Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Masatu kula 5,
Hapa JF kuna tradition ya kuangalia upande tu mmoja wa Shilingi...kukusoa tu zaidi!
Hapo nyuma kidogo nilitoa maoni tumwangalie BWM kwa ujumla wake..watu wakasema BWM ni mlafi! Well...wengi hapa JF tumekuwa tunalaumu mno.. yaani ni vigumu kuona chembe ya mazuri ya BWM!
I am yet to be convinced kama BWM alikuwa mbaya kiasi hicho.. so what was the alternative? Mara Mwinyi hakuweza.. BWM alikuwa mlafi.. sasa JK msanii! Well hii atitude saa ingine sii nzuri.
Kwa maoni yangu BWM is a better president than JK.. pamoja na mapungufu yake!
Nabii huwa hasifiwi nyumbani!


Ukishaingia kwenye ufisadi hakuna fisadi nafuu hawa wote ni vibaka sawa na wale wanaoiba kuku pale manzese au sehemu nyingine yoyote. Kuna mwizi nafuu kwa yule aliyeibiwa?
 
Mapungufu ya Muungwana so far ni kuwakumbatia viongozi wabovu, hayo ninayakubali kuwa ni mapungufu,

Mapungufu ya Mwalimu, ni kuwa na vision ambayo haikuwa realistic, yeye na Muungwana, sio wezi, kwa hiyo ninayakubali mapugnufu yao,

Isipokuwa kama mapungufu ni wizi wa mchana wa Mkapa, na kumuita kiongozi wa kimataifa Salim Ahmed Salim, kuwa ni mwarabu kwa sababu tu anagombea urais wa Tanzania, basi sitalitumia neno hilo tena, la mmapungufu!
 
Mapungufu ya Muungwana so far ni kuwakumbatia viongozi wabovu, hayo ninayakubali kuwa ni mapungufu,

Mapungufu ya Mwalimu, ni kuwa na vision ambayo haikuwa realistic, yeye na Muungwana, sio wezi, kwa hiyo ninayakubali mapugnufu yao,

Isipokuwa kama mapungufu ni wizi wa mchana wa Mkapa, na kumuita kiongozi wa kimataifa Salim Ahmed Salim, kuwa ni mwarabu kwa sababu tu anagombea urais wa Tanzania, basi sitalitumia neno hilo tena, la mmapungufu!

Babu inaonekana una personal beef na Mkapa...am I wrong?
 
Kama Mkapa, ha-fit ndani ya neno FISADI, basi hilo neno halina maana yoyote kwangu binafsi,

mambo yote uliyoyasema mkuu kuwa Mkapa ameyafanya kwa Tanzania, hayana tofauti kubwa sana na Clinton aliyoyafanya US, lakini mkuu huyo ametoka urais akiwa lamost hana hata senti moja, ni baada tu ya kutoka urais ndio ameanza kukusanya hela kwenye speech na vitabu,

Hakuondoka akiwa amajenga mahekalu Sea View, Msasani, Osterbay, Lushoto, SA, magorofa ya kupangisha Msasani, na sasa Ilala, benki mpya Bank M, Kiwira, Netgroup, the best of all akatuachia kina Karamagi,

Kama huyo mkuu Mkapa, hafafanani na neno FISADI, basi sitalitumia neno hilo tena!

Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu toleo la pili ya Taasisi ya uchunguzi wa kiswahihili neno FASIDI limetafsiriwa hivi;

Fisadi nm (ma-) mtu mbaya; mtongozaji, mharibifu, mpotevu, mwasharati kv Guberi.

Kwa msingi wa tafsiri hiyo hao juu nashindwa namna Rais wer=tu mstaafu huyu ana fit vipi ktk bill.

Hata hivyo labda tu nikushukuru kwa kufananisha utendaji wa rais wetu mstaafu na utendeaji wa Clinton ukiondoa tofauti hiyo ya "mahekalu" uliyo ya orodhesha.

Labda tuzungumzie kidogo hayo "mahekalu" ni kweli Rais mstaafu ana nyumba Sea view ( mkopo wa TIB ) ana nyumba Lushoto na Upanga. Ama kuhusu Benki sidhani kama Benki ikipanga ktk nyumba yako na wewe unakuwa mmiliki wa nyumba hiyo! hayo ya Ilala ni hadithi ninayo ifafanisha na ile hadithi mashuhuri ya Sitti Mwinyi mke wa Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi ambaye tuliambiwa RAHA tower yake, Sea cliff yake nk.

Lakini kubwa tujiulize hivi kuwa na nyumba ni dhambi? hivi wewe huna nyumba? kama huna hivi Mzee wako hana nyumba? mjomba wako hana nyumba? shangazi nk je nao ni mafisadi?

Mkapa amekuwa ktk utumishi wa serikali kwa zaidi ya miaka 40 mkewe nae amekuwa akifanya kazi, na ktk miaka kumi ya urais wake hivi akiwa na nyumba ni fisadi? Mwinyi kule Zanzibar ana nyumba zipo pamoja takriban 5 nae fisadi?

Ukitazama kwa makini maan halisi ya hili neno nadhani waandishi wana lipotosha kwani asili ya neno hili ni la kiarabu (Fasad) na maana yake hasa ni mharibifu napata taabu kuamini baada ya utumishi uliotukuka wa taifa hili kwa zaidi ya miaka 40 Mzee Mkapa anaitwa fisadi! Labda tusubiri afe kama Nyerere ndio tutaanza kusema mazuri yake.

Kweli haya yanapatikana only in Tanzania...
 
Masatu na MzalendoHalizi,
Ndugu zangu bado kabisa nyie mnakosea kuitazama shilingi hii. Nadhani Field marshal Es kaeleza vizuri sana!...
Mapungufu ya Muungwana so far ni kuwakumbatia viongozi wabovu, hayo ninayakubali kuwa ni mapungufu,

1. Mapungufu ya Mwalimu, ni kuwa na vision ambayo haikuwa realistic, yeye na Muungwana, sio wezi!
Kwa hiyo mjomba tuwatazame kwa sura zao na hakuna mtu atakayepinga na kudai maneno haya ni ya Uongo..
On the other hand Mkapa alikuwa Mtawala fisadi kiasi kwamba hizo sifa zote ulozisema ni ktk ujenzi wa ngome zake za kutibia. Ikiwa umeweka system nzuri ya kukusanya kodi basi kusiwepo na nafasi ya asilimia 40 ya makusanyo hayo kwenda mifukoni mwa watu wachache (viongozi) na kuwatangazia watu mafanikio.
Wakati wa Nyerere tulikuwa Wajamaa na maswala ya kodi yalichukuliwa kama mbinu za kikoloni na Ubepari. Tulipiga marufuku uingizaji wa bidhaa toka nje na hatukuwa na soko huria ambalo ndio sababu kubwa ya ongerzekpo la pato la taifa. Sii tanzania peke yake nchi yeyote iliyojichanganya ktk mfumo huu wa soko huria wameweza kukusanya kodi zaidi ya wakati wa Ujamaa.
Kodi ni part ya Principal za uchumi ktk utandawazi na soko huria. Hii ndio tofauti kubhwa kati ya Ujamaa ambpo serikali ndiye mwenye mali hahitaji kulipa kodi na Utandawazi na soko huria, serikali hubakia kama mweka sheria na mikakati kuwawezesha wananchi kuendesha biashara kwa hiyo pato la serikali linategemea kodi tu tofauti na Ujamaa ambapo ni serikali huwa mfanyabiashara. Mkapa came during the transition kwa hiyo lazima upime Uongozi wa mtu kulingana na mazingira. Sidhani kama Mkapa angeweza kuwa kiongozi bora kwa sifa ulizompa kama tungekuwa Wajamaa!
Pili, sio Mkapa aliyebadilisha mfumo wa siuasa zetu kutoka Ujamaa hadi kwenda sokohuria kiasi kwamba tunaweza kumpa sifa ya kuwa na vision. Mbali na hapo IMF wamehusiaka kwa kiwango kikubwa kupanga mfumo wa Ukusanyaji wa kodi na sio akili yake ama baraza lake ila the good thing ni kwamba he knew exactly what he planted! ... kuvuna kwake kulikuwa rahisi kwa sababu aliweza kuwapumbaza wengi kati yenu.

Kwa hiyo wajomba mtaona kwamba sio tu nimebisha hoja yenu na kumtangaza Nyerere ama Mkapa bila kuonyesha nachokizungumza dhidi ya hoja zenu.
 
Masatu,
Neno Fasidi na Fisadi nadhani yanatofautiana kwa maana!
Fisadi ni mnafiki, mtu wa fitna, mbinafsi mwenye kutumia watu kuficha mabaya yake!
Sijui kama kamusi inasema hivyo pia.
 
Kilio changu kwa huyu mzee ni kwenye madini, alituuza bila huruma..aligawa mali ya taifa kwa marafiki zake akina Andrew Young(barick). Nashindwa kuelewa akionekana kama anautambuzi wa mambo lakini alifanya kama mbumbumbu! Kweli huyu mzee alikuwa nyoka.
Mkandara na wenzake wamemuelezea vizuri mpaka nami nimejisikia kumuoelwa huyu mtu; maana nilikuwa najiuliza huyu jamaa ni mbumbu au vipi? Kumbe TAPELI!!!! sawa kabisa...lakini alimsaliti baba yake JK nyerere.
 
Mkandara,
1. Nimekutana na watu wengi wa nchi zingine hata huku majuu wanampa 5 BWM..wazungu kwa waafrika..kusini na kaskazi! "That Tz we have wonderful leadership on that seed planted by Mwal. until today..they actually seem to admire us- as a nation" Sasa sisi tumekuwa tunalaumu tuuuuu! Je hatuoni mazuri kujivunia?

2. BWM hakuwa Mungu- ni mwanadamu. Kukumbatia wala rushwa- na yeye kuwa mwizi -mimi sina ushahidi- ushahidi uliotolewa hapa ni wa kimazingira. Kwamba ana nyumba 2 au 3- Masatu ametoa maelezo.
Kamata kamata walarushwa- as a president you need social harmony ili uweze kutawala. May be ndo maana hata JK anasita kukamatakamata bila ushahidi tosha. JE wapi hiyo kamakamata in SSA imeleta matokeo haraka?

3. Ana mapungufu..BWM na sii malaika. Ila mimi kwa kifupi, I was and I am stil proud of him!
 
MzalendoHalisi,
1. Umesema umekutana na watu hapo ulipo, Wazungu kwa weusi wakimpa sifa Mkapa.... Sasa umewahi kujiuliza kama watu hawa wamewahi kufika Tanzania ama wamewahi kusoma magazeti ya tanzania na kadhalika?. Jibu ni Nooo! hawa jamaa wanasoma toka magazeti ya Ulaya ama wametokea kukaa na kumsikiliza TAPELI at his best - ktk hiyo mikutano akizungumzia maswala ya nchi maskini na wapi Tanzania leo imesimama According to.....

Mzalendo Utapeli hata Wazaire ama Wapopo (African Pimps) huvaa masuti na kama ujuavyo dada zetu hawaoni ndani kwa hawa jamaa hadi siku mambo yatakapo jitokeza kiukweli huwa wameisha chelewa!.. wameachiwa watoto na Mpopo kenda kuoa kwao Nigeria ama Ghana!..
2. Ni kweli unashindwa kuona Ubaya wa Mkapa ama wizi wake kwa sababu kuna msemo usemao ukikubali kutapeliwa basi mkosa ni wewe!..Nadhani unachofanya wewe ni kujilaumu wakati wewe ni victim!..tumekumbwa na depreciation ya umaskini kiasi kwamba hatuoni nje ya sisi wenyewe kuwa ndio sababu.
Kumbuka unamtazama Mkapa kama yule Mpopo alomwacha dada yetu na mimba kenda kuoa kwao. He has all the right under the sun to choose who he should live with!...
Hao watoto wewe huoni kama ni hasara ila ni faida kwa binti..nikiwa na maana mifano yote alokupa Field Marshall ES bado huoni tatizo bali ni Mtaji mzuri kwa wananchi na taifa kwa ujumla. Rais akiwa tajiri nchi inafaidika pia!
Kama nilivyosema I can't get worse than operating an office from the Whitehouse!
3. Nakupa mtihani mdogo sana nenda Dar jaribu kuhesabu Sophia House anazoweza kuziona kisha rudi tuendelee na mazungumzo!
 
Fisadi ni mnafiki, mtu wa fitna, mbinafsi mwenye kutumia watu kuficha mabaya yake!
Sijui kama kamusi inasema hivyo pia.


Mkuu Bob,

Ahsante sana mkuu kwa ufafanuzi zaidi wa maana ya neno FISADI, kwa kuongezea tu tatizo la nchiyetu sasa hivi sio viongozi wenye mapungufu, tatizo ni baadhi ya viongozi wezi,

Mkapa, alikuwa na akili sana za darasani na za kuzungumza kwenye mataifa ya nje, lakini sijui kama mwananchi hata mmoja wa bongo aliyekuwa akimuelewa, Mkapa amefaanya kazi serikalini kwa miaka 40, haiwezi kuwa sawa na miaka ya urais wa Mwalimu 28, years, can you imagine Mkapa angekuwa rais kwa miaka 28, ingekuwaje?

Ninaomba mtu mmoja anitajie mali za Mwinyi, alizozipora akiwa rais? Sasa haya magazeti ya Thisday na Kulikoni yanamsingizia Mkapa kuwa hakuiba kwenye Radar na IPTL, na kwenye ile minofu ya samaki ya Mwanza vipi harufu ya rushwa inamkuta waziri tu?

Kama nina chuki ya binafsi na Mkapa, kama alivyoshauri mujumbe mmoja huko nyuma basi huenda ninayo pia na Karamagi, mimi ni mmoja wa watu niliokuwa ninamtetea Mkapa to the end not knowing kuwa ni simply ni mwizi,,nenda kule BCS utakuta jinsi nilivyokuwa ninamsimamia, I mean kwa nchi kama Tanzania huwezi ukalimbikiza mali kiasi alichokifanya in 10 years, ni kufuru hata kwa Shetani, licha ya Mungu. Unajua hata bwawa la Mtera, limemalizwa na kijana Peter, wataalamu walikuwa wakisema maji hayatoshi yaachwe kwa muda, kijana anpiga simu Ikulu, wanambiwa waendelee tu leo umeme ni kwa mgawo kisa Mkapa na familia yake,

Dr. Slaa na Zitto, wanatuambia kwa ushahidi kuwa viongozi wetu ni wabadhirifu wa mali ya walipa kodi kama hayo matatizo ya ubadhirifu ni madogo kiasi cha kuitwa mapungufu, then kwa nini tunapoteza muda wa wananchi na maandamano ya mkataba wa Buzwagi? Kwa nini serikali inafanya uchunguzi BOT wakati gavana anatuhumiwa kwa mapungufu tu ya kibin-adam?

Mapungufu is one thing, na wizi is another Mkapa ni simply mwizi na mbadhirifu na fisadi pia, ila sioni tatizo kwa mwingine akiwa intellectual na kiongozi bora ambaye Tanzania hatujawahi kuwa naye tena, wakati umefika wa Muungwana kumuachia Mkapa afikishwe mahakamani kujibu mashitaka yaliyokwisha tolewa na magazeti ya rafiki yake mpenzi wa zamani Mengi!
 
Naona sasa unageuka ushabiki wa kimpira mpira. Napenda kusisitiza kwa mujibu Kamusi ya Kiswahili Sanifu toleo la pili ya Taasisi ya uchunguzi wa kiswahihili neno Fisadi limetafsiriwa hivi;

Fisadi nm (ma-) mtu mbaya; mtongozaji, mharibifu, mpotevu, mwasharati kv Guberi.

Sasa kama kuna mtu mwenye maana tofauti na hiyo atupe chanzo chake na yeye ndio komkoma nyani kwenyewe huko.

Ama kuhusu nyumba za Sophia hayo ni mazungumzo baada ya habari, majengo haya yamekuwa miaka kenda.

Anaweza kuwa na mapungufu mengi Mkapa lakini kumwita fisadi ni below the belt.
 
Masatu,
Unajua mjomba hata unapobisha basi kuwa na basis! unaposema majumba ya Sophia yalikuwepo toka miaka kenda una maana gani? kuwa hayo majumba yamejijenga yenyewe au kwa sababu yalikuwa ya serikali na leo yana mmiliki haipotoshi maana ya kuwa yamenunuliwa kihalali. I mean jaribu kutpa maelezo yenye mwanga kiasi kwamba hata sisi tuweze kuondoa shauku ama kupima madai yenu. Mnatuacha wazi mkichambua maneno ya upande wa pili tu lakini kinachoendelea kwa Mkapa hamtaki kusema. How he got rich hakuna hata mmoja wenu anayefahamu, yet bado mnatetea kitu msichokifahamu, nashindwa kabisa kuelewa!

Kisha mjomba kiswahili lugha yako ikiwa wewe umefikia kutazama kamusi ili kusimamia hoja yako basi mjomba hatuwezi fika na hizi cook book!.. jaribu kutoa nje ya kabati na kufikiria matumizi ya neno Fisadi ktk kiswahili zaidi ya hapo tazama maneno yote uliyoyasema hapo juu hayana uhusiano moja baada ya jingine. Mtongozaji hawezi kuwa ni sawa na mpotevu, mwasherati n.k. Mwandishi kayachukulia haya kama ni mambo mabaya kwa hiyo yule ayafanyaye ndio huitwa fisadi. Hatuhitaji kamusi wala cook books kama Kanye West alodanganywa maana ya Kanye kwa kiswahili ina maana U are the One na tafsiri imeandikwa ktk kitabu chao!..
 
Kaka Mkandara basi tusaidie mmiliki wa Sophia house ni nani mbona unazunguka zunguka tu.

Sanjali ni hili tafsiri ya fisadi nimeitoa kutoka kwenye kamusi sasa wewe ya kwako umeitoa wapi mbona hili dogo sana. Mimi sikatai kuwa kunaweza kuwa na maana nyingine kama uliyotoa lakini tusaidie source yako basi.
 
Anaweza kuwa na mapungufu mengi Mkapa lakini kumwita fisadi ni below the belt.

Ameitwa mfisadi kwanza na Dr. Slaa, kabla ya hapo ameitwa mwizi na magazeti ya rafiki yake mpenzi Mengi, Thisday na Kulikoni, sasa hawa nao ni part ya JF ambako tunadaiwa kazi yetu ni kuangalia upande mmoja tu wa ishus?

Wizi ni wizi, mapungufu ni mapungufu, kilichofanyika kwenye mkataba wa Radar na BOT, sio mapungufu ila ni wizi wa mchana kweupe, ndio maana mpaka mabalozi wa nje wanadai criminal investigation ifanyike kabla hatujaanza kukosa misaada yao, maana aliyoyafanya Mkapa ni wizi, na aliyoyafanya Mwalimu ndio hasa mapungufu!

Lakini wezi ni mafisadi, hata wawe intellectuals kama Mstaafu!


If anything, sasa hivi ninaanza kuamini kuwa huenda Sumaye, hakuwa na madhambi ya wizi kama tulivyokuwa tukiambiwa maana simuoni kwenye orodha na kwenye Thisday/Kulikoni, kwa hiyo tutaendelea kutafuta ukweli kuhusu Sumaye.
 
Ameitwa mfisadi kwanza na Dr. Slaa, kabla ya hapo ameitwa mwizi na magazeti ya rafiki yake mpenzi Mengi, Thisday na Kulikoni, sasa hawa nao ni part ya JF ambako tunadaiwa kazi yetu ni kuangalia upande mmoja tu wa ishus?

Wizi ni wizi, mapungufu ni mapungufu, kilichofanyika kwenye mkataba wa Radar na BOT, sio mapungufu ila ni wizi wa mchana kweupe, ndio maana mpaka mabalozi wa nje wanadai criminal investigation ifanyike kabla hatujaanza kukosa misaada yao, maana aliyoyafanya Mkapa ni wizi, na aliyoyafanya Mwalimu ndio hasa mapungufu!

Lakini wezi ni mafisadi, hata wawe intellectuals kama Mstaafu!

Slaa na magazeti ya mengi wako entitled kwa maoni/mitazamo yao sanjali na wewe na wa JF kwa ujumla, lakini ukweli utabaki kuwa the guy has done commendable job
 
Ni kweli ndio maana Thisday/Kulikoni wamemfahamisha kuwa wako tayari kwenda naye mahakamani at anytime akitaka,

ni kweli alifanya commendable job, ya kujificha uwizi wake you got that right, lakini hakuna siri za wizi, hao Thisday/Kulikoni wanamsubiri at anytime akiwa tayari.

Haya chini, ndio tunaita mapungufu:-

However, Nyerere's critics, particularly those from the Western corporate media, the International Monetary Fund and the World Bank, claim that because Nyerere focused on domestic needs such as health and education that he was naive. These critics argue that because he valued regional unity above Western individualism that he was misguided. They argued that because he chose self-reliance as the guide to development rather than go hat in hand to beg for high-interest rate loans from the World Bank, that he destroyed the economy. Those IMF executives were not accustomed to seeing a national leader riding in an old car rather than a shiny new Mercedes through the capital city without a motorcade, with only a single driver, stopping for red lights. Nor was Wall Street impressed by the fact that Nyerere gave military assistance to African freedom fighters throughout southern Africa, fighting to end western economic domination and apartheid. Another category of critics from within the freedom struggle, claim that Nyerere went too slow and allowed too much Western influence, and did not take seriously the requirements of building socialism. One of the spokesmen from that group is the late Tanzanian Cabinet Minister, Muhammad Babu, also a noted revolutionary African leader and author of African Socialism or Socialist Africa?. These are important debates for the new millennium that also has major relevance to community activists considering post industrial development in urban and rural America. History will judge.
 
Ni kweli ndio maana Thisday/Kulikoni wamemfahamisha kuwa wako tayari kwenda naye mahakamani at anytime akitaka,

ni kweli alifanya commendable job, ya kujificha uwizi wake you got that right, lakini hakuna siri za wizi, hao Thisday/Kulikoni wanamsubiri at anytime akiwa tayari.

Haya chini, ndio tunaita mapungufu:-
However, Nyerere's critics, particularly those from the Western corporate media, the International Monetary Fund and the World Bank, claim that because Nyerere focused on domestic needs such as health and education that he was naive. These critics argue that because he valued regional unity above Western individualism that he was misguided. They argued that because he chose self-reliance as the guide to development rather than go hat in hand to beg for high-interest rate loans from the World Bank, that he destroyed the economy. Those IMF executives were not accustomed to seeing a national leader riding in an old car rather than a shiny new Mercedes through the capital city without a motorcade, with only a single driver, stopping for red lights. Nor was Wall Street impressed by the fact that Nyerere gave military assistance to African freedom fighters throughout southern Africa, fighting to end western economic domination and apartheid. Another category of critics from within the freedom struggle, claim that Nyerere went too slow and allowed too much Western influence, and did not take seriously the requirements of building socialism. One of the spokesmen from that group is the late Tanzanian Cabinet Minister, Muhammad Babu, also a noted revolutionary African leader and author of African Socialism or Socialist Africa?. These are important debates for the new millennium that also has major relevance to community activists considering post industrial development in urban and rural America. History will judge.




MZEE NAOMBA SOURCE
 
Back
Top Bottom