Angalieni huyu naye Kibaki wa siasa anavyosema. Watu wamesaliti elimu zao, wanatumia umaskini kuomba misaada nje, wakipata wanagawana huku maskini vijijini wanaendelea kuwa maskini. Huyu jamaa sasa ndio mshika mikoba ya Mkapa.
----- Original Message -----
From: Aziz Ponary Mlima
To:
list@tanzanet.org
Sent: Wednesday, June 06, 2007 12:58 PM
Subject: Re: [tanzanet] FWD: Mkapa awe mkweli na muwazi.
Waheshimiwa, "Wasomi"
Niliamua kuwa kimya, lakini kwa suala hili nimaamua kuzungumza machacche hasa baada ya kuangalia hoja zinazotolewa na baadhi ya "Wasomi Wetu" ambao baadhi yao kama wakiwa na ujasiri kidogo na kuupata ubunge wanaweza kuukwaa uwaziri
🙂 Mjadala mzima huu na yale yote yaliyoandikwa kwenye magazeti kwa mwandishi yeyote anayeheshimu taaluma yake na kuwaheshimu wasomaji wake taarifa tulizozisoma siku zilizopita zinatia wasiwasi kiwango cha "Journalism" tuliyonayo kwasasa au tuseme kwa yule aliyeandika makala hayo.
Kilichonifanya kujitupa kwenye mjadala huu siyo yule anayeandika kwa ajili ya kuuza magazeti bali hawa "Wasomi wetu" wanaoweza kupambanua mambo lakini bado wanatekwa katika uwigo wa uandishi usiotaka kutoa taarifa bali kutoa utashi binafsi. Tatizo nilionalo hapa hasa kwa wasomi wetu ni vitu viwili hasusani kwa wale amabo wapo ughaibuni au bado wanaendelea kuishi ughaibuni.
(1) Mazoea ya "Cash-Economy"
(2) Mitazamo iliyopitwa na wakati, "Outdated views"
Nikurudi katika kipengele cha kwanza cha hapo juu, (cash economy mentality) haswa kwa hawa ndugu zangu wasomi waliopo majuu wanaoshangaa mtu kuchukuwa mkopo na kununua nyumba kuna vitu viwili ambavyo ni obvious......
(a) Wanaishi nyumba za kupanga ughaibuni na wamezoe kununua magari mitumba
🙂 kama utanunua gari jipya ughaibuni na hata Nyumbani siku hizi na una ajira inayoeleweka unapata MKOPO kama unakopesheka!
(b) Hali ilivyo nyumbani na kama ilivyo sehemu nyingine yeyote na hasa sisi tuliosomea masuala ya Mabenki na tumekwisha fanaya kazi hizo nyumbani na ughaibuni, Biashara kubwa ya BENKI ni Kukopesha! Na katika nchi yeyote iliyoendelea ukitaka kumjua JUHA au uonekane JUHA fikiria fikiria na fanya mambo kama upo kwenye "cash economy" watu wanakopa kununua magari, wanakopa kusoma, wanakopa kusomesha watoto, wanakopa kufungua makampuni na wanakopa kununua nyumba.
Kama HOJA hapa ni KIONGOZI wa nchi KUKOPA na KUNUNUA Nyumba, VIONGOZI wafuatao WALIKOPA na WALINUNUA NYUMBA wakiwa Madarakani:
Tony & Cherrie Blair (Hyde Park)
Bill & Hilary Clinton (New York)
Goran Person (Sweden)
John Major (Vauxhall Bridge, London-Uingereza)
Margreth Thatcher (Chester Square-London-Uingereza)
James Callaghan (Kennington-London,Uingereza)
Harold Wilson (Ashley Garden & Isle of Scilly)
Edward Heath (Salisbury-Uingereza)
Harold Macmillan (Birch Grove Estate,West Sussex)
Tatizo LIKOWAPI?
Tena nafikiri tukimwona KIONGOZI wa KIAFRIKA amekopa kununua nyumba hata kusomesha watoto wake au kulimia INABIDI TUMPONGEZE kwani anaweza kupiga simu kwa GAVANA NA WA BENKI na Kumwamuru Waziri wa fedha ampatie KIASI chochote bila maswali na kuondoka madarakani hana deni
🙂
Nikirejea kwenye kukopa na kuanzisha shamba, mtu aliyekopa namni hii ni "MKULIMA" na wakulima wetu wote wangekuwa wanakwenda kwa mwendo huo tungekuwa tumeacha kilimo cha jembe la mkono
🙂
Je Kunanzisha Kampuni mtu akiwa madarakani ni dhambi? Jibu ni HAPANA waulize TUME ya MAADILI , HAIKATAZWI, ilimradi kampuni yako haitegemei kupata "favours" zinazotokana na kazi au wadhifa "wako" wewe uliyeanzisha KAMPUNI hiyo.
Zaidi ya Hapo Kampuni ikiwa "LIMITED" ina "LEGAL PERSONALITY" inayojitegemea KAKOTI UPO? na hivyo inatenganishwa kisheria na mmiliki! na kwa KITAALUM, Kumiliki KAMPUNI ni KUMILIKI "HISA" JE WANGAPI LEO hii WANAHISA kwenye Makampuni? Tukianza na yale yetu kama Kiwanda cha Bia, Saruji, Oksijeni, Swissport, Sigara, UMOJA TRUST, na zinginezo? JE hawa WOTE waandikwe MAGAZETINI? Mbona huko ughaibuni haya hayaonekani kama yana mgongano wa maadili?
Nikipitia suala la Kuanzishwa KAMPUNI ya ANBEN LTD mwaka 1999. kuna vitu viwili hapa "Wasomi" inabidi kupambanua:
-Mwaka 2000 ulikuwa "Uchaguzi Mkuu" kama ilivyo kawaida yetu waafrika ukienda kwa Chifu au Ukikutana na "Chifu au Mtemi" huwa kanapelekwa KAKIBUYU ka pombe na ka-kuku" Profesa Mbele upo? Tanzania ni nchi ya Kidemokrasia mkataba wa kukaa IKULU kwa DHAMANA ya wapiga KURA ni miaka Mitano, na ikiisha watanmzania Tumekuwa na jadi ya kuwapa viongozi wetu zawadi kama ilivyokuwa tangu enzi za "Uchifu na Utemi" na kama ilivyo Chifu au Mtemi huwa hashitakiwi wala kudharirishwa hadharani. ndivyo hata taratibu ztu za KITANZANIA zilivyo, hivyo basi, ili kuepuka mambo kama KUKOPA na kushindwa kurejesha mkopo au hata kmapuni ikashindwa kutimiza masharti ya msingi, Busara na kwa Rais au Rais Mstaafu kuanzisha "LEGAL PERSONALITY" Limited Comapany ambayo INAWAJIOBIKA KISHERIA hii ni "COMMON SENSE, LOGICAL REASONABLE ACTION" kwa mtu yeyote anayeheshimu, UWAZI, na MISINGI ya SHERIA za DOLA.
Kampuni inaweza kuitwa Mahakamani lakini Rais au Rais Mstaafu ana "IMMUNITY" sasa KELELE sijuwi zinatoka wapi? au kitivo cha fikra kipo LIKIZO
🙂?
Kwa kuhitimisha, ni muhimu tukahama kutoka kwenye cash economy mentality na kuingia ndani ya ULIMWENGU wa sasa, ndiyo Maana wenzetu Wahindi na Wayahudi na Wazungu wanapinga hatua kwenda mbele kwa kuwa wanatumia MASHIRIKA NA JUMUIYA ZA FEDHA zilizopo kufanya mambo ya KIMAENDELEO wakati sisi tunaimba oooooOh hatuna mitaji wakati mitaji imelala BENKI na ianawsubiri muweze KUKOPESHEKA, USINGOJE KESHo Aaanza LEO! Na wewe Utaweza Kununua Shamba na Kumiliki Ghorofa na hata Viwanda pia na kuendesha gari jipya na Kusomesha watoto hadi Chuo Kikuu kwa Mkopo!
🙂
Siku njema!
Aziz