1.
Uzalendo ni nini? Hivi ni kweli unaishia ktk uandika makala online,magazetini TV au ? Uko wapi Utanzania wenu,mnamwita mwizi,fisadi,jeuri na wengine mnamwita mjivuni sawa tumewasikia,what next?
What is next, ni tunamuomba kila wakati rais wa sasa aruhusu kufunguliwa mashitaka kwa mhesshimiwa mstaafu Mkapa, na hasa kuhusiana na ununuzi wa Radar, ambao hata Waingereza wenyewe waliotuuzia wanadai kuna uhuni umefanyika, it is the matter of time kabla siku moja mkulu hajatinga mahakamani, mara ya mwisho aliandikiwa Mkuu Hosea, akasema kuwa sheria hairuhusu so far, kwa hiyo ishu haijafa bado iko hai na yeye mwenyewe analijua hilo sana, uzalendo sio lazima upigie kelele maovu ukiwa nyumbani, Ayatolahh Khomein, alipiga kelele akiwa France for at least 16 years, siku moja akarudi kuiongoza Iran, ambayo mpaka leo bado inafuata nguzo za uongozi wake, if the uzalenmdo thing is an ishu, kwa sababu sihitaji kuwa mzalendo kumsifia Zitto, na Dr. Slaa, au kumuuliza Mkapa alipataje mali zote alizonazo in 10 years, tena the matter of fact in 6 years baada ya kifo cha Mwalimu 1999? Je mabalozi wa nje waliopo bongo wanaouiuliza serikali kuhusiana na orodha ya mafisadi, how do you describe them as far as this uzalendo thing is concerned?
2. [
B]Who told u Mengi ni rafiki wa Mkapa? And why not Msuya?[/B]
This one ni kutokana na maneno yake mwenyewe in private, kuwa "....hata Mengi who I thought to be my friend....", viongozi wote wa juu huwa ni marafiki wa kawaida wa Mengi, akiwa rais alikuwa akisafiri na huyo mkuu kila wakti kwenye ndege yake binafsi, je mkuu umeshawahi kusaifiri na Mkapa kwenye ndege yake binafsi akiwa rais kama Mengi? Mengi alikuwa hata rafiki wa Mwalimu pia, what is wrong with that? Hivi ninahitaji kuambiwa na mtu kuwa rais hawezi kusafiri na mtu yoyote kwenye ndege yake binafsi unless ni kiongozi mwenzake au kama ni Mengi, kama Mkapa alipvyokuwa akifanya basi ni rafiki yake?
3.
Huenda tupo hapa kuwaangalia wenzetu tu lakini vivuli vyetu vikawa vinatusumbua
;
Vivuli? Vipi hivyo? Hawa kina Adam Lusekelo wanaaoukemea ujinga wa serikali tena kwenye magazeti ya serikali hiyo hiyo wana vivuli gani hivyo? If that is the case tunafanya nini hapa forum? Basi tufunge hii forum maana kila tunalolikemea serikali ni vivuli vyetu vinatusumbua tu au? Why waste time na mkataba wa Buzwagi, wakati kumbe tatizo ni vivuli vyetu vinatusumbua? I mean pamoja na wananchi mbali mbali kutoa sababu nyingi za sisi kuwepo hapa forum, ukweli ni kwamba kazi yetu muhimu hapa inatakiwa kuwa kuikosoa serikali, in the wake ya magazeti na media zetu za taifa kununuliwa na Mtandao, na tutaendelea na tabia hiyo hiyo hapa bila kujali nani anahusika au chama gani kinahusika,
vivuli? wananchi wanaowazomea mawaziri huko mikoani na vijijini wanasumbuliwa na vivuli gani mkuu? Makamba anpowatukana wapinzani bongo anakuwa anasumbuliwa na kivuli kipi Mkuu?
4.
Nina mashaka na uzalendo wetu huu,rudini hapa TZ muungane na hao waandishi na magazeti mkamshitaki tujue moja kuwa kweli sasa haki itatendeka kwa walio wengi
Uzalendo kwako ni kuikosoa serikali ukiwa bongo tu? Sasa kina Seif Khatibu, wanahangaikia nini kuzungumzia tuhuma kwenye Redio za kina MMJ walioko nje? Kwa nini rais wetu anafungua tawi la CCM London, wakati kwa your thinking wananchi walioko nje sio wazalendo, isipokuwa walioko bongo tu? What a hoja?
Kuhusu kushitakiwa, hilo halina haraka ukweli upo kuanzia IPTL, Radar, Ndege ya Rais, Mikataba ya madini, it is only a matter of time tu mkuu atatinga mahakamani, kinachihitajika kubadilika ni upepo tu wa siasa, viongozi kama Sozigwa hawana hayo matatizo ya kuishi kwa wasi wasi kama mstaafu wetu, maana hata na yeye anajua kuwa wafadhili wakiweka mguu chini ashitakiwe anakwenda na maji, kwenye hilo mkuu muulize Taylor Wa Liberia kilichomtokea, wengine wakinyolewa ni vyema kuanza kuweka maji tayari!
5.
JF iachane na mitizamo binafsi juu ya watawala,
JF kama chombo cha media kilicho huru na kilichoandikishwa kisheria, hakihusiki na mawazo yako binafsi, wala ya kwangu kwa hiyo tuwe waangalifu na hilo mkuu in the future, JF isilaumiwe kwa mawazo ya watu binafsi!
6.
niliwahi kuyaona maoni ya binadamu mmoja humu,alishauri ni vema tukawaiga Wamarekani,When ur through with presidency, to them u become the saint
Ingekuwa ni kweli Clinton asingenyang'anywa Licence ya uwakili wa binafsi, baada ya kutoka urais kwa ajili ya kesi yake na Monica, hii hoja si kweli, Nixon alipewa alternatives, kati ya kushitakiwa akiwa rais au kujiuzulu hatashitakiwa, akachagua kujiuzulu kwa hiyo na hii hoja ni hafifu kama haipo kabisaa, huko Us ndio hawataki mchezo kabisaaa, ndio maana ilibidi Clinton amlipe dola laki saba Bibie Jennifer Flowers baada ya kutoka urais, kwa kulazimishwa na sheria!
7.
na ndiyo hoja ya JK,ukiweza kupita tanuru la mamlaka pasipo kugunduliwa na kushitakiwa basi wewe ni mstaafu bora wa jumba jeupe;He is out of Magogoni house,he is the third saint from Magogoni,mwacheni akapumzike,mkubalini ni rais wenu wa tatu,ndiye mwenye nuru na wakubwa duniani hilo halina ubishi
,
Idd Amin, aliwezaje kuwa mwenyekiti wa OAU, ni kwa sababu alikuwa ni rais wa Uganda na alikuwa na nuru na wakubwa, je inapunguza nini kuhusiana na uwezo wake mdogo wa uongozi akiwa rais? Savimbi na Mobutu je hawakuwa na nuru na wakubwa wa dunia, au Botha na Smith, je hawakuwa na nuru na wakubwa? Je umesahau kuwa Osama naye pia alishawahi kuwa na nuru na wakubwa USA ambao ndio hasa waliomtengeneza kuwa what he is today? Kwa nini na hwa tusiwakubali kuwa ni walikuwa na nuru kama Mkapa na wakakubalika na wakubwa wetu USA na UK?
8.
kama tunadhani tuko sahihi kuendelea na kuwa This day na kulikoni basi ni vema tuwaulize wakubwa wa sasa kama waliweza kudhibiti media zote juu taarifa ya Slaa walishindwa vipi kudhibiti taarifa za Kulikoni na This day? Wana agenda yao ya kumzima Ben Mkapa lakini bahati mbaya hawajui madhara ya zoezi hilo,sidhani kama Ben alizuia ripoti ya Warioba kwa hofu au shinikizo la Mwalimu tu,kuna mengi yanafanyika ila hamtaki kuyasema.
Aliyemchagua Warioba na kamati ya rushwa alikuwa Mwalimu au Mkapa? Mwalimu anahusika vipi na taarifa ya uchunguzi wa Warioba kutotolewa to the public? Na Warioba kwa nini hakwenda Elimu na Sayansi kwa swahiba? Leo maswahiba wakubwa under Mwalimu, kwa nini Warioba na Mkapa hawaelewani tena? Thisday/Kulikoni kama kweli yana shida ya kuharibu sifa za Mkapa kwa kuhsinikizwa na Mtandao, then kwa nini yanamtwanga Gavana na Mbunge Mkono pia? WHY? Ni nani anyesema kuwa taarifa za DR. Slaa zilidhibitiwa? Mbona wananchi tunazo? Mbona makataba wa Buzwagi kila mwananchi anao?
Ni dhana potofu sana kwamba wananchi wakimjadili rais wao wa zamani basi wanajiunga na Mtandao kumuangamiza rais wa zamani, hapana, hapa forum sijui ni ishu gani ambayo wananchi wamewahi kuikwepa, na kama tunatumiwa na Mtandao basi hawafanyi kazi nzuri, hebu angalaia topic zote humu forum uniambie kuwa tunatumiwa na Mtandao, another joke!
9.
The only way to delete Ben is by kuvunja rekodi zake na maaskari wake makini wa miavuli,Lowasa hatasahau kuachwa kwake ktk baraza 1995-97 licha ya kuwa Alhaj Mwinyi aliwaombea kazi mbele ya wajumbe wote Mkutano mkuu wa CCM,kumbuka kauli yake ya kwanza juu ya matatizo ya umeme -
Kwanza Mkapa, ana bahati kubwa sana kwamba we gave him a big chance akiwa rais hatukumtwanga sana, kwa sababu he was smart enough kutudanganya mapaka alipoondoka ndio ukweli ukaanza kupatikana, as opposed na serikali ya sasa ambayo hata haijamaliza term ya kwanza tayari tunaitwanga, kwa hiyo we were more than fair kwa Mkapa na urais wake, serikali ya sasa haijavunja rekodi ya wizi wake hilo ni kweli, na pia haijavunja rekodi ya mazuri yake ambayo huwa tunaaambiwa na wazungu tu lakini sisi wenyewe wananchi hatuyaoni, sasa what that tells you kuhusu huyo rais anyesifiwa na wazungu kama kina Savimbi na Mobutu, lakini wananchi hawayaoni hayo mazuri? Maana under Mwinyi angalau wananchi walitajirika na hakusakamwa na jeshi hata siku moja, as the case na Mkapa, rekodi ipo mkuu kuwa mkuu aliwafanyiwa kazi njema wazungu kama unavyodai, hilo sijui kama litavunjiwa rekodi na serikali ya sasa!
10.
Ikulu itaongozwa na binadamu ambaye sifa yake kuu ni udhaifu ;ikumbukeni kauli ya mheshimiwa Bill Clinton
"I did not have sexual relations with that woman." - Clinton
Todate USA inamkubali kwa uwezo wake mkubwa wa kushawishi na kuthubutu ktk harakati za maendeleo.
Ohh yah! Maendeleo ya hesabu hewa ni kweli kama ya Mkapa, unayoyasifia, hivi mkuu umeshawahi kusoma undani wa kesi za kina Ken Lay na Enron? Mkuu unajua toka Clinton aondoke madarakani ma-CEO wangapi wamefungwa? Kama USA ingekuwa inamkubali kiasi hicho cha kwako basi Gore asingeshindwa mkuu, Clinton alikuwa kiongozi safi halina ubishi mana hakuwa mwizi hata siku moja, huko Us huwa hawazimii na viongozi wezi hata siku moja, ni sawa kabisa Ikulu kuongozwa na mdhaifu wa kina mama, lakini sio udhaifu wa kuiba, ndio maana tunampa heshima Muungwana na Clinton, maana sio wezi, ila hatutakuwa na suluhu na viongozi wezi hata kama ni Karamagi,
Clinton, ametoka madarakani akiwa hana hela kabisa wala mahekalu ndio maana mke wake akachaguliwa, can you imagine mke wa mstaafu wetu akigombea ubunge? Mdogo wake tu wananchi walimkataa kwa kumchukia dada mtu, sasa iweje dada mwenyewe akiingia! Clinton hawezi kulinganishwa na kina mkapa, ni matusi makubwa, mkuuu!
11.
Why not Ben William Mkapa? Kila heri waungwana
Hakuna mwenye tatizo na mkapa wala kiongozi yoyote wa nchi yetu, tatizo ni kama wamevunja sheria kwa makusudi, na sidhani kama kwenye hii forum tumeshawahi kuwa na macho ya kuchagua yupi wa kumpiga mawe, Mkapa anashambuliwa kwa rekodi yake mwenyewe, IPTL, Radar, Ndege Mbovu ya rais, mikataba mibovu ya madini, kupanda kwa gharama za uchaguzi, ni rekodi ambazo zimetokea under hsi watch, kwa hiyo hatujali sura ya mtu au kiongozi, hapa forum kila kiongozi huchambuliwa kama alivyo, nothing personal that is pure nonesense, in the future mkuu ukitaka kumtetea mkapa weka rekodi, achana na ishu za binafsi maana hakuna mwenye shida naye za binafsi hapa, na hizi hoja za ubbinafsi it is about time hapa forum tukaachana nazo,
Ahsante Tuendelee kukata ishu mkuu, ila hapa haangaliwi kiongozi wala sura yake, isipokuwa rekodi yake! Utakapokuwa tayari kurudi karibu tena mkuu!