Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

NAMI nasema kuwa ni kumsumbua baba wa Taifa letu Nyerere,
Alimwamini huyu jamaa badala ya kuwasaidia watanzania yeye kaamua kufanyia ujasiriamali ikulu.

Mkapa aliposema mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe ni kuwa alikuwa anamaanisha na waliopo ikulu pia watumie nguvu zao huko huko ikulu,.

This is HELL.NO MORE COMMENTS.
 
Mwalimu Nyerere akifufuka halafu apige misele State Hoouse lazima atafunga breki za visigino... huenda akafa kwa cardiac arrest!
 
The East African
November 17 - November 23, 1999
http://www.nationaudio.com/News/EastAfrican/151199/Regional/Regional31.html

By FAUSTINE RWAMBALI
SPECIAL CORRESPONDENT

THE SINCERITY of President Benjamin Mkapa's anti-graft drive has been called into question, following revelations that top officials in his government and a non-governmental organisation run by his wife, helped themselves to public funds totalling Tsh942 million ($1.18 million).

A cabinet minister, a regional commissioner and State House are among 29 institutions and individuals who bought assets with loans from the National Bank of Commerce Holding Corporation, in open violation of the Act that established the Corporation in 1997.

Its mandate was to dispose of the assets and liabilities of the defunct bank and, as such, it cannot assume the functions of a banking institution.

The managing director of the bank's Holding Corporation, Mrs Edna Lupembe, said all the 29 bodies bought real estate on the understanding that they would make a down payment of 25 per cent of the value and pay the remaining 75 per cent after two weeks.

However, most of them did not meet these conditions, and fresh contracts had to be drawn up to enable them to pay in three to four lump-sum instalments by the end of next year.

Mrs Lupembe said that the Corporation's board of directors duly sanctioned the new arrangement, a move some observers say was inherently illegal as the Corporation went beyond the call of duty.

However, Mrs Lupembe disclosed that some of the debtors had since paid back their loans. These include the Mozambique High Commission, the National Social Security Fund, the Nachingwea Education Fund, Majembe Auction Mart and 12 individuals, among them the Minister for Agriculture and Co-operatives, William Kusila, and the wife of the City Commission Chairman, Mrs Cecilia Keenja.

The Finance Minister, Mr Daniel Yona, first broke the news of the loans in the National Assembly sitting in Dodoma on November 8. But he later retracted his statement, saying the 29 had not borrowed any money but had "bought buildings under special arrangements."

The opposition reacted angrily to the revelations, charging that it was corruption by another name.

The MP for Magu, Mr John Momose Cheyo, who is also the shadow finance minister, said that the decision to issue loans contravened the Act that established the Corporation. Mr Cheyo later told The EastAfrican: "Corruption has many interpretations, one of them may entail acquiring property by virtue of one's position of power."

Other MPs had earlier expressed similar concerns in the House, and questioned both the secrecy under which the loans were given out and the positions of privilege of those who benefited from the "special arrangement".

At the centre of the controversy is a building which was sold to the the Equal Opportunities for All Trust Fund, whose chairperson is the First Lady, Mrs Anna Mkapa. The building now houses the National Bureau de Change along Morogoro Road in the city. It was sold at Tsh650 million, but before that amount was fully settled, the trust fund leased it to the bureau, which pays rents to the First Lady's trust fund.

Already, the Bureau has paid a hefty Tsh481.2 million ($601,536) in a two-year rental contract with the fund. The trust fund is registered as a non-profit making organisation. The bureau de change has rented a total of 592 sq metre at $17 per sq mt per month for a period of two years.

The trust fund took more than two-thirds of the total loans; the other third went to 28 other institutions – including the State House – and individuals.

By the end of last week, the fund still owed the Corporation Tsh457 million. According to Mrs Lupembe, Mrs Mkapa's trust fund is required to pay another Tsh167 million by the end of next month.

"We are holding all the title deeds for the buildings, and for those who fail to pay as per contract, we will revoke that offer with 10 per cent less," she said.

A top official of the National Bureau de Change who declined to be named told The EastAfrican: "We have nothing to do with the building. We do not own it. We are mere tenants. Go and ask the fund or the bank's Holding Corporation."

The official also declined to reveal details of the terms of the tenancy agreement, including the rent the bureau was paying.

Mrs Lupembe also said she knew nothing about the tenancy agreement or when and how the building was rehabilitated. However, she admitted that the Holding Corporation still legally owned the building. "We are the ones holding the title deed, so it is ours," she said, but declined to comment on who collected the rent.

A spokesperson for the trust fund, Ms Violet Maro, said curtly: "Ask the NBC Holding Corporation. They have everything you would like to know."

A day before, Ms Maro, had promised to provide all the information herself: "All the files are in the office. Get in touch with me tomorrow,'' she told this reporter.

The Acting National Chairman of the Tanzania Labour Party, Mr Augustine Mrema, said last week that, in a "clean" government, the wife of a sitting president cannot involve her charity organisations in doing business.

"They want to fool the public with contradicting statements but the whole deal was dubious," he said, adding: "The late Mwalimu Nyerere, who led Tanzania for more than 30 years, had no NGO during his tenure. He went into that business after retirement." He said that Mwalimu had avoided that because he knew that such NGOs could easily turn into family affairs under the guise of working for the public good.
 
November 24 - November 30 1999
By FAUSTINE RWAMBALI
THE EASTAFRICAN
http://www.nationaudio.com/News/EastAfrican/221199/Regional/Regional24.html


THERE WAS no statement by the weekend from an emergency board meeting reportedly called by Tanzania's First Lady Anna Mkapa, following reports that an NGO she heads had acquired public property using her position as the president's wife.

Last Wednesday, an aide to Mrs Mkapa, one Fatuma Riama, was quoted by the local press as saying the Board of Directors of the Equal Opportunities for All Trust Fund would meet the next day to discuss the accusations and later give a press statement. Mrs Mkapa was expected to chair the meeting.

Mrs Mkapa's NGO was among 29 institutions and individuals who bought real estate on loan from the NBC Holding Corporation last year, a sale opposition members of parliament say was "illegal" because NBC Holding Corporation was not established to function as a financial institution.

The fund's spokesperson, Ms Violet Maro, was said to be away in Dodoma when this newspaper sought a statement from her at the weekend. However, when The EastAfrican called her home a second time, a woman at the other end of the line said Ms Maro was actually in the city, but had gone out.

When pressed for further details, she: "She is somewhere in the city. Leave a message and please don't disturb me any more," before slamming the phone down.

The NGO bought the building located along Morogoro Road in the city on credit from the NBC Holding Corporation for Tsh650 million ($812,500), contrary to the provisions of the Act that established NBC Holding Corporation in 1997. Under the Act, the Corporation's brief was to dispose of the assets of the defunct National Bank of Commerce (NBC) and collect its outstanding debts.

However, the NBC Holding Corporation sold some of the real-estate properties on credit, a function which analysts say is the preserve of financial institutions.

Meanwhile, the Finance Minister, Mr Daniel Yona, has denied that he had told the National Assembly in Dodoma that the NBC Holding Corporation had given loans amounting to Tsh942 million ($ 1.18 million). In earlier press reports from Dodoma Mrs Mkapa's Fund was said to have taken the lion's share.

"I introduced my NBC 1997 Bill by reading a speech in which there was no mention of NBC Holding Corporation selling properties. Then the spokesman for the opposition spoke and that was when I heard about NBC Holding 'giving loans'," the minister said in a protest note to this newspaper last Monday [see letter on Page 10].

The minister also wrote: "I asked Mr Philip Magani, Chairman of NBC Holding Corporation, to clarify the matter. His clarification was similar to that given to the press by Mrs (Edna) Lupembe, the managing director of NBC Holding Corporation."

Mrs Lupembe said all the 29 bodies bought real estate on the understanding that they would make a down payment of 25 per cent of the value and pay the remaining 75 per cent after two weeks. However, most of them did not meet these conditions and fresh contracts had to be drawn up to enable them to pay in three to four lump-sum instalments.
 
Mkapa aachwe astaafu kwa amani

HabariLeo; Wednesday,May 30, 2007 @13:43


KATIKA siku za hivi karibuni, tumeshuhudia baadhi
ya magazeti yakiandika habari zinazodaiwa
kuwa za uchunguzi kuhusu mikopo ambayo ilitolewa
na benki hapa nchini kwa kampuni inayohusishwa
na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin
Mkapa na mkewe Anna.

Kwa ufupi, taarifa hizo zinahusu mkopo ambao inasemekana
Mkapa aliupata kutoka benki mbili za hapa nchini,
na ambao ameshaurejesha. Mkapa, kama Mtanzania yeyote
yule ana haki ya kuwekeza katika biashara na ana haki ya
kupata mkopo. Isitoshe, ametuonyesha kwamba mtu
anapokopa kwenye tasisi za fedha, lazima arejeshe.
Kinachotushangaza ni namna ambavyo habari hizo
zimeandikwa, kwani kuna wakati hazizingatii maadili ya
uandishi wa habari ambayo yanakemea mtindo wa kuweka
maoni ya mwandishi katika taarifa ambayo sio maoni
au uchambuzi.

Inatuwia vigumu kuamini kuwa taarifa hizo ni za
uchunguzi wa kawaida kwani uchunguzi makini ungeliangalia
namna benki zinavyotoa mikopo kwa wafanyabiashara
kwa ujumla na sio mtu mmoja tu. Kwa hali hiyo
tulitegemea kuwa magazeti hayo yangeanza mikopo iliyotolewa
na wafanyabiashara wengine, ambao baadhi yao
bado wanadaiwa na taasisi za fedha.

Tunachoona sisi, na bila shaka Watanzania wengine, ni
dalili ya wazi ya kumuandama Rais Mstaafu wa Awamu ya
Tatu kwa sababu ambazo hazina msingi zaidi ya chuki.
Aidha wale wanaomwandama hawaoni mbali, kwao
wanachokiona ni Mkapa na sio mustakabali wa nchi hii.
Tanzania imeonyesha njia kwa nchi za Afrika kwa kuwa
na mpangilio mzuri wa urithi wa kisiasa wa kidemokrasia
ambao umeshuhudia viongozi wetu wakikabidhiana
madaraka baada ya kumalizika kwa vipindi vyao vya
kidemokrasia.

Mfumo wetu wa kisiasa umewezesha viongozi wetu
wameheshimu vipindi vyao vya kuongoza nchi na kamwe
hawajatafuta mbinu za kujiongezea muda ili waendelee
kutawala ili kulinda maslahi yao binafsi kama ambavyo
tumeshuhudia katika baadhi ya nchi nyingine za Kiafrika.
Tumeshuhudia baadhi ya marais waliostaafu katika nchi
hizo wakisakamwa hadi kufikia hatua za kugawa nchi.
Kwa bahati nzuri kwa Tanzania, marais wetu
wanakabidhiana madaraka na kila mmoja anajenga
kwenye misingi iliyowekwa na mwenzake. Urithi huu umetuwezesha
kujenga umoja nchini mwetu.

Watanzania wana safari ndefu ya kujiletea maendeleo na
wasingependa kurudishwa nyuma kwa namna yoyote ile.
Mkapa amefanya mengi kwa taifa hili na tumpe nafasi
ya kustaafu na kupumzika bila bughudha yoyote.
 
Hili wazo lako binafsi kimsingi ni zuri. Lakini watu wana mitizamo tofauti ni vizuri ukaikubali na inaweza isiwe chuki binafsi. Watu wanaobebewa mabango mbona ni wengi na si rais mstaafu pekee?! Kwa nyakati tofauti!
Kwa viongozi wa Tanzania "kukabidhiana madaraka" kwa amani isichukuliwe kuwa wao ndio wako clean Afrika nzima! La hasha! Inawezekana kabisa wao walishachukua chao mapemaa na inapofikia miaka 10 hakuna noma kuachia ngazi. Na kisha wakiachia ngazi, kwa woga wetu wabongo hatuwezi kuwafanya chochote tofauti na nchi zingine za afrika ambapo watu wako more aggressive na ndio maana hawaondoki, akiondoka tu wanamlawiti, sorry, I mean wanamshughulikia. Au mwasemaje?
 
Domokrasi, leta vitu. Umetupa mwanga mpya. Barua ya Yona, iko wapi?
 
Alaaaa! mchezo huu umeanza long mjomba wewe subiri utakuja ona mengi sana huu ni mwanzo tu..Pia kumbuka ushirikiano wa huyu mjomba na Blair!...haukuanza kwa mapenzi ya Uongozi bora!.

Mwenzake anakimbia mapema Uongozi maana jikoni joto limezidi!
 
Mkapa kafanya mengim hebu yatajwe nasi tuyajue!!!!
 
Ben kafanya mengi mazuri kwa nchi hii hilo hatukatai, lakini hiyo ndio tiketi ya kumruhusu kufanya na machafu? Kiburi cha kukaa kimya kujibu tuhuma chafu dhidi yake ndicho kinacholeta kichefuchefu. Asimame ajisafishe au kuomba radhi kwa matumizi mabaya ya dhamana tuliyompa ili tumuache akae astaafu kwa amani. Huo ndio uungwana na heshima kwake. Aelewe jambo moja chafu linachafua tisini na tisa safi. Akiwa bado hai anaweza shuhudia mabadiliko katika uongozi na serikali ya "washikaji" ikaondoka wakaja wengine ambao watataka majibu hayo katika njia ambazo yeye ataziona sio za kiungwana. Amuulize mwenzie Chiluba nini kinatokea kwake.
 
Huyu mtoto wa Mkapa anaanza kutukana watu tena, kisa babake anasemwa.

On 6/2/07, S.B. Mkapa <sbm_3@yahoo.com> wrote:
Point taken! l
Lakini huyu jamaa amezidi ushabiki wa kijinga What is TOK kama sio umbeya?

Jenga Ngalawa < ngalawa@yahoo.com> wrote:
Steve,
Try to respect others, even when you have different
viewpoints ... name-calling is not helping anybody.
jenga
--- list-bounces@tanzanet-online.org
wrote:
> Can you Please say what you are stupidity is
thinking? sounding like an idiot! If you have proof
provide!!!!!!!!!!!!!!!
>
 
Mtanzania,'
Kumbe na wewe bado uko kwenye ile forum. Mbona sijakuona siku nyingi? Niandikie PM tulonge kidogo.
 
Ben kafanya nini? Angalia:

Tom ana chungwa moja; ukimpa machugwa mengine manne halafu baadaye ukamnyanganya matano atabaki na nini?

Jibu: Tom atapigana mpaka urudishe yote!!!
 
Mtanzania, Samahani kwani huyo list-bounces ndio mtoto wa Mkapa?.... naona Steve hapo juu kaandika:-
Point taken! l
Lakini huyu jamaa amezidi ushabiki wa kijinga What is TOK kama sio umbeya?


Sioni tusi!
 
Mkandara,

Aliyetukana hapo chini ni yeye steve, bahati mbaya kwenye reply jina lake halikuonekana. Mails zote mbili ni za kwake yeye. Haya meneno ya
"Can you Please say what you are stupidity is
thinking? sounding like an idiot! If you have proof
provide!!!!!!!!!!!!!!!" ni ya Steve
 
Naomba mtazamo wenu katika hili. Naomba hii thread isiunganishwe na ile ya Mkapa kwani kufanya hivyo kunapunguza sana uchangiaji toka kwa wajumbe wa forum hii. Natanguliza shukrani.
 
Rais Mkapa Azungumzie utajiri wake na awe mkweli na muwazi!

Tangu kuondoka madarakani kwa aliyekuwa Rais wa Tanzania Bw. Benjamin Mkapa tuhuma na madai mbalimbali yamekuwa yakimuandama mstaafu huyo kila kukicha. Madai ya hivi karibuni ambayo yamekuwa ni kama chumvi kwenye kidonda na mafuta ya taa kwenye moto wa kuni, ni yale ya Bw. Mkapa kujipatia mkopo wa benki na hatimaye kuanzisha kampuni ya biashara wakati akiwa bado katika kiti cha urais. Kabla ya madai haya ya sasa kulikuwa na madai mengine mengi ambayo yanamhusisha Rais Mkapa mwenyewe, mkewe au familia yake ya karibu.

Mara hizo zote, juhudi za kumtaka Rais Mkapa azungumzie na kujibu madai na tuhuma zinazotolewa dhidi yake zimegonga mwamba. Lakini kwa vile Tanzania hatuna wafalme, na viongozi hutawala kwa ridhaa ya watu, na ya kuwa katika nchi ya kidemokrasia kama ya kwetu viongozi huwajibika kwa watu basi hatuna budi kwa mara nyingine tena kumtaka Rais mstaafu Bw. Benjamin William Mkapa kuzungumzia utajiri alioupata akiwa madarakani na kuonesha kwa vielelezo kamili kuwa utajiri wake kaupata kwa njia ya halali na siyo kwa sababu ya kutumia cheo na nafasi yake ya Urais.

Kwa watu wengi ambao wanafuatilia tuhuma zilizotolewa na zinazoendelea kutolewa kwa Rais Mkapa watakumbuka kuwa kati ya tuhuma zote kubwa ya zote ni ile tuhuma ya kuhusika kwake katika ununuzi wa rada ya kijeshi ambayo Benki ya Dunia ilisema ni ghali mno na haikufaa kwa matumizi ya Tanzania. Baada ya mamlaka za Uingereza kuanza kufanya uchunguzi wa kampuni iliyohusika na uuzaji wa rada hiyo, watu na taasisi mbalimbali hapa nyumbani na nje ya nchi walijenga hoja kuwa Bw. Mkapa azungumze na wananchi na awaambie ni kwa kiwango gani alishiriki katika ununuzi wa rada hiyo. Kelele hizo zilipozidi, Rais Kikwete akiwa katika moja ya ziara zake nje ya nchi (Brussels, Ubelgiji) aliingilia kati na kuwauliza Watanzania “Hivi mnataka mzee Mkapa atoe sauti, sauti kuhusu jambo gani? Mnataka aseme nini, mimi naona tumwache mzee wa watu”.

Suala hili la uanzishaji wa kampuni uliofanywa na Rais Mkapa na mkewe mwaka wa nne tu wa Urais wao umezidi kuzua wasiwasi na hisia za kuwa Rais Mkapa hakuwa mtu “msafi” kama tulivyofanywa kuamini wakati wa uchaguzi wa 1995. Hata hivi sasa watu na taasisi mbalimbali zinapomtaka Rais mstaafu huyo kuzungumzia miradi yake wakati akiwa katika ofisi ya juu kabisa nchini, kelele za “mwacheni mzee wetu” zimeanza tena kusikika. Tahariri ya mojawapo ya magazeti ya serikali wiki iliyopita ililitamka bila haya au kigugumizi chochote kile kuwa “Mkapa amefanya mengi kwa taifa hili na tumpe nafasi ya kustaafu na kupumzika bila bughudha yoyote.”

Kwa baadhi ya watu kumtaka Mtanzania mwenzetu huyo kutuambia na kututhibitishia kuwa hakutumia nafasi yake vibaya alipokuwa madarakani ni “bughdha” isiyo ya lazima na ni sawa na “kumuandama Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu kwa sababu ambazo hazina msingi zaidi ya chuki.”. Kwa watetezi hawa wa usiri, kuulizia kiongozi aliyepita katikati yetu na kuomba kura zetu mara mbili akiahidi kupigana vita dhidi ya ufisadi huku akipepea bendera ya "uwazi na ukweli" basi imekuwa tatizo. Tunapouliza ni jinsi gani kiongozi tuliyemweka madarakani kwa kura alitumia ridhaa hiyo na kama hakuitumia ridhaa hiyo kujinufaisha yeye na familia yake imekuwa nongwa.

Ndugu zangu kama waswahili wasemavyo, “akutukanaye hakuchagulii tusi”. Mtanzania mwenzetu tulimchagua atuongoze kwani tuliambiwa kuwa kati ya wale wote walioonesha nia ya kutaka kwenda Ikulu mwaka 1995 yeye ndiye aliyekuwa “msafi”. Nakumbuka alivyonadishwa na Mwalimu Nyerere pale uwanja wa Nyamagana. Tukamchagua na kumpa dhamana ya uongozi wa nchi yetu. Miaka kumi baadaye Mtanzania huyo anaondoka Ikulu akiwa Bilionea na watetezi wake wanatuambia tusiulize kazipataje, kweli woga mwingine! Kiongozi ameondoka akiwa na majumba bwelele ya kupanga na makazi, ndani na nje, akiwa na akaunti za fedha hapa nyumbani na ugenini, na akiendelea “kutesa” kiulaini kwa pensheni na mafao kadha wa kadha yanayotokana na ofisi yake iweje kumuuliza kuwe kosa? Kumuuliza “mzee utuambie umevipataje vitu hivi vyote ndani ya miaka 10, wakati yule aliyetawala nchi yetu miaka 25 hakuweza” tunaambiwa ati tunambughudhi mzee. Hoja nyingine ni za kutupa zinapotolewa tu hadharani.

Ukweli ni kuwa watetezi wa Mkapa wanatutaka tukae kimya kwa vile hata tuulize vipi hatutapewa majibu. Binafsi naona kuwa wale wanaotutaka tunyamaze tusiulizie utajiri wa Rais Mkapa wanatumia visingizio vya "Amani ya Tanzania", "Kubadilisha uongozi kwa ustaarabu" na "uzee wa Mkapa" kama mbinu ya mazingaombwe ili tusione viini macho vinavyotendeka au vilivyokwisha tendeka. Mbinu zao hizo zinatokana na hofu moja tu, nayo ni hofu ya ukweli. Watetezi wa Rais Mkapa wanaogopa ukweli kujulikana na watu wa kawaida kwani sifa zote za "amefanya mengi kwa Taifa hili" zitapeperuka hewani kama vumbi kwenye jani kavu lipeperushwapo na upepo. Watetezi hawa siyo tu hawako tayari kuuacha ukweli ujulikane bali hawawezi kustahili kuona ukweli huo! utawaumbua.

Kuhusu hili suala la Rais kupewa mkopo wa dola laki tano na kuweza kuanzisha biashara akiwa ofisini na kutajwa ati huo ni mfano mzuri wa kukopa kutoka benki na klipa. Wazo hilo kwanza linatuchekesha na linasikitisha mno. Kama alikuwa ni mfano mbona hatukuambiwa wakati anakopa na kurudisha fedha hizo ili tumuige? Kwanini awe mfano baada ya siri kufichuka? Hivi wanataka Watanzania tuamini kuwa Rais Mkapa alikwenda mwenyewe benki kimya kimya au waseme tu kuwa benki ilimfuata Ikulu.

Sitashangaa kabisa kuwa imekuwa vigumu kwa Rais Mkapa kufuatilia kwa makini na kwa uzito unaostahili tuhuma na madai yote yanatolewa dhidi yake binafsi na familia yake. Hili linawezekana aidha kutokana na wingi wake au kwa sababu nyingine yoyote, nimeona nijitolee basi kwa moyo wangu wa ukarimu kuorodhesha tuhuma na manung’uniko ambayo yamejaa mitaani kuhusu utawala wake na hasa kwenye suala hili la kujitengenezea utajiri wa haraka haraka ndani ya miaka kumi ya kukalia kiti urais wa jamhuri yetu. Madai hayo ni haya:

Kwamba akiwa Rais na kwa kutumia nafasi hiyo aliweza kujipatia mkopo mkubwa kutoka benki miaka minne tu ya utawala wake tena alifanya hivyo wakati watanzania wako katika kumuuguza baba wa Taifa. Kwa mtu aliyepewa kwa dezo nafasi hiyo na Mwalimu Nyerere kitendo hicho kinaonekana ni cha kisaliti na kuvunja vunja kila ambacho Mwalimu alisimamia.
Kwamba katika kipindi chake hicho kifupi aliweza kukusanya fedha kiasi cha kujenga jumba Lushoto, kufanyia matengenezo nyumba ya Sea View, kujenga jumba jipya Msasani, na kununua nyumba/hoteli huko Afrika ya Kusini na ikadaiwa alimuomba mzee Madiba aipe baraka zake, na mzee huyo akamkatalia.
Kwamba ilikuwa ni kutokana na baraka zake Taifa letu likaingia kwenye Mkataba wa kununua rada ya kijeshi ambayo kwa mujibu wa Benki ya Dunia ilikuwa ni “ghali na kwa Tanzania haifai”. Baadaye imekuja kugundulika kuwa dalali aliyeshiriki kutuuzia rada hiyo alimegewa karibu dola milioni 12 kwa kazi yake huku akiwagawia watu wachache serikalini. Je yeye (Mkapa) alijua kuhusu mgao huu kwa “namna yoyote” ile.
Kwamba ilikuwa ni katika uongozi wake Taifa letu likaingizwa kwenye mikataba ya ajabu ya uwekezaji na ile ya ubinafsishaji. Ilikuwa vipi yeye kama Rais kushindwa kabisa kuweka maslahi ya Taifa mbele hadi mrithi wake anapokuja ndipo makosa yanaonekana hadi kudaiwa kuwa Tanzania “hatuna wataalam wa mikataba”? Kama alijua wataalam wetu hawajabobea katika mikataba hii mikubwa ya biashara kwanini hakuomba msaada mapema hadi leo tunalazimika kuwaomba watuonee huruma na kuanza “kupitia tena mikataba”?
Kwa vile alianza biashara zake na “ujasiriamali” akiwa bado Rais, ni kwa jinsi gani shughuli zake hizo ziliingilia utendaji kazi wa ofisi yake au yeye mwenyewe na hivyo kuathiri matokeo ya kazi zake alizoapishwa kikatiba. Je, haoni kuwa wazo la Rais kuanza kufanya biashara kubwa akiwa ofisini inaleta picha mbaya na hasa kuonesha mgongano wa maslahi?
Kama kweli katika kufanya biashara hizo akiwa Ikulu alitaka kuwa mfano kwa Watanzania wengine ni kwanini Watanzania hawakuambiwa kuwa Rais wao ni mjasiriamali na ameanzisha biashara kama wengine, na kwanini hakujitolea kuwa mfano wa kukopa kutoka benki na kulipa?
Kwamba, kwa kutumia vyombo vya dola alilazimisha mali ya Watanzania kuendeshwa na wageni ambao baadaye tukagundua kuwa hawakuwa na uwezo wa kutuendeshea kampuni yetu. Je haoni haja ya kuwaomba wananchi msamaha kwa kutudhalilisha kiasi hicho wakati mapolisi na mitutu yao walipowaingiza kwa nguvu watendaji wa Tanesco toka Afrika ya Kusini?
Kwamba, alipokuwa kwenye mkutano wa baraza la kiuchumi kule Davos, Uswisi ilipigwa haramba iliyoongozwa na mcheza filamu maarufu Bi. Sharon Stone ambapo kiasi cha dola milioni moja zilichangwa ndani ya dakika tano ili kumpa Rais Mkapa katika juhudi za “nchi yake kupambana na ugonjwa wa Malaria”. Aliporudi na hata baadaye, Watanzania hatujaambiwa ahadi ya kiasi hicho ilitimizwa vipi? Ni kiasi gani kiliweza kupatikana taslimu na fedha hizo zilitumiwa vipi na kikundi gani katika juhudi za kuangamiza ugonjwa wa Malaria? Kwanini hakutuambia wakati huo?

Basi, hayo ni maswali machache ambayo yako mitaani na Watanzania kwa kweli wangependa wasikie majibu yake kwa ukweli na uwazi. Kwa kufanya hivyo atajijengea heshima kwa wananchi na kuonesha mfano wa ujasiri wa kiongozi kutoogopa maswali. Hata hivyo kama ataendelea kuwa kimya (kama ilivyo kawaida ya baadhi ya viongozi) basi anawapa Watanzania idhini ya kujaribu kutafuta ukweli kwa njia yoyote ile zikiwemo njia za kisheria. Itakuwa ni jambo la kusikitisha sana na la aibu endapo kesi itafunguliwa katika mahakama ya nyumbani au nje ya nchi ili kutafuta ukweli wa utawala wa Rais Mkapa. Viongozi wetu lazima waanze kubadilika kwani Watanzania waliowazoea miaka ya nyuma waoga oga hivi na wasiothubutu sasa hivi wameanza kuamka.

Kuendelea kukaa kimya na kupuuzia madai dhidi yake Rais Mkapa hajitendei fadhila, hawatendei haki wananchi waliomweka madarakani na haimsaidii kitu zaidi ya kuanza kuonekana amejiunga na jumuiya teule ya viongozi wa kiafrika ambao kwa nguvu zote wameingia Ikulu wakiwa masikini na wakatoka matajiri. Kwa kuendelea kuwa bubu kuhusu madai dhidi yake na familia yake Rais Mkapa ataanza kuonekana ni mmoja wa viongozi wa kiafrika waliotumia nafasi zao kujitajirisha kupitia migongo ya wananchi wao. Licha ya sifa ambazo amezipata nje ya nchi, wakati umefika "mzee wetu mstaafu" azungumze na wananchi wenzake ili aonekane mwenye hekima na siyo kiburi.

Vinginevyo sisi Watanzania wenzake tutaanza kupata jibu la lile swali alilouuliza Mwalimu wakati wa vuguvugu la uchaguzi wa mwaka 1995 baada ya vigogo wengi wa CCM na upinzani kujitokeza kutaka kugombea nafasi ya kuingia Ikulu. Mwalimu aliuliza "watu wengi wanakimbilia Ikulu, Ikulu kuna nini?" Hatujui kama Rais Kikwete naye ameshaanza biashara huko Ikulu au ana mpango huo, hata hivyo inaonekana Rais Mkapa ameanza kutupa jibu la hicho kilichoko Ikulu ambacho "watu wengi wanakimbilia". Tulichobaki kushangaa ni kama ule "utakatifu" wa Ikulu bado upo au uliondoka na Mkapa.

Wasiliana nami: mwanakijiji@jamboforums.com
Piga Simu: +1248 686 2010
 
Mtanzania,

Huyu dogo nafikiri kidogo inam-touch mnapozungumzia baba yake!.. haya ni mapenzi ya baba kwa hiyo nampa benefit of the doubt!..
My guess, accusation did force him to take sides with his dad.
Hata hivyo kulingana na habari nazosikia Steve kabadilika sana! zamani akija club alikuwa mtu wa watu, mtu wa kujichanganya ingawa alikuwa dogo kwetu!
Sasa tabia kama hizi ndio zinatupa taabu sana sisi kutoamini kwamba mtoto wa nyoka sii lazima awe nyoka pia!
 
Mzee Philemon,

Umeyaona haya? Hebu tuwekee mkuu ulisema hawa wana posho na marupurupu ndo maana wanajenga mahekalu kila kona, sasa umeyaona haya?
 
Back
Top Bottom