Kuna uwezekano mkubwa (ukizingatia uchumi wa Tanzania) mtu anayeendesha GX, VX, etc. kuwa fisadi. Sasa, hata katika ufisadi kuna viwango. Kuna mafisadi wa small scale, medium scale, na kina Mkapa na Chenge ambao hamna hata daraja la kuwaweka. Kwa hiyo sishangai kabisa kwa walalahoi wasukuma mikokoteni, watembea kwa miguu, waendesha baiskeli, na wapiga debe kuwaona waendesha magari ya thamani kuwa ni mafisadi. Disparity iliyopo ni ya ajabu sana kiasi kwamba huwezi kuamini mtumisha wa serikali kuwa tajiri kupindukia.
Halafu kama ni utani kwa nini sasa watu wakamatwe? Na kama walikuwa hawamzomei Mkapa, ina maana na mimi Ngabu nikikuzomea wewe Fikiraduni nitakamatwa? Or in other words siku hizi kuzomea limekuwa kosa linalo-warrant kukamatwa na polisi?