspected hard core thieves at Tengeru town. In the recent past, he had been arrested by police and linked to several armed robbery cases,” said Mr Matei. However, the RPC warned the people against taking the law into their hands, saying any suspect should be arrested and tried before the law courts.

Meanwhile, a suspected robber was on Saturday night seriously injured when he tried to break the gate of a house at Njiro area, in the suburbs of Arusha city. Arusha RPC Basilio Matei said yesterday that Haruna Jumanne (24) was wounded by his house helper, Michael Urassa, who was coincidentally returning home from hospital.

Mr Matei said that Mr Urassa was invaded by four people and since he was carrying his gun he opened the fire and managed to wound the suspect. “The other three escaped and we are still looking for them. Jumanne has already tipped us off, and we are sure that we will arrest them soon,” Mr Matei said.

The suspect who is now admitted to Mount Meru regional hospital is under police guard until he will appear before the court.

Anyway watakuja kusema hawa vijana hawakupigania Uhuru na wanatumiwa na mabeberu wa magharibi yaani UK na USA. Wanawasupport wakolomi.
 
Mimi naomba wana blog wote mziweke habari hizi ktk mitandao ytenu iwe kwa kiingereza ama kiswahili maadam habari kama hizi zisambae hadi ktk vyombo vya haki za kibinadamu.
Tusiyazungumze humu tu na kuyaacha kama yalivyo ni wakati wa hata kupeleka hoja kama hii kwa wabunge wetu....
Ni matukio kama haya yanaweza badilisha kabisa vitendo vya watawala kama tutaweza kusimama imara...

Kamanda umesomeka mkuu

Sasa hivi dunia nzima inaelewa jinsi Mkapa alivyofanya biashara, hata polisi waliowakamata vijana wanajua hilo sasa ngoja wataalamu wa mambo ya sheria waanze kuchambua jinsi Mkapa alivyo vunja sheria na kuangalia uhalali wa vijana kukamatwa.

Hili la Mkapa sasa litakuwa big. ishue ni afadhali vijana wamesaidia hili liweze kujulikana dunia nzima.

Itabidi Mkapa sasa anyimwe viza za kuingia nchi mbali mbali.

Naona Mkapa kwa kutaka yaishe aombe polisi wawaachie hao vijana bila masharti yoyote maana inajulikana kwamba yeye na UFISADI ni kama pete na kidole
 
freedom is not free.
Kama uhuru wa siasa haupatikani bure je wa kiuchumi itakuwaje????
Mafisadi yanatumia na yatatumia nguvu zao zote kujilinda. Uhuru wa uchumi ni mchungu sana na utapatikana kwa jasho la damu.

Hawa vijana kukamatwa inaweza kuwa ni chachu ya uhuru wetu dhidi ya mafisadi. je kama wataaamua kuwashikilia na kuwafikisha mahakamani tutafanya nini? tutaandika tu na kusubiri hukumu?

Nchi nyingi duniani zimebadilishwa na watu wachache walioamua kujitoa mhanga. Mkapa ni fisadi inatupasa kupiga kelele nchi nzima. Sasa wakati umefika kuwaonyesha mafisadi tumechoka na ufisadi wao.

Kazi ya usalama wa taifa sio kulinda mafisadi ni kuwafichua mafisadi, sasa kama wameanza kuwalinda usalama wa taifa ubadilishwe jina uwe ni usalama wa mafisadi. Usalama wa raia sasa ni usalama wa mafisadi.

Wote sasa tupige kelele mkapa fisadi ! mkapa fisadi!.........
 
Nyani Ngabu,

Kwanini Wamrushie Mawe,Kwa kosa gani??hakuna aliye juu ya sheria,kama watanzania tunaona ana kosa basi ttumpeleke Mahakamai ili asurubiwe na sio kumuita Mtu fisadi.

So Mr Gembe, tunapopiga kelele mwizi mwizi mwizi, kwani tunakuwa na maana gani? Sin tuna maana tunataka tumkamate tumtie kibano na tumpekele polisi, then mahakamani and then gerezani? In other words do you think it is not fair to call Mkapa so and fair to call vibaka so, is that right?
 
Naelekea Kufikiri kuwa Huyo Bwana(Ben)keshapewa taarifa ya kilichotokea,na atakuwa keshapiga simu kuwa hao Vijana waachiliwe maramoja!!kwani bila ya kufanya hivyo,hatoishi kwa amani hata kidogo.
Kwasababu leo ni pale kijiweni yametokea hayo,hivi Kesho pale uwanja wa taifa:Anaingia Salmin-"Komando,komando",Mwinyi-"Ruksa,ruksa",Mkapa-"Fisadi,fisadi" Je polisi watamkamata nani,wamwache nani??
 
Ni vizuri Watanzania tukaanza kumzomea Mkapa popote atakapoonekana hadharani kwa ufisadi mkubwa alioufanya halafu hataki kujibu tuhuma zozote dhidi yake. Ikitokea bahati mbaya kukutana na fisadi Mkapa popote pale ulimwenguni sintamsalimia, nimsalimie kwanini? kipi alichokifanya Tanzania mpaka nimsalimie. Watanzania natoa wito hawa mafisadi wote akina Mkapa, Chenge, Lowassa, Msabaha, Karamagi, Mramba, Mkono, Mzindakaya na wengineo popote tukiwaona hadharani tuwazomee kwa ufisadi wao dhidi ya nchi yetu.

Sijui hili litakuwa na matokeo gani, lakini mtu mzima kuzomewa hadharani ni aibu ya hali ya juu.
 
Mkapa ni mwizi sawa na wezi wengine, kama wananchi tunaweza kuwachoma moto vibaka wanaoiba simu ya mkononi ya sh 20,000 sioni sababu kwanini wananchi wasifanye hivyo kwa mkapa ambaye kwa kiasi kikubwa sana ametufikisha sehemu hii mbaya tulipo. ametuibia mali zetu nyingi kwa wimbo wake wa sera ya ubinafisishaji wa mashirika ya uma, migodi, alipoambiwa au kuulizwa na wananchi alisema ni wivu wa kijinga. Hawa watu hakuna haja ya kuwalea tuwazomee, tuwaponde mawe na kuwachoma moto.
 
Haya la mgambo likilia ujue kuna jambo NGUCHIRO HAO WAMETOKA MATUNDUNI MWAO NI MAWE TUUUUUUUU!!!!!!!!

Nguchiro 2.jpg

Nguchiro 1.jpg

Nguchiro 3.jpg
 
kwi kwi kwi,

Kuanzia leo Mkapa atabadili ratiba baada ya kilichotokea! Nadhani the best way ni kufanya shtukizo hadi yeye na walinzi wake washangae. Unasubiria akiwa kwenye good moments zake (hasa kwenye ile hotel .....x..... anayotembelea ijumaa jioni kuchati na mafisadi wenzake) kisha unatokea na bonge la bango limeandikwa fisadi fisadi fisadi na kutumia vipaaaza sauti ukicheza muziki wa I work it out ... i work it out... i work it out....

aaaaaaaaaaaa.... mshkaji unaniangusha TAJA JINA LA HOTEL WE DARE TO TALK OPENLY
 
Hawa wanawaonea, si mkuu Pinda alishasema majuzi Iringa vijana wasisite kumwita fisadi mtu yeyote anayetafuna mali ya umma! sasa hii imekaaje ina maana hawa Polisi wanakiuka maagizo ya mkuu Pinda?
 
Tuandamane una maananisha "FUSADI au FISADI?? Kama ni Fisadi ni mwizi na mdanganyifu. zaidi ilitumika kwa watu wanaoiba wake za watu..lakini mi naamini mwizi ni mwizi tu bila kuangalia haiba ya mtu na alichoiba... Any more clarification please...
 
Yani mtu ukisema ukweli siku izi unakamatwa???dah!!! sijui tatizo liko wapi wakati jamaa ni fisadi kweli..bora wangesema shooga uyoo'' hapo sawa ingekua uzushi wangeamwatwa kwa ku shout uongo na uzushi lakini sio kwa hili.. ila tuache labda sababu haijathibitishwa na mahakama kama ni fisadi kweli au la
 
He will retain the title no matter what. He did it and he deserve the concequences . He can not rub it through police.Hawa vijana ni symbol tu ya what is pending for him. Akumbuke hii ndio itakuwa alama yake ya maisha yaliyobakia. Aliitaka mwenyewe.Inasemekana 666 ni alama ya mpinga Kristo, na FISADI ni alama ya ant Tanzanianism
 
aaaaaaaaaaaa.... mshkaji unaniangusha TAJA JINA LA HOTEL WE DARE TO TALK OPENLY


Ni kweli hiyo Hotel X iko wapi?
Sema hapa openly tujue.
kuna watu majasiri hap[a wanaweza kufanya kile ambacho wengi wanaogopa kukifanya.
Ukitaka kuondoa UFISADI then ondoa Shina lake
 
Gembe amethibitisha tetesi kuwa JK is behind all of these games against his successor. Ni wazi hii iko planned, tokea msafara wake,Dar leo/aka Majira na hata hao polisi walioshiriki ktk ukamataji. Msafara wa kiongozi mara zote hauna hata hiyo nafasi ya kushuhudia makelele ya hao vijana kutokana na maandalizi yake kwa maana ya njia,spidi n.k, hata huyo mwandishi aliyeripoti pamoja na timu yake ya uzomeaji wametuachia maswali mengi sana. Kwanini tunamuona JK kwa sura mpya ambayo FMES alishawahi iandika hapa na BCS? Inakuwaje watu wa usalama ndio wawe chanzo cha vurugu na zile siasa za kiwango cha chini, huu ni mchezo ambao ipo siku wasipojihadhari wajue ipo siku JK atazomewa tena hakutakuwa na maandalizi ya namna hii tuionayo sasa, nadhani wakubwa hawa wanakokwenda si salama, vita hii ya UFISADI ni vema ikapiganwa kisayansi zaidi kuliko hii style ya mediazation na kukodi wazomeaji, naiona hatari ya kukwama kwetu ikikaribia, je tukishazomea mpaka 2015 then wat? Je wakiingia tusiowatarajia ktk game hii itakuwaje? Tumeshamuona Kakobe akikemea hilo na Marando akitoa picha zaidi ya nne ktk story zake na sasa Jaji Warioba naye ktk namna mupya.

Nadhani wasaa umefika wa sisi waTZ kujitizama kwa kina na tutafakari wenyewe nini hatima yetu.
 
Ni vizuri Watanzania tukaanza kumzomea Mkapa popote atakapoonekana hadharani kwa ufisadi mkubwa alioufanya halafu hataki kujibu tuhuma zozote dhidi yake. Ikitokea bahati mbaya kukutana na fisadi Mkapa popote pale ulimwenguni sintamsalimia, nimsalimie kwanini? kipi alichokifanya Tanzania mpaka nimsalimie. Watanzania natoa wito hawa mafisadi wote akina Mkapa, Chenge, Lowassa, Msabaha, Karamagi, Mramba, Mkono, Mzindakaya na wengineo popote tukiwaona hadharani tuwazomee kwa ufisadi wao dhidi ya nchi yetu.

Sijui hili litakuwa na matokeo gani, lakini mtu mzima kuzomewa hadharani ni aibu ya hali ya juu.

hali halisi ni kwamba kuna wanadamu tanzania hii ukisema tu lowassa fisadi au mkapa fisadi unaweza ukaishia hata kupigwa. na wengi wa hawa binadamu hawajafaidi chochote kutoka kwa hawa mafisadi zaidi ya shida.

Mtu unakaa unajiuliza what else can be done kuonyesha kwamba hawa watu ni waovu na wametumia rasilmali za nchi hii kwa manufaa yao.
 
Back
Top Bottom