Naona kama wewe unataka kupotosha kama siyo utani tu. Kutunza familia yake ni sehemu ya marupurupu ya kazi zote hapa duniani, isipokuwa labda utawa tu. Kazi ya rais nayo inapata marupurupu hayo ya kutunza familia. Kinachoongelewa hapa ni kwa Rais kuwa mkurugenzi wa kampuni binafsi ya biashara.
Kichuguu,
Sijapotosha wala kutania. Nilitafakari sana kabla ya kuandika hayo maneno.
Na utata unazidi pale tunapomtaka Rais aliyepo madarakani asifanye biashara au kumilki kampuni binafsi, na wakati huo huo tunao wafanya biasahara na wakurugenzi wa kampuni zao binafsi wanaotaka kuwa marais. Inabidi tuwazuie hawa ama tutaifishe hizo kampuni zao kabla ya kuwaapisha (wakishashinda uchaguzi) ama itakuwaje? Maana kwa vyovyote vile bado wataendelea kunufaisha hizo kampuni zao hata kama kuna watakaokuwa wanakaimu ukurugenzi or whatsoever!
Ndugu zake watakaokuwa wanamiliki kampuni au biashara mbalimbali wanaweza kunufaika kwa njia hiyo pia, licha ya kwamba huyo Rais atakuwa si mfanyabiashara (akiwa madarakani).
Na ni kwamba Katiba yetu tuliyo nayo iko kimya katika haya yote. Wala haisemi kuwa ukishakuwa Rais basi unanyimwa uhuru wako kama raia kujiongezea kipato (kwa kufungua biashara ama kampuni binafsi) kwa kufuata sheria zilizopo. Kwanza inawezekana ni fursa ya kipato ulichonacho kwa wakati huo ndiyo imekusukuma kutimiza malemgo yako uliyojiwekea kwa muda mrefu.
Nimejaribu kuielewa "common sense" tunayotaka kiongozi aitumie katika mazingira hayo, bado inanirudisha kule kule tu kwamba common sense yangu mimi ni kufuata taratibu na sheria zilizowekwa. Kuna ubaya gani hapo?
Mr. Zero,
Unajua imenibidi nicheke wakati naandika jina lako (nimeikumbuka katuni ya Mtanzania, teh teh teh).
Maneno yako ni mazito. Hata mimi naona ni muhimu kutumia fursa zilizopo kihalali kutimiza malengo yetu ya kupata maisha bora. Vinginevyo turudi kwenye katiba kama nilivyojaribu kuhoji hapo juu.