Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Kuwa trained lawyer si tija. Hata Chenge ni trained lawyer lakini mnakumbuka alisema kuwa takrima ni legal? Hawa watu wanatafsiri sheria kukidhi mtazamo wao. Hapa ninakubaliana zaidi na Tindu Lisu.
Kama Zambia waliweza kumshitaki Chiluba, why not us?

Way to go Bro! I agree 100% with you on this issue. It is about time we get serious about rampant corruption in our beloved country.
 
Swali ambalo ni la msingi na linahitaji kuamuriwa na mahakama ni wakati gani Rais anatenda kama Rais na ni wakati gani anatenda kama mtu binafsi? Kwa mfano, RAis anatembelea mji fulani na anapoita ripoti ya maendeleo ya mahali hapo, ripoti hiyo haimridhishi na anaanza kumgombeza mtendaji aliyeleta ripoti hiyo. Yule mtendaji anajaribu kuelezea kwa nguvu zote lakini Rais hasira zinazidi kumpanda na kwa jazba anamchapa kibao cha nguvu mama yule, mdomo mama unampasuka na jino moja linang'oka... what do we do to the president.. did he assault the woman in his personal capacity or as a president while conducting his constitutional duties?
 
Sisi Wabongo tunapenda sana kupachika mimba vitu ambavyo havihusiani kabisa.
Kitu kinachozungumziwa ktk katiba ni matumizi ya wadhifa URAIS ktk Uongozi. mathlkan leo hii Bush na matatizo yote aliyokuwa nayo maamuzi mabaya alowahi kuyafanya na pamoja na hata kura za veto alizowahi kutumia dhidi ya baadhi ya madai ambayo Senate, Cogress na hata wananchi wamekuwa upande wa pili unaopingana naye.
Matumizi ya uongozi wa namna hii hauwezi kushtakiwa mahakamani kwa sababu kila kitu kinapitia ktk taratibu za kikatiba. Hata tukija tazama vita ya Iraq, pamoja na lawama zote za maamuzi mabaya ya Bush lakini hakuna kitu kilichofanyika bila kupitia utaratibu unaotakiwa. Toka walipopiga kura kuivamia Iraq hadi leo hii huwezi kuona ukiukaji wowote wa katiba ya Marekani.
Tatizo la Tanzania ni kwamba kuna vitu elfu kidogo vimetolewa maamuzi bila kupitia taratibu ambazo zinazokubalika, bado tunampa mtuhumiwa kinga kwa sababu tu alikuwa RAIS!!!!!
 
Mkandara... tatizo la Katiba yetu ni kuwa process ya kumwadhibu Rais is very complicated na wameifanya iwe ngumu kweli.
 
Jambo hili nililizungumza hapa. Katiba inamlinda tu kwa maamuzi aliyofanya katika madaraka yake kama rais wa nchi kwa niaba ya taifa. Haimlindi kwa maamuzi yake binafsi kwa niaba yake mwenyewe na familia yake. Jambo hili liko wazi sana katika vifungu vile viwili. Kifungu cha 46(2) kinamlinda asishtakiwe kwa maamuzi yake binafsi na yale ya kitaifa wakati bado yuko madarakani. Nadhani hii ni kuzuia asije akatumia madaraka yake kuvuruga kesi hiyo na vile vile kujitahidi kumlinda against distractions zinazoweza kumfanya asitekeleze majukumu yake sawasawa. Kifungu cha 46(3) kunamlinda kwa maamuzi ya kitaifa aliyofanya kama rais tu. Kufungu hiki hakimlindi tena kwa mambo yake binafsi. Mkapa anakabiliwa na tuhuma za kutumia ofisi yake kwa mambo yake binasfi na kwa msingi wa katiba, anaweza kabisa kushtakiwa bila mtafaruku wowote wa kikatiba.
 
Swali ambalo ni la msingi na linahitaji kuamuriwa na mahakama ni wakati gani Rais anatenda kama Rais na ni wakati gani anatenda kama mtu binafsi? Kwa mfano, RAis anatembelea mji fulani na anapoita ripoti ya maendeleo ya mahali hapo, ripoti hiyo haimridhishi na anaanza kumgombeza mtendaji aliyeleta ripoti hiyo. Yule mtendaji anajaribu kuelezea kwa nguvu zote lakini Rais hasira zinazidi kumpanda na kwa jazba anamchapa kibao cha nguvu mama yule, mdomo mama unampasuka na jino moja linang'oka... what do we do to the president.. did he assault the woman in his personal capacity or as a president while conducting his constitutional duties?
Anaposaini mkataba wa kibishara wa Anben kwa niaba yake binafsi na Anna, anakuwa anafanya kama Mkapa na anaposaini mkataba wa madini wa Buzwagi kwa niaba ya taifa anakuwa anafanya hivyo kama Rais. issue hapa ni kuwa alikuwa anafanya kwa interest za nani. Katiba inalinda interest za taifa siyo za mtu binafsi.
 
Swali ambalo ni la msingi na linahitaji kuamuriwa na mahakama ni wakati gani Rais anatenda kama Rais na ni wakati gani anatenda kama mtu binafsi? Kwa mfano, RAis anatembelea mji fulani na anapoita ripoti ya maendeleo ya mahali hapo, ripoti hiyo haimridhishi na anaanza kumgombeza mtendaji aliyeleta ripoti hiyo. Yule mtendaji anajaribu kuelezea kwa nguvu zote lakini Rais hasira zinazidi kumpanda na kwa jazba anamchapa kibao cha nguvu mama yule, mdomo mama unampasuka na jino moja linang'oka... what do we do to the president.. did he assault the woman in his personal capacity or as a president while conducting his constitutional duties?

Mkjj, umenikumbusha jamaa mmoja huko Uingereza wanamwita 'mr.two jags'; huyo ni John Prescot, alivuma hivyo baada ya kutembelea kwenye Jaguar mbili kila anapoenda hali akipinga matumizi kama hayo bungeni, alikuwa deputy PM wakati wa Tony Blair. Basi, ilitokea siku moja alirushiwa yai ziarani, wee acha bwana.. jamaa aliuvua udeputy wake mara moja na kumtwanga ngumi jamaa aliyerusha papo hapo! Hivyo basi ni kweli kuna mambo mengi kiongozi wa juu anaweza akafanya kama kiongozi, lakini pia kuna mengi pia anawezafanya kama raia mwingine tu na kwa haya kama yanakiuka sheria na katiba anapaswa kuadhibiwa kama raia yeyote yule.

SteveD.
 
bado hamjajibu swali langu la mfano... RAis akimtoa ngeu mtu wakati Rais amepandwa na jaziba wakati wa kazi, atashitakiwa kwa kosa gani... now kabla hamjajibu angalia kifungu cha 46 cha Katiba mwanzoni kabisa.... utaona nazungumzia nini? Kinga aliyo nayo Rais aliye madarakani ni kubwa kuliko mnavyofikiria. Ninachouliza hasa ni kama inawezekana kumkamata Rais kwa kosa la jinai akiwa madarakani...

Njia nyepesi zaidi ni Rais mwenye kujiuzulu baada ya kufanya kosa ambalo ni dhahiri
 
Mkandara... tatizo la Katiba yetu ni kuwa process ya kumwadhibu Rais is very complicated na wameifanya iwe ngumu kweli.

Technically wameifanya kuwa nguma, lakini ki ukweli inawezekana.
Eg Hiyo sheria ya Bunge kumu-impeach the president kwa makosa ya kiutendaji , nyingine ni hiyo ya Mahakama Kuu, kwa makosa ya wizi na Rushwa, na nafasi inakuwa wazi saana akiwa amestaafu.
 
MKJJ,

Ni kweli kifungu cha 46, vifungu vidogo (1) na (2) vinamlinda rais wakati akiwa bado yuko madarakani ili asishtkiwe kwa makosa yoyote yale, yawe ya jinai au ya madai; hata kama makosa hayo aliyafanya binasfi na wala siyo katika capacity yake kama president.

Kifungu kidogo cha (3), kinamlinda rais baada ya kutoka madarakani kwa makosa yale aliyofanya katika capacity yake kama president; mifano ndiyo kama iliyotolewa na kaka Mkandara kuwa ni pamoja na kuwafukuza watu kinyume cha sheria, au kuwaweka watu kizuizini na kuwapotezea uwezo wao kutunza familia za kwa makosa. Kifungu hiki hakimlindi kwa makosa aliyofanya binafsi ambayo hayahusianai na kazi zake kama president.

Kumtoa mtu ngeu mtu kutokana na kupandwa na jazba siyo sehemu ya mamlaka yake kama president. Ikitokea hivyo, huyo mtu aliyetolewa ngeu itabidi asubiri hadi rais huyo atoke madarakani ndipo amfungulie mashitaka.
 
Jamani mweeee, mbona mnakuwa hamuelewi kinachozungumzwa hasa kuihusu Mkapa.
Mkapa ni sawa na Pimp anaijua lugha yote ya kulaghai watu aonekane mwema hali hakuna mshenzi kama yeye. Huyu ni sawa na matapeli wale wavaa suti ambao hujijengea uaminifu kwa maneno huku malengo yao hayana huruma kabisa!..
Kinachofanya Mkapa awe kiongozi mbaya na hatari kuliko wote ni kwa sababu anayo elimu ya dunia zote mbili. Msomi mzuri na alitegemewa kuwa muadilifu badala yake katumia zifa zake kutunyonga!..
Huyu ni kiongozi mbaya na hatari sana kuliko JK ambaye hajui anachokifanya!..
Let me tell you something .. this guy is very smart na inasemekana hata hizi scandal za Karamagi & cos zimeanzishwa toka kambi ya Mkapa (Mkataba wa Buswagi) kuondoa joto la scandal zilizokuwa zikimzungumzia yeye!...
Well kama ndivyo basi huyu mzee kiboko yao!
 
Jamani mweeee, mbona mnakuwa hamuelewi kinachozungumzwa hasa kuihusu Mkapa.
Mkapa ni sawa na Pimp anaijua lugha yote ya kulaghai watu aonekane mwema hali hakuna mshenzi kama yeye. Huyu ni sawa na matapeli wale wavaa suti ambao hujijengea uaminifu kwa maneno huku malengo yao hayana huruma kabisa!..
Kinachofanya Mkapa awe kiongozi mbaya na hatari kuliko wote ni kwa sababu anayo elimu ya dunia zote mbili. Msomi mzuri na alitegemewa kuwa muadilifu badala yake katumia zifa zake kutunyonga!..
Huyu ni kiongozi mbaya na hatari sana kuliko JK ambaye hajui anachokifanya!..
Let me tell you something .. this guy is very smart na inasemekana hata hizi scandal za Karamagi & cos zimeanzishwa toka kambi ya Mkapa ili kuondoa joto la scandal zilizokuwa zikimzungumzia yeye!...
Well kama ndivyo basi huyu mzee kiboko yao!

Heshima yako mkuu,yaani unamjua Mkapa kuliko hata yeye mwenyewe anavyojijua,Mkapa ni laghai sana.
 
watu wagumu sana kumpa mzee Benny props ! sijui kwa nini, nadhani hii inatokana na chuki inayojijenga mpaka kizuri kwao kinakuwa kibaya !
 
Ohhh Yah! alikuwa akielewa matatizo yetu na dawa ya kuyatatua akatuapatia serikali tuliyonayo sasa ya akina Karamagi!

Kuwa na JK leo hii wala simlaumu sana BWM..................hivi umeshawahi kufuatilia au kujiuliza ni kwanini Tom leo ni mbunge wa kuteuliwa!!??
 
Mkuu Ogah,

Heshima mbele, umesahau kuwa nitawa-suprise Wa-Tanzania kwa kuwapatia rais anayefaa na wasiyemfikiria, unakumbuka ilikuwa ni kauli ya nani hiyo mkuuu?

Baada ya uchaguzi akaenda kukaa chini na Wakuu wa Dini, ili wahalalishe suprise yake, umesahau ya nabiii?

Au hujui aliyewashinikiza hao hao wakuu wa dini ni nani?

Mkuu Ogah, ninajua kuwa una upeo mzito wa kuona ishus, Biblia inasema mkuu shetani ni sungura sana katika kujigeuza geuza, maana akija kwetu wana-adam kama alivyo wote tutamkimbia, kwa hiyo hujifanya malaika, au sometimes intellectual kama Mkapa, halafu hujifanya mtiifu kwa Baba Wa Taifa na kuwa ni mwanafunzi wake hodari sana, halafu hutengeneza uchumi wa nchi na baadaye kupigia kelele sana rushwa, halafu pia hutoa hotuba nzuri sana huko majuu kuhusu matatizo yetu,

ni mpaka akishaondoka madarakani ndio wananchi mnakuja kugundua kuwa yeye na famili a yake, walikusanya kila kitu, lakini hakuna ushahidi na hata ukiwepo aliowaweka madarakani wanamkingia kifua, Mkuu wangu yanayotukuta sasa hivi as a nation ukweli ni kwamba yanaanzia kwake, maana ni yeye peke yake ambaye Mwalimu alikuwa akimuamini kuwa wanafanana kwa kila kitu, wewe leo kiongozi mtuhumiwa wa mauaji aliyeko nje kwa dhamana, anawekwa kwenye safari za mawaziri kuhutubia wananchi hao hao ambao mmoja wao alimpiga kwa bastola bila sababu,

Nasikia kuwa Mungu, aliwaadhibu Sodoma na Gomora kwa kuwa a lawless nation, sasa kama anatuachia sisi Tanzania bila kutuadhibu, basi anahitaji kwenda kuwaomba radhi wale wakuu wa Sodoma na Gomora, au?
 
watu wagumu sana kumpa mzee Benny props ! sijui kwa nini, nadhani hii inatokana na chuki inayojijenga mpaka kizuri kwao kinakuwa kibaya !

Watu hawamchukii Mkapa, wanachochukia ni mambo aliyoyafanya akiwa Ikulu ikiwemo kufanya biashara akiwa Ikulu, ununuzi wa rada ya $40 millioni ambao yule wakala wa kihindi alilipwa $12 million hizi zingefanya mambo mengi sana katika kuinua hali ya maisha ya wabongo au kusaidia huduma muhimu kama hospitali, shule, maji safi n.k. Muhindi huyo huyo ndiye aliyekuwa wakala wa kununua magari ya jeshi na helicopters, inasemekana pia kwenye ununuzi wa ndege ya Rais alikuwa wakala, kusaini mikataba ya uchimbaji wa madini ambayo hadi hii leo bado ni siri na wakati huo huo kumbuka huu wa Buzwagi uliovuja tunaambiwa uliboreshwa sana ukilinganisha ni hiyo mikataba iliyopita. Sasa hiyo mikataba mingine badala ya kukutoa machozi unaweza ukapata wehu kabisa! Jinsi alivyokuwa mmiliki wa Kiwira Coal Mining pamoja na Yona na kuishinikiza TANESCO kusaini mkataba wa shilingi 340 billion ambao hauna tofauti na wa IPTL kwa maana nyingine hauna maslahi kwa Watanzania. Kwa hiyo kama binadamu watanzania hawamchukii, ila kujifanya alikuwa kiongozi bora kumbe alikuwa busy kujilimbikizia mali yeye na familia yake.
 
Kasana,

Ndugu yangu JK hajui anachokifanya kwani Ikulu sii mahala pa lelemama!..Tuachikiona ni Usanii yaani lelemama.
Ebu rudia kusoma vizuri mahojiano yake utaona kila sababu inayosemekana kuturudisha nyuma yeye hujibu hiyo sio tatizo kwetu!.. That's not a problem, yet haelewi sababu zinazoturudisha nyuma!
Umewahi kuona hiyo! kweli huyu mtu anafahamu huko tuendako maanake kama safari ina vikwazo na haelewi kinacho kwamisha atakuwa kweli kiongozi wa msafara ama kamwachia Mungu!
Mkapa knew every move he made. Mkapa alifahamu kwamba alikunywa utajiri wa Tanzania akiwa na kina Yona na aliweza kujibu maswali mengi vizuri sana kwa kutumia elimu yake ya Utapeli.
Huko nje kulikuwa hakuna mtetea Umaskini kama yeye hali nyumbani akifuta John Mtembezi kila kukicha. Mwenzetu JK hafahamu hata la kusema kwanza haamini kwamba kuna ufisadi unaotendeka. Na tatizo kubwa zaidi ni pale anapodai ushahidi wakati mikataba yenyewe ni ushahidi tosha! Huyu JK haamini hadi leo kwamba Msabah alikuwa fisadi na kauza nchi ktk mkataba wa Richmond.. pamoja na kwamba ilikuwa ni lazima atolewe kafara. Hiyo inamuuma hadi kesho kwa sababu anaamini hakuna ufisadi ulotendeka.

Nyerere hakuamini kabisa kwamba Mkapa alikuwa akitaka kuuza miundo mbinu yetu kwa wageni akitumia neno kubinafsisha toka alipoingia madarakani. Kutoamini kwake ndiko kulikomwachia nafasi Mkapa akaja yafanya madudu yote baada ya kifo chake!..Na Mkapa aliweza cheza karata kuonekana kiongozi anayejali sana maslahi ya taifa letu kwa kuweka report za kina Warioba dhidi ya rushwa ndogo ndogo.
Kumbuka wenzetu nchi za magharibi wanaposema Kubinafsisha sio lazima kuuza mali hizo kwa watu binafsi ama wageni bali kuziweka miundombinu ktk usimamizi wa makampuni binafsi (contracting) na sio kuuza hata umilikaji wa miundo mbinu. Mara nyingi neno hili kubinafsisha tumelitumia vibaya na Mkapa knew kuwa ndio njia pekee ya kujipatia Utajiri! Kule Bcstimes mwaka 2002 niliwahi kusema kwa nini tusiziweke miundo mbinu yetu ktk contract na wageni kama tulivyowahi fanya katika mashamba ya mkonge, kahawa, sukari n.k na tukaweza kuzidisha production kishenzi ktk muda mfupi sana hadi pale Nyerere alipojaribu kubadilisha uongozi toka kwa wageni kuwapa Wadanganyika wenye njaa na elimu ya kuiga!..

Binafsi naamini kwamba JK ni innocent in a sense kwamba yeye hachukui kitu isipokuwa kawawezesha watu wengine kuhujumu uchumi wetu kama alivyokuwa akifanya mwl. Nyerere. Tofauti kubwa kati ya Nyerere na JK ni kwamba Nyerere alikuwa akifichwa ufisadi wote unaotendeka na ndio maana baadhi ya viongozi wetu Utajiri wao umekuja onekana ghafla baada ya yeye kuondoka na wengine wamekufa wakiwa maskini kwani kulingana na Ujamaa wengi wetu tuliamini kuwa Tanzania hakuna mafisadi ndani ya serikali ila ni wahindi na wageni toka nje!. Imani ambayo Mugabe pia anajaribu kuijenga kwa Wazimbabwe!
On the other hand Mkapa namuogopa sana kuliko kiongozi yeyote kwa sababu mtu huyu alikuwa na sifa zote za Utawala na mambo mengi yamepitia mezani kwake. Kaweza kuitumia elimu yake dhidi ya maslahi ya Taifa. Wee kionmgozi kuweza kufungua kampuni yake Ikulu sii mchezo mdogo, yaani kafunga record ya uongozi wa demokrasia duniani isipokuwa ule wa Monarch na Kijeshi.
 
Mkapa atabaki kuwa ni mmoja wa viongozi wazuri Tanzania amepata kuwa nao. Amechukua madaraka nchi ikiwa imeoza mpaka kwenye msingi, akasimamia vizuri makusanyo ya kodi, ndani ya muda mfupi wa utawala wake nchi baada miongo mingi ikiwa na uwezo wa kulipa madeni ya ndani na nje hii akapelekea wahisani wakashashishika na kutufutia madeni mengi.

Mkapa ameboresha vipato vya wafanyakazi wa serikali ambako watu wengi walikuwa hawataka kufanya kazi, ameboresha pia vitendea kazi makazini maofisi ya serikali yakaanza kupakwa rangi na kuwekwa fanicha zenye hadhi, usafiri magari ya serikai ndio yalikuwa yanaongoza kwa ubovu ktk utawala wake serikali imenunua magari yenye hadhi.


Mkapa amerejesha heshima ya nchi ktk kilinge cha kimataifa, mfano wa video iliyowekwa na ndugu yetu Nyani ni ushahidi tosha wa performance yake into international arena.


Kama binadamu na kiongozi kuna mapungufu hilo halina shaka, lakini kama tukiwa wakweli wa nafsi zetu tukipima mazuri na shortcomings za huyu jamaa mazuri yana outweigh mapungufu kwa wengi kabisa.

Ikiwa Mkapa alikuwa kiongozi fisadi kama tunavyolazimishwa tuamini hapa, basi naamini neno FISADI halina maana, na Tanzania hata akiletwa mtume kuongoza tutamuona ni fisadi
 
Kama Mkapa, ha-fit ndani ya neno FISADI, basi hilo neno halina maana yoyote kwangu binafsi,

mambo yote uliyoyasema mkuu kuwa Mkapa ameyafanya kwa Tanzania, hayana tofauti kubwa sana na Clinton aliyoyafanya US, lakini mkuu huyo ametoka urais akiwa lamost hana hata senti moja, ni baada tu ya kutoka urais ndio ameanza kukusanya hela kwenye speech na vitabu,

Hakuondoka akiwa amajenga mahekalu Sea View, Msasani, Osterbay, Lushoto, SA, magorofa ya kupangisha Msasani, na sasa Ilala, benki mpya Bank M, Kiwira, Netgroup, the best of all akatuachia kina Karamagi,

Kama huyo mkuu Mkapa, hafafanani na neno FISADI, basi sitalitumia neno hilo tena!
 
Masatu kula 5,
Hapa JF kuna tradition ya kuangalia upande tu mmoja wa Shilingi...kukusoa tu zaidi!
Hapo nyuma kidogo nilitoa maoni tumwangalie BWM kwa ujumla wake..watu wakasema BWM ni mlafi! Well...wengi hapa JF tumekuwa tunalaumu mno.. yaani ni vigumu kuona chembe ya mazuri ya BWM!
I am yet to be convinced kama BWM alikuwa mbaya kiasi hicho.. so what was the alternative? Mara Mwinyi hakuweza.. BWM alikuwa mlafi.. sasa JK msanii! Well hii atitude saa ingine sii nzuri.
Kwa maoni yangu BWM is a better president than JK.. pamoja na mapungufu yake!
Nabii huwa hasifiwi nyumbani!
 
Back
Top Bottom