Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

I can't beleave when I hear people talking good things about AHM. I think people in TZ are like chickens, we cannot remember things of the past. My old friend asked me a question one day: Why chickens fogerts very fast than most of the animals. I could not answer but he told me chickens have parabola type of brain while most of the animal have complex type of brain (Biologists can say if he was wrong).

Anyway, Hivi wakati ule tunalalamikia majumba ya mama Sitti Mwinyi mnataka kuniambia haikuwa kweli? Madeal ya wahindi na mambo kibao linked to AHM yalikuwa umbeya. From my opinion AHM for whatever reason either for his negligence or for failure to know (which he was supposed to know as a president) hawezi kuwekwa kwenye kapu tofauti.
 
HOj ILIYOPO HAPA NI YA ANBEM na Mkapa akiwa madarakani na mkewe. Hoja ya Ali Hassan Mwinyi ama Mwalimu Nyerere kama kama zipo ziletwe hapa kwa ushahidi kama ulivyoletwa huu wa Ben. Kuna kila dalili za kuleta suala la AHM ili kumuopoa Mkapa. Hilo haliwezekani. AHM na Mwalimu hawakuwa wezi labda Mwinyi alikua mpole mno na pengine alielemewa na wakati wa mpito baada ya muda mrefu wa utawala wa Nyerere. Wakati wote kulikua na hoja kuhusu AHM na hakuna aliyethubutu kuweka wazi tuhuma dhidi yake kwa maandishi. Kwa kifupi tusitumie migongo ya viongozi wengine kumuopoa MKAPA. Kuna mifano ya mwizi mmoja alipokamatwa akasema, "mimi si mwizi peke yangu, mimi nilichukua kofia tu, mwenzangu Juma ndiye kaiba simu na pesa." Sasa kama kweli sisi ni askari wa kweli, tutamwachia mwizi wa kofia aliye mkononi na aliyekiri ( ama ambaye tuna ushahidi) kuwa kaiba na kuanza kumtafuta mwizi wa simu na pesa? Hebu tukatae kubadilishwa mwelekeo. MKAPA ana KESI YA KUJIBU KWA WATANZANIA. Kwa waliosoma gazeti la MWANAHALISI la leo kuna habari kumhusu Mkapa kwamba wana ushahidi wa kutosha kwamba Mkapa alipokea Bakshish ya Dola za Marekani 10,000 kutoka NBC, najaribu kutafuta soft copy au mwenye kuwa nayo atuwekee hapa
 
Uchunguzi wa kina wa mwendendo wa biashara za Mkapa akiwa Ikulu umethibitisha pasi na shaka kwamba fedha hizo alilipwa siku ya Ijumaa Mei 21, 2004 kupitia mtumishi mmoja wa benki hiyo akiwa anafanya kwenye idara nyeti, jina na wadhifa wake kwa sasa vimesitiriwa. Kiwango hicho cha dola sawa na Sh milioni 10 wakati huo.
 
Baada ya kusoma gazeti hilo, nimezungumza na watu mbalimbali wamethibitisha kwamba aliyemlipa Mkapa fedha hizo kupitia kampuni yake ya ANBEM ni Secretary wa MD wa NBC LImited wakati huo.
 
Halisi,
Hala hala basi utuwekee hiyo nakala ya Mwanahalisi hapa.
 
Ni 10,000 au 10m? hivi kweli (if 10m) secretary ndio akamlipe rais cash?
 
Halisi,

Dola 10,000 ni hela ndogo sana kumuhonga Rais. Although I am still struggling with my life but 10,000 USD = 10, 000, 000 TShs that is a joke to our former president. A president could make equivalent amount of monies in only one trip to abroad. Anyway, bring the evidence and we will analyse but I am still not convinced unless you start talking about x100,000 and x1,000,000 USD!!!!
 
Mr.Zero,
I am with you on this one. It must be in millions otherwise how did the guy get to be a billionaire?
 
Jasusi,
Tatizo la viongozi wetu Tanzania ni kwamba hakuna kesi hata moja inayoweza make sense!.. Hawa watu wapo radhi kuuza nchi kwa malipo ya mwanaye kupata shule nchi za nje!.. Hawa jamaa wanaweza fanya yasiweza fanyika nchi nyingine yeyote!.. ONLY in Tanzania!
Hata kama ni Usd 10,000 kwa rais mbongo bado ni fedha, yaani kama vile wametiwa laana ya wizi. Kwa hiyo tutazame kosa lenyewe na sio kiwango cha fedha. Hata hizo Usd 500,000, Mkapa alizokopa benki haziingii akilini kama tutataka kutazama na kupima na wadhifa wake, yaani rais anakopa benki Usd 500,000 kuanzisha biashara?..
Mimi nachotaka ni kuhakikisha hawa watu mmoja baada ya mwenziye wanafikishwa mahakamani hata kama ni kwa Usd 10,000 hayo mengine yote yatakuja jitokeza!.
Mwanzo ndio mgumu, kama ulivyoona rais kasema mwacheni astaafu mzee wa watu na kweli sheria imemwacha. Hakuna korti wala hakimu anayeweza pingana na usemi huo wa rais!
 
NAdhani mutakumbuka Aden RAge alihukumiwa kwa kiasi gani cha fedha. Kesi ilihusu mamilioni ya fedha, lakini kiasi alichohukumiwa nacho ni kiasi kidogo sana ambacho hakifanani hata na matumizi yake ya siku moja. Ninachotaka kusema hapa ni kwamba, Dola 10,000 ni kama vile kateleza, kwani katika mlolongo wa fedha alizopokea, hizo ni tayari kuna kila ushahidi wa kwamba alipewa katika mazingira anmbayo yanatia shaka. Alipewa binafsi na mtumishi wa NBC akimwakilisha MD. HApo kuna siku, tarehe, mkapa na ushahidi wa maandishi. Ni ushahidi usio shaka. Achia mbali dola 500,000 ambazo zimepewa jina la mkopo, achilia mbali fedha nyingine nyingi ambazo hakuna anayejua zilitoka kwa nani na kwa makusudio gani. Hizo munazoziona ndogo, zimethibitishwa zilikotoka. HIVI polisi, mahakimu, madaktari na maofisa wa serikali wanaokamatwa kwa rushwa ya Sh 100,000, unadhani ni masikini? Dhambi ni dhambi, wizi ni wiwi, rushwa ni rushwa, haijalishi ni kiwango gani
 
Jasusi,
Tatizo la viongozi wetu Tanzania ni kwamba hakuna kesi hata moja inayoweza make sense!.. Hawa watu wapo radhi kuuza nchi kwa malipo ya mwanaye kupata shule nchi za nje!.. Hawa jamaa wanaweza fanya yasiweza fanyika nchi nyingine yeyote!.. ONLY in Tanzania!
Hata kama ni Usd 10,000 kwa rais mbongo bado ni fedha, yaani kama vile wametiwa laana ya wizi. Kwa hiyo tutazame kosa lenyewe na sio kiwango cha fedha. Hata hizo Usd 500,000, Mkapa alizokopa benki haziingii akilini kama tutataka kutazama na kupima na wadhifa wake, yaani rais anakopa benki Usd 500,000 kuanzisha biashara?..
Mimi nachotaka ni kuhakikisha hawa watu mmoja baada ya mwenziye wanafikishwa mahakamani hata kama ni kwa Usd 10,000 hayo mengine yote yatakuja jitokeza!.
Mwanzo ndio mgumu, kama ulivyoona rais kasema mwacheni astaafu mzee wa watu na kweli sheria imemwacha. Hakuna korti wala hakimu anayeweza pingana na usemi huo wa rais!


Kulingana na analysis iliyofanywa na jamaa wa Thisday, inaonyesha kuwa constitution ina vifungu vinavyoruhusu rais kushitakiwa kutokana na mambo aliyofanya in his private life. Linalonishangaza ni kuwa rais yuko kazini 24-7 kwa kipindi chote cha utawala wake, kwa hiyo ni lini unaweza kutofautisha private life na official life.


Thisday said:
New argument offered on why: Mkapa not immune from prosecution




-Constitution does not protect president from actions done in private capacity

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

THE Constitution of the United Republic of Tanzania does not guarantee immunity to the president for actions done in a personal capacity while occupying the highest public office in the land, an impeccable THISDAY source has stated.

The source, who happens to be a high-ranking official within government and also a qualified lawyer, made the clarification in the wake of a growing public debate over former president Benjamin Mkapa’s reported private business dealings while still at State House.

Commenting on possible prosecution options that the former president may face, the impeccable source said the Constitution guarantees immunity only where the president is carrying out official duties.

He explained that the relevant Article 46 of the Constitution makes it clear that the president is guaranteed immunity from prosecution ’’when executing his duty as president’’, and not otherwise.

During his first tenure as president in 1999, Mr Mkapa and the then first lady Anna Mkapa registered a private company, ANBEM Limited, and went on to operate it from a registered office within the Ikulu estate walls up to 2005 when he retired from the presidency.

Official registration documents for ANBEM Limited described Mr and Mrs Mkapa as ’entrepreneurs’ and sole shareholders/directors of the limited liability company, and ANBEM Ltd’s stated objectives include: ’’To carry on business and to act as merchants, general traders, warehouse, stockists, shopkeepers and operators of supermarkets, commission agents and carriers.’’

The exclusive THISDAY reports regarding ANBEM Limited and related business dealings have triggered a national debate over the ethical considerations of Mr and Mrs Mkapa’s actions while still at State House. While one school of thought argues that the couple did not break any law in registering their own private company while at Ikulu, another contends that the move - being mainly geared at ensuring personal gain - could well be interpreted as an abuse of office.

Issues of possible conflict of interest and undue influence, on the part of a sitting president endeavouring to balance official responsibilities and private business affairs, have inevitably been brought up.

THISDAY’s own efforts, through written questions sent to Mr Mkapa’s office in Dar es Salaam, to obtain clarification on the nature of the business transactions conducted by himself and Mrs Mkapa while at Ikulu, have drawn nought so far.

According to our source, any argument of the president being immune from prosecution - if found to have abused his office in this particular instance - would be misplaced.

’’If there is any finding that conclusively proves abuse of office, there is nothing in the country’s laws or Constitution that discounts the possibility of investigations being initiated against Mr and Mrs Mkapa’s properties and financial status,’’ he explained.

Article 46 (3) of the Constitution asserts: ’’Except where he ceases to hold the office of President pursuant to the provisions of Article 46A (10), it shall be prohibited to institute in court criminal or civil proceedings whatsoever against a person who was holding the office of the President after he ceased to hold such office for anything he did in his capacity as President while he held the office of President in accordance with this Constitution.’’

But according to our source, when Mr Mkapa registered ANBEM Limited with Mrs Mkapa and listed an official State House building as its physical address, he did not do that ’’in his capacity as president, in accordance with the constitution.’’

He cited the Prevention of Corruption Act as a possible legislation that could be used to prosecute Mr and Mrs Mkapa, saying this law clearly lists use by a government official of a government office or state property for personal gain as an act of corruption and abuse of office.

Various opposition party leaders and activist organizations including the Lawyers Environmental Action Team (LEAT) and the Legal and Human Rights Centre (LHRC) have openly criticized Mr and Mrs Mkapa’s actions in starting a private business company from Ikulu.

Incumbent President Kikwete has already said his administration will not pursue the matter of Mr and Mrs Mkapa starting and operating a private business company from State House. But he also maintained that the government of the day would not hesitate to take action against proven allegations of serious wrongdoing in the matter.

According to our source, the president appeared to be ’’carefully avoiding any witch-hunting.’’


Source: Thisday
 
Kichuguu,
Mimi naona kuna kila haja ya hiyo Ofisi kufanyiwa Auditing toka ifunguliwe kuona ni sehemu gani imejihusisha! Nina hakika watakuta mengi sana unless watachoma baadhi ya makaratasi. Habari za kuaminika toka kwa wajuzi zinasema - Watanzania will be shocked!..
Bank account za hii kampuni ni mshuhuda tosha!
 
JF muliopo nje ya nchi, kuna mali nyingi za hawa jamaa, wekeni humu ili watu wazijadili na kama THISDAY wakiona wazifuatilie maana hatuwezi kudhibiti UFISADI kwa kujadili bila kufichua. Tuwasaidie wanaoonyesha njia kwa kuwapa facts za kuwaongoza kufanya uchunguzi zaidi kuhusu fedha zetu za kodi ambazo pengine leo tusingekua na haja ya kusubiri mikopo kutoka kwa kina Mkono na wenzake, ambao sasa wanaanzisha benki. Kesho tutaambiwa tunaotaka kusoma Chuo Kikuu tukakope bank M ya mkono na wenzake na si tena Bodi ya Mikopo inayoongozwa na huyo huyo Mkono. Lakini kwa kifupi, pesa nyingi zimeporwa na sasa hatuna hata fedha ya kusomesha wanafunzi 29, na sasa wanaadhirika huko Ukraine...

Kuhusu kiwango, tusijadili viwango. Najua hata $500,0000 ni ndogo maana MAnji na wenzake (kwa amri ya Mkapa) wamejichotea zaidi ya Sh bilioni 80, hapo tunazungumzia mamilioni ya dola. Sasa kama alitosheka kwanini akakopa (akahongwa) $500,000? Si hizo za NSSF na PSPF zingetosha?
 
THISDAY ni gazeti lenye malengo MAALUM....sasa hivi sintaeleweka lakini itakuja kudhibitika SOON!!!!!!
 
THISDAY ni gazeti lenye malengo MAALUM....

PM, malengo yake ni yapi? Tafadhali tuambie tufahamu kwani wengine tunaliheshimu sana gazeti lile kwa vile linafanya investigative reporting ambayo na taaluma kubwa sana katika uhandishi wa habari. Sijaona gazeti lingine lililospecialize katika investigative reporting. Naamini kuwa kila article wanayoandika inakuwa imefanyiwa utafiti wa kina na kupata ushauri wa kisheria.
 
With regard to the Anbem saga!!!!!

Mimi nadhani dhambi kuu ktk hili ni kuregister kampuni kwa kutumia majengo ya Ikulu....Ama kwa hakika huu ni uozo wa hali ya juu.

Ikulu pale ni mahali 'penye hadhi ya kipekee' , si milki ya familia fulani, mtu fulani au kikundi fulani. Now how can any one have the nerve to register the private company using the part of 'that unique building as its physical address?'

Undoubtedly the former Pres. has loads to answer to Tanzanians like you and I who believed that he was Mr. clean as sold to us by the late Mwl. Nyerere.

Without any shadow of doubt kama mzee Nyerere angekuwa hai , hili angelipigia kelele kwa nguvu zake zote!! maana alitufundisha vyema miiko na maadili ya uongozi, iweje leo mmoja kati ya wanafunzi wale tulioamini aliamini masomo yale vizuri atusaliti.

Mzee Mwankijiji kwa 'nyundo na yale mawe yako' ya nguvu tunaomba tuanzishie kampeni maalumu ya kutaka kuomba tume huru kuchunguza kadhia hii, na endapo itathibitika beyond any reasonable doubt any wrong doing by the former Pres. basi mali zile alizozipata kinyume na taratibu zitaifishwe na kwenda kuhudumia mahospitali, shule na huduma nyingine za kijamii.

Hapo ndio tunasema Mungu usiwabariki viongozi wote wabinafsi na wasio na uchungu na wananchi wa kawaida.
 
Prudence Karugendo

ZIPO kashfa za wazi zinazomwandama Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin William Mkapa.

Pamoja na hulka za mwanadamu za kumuogopa na kumstahi mtu anapokuwa ameshika mpini huku akiwaachia wengine wajaribu kushika upande wenye makali, lakini baadaye walio upande wa makali wakaamua kumgeuzia kibao pindi anapoachia mpini, hali ni tofauti linapokuja suala la Mkapa, kwani yeye kama rais wa tatu wa nchi yetu, yanayosemwa juu yake baada ya kustaafu yakirejea aliyoyafanya wakati akiwa amekalia kiti cha enzi ni tofauti na ya wale wawili waliomtangulia.

Utofauti wake unaletwa na jinsi kila mmoja wao alivyopata nafasi ya kukalia kiti hicho cha enzi na namna alivyokitumia kuliongoza taifa letu.

Tunakumbuka kuwa Rais wetu wa kwanza, Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere, alipata nafasi ya kukalia kiti hicho baada ya harakati za kudai uhuru wetu.

Yeye akiwa kiongozi wetu katika harakati za kuudai uhuru wa nchi yetu, matumaini ya wananchi wote yalielekezwa kwake. Baada ya mafanikio ya kuupata uhuru matumaini ya wananchi yakageuka kuwa ushindi na wananchi wakajenga moyo wa kumwamini kwa kukikubali kile alichokuwa anawaeleza kuwa ni cha ukweli. Imani hiyo ilichangiwa na furaha ya wananchi ya kuona wanaongozwa na mzalendo mwenzao baada ya miongo mingi wakiwa chini ya utawala wa wakoloni, Wazungu kutoka ughaibuni. Sifa kuu ya Baba wa Taifa ni kwamba hakukubali kuyumbishwa na ulevi wa madaraka. Aliendelea kuwa yuleyule ambaye wananchi walimkubali, wakamwamini na kumkabidhi unahodha wa kuliendesha jahazi lao. Na kweli hakuwasaliti mpaka alipoamua kuachia madaraka.

Awamu ya pili kidogo ilionekana tofauti kutokana na tabia aliyoumbwa nayo mwanadamu ya mazoea. Kidogo Rais aliyefuatia, Ali Hassan Mwinyi, alionekana kuyumba katika misimamo ya mambo kadhaa. Ila bado siamini kama alifikia kiwango cha kuonekana anayefuja mamlaka aliyopewa na umma.

Ndipo kikaja kipindi cha awamu ya tatu, awamu iliyokuwa imelengwa kusafisha kasoro zote zilizojitokeza katika awamu iliyokuwa imetangulia. Baba wa Taifa kwa kuhisi kuwa awamu iliyofuatia awamu yake ilionyesha kutetereka akaamua kujiingiza kwenye kindumbwendumbwe cha kumtafuta rais wa awamu ya tatu. Lengo lake likiwa ni kuipatia nchi Rais safi mwenye kuulinda na kuutunza vyema uadilifu wa kiongozi mkuu wa nchi kama yeye alivyowahi kufanya.

Huku akizinyooshea kidole dosari zilizojitokeza katika awamu ya pili, ndipo akatuonyeha kuwa Mkapa ni mwenye uwezo wa kuzirekebisha dosari hizo. Kwa hiyo wananchi, pamoja na imani waliyokuwa nayo kwa Nyerere, pia wakizingatia kuwa aliyekuwa akimtaja aliwahi kuwa mwanafunzi wake aliyemjua vyema, wakajawa na matumaini ya kumpata kiongozi mwingine mwadilifu. Hiyo ndiyo sababu inayoleta tofauti ya yanayorejewa na wananchi katika uongozi wa marais hao watatu baada ya kustaafu kwao.

Ni kwamba Mwinyi alitarajiwa kuendeleza yale ya Nyerere, lakini kutokana na sababu za kibinadamu akatetereka kwa vile wao, yeye na Mwalimu, ni binadamu tofauti. Lakini Mkapa tuliyehakikishiwa na Baba wa Taifa mwenyewe kuwa ndiye mwenye kuweza akaonekana kuanguka kabisa badala ya kutetereka! Kwa nini sasa tusimjadili?

Kashfa zinazomwandama Mkapa zinajadiliwa na wananchi ili kutoa funzo kwa rais wa sasa na atakayekuja baadaye asiweze kurudia makosa yale yale ili yasije yakajijenga na kuwa sehemu ya utamaduni wa marais wa nchi hii. Tunajifunza kutokana na makosa.

Tukikubaliana na madai ya kwamba tumwache Mkapa apumzike kwa amani tutakuwa tumewahalalisha marais wetu kuendelea kufanya mambo yaliyo nje ya uadilifu wa mamlaka yao wakiamini kuwa katiba inawakinga dhidi ya shutuma na mashitaka wakiwa madarakani na kanuni ya wananchi ya kuwaacha wapumzike kwa starehe baada ya kustaafu inawalinda. Tukikubali kufanya hivyo tutakuwa tumewaondolea kabisa uadilifu marais wetu na tutakuwa tumejimaliza sisi wenyewe. Ndiyo maana nasema haya ya Mkapa ni lazima tuyajadili.

Ninachoamini ni kwamba, Mkapa kakiuka uadilifu, sina uhakika kama hilo linatosha kumfungulia mashitaka. Lakini hata hivyo suala la kumshitaki sidhani kama bado linaweza kusaidia kwa sasa, ameishatenda na kung'atuka. Cha muhimu ni kuganga yaliyopo na yajayo. Tulizungumzie suala lake na kulilaani kwa nguvu zetu zote ili lisijirudie tena. Hii ni kwa faida ya baadaye.

Uwezekano wa kushitakiwa Mkapa, kwa wale ambao wangependa iwe hivyo, bado naona upo tukiondoa utaratibu ulioota mizizi wa kulindana. Sababu huyu kajipatia mali kwa njia zisizo halali. Kutumia heshima ya urais aliyokabidhiwa na umma na kuigeuza mtaji wa ujasiriamali ni jambo lisilokubalika hata kidogo. Sababu pamoja na matatizo ya kiuchumi iliyo nayo nchi yetu bado tunao uwezo wa kumwezesha rais wetu awe juu ya matatizo hayo ya kiuchumi ili aweze kuyashughulikia kwa kuwakwamua watu wake walionaswa ndani ya matatizo hayo. Sababu tukionekana tumenaswa wote nani atamnasua mwingine?

Kwa hiyo njia ya kuutumia uraisi kuwa mjasiriamali ni haramu kabisa. Ni zaidi ya mtumishi wa umma anayetumia fedha za umma kujifanyia biashara zake. Urais ni mali ya wanachi wote kwa ujumla. Kwa hiyo inategemewa kinachopatikana kupitia jina la urais kiwe mali ya wananchi na wala siyo mali binafsi ya yule anayekuwa Ikulu kwa wakati huo. Mkapa anaweza kuwa hana hatia iwapo mali zote alizozipata kwa kutumia wadhifa wake atazisalimisha mikononi kwa serikali. Nyerere alifanya hivyo kwa kusalimisha serikalini nyumba yake ya Msasani aliyoijenga kwa mkopo wa benki alioupata kwa kudhaminiwa na wadhifa wake.

Tukumbuke kwamba kuvunja sheria ni kitu kimoja na kukiuka maadili ni kitu kingine.

Kuna mambo ambayo maadili yanatuzuia kuyatenda ingawa kuyatenda huko hakumaanishi kuvunja sheria. Mfano, mtu mzima hawezi kutoa ushuzi katikati ya kadamnasi japo kufanya vile si uvunjaji wa sheria.

Kwa hiyo wanaomtetea Mkapa kwa ukiukaji wa maadili ya urais wakidai kuwa hakuvunja sheria wajue kuwa hawamtendei haki.

Japo wanaonekana wanamtetea. Haki ni pamoja na kumpa mtu stahiki yake.

Pamoja na mambo mengine jambo moja kuu ambalo watu wanataka kumshitaki nalo Mkapa ni lile la kuisaliti imani na mategemeo yao kwake waliyojengewa wakati wa kumnadi ili apewe funguo za Ikulu.

Baba wa Taifa, wakati akimnadi alitahadharisha kuwa Ikulu ni mahali patakatifu. Kwamba pale hapafanywi biashara. Akawa anawashangaa waliokuwa wanafikia hata kutoa pesa ili wapate nafasi ya kuwa wapangaji wa Ikulu.

Akamnadi vizuri Mkapa kuwa ndiye ambaye alimuona kuwa angeweza kutunza utukufu wa Ikulu. Watu wakamuamini na hivyo kuwaacha wale walioonyehsa kwamba wangeweza kuigeuza Ikulu soko la biashara.

Sasa wananchi kwa nini wasishangae kuambiwa kuwa Mkapa aliamua kuwa mjasiriamali, au tuseme mchuuzi, baada ya kuingia Ikulu na kuigeuza duka binafsi kwa kutumia jina linaloonekana kama kifupi cha majina yake na mke wake (ANBEM)? Kwa nini hilo lisimfanye aonekane msaliti? Kwa nini asishitakiwe?

Rais ni baba wa wananchi wote, ndiye mwenye kuwaangalia watu wake wanavyohangaikia maisha yao na kujipatia riziki.

Jukumu lake ni kuwawezesha ili wafanikishe ujasiriamali wao. Sasa rais naye anapoamua kuwa mjasiriamali inaleta picha gani?

Yaani akashindane na wanawe katika kutafuta riziki? Ni uadilifu gani huo? Jaribu kufikiria baba anayegombania kiporo na wanawe na kisha kuanza kuwatambia kuwa amewashinda na kukila yeye.

Mjasiriamali wa Ikulu naye alikuwa anaomba mikopo benki. Kumbuka ombi la mkubwa ni amri, ni kiongozi wa benki gani angethubutu kusema kuwa mwombaji mkopo huyo wa Ikulu alikuwa hajatimiza sifa za kupata mkopo aliouhitaji? Ndiyo yale tunayoambiwa ya kuweka rehani nyumba ambayo ndiyo iliyokuja kununuliwa kwa mkopo ule ule uliokuwa unatafutwa.

Nani angesema kuwa hiyo ilikuwa nje ya utaratibu wa kibenki? Je, huo ni utumiaji mzuri wa mamlaka ambayo mtu anakuwa amepewa na umma?

Mali zinazopatikana kwa njia hiyo tuziite za halali?

Tukumbuke kuwa Mkapa, katika kipindi chake chote cha urais alikuwa akipendelea kutumia neno la "uvivu wa kufikiri". Nashawishika kuamini kuwa ni uvivu huo wa kufikiri aliokuwa akiuona kwa wananchi uliomsukuma kufanya mambo yanayokinzana na wadhifa wake akiamini kuwa wananchi walio na uvivu wa kufikiri wasingeweza kuliona hilo. Kwa hiyo kuyanyamazia aliyoyatenda kinyume na wadhifa wake ni kuukiri uvivu huo wa kufikiri. Bora tuwaachie wanaomtetea tukiamini kuwa ndio aliokuwa akiwamaanisha, wavivu wa kufikiri. Ila tukubaliane kuanzia sasa kuwa hatutakubali marais wetu wautumie udhaifu huo walio nao baadhi ya wanachi, udhaifu wa uvivu wa kufikiri, ili kujipatia manufaa binafsi yaliyo nje ya kipimo cha wadhifa wanaokuwa wamekabidhiwa na wananchi.

Mwisho, itabidi tuiangalie upya kinga aliyowekewa rais dhidi ya mashitaka akiwa madarakani au baada ya kustaafu.

Kinga hii inaonekana kuwaweka sana majaribuni marais hususan hawa wa nchi zetu za dunia ya tatu. Ni kinga ya kuwaondolea uadilifu katika utendaji wao wa kazi.

Ni kinga ya kuwaruhusu wafanye lolote wanalotaka wakiamini kuwa hakuna lolote litakalowasibu kwa vile wao wako juu ya sheria. Hii ni kinga ya udhaifu. Inabidi tuondokane na uvivu wa kufikiri, tujiulize, iwapo rais hapaswi kushitakiwa, kwa nini tunamuapisha?

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa simu: 0784 989 512 au baruapepe: prudencekarugendo@yahoo.com
 
HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI MHE. GRACE KIWELU KUHUSU OFISI YA RAIS MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA JUU YA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA WA FEDHA 2007/2008.

I. UTANGULIZI

1. Mheshimiwa Spika, napenda kutumia fursa hii kwa mujibu wa Kanuni za Bunge kifungu cha 43 (5),(b),(c) na 81(1) toleo la 2004 kutoa maoni ya Kambi ya Upinzani kuhusiana na Bajeti ya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kuwepo hapa leo kujadili mambo muhimu kwa maslahi ya umma wa Watanzania, na kwa mema yote amabayo amekuwa akitujaalia. Ni matumaini yangu kwamba majadiliano yetu yataweka mbele maslahi ya Umma. Mungu atusaidie.

3. Mheshimiwa Spika, napenda kwa nafasi ya kipekee kabisa kukishukuru chama changu cha CHADEMA kwa kuendelea kuniunga mkono katika kazi walizonikabidhi katika kipindi cha 2005-2010. Nawaahidi kuwa kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu nitawatumikia wananchi kwa uadilifu mkubwa. Aidha, natoa shukurani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Shoka Khamis Juma (MB), Msemaji Mkuu wa upinzani - Utawala Bora na Mheshimiwa Phares Kabuye (MB), Msemaji mkuu wa upinzani - Siasa na Mahusiano ya Jamii, kwa mchango wao mkubwa katika kufanikisha uandaaji wa hotuba hii, kwani na wao ni wasemaji wakuu katika wizara zinazojumuishwa katika hotuba hii. Vile vile, natoa pongezi za dhati kwa viongozi wetu wa Kambi ya Upinzani Mhe. Hamad Rashid Mohammed (MB) na naibu wake Mhe. Dr. Wilbrod Slaa (MB) kwa kutoa muongozo sahihi kwa mujibu wa kanuni za Bunge.

4. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2006/2007 tumempoteza mwenzetu, Hayati Juma Jamaldin Akukweti na hivi majuzi tu Hayati Amina Chifupa. Hivyo kwa majonzi makubwa, kwa niaba ya Kambi ya Upinzani naomba kutoa salamu za pole kwa ndugu, rafiki, jamaa na familia za marehemu. Mungu aziweke roho zao mahali pema peponi. Amin.

5. Mheshimiwa Spika, napenda pia kuungana na wenzangu kutoa pole kwa wale wote waliofikwa na misiba na ajali katika kipindi hiki chote tukiwa hapa Bungeni. Mungu awafariji katika wakati huu mgumu.

II. MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA

6. Mheshimiwa Spika, kambi ya upinzani inatambua kwa kina umuhimu wa Ofisi ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma kama sehemu muhimu sana katika kuimarisha utawala bora katika uendeshaji wa shughuli za serikali, kuweka mfumo wa uendeshaji wa serikali unaoleta tija na ufanisi, kujenga uwezo wa watumishi wa umma, na kuboresha maslahi ya Watumishi wa Umma. Mheshimiwa Spika, kwa kuelewa hilo ni muhimu sana idara hii iangaliwe kwa umakini kwa sababu Watumishi wa Umma ni moja ya kiini cha maendeleo ya Taifa.

7. Mheshimiwa Spika, kambi ya upinzani inayaona mengi ambayo kimsingi yamekuwa yakidhoofisha swala zima la utendaji na uwajibikaji wa Watumishi wa Umma. Mambo haya yanatokana na kutokuwepo kwa umakini na ufuatiliaji thabiti ambao umepelekea kuporomoka kwa maadili na uwajibikaji wa Watumishi wa Umma, maisha duni, ubinafsi, na urasimu na hivyo kurudisha nyuma maendeleo ya taifa hili.

ONGEZEKO LA MISHAHARA KWA WATUMISHI WA UMMA.

8. Mheshimiwa Spika, maboresho ya maslahi ya Watumishi wa Umma ni jukumu muhimu sana la Ofisi ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Kwa kutambua hilo, Serikali ya Awamu ya nne haikubaki nyuma na ndio maana ikaahidi ‘Maisha bora kwa kila Mtanzania’. Tumaini la kila mtumishi lilikuwa ni nyongeza ya mshahara kulingana na kiwango cha kupanda kwa hali ya maisha kiujumla.

9. Mheshimiwa Spika, tofauti na matarajio ya wengi, hususan wale walipwao kima cha chini, hali imeendelea kuwa ngumu kutokana na kutopanda kwa mshahara kwa kiwango kinachoridhisha. Bajeti kuu ya Serikali mwaka 2007/2008 inaonesha kwamba mshahara utaongezeka kwa 12%. Hili ni ongezeko dogo sana ukizingatia kwamba kima cha chini cha mshahara ni shilingi 75,000 tu. Hii inamaanisha kwamba kima cha chini kitaongezeka na kufikia shilingi 84,000 tu. Kwa hali hii bado maisha ya Mtanzania yataendelea kuwa magumu sana huku gharama za maisha zikiendelea kupanda kutokana na Bajeti ngumu iliyowasilishwa na Serikali mwaka huu wa fedha.

10. Mheshimiwa Spika, wakati wa sherehe za Mei Mosi mwaka huu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alikisikia kilio cha Wafanyakazi nchini wakiomba nyongeza ya mshahara ifikie Shs.315,000 kwa kima cha chini kutokana na kupanda kwa hali ya maisha.

11. Mheshimiwa Spika, naomba kunukuu sehemu ya Risala ya Wafanyakazi iliyowasilishwa na Katibu Mkuu wa TUCTA Ndugu Nestory Ngula katika kilele cha maadhimisho ya Mei Mosi kwenye uwanja wa CCM Kirumba Mjini Mwanza mwaka 2007. Wafanyakazi walisema “…. Vyama vya Wafanyakazi viliwasilisha mapendekezo ya kuboresha kima cha chini cha mshahara kwa watumishi wa Umma cha Shs. 75,000/= kwa mwezi kinacholipwa sasa hadi kufikia Shs. 315,000/= kwa mwezi. Kima hicho cha chini cha mshahara tulichopendekeza cha Shs. 315,000/= ndicho kiwango cha chini kabisa cha mshahara kitakachomwezesha mfanyakazi wa ngazi ya chini mwenye familia ya watu sita yaani Mume, Mke na watoto wanne chini ya umri wa miaka 18 kuweza kumudu mahitaji muhimu ya maisha kwa mwezi. Mshahara huu wa Shs. 315,000/= wa kima cha chini unamwezesha Mfanyakazi kutumia Shs.142,000/= kwa ajili ya kupata mlo asubuhi, mchana na jioni kila mwezi kama kima hiki cha mshahara hakitakatwa kodi yeyote wala michango mingine. Kima hicho pia kitakidhi pia gharama zingine za Shs.173000/= kwa mwezi mmoja kulipia usafiri wa kwenda kazini, usafiri wa watoto wanne wa shule ya msingi, sare za watoto, kodi ya nyumba (vyumba vitatu), Mavazi, matibabu, maji, umeme na akiba ya dharura…” Mwisho wa kunukuu.

12. Mheshimiwa Spika, cha kushangaza ni kwamba kiasi kilichoongezeka hakifikii hata robo ya maombi yao. Hili linasikitisha sana. Hata hivyo, kambi ya upinzani inatambua kwamba kutokana na hali ya uchumi ongezeko hili kwa ghafla lisingeweza kufikiwa. Pamoja na hayo, bado tunaamini ya kwamba kama serikali ingepokea ushauri wa kuboresha bajeti uliotolewa na Kambi ya Upinzani, ongezeko hilo lingeweza kufikiwa angalau nusu.

13. Mheshimiwa Spika, Bajeti mbadala ya fedha mwaka 2007/2008 kama ilivyowasilishwa na Waziri Kivuli wa Fedha inaonyesha kwamba kima cha chini cha mshahara kingefikia kiasi cha shilingi 215,000 kutokana na kuongezeka kwa makusanyo ya mapato ya ndani. Kwa ngazi nyengine mshahara ungepanda kwa asilimia ambayo ingeleta uwiano baina ya kipato cha chini na cha juu. Ni wazi kwamba hili limeshindikana kwa serikali ya awamu ya nne kukataa mapendekezo yaliyotolewa ambayo yangeongeza makusanyo ya mapato ya ndani katika sekta mbali mbali kama vile madini, utalii, uvuvi wa bahari kuu, misitu na bandari, bila kusahau kupunguza misamaha ya kodi.

14. Mheshimiwa Spika, licha ya kupendekeza kima cha chini kuwa Shs. 215,000, hatukubaliani na ushauri wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini kuwa kima cha chini kisilipwe kodi. Kambi ya upinzani inasema, kima cha chini kingeongezwa mpaka kufikia kiasi tulichotaja lakini pia lazima kodi ilipwe. Kulipa kodi ni wajibu wa kila raia.

15. Mheshimiwa Spika, haitakuwa busara kwa kambi ya upinzani kusahau kutetea maslahi ya watumishi wasiokuwa wa Umma. Sekta binafsi nayo imekuwa chachu ya maendeleo kwa kutoa ajira kwa Watanzania, lakini ubaya wake unaonekana pale sekta hii inapojilimbikizia faida na kuwanyonya watumishi wake. Kwa sasa kima cha chini katika sekta binafsi ni kati ya shs.35,000 na shs. 48,000, kiasi ambacho ni kidogo sana kulingana na hali ya maisha ilivyo sasa. Kiwango hiki cha mshahara kinamwezesha mfanyakazi kugharamia chakula cha asubuhi, mchana na jioni kwa muda wa wiki moja tu bila kulipia gharama zingine. Kambi ya upinzani inaiomba serikali itangaze kiwango kipya cha kima cha chini kwa watumishi wasio wa Umma.

16. Mheshimiwa Spika, kwa kuangalia Bajeti kuu ilivyo ni wazi kwamba vipengele vyengine si vya msingi kiasi cha kutengewa mabilioni ya fedha kila mwaka, huku watumishi wa Umma wakiachwa solemba. Mfano, katika Bajeti ya mwaka huu 2007/2008 zimetengwa bilioni 5.5 kwa ajili ya ukarabati wa Ikulu, mwaka 2006/2007 zilitengwa bilioni 6.125 na mwaka 2005/2006 zilitengwa bilioni 3.2 kwa ukarabati huo huo wa Ikulu. Kambi ya upinzani inahoji uhalali wa mabilioni haya yanayotengwa kila mwaka kwa ajili ya ukarabati wa Ikulu. Kuna nini huko? Je, serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kupunguza baadhi ya matumizi ili kujali maslahi ya Watumishi wa Umma?

17. Mheshimiwa Spika, TUCTA pia katika Risala yao wanahoji juu ya matumizi ya kifahari na yasiyo ya msingi. Naomba ninukuu “…Hatukatai sababu zinazotolewa na Serikali kuwa uchumi wetu bado ni mchanga, lakini tunashangaa kuona kwamba pamoja na uchumi kuwa mdogo bado matumizi ya Serikali katika baadhi ya maeneo ni makubwa kuliko hata katika nchi ambazo uchumi wake ni mkubwa kuliko wa nchi yetu. Matumizi haya ya Serikali yasiyofanana na hali ya uchumi ni katika manunuzi ya magari makubwa ya kifahari aina ya VX (Landcruiser, Mitsubishi Pajero, Prado, Nissan Patrol n.k) ambayo yananunuliwa kwa bei kubwa na yenye gharama kubwa katika matumizi ya mafuta na matengenezo. Inashangaza kuona kwamba kuna magari mengi ya aina hiyo katika ofisi nyingi za Serikali kuanzia Wizarani, Mikoani, Wilayani na Taasisi nyingine za Umma.

Takwimu toka Wizara ya Miundombinu zinaonyesha kwamba hadi kufikia mwishoni mwa mwaka wa fedha wa mwaka 2005/06 jumla ya magari makubwa na ya kifahari yapatayo 6,000 yalikuwa yamenunuliwa na Serikali kwa gharama kubwa inayokadiriwa kufika T.Shs.Bilioni 160. Miongoni mwa magari hayo ya gharama kubwa na ya kifahari yaliyonunuliwa na Serikali hadi mwaka 2005/2006 ni aina ya Toyota Landcruiser (VX/GS, STD, Prado) yapatayo 1,655, Nissan Patrol na Landcruiser 885, Mitsubishi Pajero 400 na mengineyo. Serikali ingekuwa inafanya matumizi yake kwa kuzingatia hali ya uchumi kama inavyofanya kwa wafanyakazi kwa kuwalipa mishahara isiyotosheleza mahitaji muhimu ya maisha, basi ingeweza kubana matumizi kwa kununua magari madogo ya kawaida na kuweza kuokoa mabilioni ya fedha ili kuboresha mishahara ya wafanyakazi au kuimarisha huduma za jamii.

Aidha umezuka mtindo wa kununua samani (furnitures) za ofisi za Serikali toka nchi za nje kwa gharama kubwa badala ya kununua kwa watengenezaji wa samani hizo toka hapa nchini ili kubana matumizi, kuongeza ajira, na kuinua uchumi wa nchi yetu. Wakati vyama vya Wafanyakazi vilipokutana na Tume ya Rais ya kuboresha Mishahara ya Watumishi wa Umma wakati inakusanya maoni, tulishauri mambo mengi ambayo yangesaidia kupatikana kwa fedha kwa ajili ya kuboresha mishahara ya wafanyakazi. Ushauri tuliotoa ni pamoja na kupunguza magari ya kifahari, kupunguza misafara mikubwa ya viongozi ndani ya nchi wakati wanatembelea Mikoani na Wilayani. Misafara hiyo hutumia gharama kubwa kugharamia mafuta na matengenezo kwa ajili ya misululu mikubwa ya magari yanayotumika kwenye ziara hizo ikiwa ni pamoja na kulipa posho za kujikimu viongozi na watendaji. Matumizi ya aina hii huwafanya wafanyakazi wasielewe kabisa wanapoelezwa kuwa uchumi wetu ni mdogo na hauwezi kubeba gharama kubwa za mishahara wakati wanaona matumizi ya Serikali hayalingani na hali ya uchumi mdogo…” Mwisho wa kunukuu.

18. Mheshimiwa Spika, kama kumbukumbu zetu zitakuwa sawa wakati Mheshimiwa Rais anaingia madarakani na kulihutubia Bunge, pamoja na mambo mengine aliunda Tume ya kurekebisha mishahara ya watumishi wa umma ambayo ilikuwa chini ya Mwenyekiti Ndg. Deogratias Ntukamazima, na kwa sasa ni dhahiri tume hiyo itakuwa imemaliza kazi. Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali iiweke hadharani ripoti hiyo ili wabunge na wawakilishi wa wafanyakazi waweze kuona kama yaliyopendekezwa yanalingana na mapendekezo ya maoni ya vyama vyao vya wafanyakazi.

19. Mheshimiwa Spika, kuchelewa kulipwa kwa nyongeza ya mshahara kwa Watumishi wanaopandishwa cheo ni kero nyengine miongoni mwa kero zinazowasumbua Watumishi wa Umma. Kambi ya upinzani inaomba kuelezwa sababu zinazopelekea kucheleweshwa kwa malipo ya nyongeza ya mshahara kwa baadhi ya watumishi.

III. UTAWALA BORA

20. Mheshimiwa Spika, Utawala Bora ni pamoja na kutoa taarifa sahihi na kwa wakati kwa umma. Utawala bora pia ni pamoja na kutoa majibu kwa wakati kulingana na masuala yanayoulizwa na muulizaji. Katika kipindi hiki cha uongozi, Serikali inashindwa kuwapatia majibu wananchi ambao wanaandika barua zao kwa misingi ya kupata ufafanuzi kulingana na masuala mbali mbali. Na jambo hili kwa ujumla wake linadhalilisha nchi inayojiita kuwa inafuata sheria na utawala bora. Mfano mzuri ni Mheshimiwa Waziri kivuli wa Utawala Bora alipoandika barua kupitia Kiongozi wa Upinzani alipomuandikia Mhes. Rais kuhusu maafa Jimboni kwake, alipata majibu baada ya miezi mitatu. Je, Watanzania wa kawaida inawachukua miaka mingapi?

21. Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia haya ni lazima Ofisi hii itupiwe jicho makini na pembuzi zaidi ili kugundua mianya yenye kudhoofisha utendaji wake.

HAKI ZA BINADAMU

22. Mheshimiwa Spika, Utawala Bora unahusu pia utawala wa sheria na kuheshimiwa kwa misingi ya haki za binadamu. Hivi karibuni tu jumuiya mbili za kiraia, Legal and Human Rights Centre (LHRC) na Zanzibar Legal Service Centre (ZLSC), kwa pamoja zilishirikiana kutoa Ripoti ya Haki za Binadamu nchini Tanzania kwa mwaka 2006. Ripoti hiyo imeonyesha kukithiri kwa matukio ya uvunjwaji wa haki za binadamu yanayofanywa na raia na pia vyombo vya dola. Inataja matukio ya kuendelea kutumika kwa adhabu ya kifo, kutozingatiwa kwa haki za wafungwa na mahabusu, matukio ya vikosi vya ulinzi na usalama vya Muungano na vikosi vya SMZ kutumia nguvu za ziada na kuvunja haki za binadamu yakiwemo kuua, kuuliwa kwa vikongwe kwa kudhaniwa wachawi, uhuru wa vyombo vya habari kufinywa, kutoheshimiwa kwa haki na uhuru wa kisiasa, wa kujikusanya na kujumuika, kutozingatiwa haki za wafanyakazi, haki za makundi maalum yakiwemo wanawake na watu wenye ulemavu, wazee, wakimbizi, wagonjwa wa UKIMWI, rushwa na utumiaji mbaya wa madaraka.

23. Mheshimiwa Spika, hali inayoelezwa katika Ripoti hii inatisha na haiendani na majigambo ya Serikali kwamba Tanzania inafuata na kuongozwa na misingi ya utawala wa sheria na haki za binadamu. Kambi ya Upinzani inapenda kupata maelezo juu ya hatua zinazochukuliwa na Ofisi ya Rais (Utawala Bora) katika kufanyia kazi yale yaliyomo katika ripoti hii ili matukio ya aina zilizotajwa yasijirejee tena.

UTEKELEZWAJI WA HUKUMU ZA MAHAKAMA

24. Mheshimiwa Spika, tunategemea utawala bora katika nchi unaendelezwa kupitia mihimili mitatu ya dola ambayo ni Bunge, Mahakama, na tawi la utendaji kwa kutengana kimamlaka (Separation of Powers) kwa mujibu wa Katiba. Kila mhimili kati ya hiyo mitatu unapaswa kuwa huru na kuwa na mamlaka ya kuangalia utendaji wa mhimili mwengine (Checks and Balances). Hivyo basi, maamuzi ya kila mhimili yanapaswa kuheshimiwa kikatiba na mihimili mengine. Kwa mfano; uamuzi unaopitishwa na Bunge juu ya sera na sheria unapaswa kutekelezwa na tawi Tendaji (Executive) huku Mahakama ikiwa na jukumu la kutafsiri na kusimamia sheria hizo.

25. Mheshimiwa Spika, ili maamuzi ya Mahakama yatekelezwe ni lazima Bunge lipitishe sheria inayohusu kadhia hiyo. Cha kushangaza ni kwamba tangu Mahakama Kuu ya Tanzania ilipotoa hukumu ya kufuta sheria ya takrima Serikali haijaleta Bungeni muswada unaohusu hukumu hiyo. Aidha, tangu Mahakama Kuu ilipotoa hukumu juu ya mgombea binafsi Serikali haijaleta Bungeni muswada wa kutekeleza hukumu hiyo? Na je kisheria ni muda gani tangu mahakama kuu inapotoa hukumu juu ya jambo fulani na Serikali au chombo kingine cha dola kinatakiwa kutekeleza hukumu hiyo? Kambi ya Upinzani inaitaka mihimili hii mitatu kuheshimiana na kuangaliana kiutendaji kama katiba inavyotaka. Ili dhana ya utawala bora ionekane, maamuzi ya kila muhimili yaendanayo na katiba, lazima yatekelezwe katika muda wake.

USALAMA WA TAIFA

26. Mheshimiwa Spika, Katika Idara ya Usalama wa Taifa kumekuwepo na ongezeko kubwa la fedha. Kutokana na unyeti wa kitengo hiki tunaweza kuona hata bajeti yake inakuwa kubwa kuliko bajeti ya mihimili miwili ya dola kwa pamoja yaani bajeti ya Ofisi ya Spika, ambayo ni Tshs.42 bilioni, na Mahakama ambayo imetengewa Tshs.37 bilioni. Kwa ujumla mihimili hii imetengewa Tshs. 79 bilioni ikilinganishwa na kitengo cha Usalama wa Taifa ambacho kimetengewa Tshs. 110bilioni kama inavyoonyesha kwenye vote 30 programu ya kumi, Utawala.

27. Mheshimiwa Spika, pamoja na kuwa kufuatana na Sheria ya Usalama wa Taifa, kitengo hiki shughuli zake nyingi huwa hazizungumzwi wazi wazi, ndio maana hata waheshimiwa Wabunge huwa hatuulizi maswali mengi juu ya kitengo hiki. Lakini pamoja na utamaduni huo wa usiri, Kambi ya Upinzani inaomba ielezwe sababu za kitengo hiki kuongezewa mabilioni ya fedha kadiri siku zinavyoongezeka.

MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

28. Mheshimiwa Spika, Serikali ilianzisha utaratibu wa kutoa fomu za maadili kwa madiwani. Kwa mujibu wa maelezo ya Mhe. Waziri anayeshughulikia masuala ya Utawala Bora, asilimia 70 ya madiwani hawakujaza fomu hizo. Kwa kuwa sheria zinamlazimisha kiongozi wa umma kufanya hivyo, kambi ya upinzani inamuomba Mhe. Waziri atuambie kwa nini nafasi hizo zisitangazwe kuwa ziko wazi kutokana na wahusika kushindwa kutekeleza matakwa muhimu kisheria kama hayo?
29. Mheshimiwa Spika, pia Waziri alikiri kwamba sio fomu zote zinazokaguliwa bali mtindo wa ‘sampling’ hutumika akitoa sababu kuwa viongozi ni wengi. Mheshimiwa Spika, kambi ya upinzani inaona kuwa mtindo huu wa ukaguzi kwa njia ya ‘sampling’ (yaani kupitia fomu chache tu) unaua dhana nzima ya sheria husika ambayo lengo lake ni kuhakikisha kwamba Watumishi wa Umma wakiwa kwenye madaraka hawatumii madaraka yao kujilimbikizia mali.

30. Mheshimiwa Spika, suala hili la uzembe wa kuwawajibisha viongozi wanaoshindwa kujaza fomu za maadili inathibitisha jinsi ambavyo Sekretarieti ya Maadili ya Watumishi wa Umma ama imeshindwa kufanya kazi yake kiumakini (kwa kuwa iko juu) ama imezidiwa na kazi hivyo kuwa na haja ya kupanuliwa zaidi kufikia ngazi ya halmashauri.

31. Mheshimiwa Spika, hivi karibuni vyombo vya habari vimeandika juu ya madai kwamba Rais mstaafu, Mhe. Benjamin Mkapa, alitumia Ikulu ya Watanzania kufanya biashara kwa manufaa binafsi. Je, Serikali inaweza kuweka utaratibu utakaomruhusu raia wa nchi hii kupekua nyaraka za matamko ya Mali na Madeni ya Mhe. Mkapa ili kujiridhisha kuwa, biashara yake iliendeshwa sawa sawa kwa kufuata sheria za nchi?

32. Mheshimiwa Spika, na kama Rais anaruhusiwa kufanya biashara akiwa Ikulu kwa ajili ya kujitafutia maisha yake ya baadae akitoka katika Ofisi hiyo, Kambi ya Upinzani ingependa kujua nini ulikuwa msingi wa Bunge hili tukufu kupitisha Sheria Na. 3 ya 1999 (Political Service Retirement Benefit Act, 1999) pamoja na marekebisho yake?



UBADHIRIFU WA MALI ZA UMMA

33. Mheshimiwa Spika, kumekuwepo na ubadhirifu mkubwa wa mali za Umma kutokana na rushwa na ufisadi ambapo kila mwaka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali anatoa taarifa Bungeni akionyesha fedha nyingi ambazo zimepotea na hazina maelezo ya kutosha kwenye Wizara na idara husika za serikali. Katika mwaka wa fedha 2002/2003 Shilingi 65 bilioni ziliripotiwa kupotea, mwaka 2003/2004 Shilingi bilioni 82, mwaka 2004/2005 shilingi bilioni 203, na mwaka 2005/2006 shilingi bilioni 273. Kati ya hizo shilingi bilioni 242 ni za serikali kuu. Ni dhahiri kuwa hakuna hatua zinazochukuliwa kwani kama si hivyo tunaelezaje ongezeko hilo la fedha zinazokosa maelezo kila mwaka? Kambi ya upinzani inahoji ni hatua gani zimechukuliwa kwa upotevu huu mkubwa wa fedha kwa maana ya kuwawajibisha wahusika.

34. Mheshimiwa Spika, ni muhimu pia ikaeleweka kwamba kiasi cha bilioni 242, ambazo zilifanyiwa ubadhirifu na idara mbali mbali za serikali kuu, zingeweza kufanya kimoja kati ya yafuatayo kwa ukamilifu wake:-
i) Kulipa mishahara ya mwaka mzima ya walimu zaidi ya 160,000 wa shule za msingi.
ii) Kununua vitabu zaidi ya 100 milioni.
iii) Kujenga ofisi za serikali na maktaba ya kila kijiji Tanzania.
Mheshimiwa Spika, takwimu hizi ni kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Haki Elimu.

35. Mheshimiwa Spika, katika kupambana na ubadhirifu mkubwa wa mali za serikali, mara baada ya kuchaguliwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania alitangaza kwamba CAG atapewa mamlaka ya kisheria ya kufuatilia taarifa mbaya za fedha. Vile vile, alisema kwamba watumishi watakaohusika na makosa ya matumizi mabovu ya fedha za Umma watafikishwa mbele ya vyombo vya dola washitakiwe na si kupitia mabaraza ya kiutawala ambayo hutoa hatua za kinidhamu zaidi. Kambi ya upinzani si tu inaomba ielezwe kauli hii ya Rais imetekelezwa kiasi gani, bali pia inataka wahusika katika ubadhirifu wa mali za serikali wawajibishwe kama Mhe. Rais alivyoahidi bila kujali cheo au madaraka ya mhusika.

36. Mheshimiwa Spika, kwa ujumla dhana ya Utawala Bora imeendelea kudhoofika kwa kuwepo ubadhirifu mkubwa wa mali za Umma, matumizi mabovu ya fedha za Umma na upotevu wa fedha za umma usiotolewa maelezo ya kutosha. Mambo mengi ambayo yanaweza kutajwa katika kadhia hii ni kama vile; masuala yanayohusu mijadala ya mikataba ya Richmond, ununuzi wa Rada, ununuzi wa Ndege ya Rais, mikataba mibovu ya madini, ujenzi wa Majengo marefu ya Benki Kuu kwa thamani kubwa mno kuliko hata gharama za kujenga New York, London na Tokyo, na matumizi mabaya ya nyadhifa za Serikali kwa kujipatia maslahi binafsi. Kama Serikali itafumbia macho uoza kama huu Tanzania kamwe haitaweza kujigamba kuwa na Utawala Bora ambao utaleta maendeleo.

MUINGILIANO BAINA YA SERIKALI KUU NA ZA MITAA

37. Mheshimiwa Spika, ili kuboresha ushirikishwaji wa wananchi katika masuala ya kimaendeleo serikali za mitaa zinapaswa kupewa kiasi kikubwa cha uhuru ambacho kitaziwezesha kusimamia shughuli za kimaendeleo. Shughuli hizi pamoja na kushirikisha wananchi kwa ukaribu zaidi, pia huhitaji fungu maalum lenye kutosheleza utendaji wa shughuli hizo.

38. Mheshimiwa Spika, Kwa mujibu wa programu ya kurekebisha mfumo wa serikali za mitaa ulioanza mwaka 1996 (Local Government Reforms Programme) serikali za mitaa zimepewa uhuru fulani wa kiutendaji (Devolution). Lakini pamoja na juhudi hizo zote, kambi ya upinzani inaona bado uhuru huo wa serikali za mitaa unadunishwa katika maeneo yafuatayo:-

i) Katika uandalizi wa bajeti. Imebainika kwamba vipaumbele vya bajeti vinavyopendekezwa na wananchi kupitia halmashauri zao huwa havizingatiwi katika ngazi za juu za uandaaji wa bajeti kama vile katika ngazi za Wizara. Matokeo yake ni kupangwa kwa fungu la bajeti lisilowiana na matatizo na mahitaji ya halmashauri husika.

ii) Kupitishwa kwa muswada unaompa mamlaka Waziri anayehusika na serikali za mitaa kuteua madiwani watatu kwa ridhaa yake, kunafinya demokrasia ya wananchi kujichagulia viongozi wao wote katika ngazi za halmashauri.

39. Mheshimiwa Spika, kambi ya upinzani inaona muingiliano huo si jambo bora hata kidogo katika suala zima la kuziimarisha serikali za mitaa na kuleta maendeleo katika halmashauri. Hivyo basi, tunapendekeza yafuatayo:-

Kwanza, vipaumbele vya bajeti vinavyopendekezwa na wananchi katika ngazi za serikali za mitaa vizingatiwe katika uandaaji wa bajeti kuu kwani vipaumbele hivyo huendana na uhalisia wa matatizo na mahitaji ya wananchi. Kambi ya Upinzani ina kila sababu ya kulizungumzia suala hili kwani, tunaelewa kuwa Serikali kuu inatumia takriban robo tatu ya fedha yote. Fedha hizi hugharamia mlolongo wa huduma kadhaa ambazo husimamiwa kwenye ngazi ya serikali kuu, kama vile mishahara ya wafanyakazi, miradi mikuu ya ujenzi, elimu ya sekondari na afya huku Serikali za mitaa zikipewa kiasi kidogo tu cha fedha kisichotosheleza mahitaji.

Pili, wananchi wapewe mamlaka kamili katika kujichagulia wawakilishi wao wenyewe. Mheshimiwa Spika, ni jambo la kushangaza katika nyakati hizi za kidemokrasia, bado viongozi wanapewa mamlaka ya kuwachagulia wananchi wawakilishi wao!!!



MALALAMIKO YA URASIMU TASAF

40. Mheshimiwa Spika, Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tanzania Social Action Fund - TASAF) ni moja ya chachu za maendeleo ya kijamii. Hata hivyo, yamekuwepo malalamiko mengi yanayohusu urasimu katika TASAF hasa baada ya kuhusishwa kwa Ofisi ya TAMISEMI. Kama baadhi ya Wabunge wengi walivyoweza kuchangia katika kipindi cha maswali na majibu kumebainika kuwepo kwa ucheleweshaji wa fedha za utekelezwaji wa miradi ya maendeleo. Zaidi ni kwamba kuchelewa kwa michakato inayofanywa wilayani imetajwa kuwa ndiyo moja ya sababu za ucheleweshwaji wa fedha hizo.

41. Mheshimiwa Spika, Kambi ya upinzani inataka mfuko huu utambuliwe kisheria ili kuwezeshwa kuwa endelevu mpaka pale mkopo wa benki ya dunia utakapokwisha mwaka 2009 hasa ikizingatiwa kwamba gharama kubwa zimeshatumika kuwajengea uwezo watalaam mbalimbali wa TASAF.

UANZISHWAJI WA IDARA YA MIPANGO NA SERA, NA KITENGO CHA UKAGUZI WA NDANI

42. Mheshimiwa Spika, Idara mpya ya Mipango na Sera imeanzishwa katika Ofisi ya Rais. Kambi inahoji uhalali wa kitengo husika hasa ikizingatiwa kwamba kuna Wizara inayohusika na Mipango, ambayo ina idara lukuki. Ni muhimu serikali ikatueleza kama Mhe. Waziri na Wizara yake wameshindwa kufanya kazi kiasi cha kuhitaji usaidizi wa idara mpya. Mheshimiwa Spika, kuundwa kwa idara nyingi zenye muingiliano wa kimajukumu ni matumizi mabovu ya fedha za Umma. Kambi ya Upinzani inaamini kabisa kwamba Wizara ya Mipango, Uchumi na Uwezeshaji inatosheleza kushughulikia majukumu hayo.

43. Mheshimiwa Spika, dhana mpya ya Utumishi wa Umma inatilia mkazo kuipunguzia Serikali shughuli kwa kuachia shughuli zake kufanywa na taasisi mbali mbali kwa niaba yake. Dhana hii kwa kiasi kikubwa inapunguza matumizi ya Serikali na vile vile kuongeza ufanisi katika sekta husika. Hivyo, kitendo cha kuanzishwa kwa idara ya mipango katika Ofisi ya Rais ni kuongeza ukiritimba na kinapingana na dhana hiyo ambayo ilikwisha anzishwa na ilitakiwa iendelee kwa manufaa ya Serikali na Watanzania kwa ujumla.

44. Mheshimiwa Spika, tunaitaka Serikali itueleze sababu za msingi kabisa za kuwepo kwa idara hiyo mpya.

45. Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani pia ingependa kuelezwa sababu za kuanzishwa kwa kitengo cha ukaguzi wa ndani. Ongezeko la bajeti ndilo linalotajwa kama sababu ya msingi kwa kuanzishwa kwa kitengo hicho. Kambi ya upinzani inaelewa kwamba taasisi zote nyeti za serikali zina wakaguzi wa ndani. Je uundwaji wa kitengo hiki unamaanisha kwamba wakaguzi wa ndani hawapo kama ambavyo tunafahamu au wameshindwa kufanya kazi kama inavyotakiwa? Kambi ya Upinzani inatiwa shaka na uundwaji wa kitengo hiki kwani bado sababu za msingi hazijawekwa bayana na hivyo hatuoni sababu za kitengo hiki kuendelea kuwepo. Lengo la hoja hii ni kuhakikisha kwamba hakuna muingiliano wa kimajukumu au uundwaji wa vitengo ama idara zenye majukumu sawa. Hili likizingatiwa litaokoa matumizi holela ya fedha za walipa kodi na kuzielekeza fedha hizi katika shughuli za maendeleo.

IV. SIASA NA MAHUSIANO YA JAMII

46. Mheshimiwa Spika, halitokuwa jambo la busara kwa Kambi ya Upinzani kutoshukuru kwa uwepo wa Ofisi hii muhimu sana. Ofisi hii ina wajibu mkubwa wa kuhakikisha uwepo wa siasa bora na mahusiano mema ya jamii katika taifa letu. Ofisi hii inatarajiwa kuhakikisha kuwa migogoro ya kisiasa na ya kijamii inatafutiwa ufumbuzi wa kudumu ili kudumisha taifa lenye umoja na amani ya kweli. Pamoja na umuhimu wa ofisi hii bado yamekuwepo mapungufu ambayo yamedhoofisha ama utendaji wa ofisi hii au kuhatarisha amani ya taifa letu (hususan kule visiwani Zanzibar).

MAMBO YA SIASA

47. Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inapongeza kuanzishwa kwa mazungumzo kati ya CCM na CUF ya kuupatia ufumbuzi wa kudumu mgogoro wa kisiasa Zanzibar. Hata hivyo, mazungumzo hayo yamechukua muda mrefu hasa ikizingatiwa ni miezi 18 tokea Mheshimiwa Rais alipotoa ahadi ndani ya Bunge hili tukufu ya kulishughulikia suala hili na hadi sasa hakuna maelezo juu ya hatua iliyofikiwa. Kambi ya Upinzani inapenda kupata maelezo juu ya mazungumzo hayo ambayo yakiendelea kuchelewa yanaweza kuiweka nchi yetu katika mtihani mkubwa wa utulivu wa kisiasa.

48. Mheshimiwa Spika, tunaamini kabisa kuwa Watanzania wengi ambao walipiga kura kwa ujumla wao walimpatia Mhe. Rais ridhaa ya kuongoza nchi yetu bila ya kuangalia kuwa ni wa itikadi gani. Kwa imani yao hiyo kwa Rais wao, ni matarajio yao pia kuwa Rais huyo atakuwa ni wa wote bila ya kubagua.

49. Mheshimiwa Spika, vile vile, kwa kuwa Rais Kikwete ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa wakati mmoja, hivyo, kutokana na nyadhifa zake hizo mbili, tunategemea kwa kufuata katiba ya nchi, atatumia kila kofia yake kwa mahali, wakati na rasilimali mwafaka kufanya shughuli inayoendana na kazi mojawapo ya kofia zake hizo mbili.

50. Mheshimiwa Spika, tumeamua kulisema hili ili liwekwe bayana kwa ukweli na Serikali kwamba katika ziara za mikoa ya Kigoma na Rukwa, Mhe. Kikwete alikwenda huko kama Rais wa nchi, na kwa kutumia pesa za walipa kodi wote wa Tanzania. Kitendo chake cha kugeuza mikutano ya hadhara ya kiserikali kuwa uwanja wa kubomoa vyama vya upinzani kinakwenda kinyume na misingi ya utawala bora, hakikubaliki, hakivumiliki, na si cha kistaarabu kwa mpenda demokrasia yeyote yule.
51. Mheshimiwa Spika, hili lilikuwa ni msingi wa malalamiko yaliyotolewa na viongozi wa vyama vya siasa nchini kama ilivyolalamikiwa katika tamko la Wakuu wa Vyama Vilivyoko Kwenye Ushirikiano (CHADEMA, CUF, TLP, NA NCCR MAGEUZI) lililotolewa kwa Wananchi na kwa vyombo vya Habari mnamo tarehe 7 juni, 2007 makao makuu ya CHADEMA Kinondoni, lililobeba kichwa cha habari “TAMKO LA KULAANI JITIHADA ZA RAIS JAKAYA KIKWETE ZA KUUVUNJA UPINZANI NCHINI TANZANIA”.

52. Mheshimiwa Spika, kwa Rais yeyote anayefuata maadili ya utawala bora na anayependa kukuza demokrasia katika nchi yake, kitendo cha kuwa katika ziara ya kiserikali, na kutumia fedha za walipa kodi na madaraka yake kuvunja maadili na misingi ya utawala bora kwa kufanya kazi za kisiasa, ni kitendo cha kumfedhehesha Rais wetu aliyechaguliwa na Watanzania bila kujali itikadi zao.

53. Mheshimiwa Spika, zaidi ya hayo, katika kupitia vitabu vya bajeti kwa Wizara na Idara za Serikali kwa mwaka huu wa fedha, Serikali imetenga kiasi cha Tshs. 220,000,000/= kwa ajili ya mambo ya siasa. Je, Serikali inataka kufanya siasa gani nje ya siasa zinazofanywa na vyama vya siasa? Ikumbukwe kuwa ahadi ya kuonana na vyama vya siasa iliyowahi kutolewa na Rais haikuwahi kutekelezwa. Je, fedha hizo zitatumiwa na Rais kukutana na viongozi wakuu wa vyama vya siasa? Kama siyo hivyo, ni kwa nini hasa itajwe kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya siasa? Tunamuomba Mhe. Waziri afafanue matumizi halisi ya fedha hizo ili kama ni mkopo kwa vyama vya siasa vielewe ili viweze kwenda kukopa huko kwa ajili ya shughuli zao za kisiasa.

54. Mheshimiwa Spika, katika kikao cha Bajeti cha mwaka jana, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Siasa na Mahusiano ya Jamii) alilieleza Bunge lako tukufu kuwa Ofisi yake haikuwa imeanza kazi zake rasmi kwa vile ilikuwa ikijijenga kitaasisi na kazi hiyo ilikuwa ndiyo kwanza imekamilika. Kambi ya Upinzani inapenda kujua sasa baada ya mwaka mzima kupita tokea kauli hiyo kutolewa, Ofisi hii imefanya lipi katika kumsaidia Rais kuimarisha mahusiano ya kisiasa na ya kijamii hapa nchini.

AHADI ZA RAIS

55. Mheshimiwa Spika, moja ya sifa kuu ya Serikali ya awamu ya nne ni jinsi ambavyo iliweza kuwajaza wananchi matumaini kwa ahadi kedekede wakati wa kampeni na hata baada ya Serikali hiyo kuingia madarakani. Ahadi hizi zililenga kutoa picha ya Maisha bora kwa kila Mtanzania. Cha kusikitisha ni kwamba kadiri siku zinavyokwenda maisha ya Mtanzania yanazidi kuwa duni. Baya zaidi ni uamuzi wa serikali kupitia Bajeti kuu mwaka 2007/2008 kupandisha kodi katika mafuta, bidhaa ambayo inagusa na kuathiri maisha ya kila siku ya Mtanzania kwa namna tofauti tofauti. Kinachojidhihirisha ni kuwa ahadi hizi zilitumika kama danganya toto tu kwa wapiga kura

56. Mheshimiwa Spika, swali ambalo kambi ya upinzani inajiuliza ni kama wananchi wamesahaulika au ahadi hizo zimeshindwa kutekelezeka? Ahadi hizo ni nyingi sana, kama baadhi yake zilivyoorodheshwa katika makala iliytolewa na HAKIELIMU kwa jina la “Government Promises” ya mwaka 2006 na nyenginezo ambazo zimeendelea kutolewa wakati Rais akiwa madarakani. Kambi ya upinzani inayo shauku ya kujua zimeshatekelezwa ahadi ngapi katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu wa Serikali ya Awamu ya Nne na ngapi zimebaki, hasa ikizingatiwa kauli ya Mheshimiwa Waziri kwenye kamati kwamba ahadi zinatolewa katika kipindi cha miaka 5 na hivyo ahadi hizo zote zinatakiwa ziwe zimetekelezwa katika kipindi cha miaka 5.

57. Mheshimiwa Spika, Baada ya kuyasema hayo, kwa mara nyengine natoa shukurani zangu kwako kwa kunipa fursa hii, na Waheshimiwa Wabunge wote kwa kunisikiliza. Nasema Asanteni sana. Na naomba kuwasilisha.

………………………..
SHOKA KHAMIS JUMA (MB)
K.N.Y MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI,
OFISI YA RAIS MENEJIMENTI YA UMMA.
02. 07. 2007
 

Attachments

Tunaendelea kukumbusha, nyumba zetu zirejeshwe


HII si mara ya kwanza, ya pili na ya tatu kukumbusha kuhusu hili tunalotaka kulikumbusha. Tuliandika, tukaandika tena na sasa tunaandika kwa mara nyingine, tukijua vyema kwamba Bunge la Bajeti linakutana Dodoma na bado lina siku kadhaa za kuendelea kukutana.
Kama tulivyopata kuahidi siku zilizopita, tunaamini kwamba, Rais Kikwete, mawaziri wake na wabunge kwa ujumla wao walisikia kile tunachokililia na kimsingi tutaendelea kulipigania hilo hadi hapo tutakapoona limemalizika na kuhitimishwa.

Uamuzi wa serikali kuzirejesha nyumba hizo za serikali ulitangazwa hadharani kwa mara ya kwanza na Rais Jakaya Kikwete wakati alipokuwa akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari, Ikulu jijini Dar es Salaam mwanzoni mwa mwezi Oktoba mwaka jana.

Zaidi ya mwezi mmoja tangu atoe kauli hiyo, Naibu Waziri wa Miundombinu, Dk. Makongoro Mahanga, aliusisitizia uamuzi huo bungeni mjini Dodoma.

Kama alivyosema Rais, Makongoro katika kauli yake hiyo ya bungeni alieleza kwamba, baadhi ya nyumba zitakazorudishwa ni zile ambazo ziko katika maeneo nyeti kama vile hospitalini na katika maeneo ya majeshi.

Hata hivyo, Makongoro hakuishia hapo, bali alikwenda mbali zaidi na kusema kwamba, sehemu ya nyumba zitakazorejeshwa ni zile ambazo uuzwaji wake haukufuata taratibu halali za kiserikali.

Tukiwa ni sehemu ya Watanzania ambao tumekuwa tukilifuatilia jambo hili kwa muda mrefu, msimamo wetu wa kupingana kabisa na maamuzi ya serikali kuuza nyumba za serikali unaendelea kubakia ule ule.

Kama tulivyokwisha kuandika mara kadhaa siku zilizopita, sisi wa Tanzania Daima, kwamba maamuzi ya Baraza la Mawaziri ya kuuza nyumba za umma kwa watumishi wake, bila kujali iwapo walikuwa na sifa au hawakuwa nazo, ni mabaya na ambayo kimsingi yanapaswa kubatilishwa.

Tunasema ni ya ovyo kwa sababu, maamuzi hayo yalifanywa katika misingi ya kibinafsi na yaliyolenga kulisaidia kundi dogo la viongozi na kusahau kwamba, dhamana ya mtu kuwa mtumishi au kiongozi wa serikali ni ya muda tu na wala haimpi nafasi ya kumiliki mali ambazo kimsingi zingekuja kutumiwa na viongozi wajao wa umma.

Ni kwa kuzingatia ukweli huo basi ndiyo maana tunakiona hata hiki kitendo cha serikali kuendelea kukaa kimya pasipo kueleza mahali ilikofika katika kufanikisha zoezi hili muhimu kwa masilahi ya taifa kuwa si kizuri.

Hata hivyo wakati tukitaka kusikia matokeo ya operesheni hiyo ya kimya kimya ya serikali tunapenda kutumia fursa hii kusisitiza msimamo wetu wa kutaka nyumba zote zilizouzwa zirejeshwe na si baadhi ya nyumba.

Tunasema hivyo tukitambua kwamba uamuzi mzima wa kuziuza zile nyumba ulifikiwa kwa makosa tu na kwa hiyo unapaswa kutenguliwa na serikali kuangalia namna ya kulipana na hao wanunuzi wake.

Ni jambo lisiloingia akilini kwa serikali kudai kwamba kulikuwa na kasoro katika suala zima la uuzwaji wa nyumba hizo, na halafu ikasisitiza tu kuwa zitakazorejeshwa ni baadhi tu ya nyumba.

Kwa sababu hiyo basi, wakati huu tunapowasubiri wabunge wetu waanze kuijadili bajeti, tunawaomba wasisahau kudai kurejeshwa kwa nyumba zetu zote zilizouzwa kwa mlango wa nyuma.

Kama alivyopendekeza Mbunge wa Wawi jana, Hamad Rashid, wakati akisoma maoni ya wapinzani kuhusu bajeti ya mwaka ujao wa fedha juu ya haja ya kuuzwa kwa ndege ya rais, suala la urejeshwaji wa nyumba zetu nalo lifanywe kuwa moja ya ajenda muhimu wakati wa kikao hiki cha Bunge.

Baadhi yetu tumekuwa tukishangazwa na ukimya wa wawakilishi wetu kuamua kuliacha suala hili likasahaulishwa kwa sababu tu ya kuweka macho yetu yote katika masuala mengine mapya na kusahau dhoruba mbaya kama hii iliyowahi kulikumba taifa. Wabunge daini nyumba zetu.
 
xx50.jpg


MKAPA YUKO BIZE ANAKULA BWANA AAAGH
 
Back
Top Bottom