KadaMpinzani
JF-Expert Member
- Jan 31, 2007
- 3,715
- 93
hii hoja ni nzito na nitaijibu kwa umakini baadae kidogo, nasikiliza taarabu sasa hivi !!
Tahariri Habari nyingine zaidi!
Mkapa aachwe astaafu kwa amani
Mhariri
HabariLeo; Wednesday,May 30, 2007 @00:02
KATIKA siku za hivi karibuni, tumeshuhudia baadhi ya magazeti yakiandika habari zinazodaiwa
kuwa za uchunguzi kuhusu mikopo ambayo ilitolewa na benki hapa nchini kwa kampuni inayohusishwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa na mkewe Anna.
Kwa ufupi, taarifa hizo zinahusu mkopo ambao inasemekana Mkapa aliupata kutoka benki mbili za hapa nchini, na ambao ameshaurejesha. Mkapa, kama Mtanzania yeyote yule ana haki ya kuwekeza katika biashara na ana haki ya kupata mkopo. Isitoshe, ametuonyesha kwamba mtu anapokopa kwenye tasisi za fedha, lazima arejeshe.
Kinachotushangaza ni namna ambavyo habari hizo zimeandikwa, kwani kuna wakati hazizingatii maadili ya uandishi wa habari ambayo yanakemea mtindo wa kuweka maoni ya mwandishi katika taarifa ambayo sio maoni au uchambuzi.
Inatuwia vigumu kuamini kuwa taarifa hizo ni za uchunguzi wa kawaida kwani uchunguzi makini ungeliangalia namna benki zinavyotoa mikopo kwa wafanyabiashara kwa ujumla na sio mtu mmoja tu. Kwa hali hiyo tulitegemea kuwa magazeti hayo yangeanza mikopo iliyotolewa
na wafanyabiashara wengine, ambao baadhi yao bado wanadaiwa na taasisi za fedha.
Tunachoona sisi, na bila shaka Watanzania wengine, ni dalili ya wazi ya kumuandama Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu kwa sababu ambazo hazina msingi zaidi ya chuki.
Aidha wale wanaomwandama hawaoni mbali, kwao wanachokiona ni Mkapa na sio ustakabali wa nchi hii.
Tanzania imeonyesha njia kwa nchi za Afrika kwa kuwa na mpangilio mzuri wa urithi wa kisiasa wa kidemokrasia ambao umeshuhudia viongozi wetu wakikabidhiana madaraka baada ya kumalizika kwa vipindi vyao vya kidemokrasia.
Mfumo wetu wa kisiasa umewezesha viongozi wetu wameheshimu vipindi vyao vya kuongoza nchi na kamwe hawajatafuta mbinu za kujiongezea muda ili waendelee kutawala ili kulinda maslahi yao binafsi kama ambavyo tumeshuhudia katika baadhi ya nchi nyingine za Kiafrika.
Tumeshuhudia baadhi ya marais waliostaafu katika nchi hizo wakisakamwa hadi kufikia hatua za kugawa nchi.
Kwa bahati nzuri kwa Tanzania, marais wetu wanakabidhiana madaraka na kila mmoja anajenga kwenye misingi iliyowekwa na mwenzake. Urithi huu umetuwezesha kujenga umoja nchini mwetu.
Watanzania wana safari ndefu ya kujiletea maendeleo na wasingependa kurudishwa nyuma kwa namna yoyote ile.
Mkapa amefanya mengi kwa taifa hili na tumpe nafasi ya kustaafu na kupumzika bila bughudha yoyote.
Kaka Mkandara kwa kweli nami hilo limenikera sana! We are together against huu umbu-mbu-mbu wa Mhariri wa Habari Leo, bila shaka hiyo kazi amepewa tu bila kuwa na sifa zinazostahili, labda ni Mwana CCM.
Nchi hii, kila kitu siasa tu! Hata mambo yanayohusu mustakabali wa nchi yetu ni siasa! Siasa, siasa, siasa itatufikisha wapi? Nahofia itaua mustakabli wa nchi yetu.