Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Katika mailing list moja nimewahi kusoma malalamiko kuwa serikali, kupitia TCRA illiweka deadline kwa haya makampuni ya simu za mkononi kubadili namba za wateja kutoka tarakimu sita kuwa tarakimu saba, providers wote wakaonekana kujitahidi kumeet hiyo deadline (0748[XXXXXX] zikawa 078[4XXXXXX] etc).. vodakomu wakaonekana ku-take their time na mpaka deadline ikapita hawakufanya hivyo. Tukajiuliza where is this confidence coming from? Hivi vihabari vinavyoandikwa hapa vinaaashiria kunipa jibu.

Mara ya mwisho nliskia eti wangebadili kuanzia hii septemba, lakini mpaka leo nlipopiga namba za zamani bado zinapeta.
 
Ama kweli kikulacho kipo nguoni mwako. Kama viongozi wamejitengea maslahi ya kutosha kujilipa hadi dola milioni 3 wanapong'atuka, basi wabaya wetu kumbe ni hawa viongozi wetu!

Masikini, kweli possession mania waliyonayo viongozi wetu inatisha. Naomba wakumbuke haya mambo 2 ya msingi:

(1) None of us is getting out of here alive
(2) We take nothing with us.

Dola milioni 3 ni sawa na shillingi billioni 3 na milioni 750. Ni fedha za kutosha kujenga madarasa 375 ya gharama ya shilingi milioni 10 kila moja. Ulafi wa Mtanzania mmoja kuzihodhi zote unatisha.

Tunajisahau. Leo hii mtu aliyeiba mapesa nyumba nzima anaweza kupata kiharusi akajinyea hadharani, na mapesa hayo yakampotezea uzima wa milele. Fedha nyingi za wizi hazileti raha wala furaha. Fedha za kutosha, za halali, zinaweza kuleta furaha kama zikitumika kwa faida ya jamii. Zikitumika kibinafsi zinaleta raha ya kidanganyifu, ya muda mfupi, lakini haziwezi kuleta furaha. Happiness is never found in happenings.

Nazidi kuelewa kwa nini Tanzania haiwezi kutumia asilimia 27 ya bajeti yake kwenye Elimu kama ifanyavyo Kenya. Karibu nusu ya fedha za nchi zinawekwa kwenye hilo li-consolidated fund na kuibiwa, kisheria, na viongozi.

Nimalizie kwa kichekesho. Labda Mkapa ameona ukosefu wa maji na umeme Dar umemshinda, wacha ahamie bondeni. Ameona mtu aliyekuwa Waziri wake wa Maji na Ng'ombe, ambaye alishindwa kabisa kufanya chochote, sasa amekuwa Waziri Mkuu. Inatisha sana. Ameona akimbie kabla hajazimia, maana mtu mwenyewe anataka sasa kujaza mabwawa yetu kwa maji ya kufuatia kwa ndege angani.

Augustine Moshi
 
Members
Kuhusu Vodacom, naweza kuongezea kwa kuwakumbusha muda kidogo umepita. Ligi kuu ya soka ilikuwa ikidhaminiwa na safari lager/TBL. Na dau lilikuwa kubwa. Lakini mara mizozo ikaanza. Hiyooo...ikahamia kwa Vodacom kwa dau dogo. Hapo pia kunaweza kuwa na kamchezo kanakostahili kadi ya njano au nyekundu kabisa. Ama kweli Tanzania ina wenyewe.

Tibwilitibwili habari za kukaya. Sisi wengine asili yetu hukooo Mfaranyaki....nyumbi....i...bombi...i
 
Mwanagenzi said:
Nikiri kuwa japo nimekuwa nikirambaza ndani ya hili baraza kwa muda sasa, bado najiona kuwa Mwanagenzi kwa kujilinganisha na waliotangulia kujiunga na kwa michango yao mzo mzo katika mada na mijadala mbalimbali.

Mpaka sasa, nadiriki kusema kuwa baraza linavutia kwa mijadala ya wanabodi na pia malumbano, vibwagizo na vijembe vya hapa na pale, ambavyo ni kama chachandu katika pilau.

Pamoja na hayo niseme kuwa bado tuna nafasi ya kuliboresha baraza letu kwani ubora hauna kikomo.

Kwa maoni yangu, tujaribu kuepuka yafuatayo:
1. Kutuhumu na kushutumu kwa nguvu kabisa (siyo kwa namna ya mzaha) baadhi ya waanzilishi wa hoja (wachokozi) au wachangiaji kuwa ni wanachama, wafuasi, wapenzi, wakereketwa, wafurukutwa, au washabiki wa chama fulani cha siasa ilhali wao hawajatuambia hivyo. Daima tuzingatie hoja na si nani katoa hoja.

2. Kutuhumu na kushutumu baadhi ya wachangiaji kuwa "wametumwa" na kikundi cha watu fulani na hata serikali. Hata kama hilo linawezekana, na huenda baraza halina haja wala jinsi ya kulizuia, hoja iwe kuchangia, kukosoa, kupinga, kurekebisha nk "hoja", badala ya kutoa madai ya kijumlajumla. Isitoshe kwa nini mtu uamini kuwa fulani katumwa? Kwani huyo mchangiaji hawezi kuwa na mawazo yake binafsi kama wajumbe wengine? Kwani watoao madai kama hayo wao wanakuwa "wametumwa" na nani? Naamini wengi, kama si washiriki wote, barazani ni wazalendo na wana uchungu na nchi hii. Vinginevyo hatuna kipimo cha kujua nani mzalendo na nani siyo (si hata baadhi ya viongozi wa taifa letu wanaonekana kuwa si wazalendo?).

3. Kujenga dhana kuwa kuna makundi ndani ya baraza, na kwamba hoja hutolewa kwa kufuata makundi, au kuunga mkono hoja za kina fulani tu, na kupinga za wengine. Tuaminiane kuwa washiriki ni watu wazima, wenye uwezo wa kupima mantiki za michango mbalimbali, na kwamba wanashiriki barazani
kwa hiari yao, na wanajiwakilisha wao na nafsi zao.

4. Kama ambavyo imekuwa ikisisitizwa, tuepuke lugha ya matusi, na kumlenga mchangiaji binafsi badala ya hoja yake. Hoja ijibiwe kwa hoja. Kama Mwalimu alivyotuasa, "Tutumie nguvu ya hoja badala ya hoja ya nguvu, na tupingane bila kupigana", kwani sote tuna nia ya kuchangia ujenzi wa Tanzania yetu.

Kwa kumalizia , nadhani ni muhimu tupitishe kanuni na tuziheshimu. Naamini baraza hili ni bora na tusilibomoe kwa mikono yetu wenyewe!

Mungu libariki Baraza,
Mungu Ibariki Afrika,
Mungu Ibariki Tanzania!

Mawazo yako mazuri lakini naomba kukuuliza swali moja:hivi unapata fikra gani unapomsikia mtu anatetea tu ulaji rushwa,ujambazi na ubadhirifu wa nchi yetu (eg mtu anayejiita Tafiti Then Jadili) hata kama yeye pia ni mwathiriwa wa matendo haya ya kiuanaharamu?Let me tell you,kuna nyakati hatuwezi kusubiri hadi mtu ajitambulishe kuwa "ametumwa",they never say that,by the way.Kuheshimu mawazo ya mtoa/mchangia mada ni kitu kimoja,kuisoma na kuijibu/kutoijibu ni kitu kingine,as it is in ku-conclude kwamba flani ametumwa,au hajaelewa mada,au upeo wake ni finyu,au pengine ametoa mchango wake akiwa ana njaa au amelewa.🙂

Ni vizuri kuzingatia hoja iliyotolewa na si nani aliyeitoa,lakini what if kila siku mtu anatoa hoja za ajabuajabu?Jamii inamtambua mtu kutokana na mazowea yake.Circumstantial evidence inakubalika kwenye labelling of a person:na inaweza kuwa too theoretical to differentiate between hoja na mtoa hoja hasa kwa vile hoja hazitoki hewani bali kichwani kwa mtoa hoja.Logically,kama mtu anatoa hoja za kupinga tu,then what's wrong with labelling him "mpingaji".Kama "Tafiti then Jadili" ni mtetezi wa kila skendo inayoihusu serikali na viongozi wake (hata pale ambapo hana data za kutetea),then sidhani kama kuna dhambi kuhisi kuwa anafanya hivyo kwa vile aidha ametumwa na hao anaowatetea,au ni mmoja wao,au anajipendekeza,au ndio full-time job yake (msemaji asie rasmi wa serikali).

Hata hivyo,nakupongeza kwa kuitakia mema jambo forums.:-D
 
kuna sehemu gani imeandikwa mtu au rais asinunue nyumba kokote duniani?
kama hakuna evidence kuwa kala rushwa sasa whats the big deal

au kwa sababu rais MMAKONDE?
 
DrWho,

Kuna mambo mengi hayakuandikwa popote na bado hayakubaliki. Rais mstaafu wa Tanzania kununua nyumba Afrika ya Kusini ni dharau kwa Watanzania. Kama anataka kuhamia huko, basi atueleze kwa nini alipoteza muda wetu akitudanganya anaboresha maisha yetu, wakati hakuyaboresha kiasi cha yeye kukubali kukaa nasi?

Unatutawala sisi kwa nyimbo za uzalendo, kisha muda wako wa kutawala ukiisha unachukua sehemu kubwa sana ya utajiri wa taifa unahama kambi! Ni tusi la nguoni.

Kama Rais Mstaafu amenunua hilo jumba kama njia ya kuwekeza, bado kuna donda. Kwa nini ametumia miaka mingi ya uongozi kutuhimiza sisi tuwekeze nyumbani? Alikuwa anasema kinafiki?

Kiongozi wa kweli wa Tanzania hawezi kutumia mbinu akajipatia shilingi milioni elfu tatu na zaidi anapongatuka. Huwezi kutawala masikini wa kupindukia kisha ukaondoka na utajiri wa kupindukia. Kama ulitengeneza maslahi yako yawe makubwa hivyo, basi ulitumia vibaya madaraka, na umewasaliti masikini uliokuwa unawaongoza.

Kiongozi au viongozi wanaotumia madaraka yao kuunda vipengele vya kujipatia mali isiyolingana na hali halisi ya Watanzania ni wezi wabaya kuliko hata wezi wa silaha. Ni majambazi ya kutupwa.

Augustine Moshi
 
DrWHO said:
kuna sehemu gani imeandikwa mtu au rais asinunue nyumba kokote duniani?
kama hakuna evidence kuwa kala rushwa sasa whats the big deal

au kwa sababu rais MMAKONDE?

Ingekuwa mtajwa ni mfanyabiashara flani wala isingekuwa ishu.By the way,hata jirani yako akinunua nyumba huna haki ya kujua katoa wapi fedha za kununlia nyumba hiyo.Anaezungumziwa hapa ni Ben William Mkapa ambaye tangu 1995 hadi 2005 ni wazazi,familia,jamaa na ndugu zako DrWho,pamoja na wangu na wa Watanzania wengine waliokuwa wakimlipa mshahara na marupurupu mengine in the form of tax.As taxpayers,kwanini tusihoji?Commonsense can tell you that,cant it DrWho?
 
DrWho,

Hivi unajua kuwa ni huyo mtoto wake anayekaa kwenye hilo jumba huko SA, ndiye aliyeyamaliza maji yetu kule Mtera? Hivi unajua kuwa huyo mtoto ndiye aliyeumalizia maji yetu kule Mtera? Maana Netgroup ambako huyo kijana alikuwa akifanya kazi walimbiwa kuwa maji ya Mtera yasishuke kwa kiwango fulani, lakini huyo mtoto akampigia simu Mkapa, na amri ikaja toka Ikulu fungulia maji?

Matokeo yake ni kwamba itachukua miaka mitatu toka sasa hilo bwawa kujaa tena, na tutagawana umeme kwa miaka mitatu zaidi? Wakati yeye huyo mtoto na Step/dad wake watakuwa huko wanajirusha kwenye hela za walipa kodi?

Kama huna la kusema vipi ukinyamaza?
 
Labda huyu DrWHO, ndiye huyo mtoto wa BMW!

Unaona kumbe ni yale yale baada ya kutuletea taabu za kila aina na hata kwenye umeme sasa wanatesa SA!

Hapa ndipo huwa inaniuma ninaposikia JK anasema ataendeleza yote ya Mkapa!

Ni vema awe anaongea maneno haya kuwa yote yaliyo mazuri ya Mkapa na mabaya atayatupa ...
 
Unajua Mzee wangu, look at this kazi ya Netgroup, ilikuwa kukusanya madeni ya Tanesco kutoka kwa wanaodaiwa na Tanesco, na Net group were making $3,000, 0000, yaani DOLA MILLIONI TATU kwa mwezi mmoja!, I bet you hizi hela nusu ilikuwa ya Mkapa!,

kwa hiyo kufungwa kwa lile bwawa kungepunguza kipato cha Netgroup, jamani this time nilienda mwenyewe Mtera na kuongea na wafanyakazi wa lile bwawa, na wakasema bila uoga kuwa aliyelimaliza hili bwawa ni yule mtoto wao wanamuita Maro!, maana "....kila tukiwaambia wazungu kuwa bwawa halitakiwa kushushwa maji kutoka yalipo sasa, mara tulimuona yule kijana akipiga simu kwa jeuri na kuongea na baba yake, na muda si mrefu amri toka Ikulu ilikuwa inakuja kuwa fungulia maji haraka sana......", Yes! tena sio mara moja au mbili,

Mkira you might have a point kuwa heunda huyu jamaa ndio mwenyewe huyo!
 
Mzee ES,

Just as a matter of curiosity, nani Mkurugenzi wa SIMU 2000 Limited, baada ya huyo Maro kwenda huko SA?
 
Napata tatizo na utabiri wa Mzee ES kwamba JK atawamaliza wapora mali za nchi yetu. Labda kama ataanza na PM wake, kisha Karamag, nachelea kusema hiyo kazi itakuwa ngumu sana. Baada ya JK kuingia madarakani kwa madaha, PCB walimpelekea majina ya vigogo 40 ambao ni wala rushwa wakubwa kwa ushahidi mwanana. Akawaita katika kikao cha siri pale Mbeya; alichowaambia ni kuwa yeye hawezi kuwafanya chochote zaidi ya kuwafukuza kazi na kuwahamisha! Aliwauliza swali watu wa PCB kuwa:'unategemea mimi anye nini mtu aliyeitumikia nchi kwa miaka zaidi ya 20 halafu nimpeleke mahakamani kwa rushwa-itakuwa very devastating kwa huyo mtu'. Ndicho alichwajibu PCB huyu Rais tunayetarajia apambane na wala rushwa.

Kuhusu matatizo ya umeme, pamoja na matatizo ya Mkapa, haitakuwa busara kutafuta mchawi. We have a crisis which the private sector is urging the government to declare it a national disaster. The last thing we can do is to wove around for a witchcraft instead of solving the problem as a matter of urgency. Zaidi ya yote, kama ni uchawi, JK ni sehemu ya uchawi uliotufikisha hapa tulipo. Mpaka kesho, hakuna mwenye uwezo wa kumtenganisha Kikwete na madhira ya IPTL!
 
Jamani mnaumia kichwa burena DrWHO.

Huyu DrWHO anaishi UK kama mkimbizi ama mla mapesa yetu .Kama anabisha aseme halafu mimi nitatoa nyeti zaidi akiendelea kukataa .Je hukai UK wewe ? Ndiyo maana hana uchungu na lolote .
 
Mzee Mwanasiasa,

Maneno mazito na heshima mbele mzee kuna data hapo nimeziona na zilinipita kwa kushoto bro!
 
Mzee Es
Bado unataka tuamini kwamba JK atafanya lolote na wezi hawa ama ? Maana baada ya maelezo hapo juu toka kwa mwanasiasa yanapingana na utabiri wako wa sisi kungoja .Je tuendelee kuamini kwamba JK ndiyo kaanza kufanya kweli ?
 
Wazee,

Kwa maoni yangu, ni kuwa at the right time hawa vigogo wezi watazitema in one way or another, Je atawasafisha wote katika system hilo ni 1 Million dollars question,

Lakini ninaamini kwamba hawa kina Sumaye wanapokwenda kusoma Boston saa hizi, na kukutana na BM kila wakati huko, kuna jambo linakuja!
 
Mkira said:
Labda huyu DrWHO, ndiye huyo mtoto wa BMW!

Unaona kumbe ni yale yale baada ya kutuletea taabu za kila aina na hata kwenye umeme sasa wanatesa SA!

Hapa ndipo huwa inaniuma ninaposikia JK anasema ataendeleza yote ya Mkapa!

Ni vema awe anaongea maneno haya kuwa yote yaliyo mazuri ya Mkapa na mabaya atayatupa ...

Hapo umenena mwanangu.Yawezekana kabisa DrWho ni mwanae Mkapa
 
Back
Top Bottom