Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

turudishe MIIKO JAMANI ..kama leo tunamuongelea mkapa ..vijana wetu watamuonelea kikwete na lowassa ..mungu akipenda tukishuhudia...na wajukuu zetu watasema "rais" mstaafu nchimbi miaka hiyo..kajengea machangudoa wote nyumba{kiddin]...sasa tuanzie hapa BUNGE LIPELEKE UPYA SHERIA YA MIIKO YA VIONGOZI..Hivi ile tume ya tabia za viongozi alikuwapo jaji meena ipo?...wanasiasa hawataki kuishi kwa maadili kwa nini....majaji ..maafisa wa jeshi ..wote wanazingatia maadili...ndio maanna siku hizi wanasiasa tunagimbea nao rose garden na kwingine wote tukiwa na makaputula yetu tunaumwa mbu...kina jk wanaita kujichanganya ...wamegundua huku uswahilini kwetu ndio kuna mambo...mabinti zetu ,samahani ..wake zetu ..yes hawawezi kuwa na uwezo wa kufika gymkhana au obay..MIIIKO..MIIKO ..MIIKO..MAADILI
 
Kama ni kujichanganya wanasiasa wekeni maadili jamani..mbona sijawahi kumuona nyallali,sammatta,waitara,musuguri,mahundi,mahita,,,,wakijichanganya na makaputula viwanja ..hawa si mnawachagua ninyi??? tunashindwa nini kukubaliana affirmatively kurudisha maadili kama kipindi cha mwalimu?????
 
Hivi Mkapa, alipata posho na marupurupu kuliko Mwalimu, Salim, na kina Mwinyi? I mean as wananchi ukweli ni kwamba hatuna ushahidi at hand kuhusu utajiri wa within miaka kumi wa Mkapa, Mwalimu 28 years za urais lakini hakuwa na mali hata robo ya huyu mzee in ten years,

Hakuna wa kulaumu ila ni sisi wananchi, kwa sababu kama rais anachota kuwa kujikinga na mikopo na posho, je vipi mawaziri? Hela alizokuwa akiwapa Nyerere Foundation, zilikuwa zikipitia bajeti ya wapi?

Ushahidi hatuna, lakini basi hata kwa macho tunaona na tunazo akili za kufikiri, ukweli ni kwamba mali za Mkapa ni nyingi mno kulinganisha na muda mfuri aliokaaa madarakani, ndio maana ilibidi Mtandao washinde, maana nasikia walikuwa na kafaili ka mzee Mkapa, ambako wangekaachia kama wasingepata, at the end tulioliwa ni wananchi, maana Mkapa ndiye rais wa kwanza Afrika kutajirika kwa mikopo na posho tu, maana yeye pia ni mu-Afrika wa kwanza kushika nfasi kubwa kubwa mno za kumlipa posho kubwa kufikia kuwa na mali zote alizonazo in ten years, alipoingia alitangaza mali zake, lakini alipokuwa anatoka akawa bubu mpaka leo!

Huenda bongo tunawalipa posho marais wetu kuliko nchi zote za Afrika kama sio duniani! Hatuhitaji maadili tunahitaji sheria, maadili, Azimio na wahujumu uchumi yalikuwa ni NONESENSE kuliko anything tulichowahi kupitia toka tupate uhuru, hata Kaduma mwenyewe sidhani kama ni msafi kiasi hicho cha kufikia kuwa na hela za mpaka kufanya shopping za harusi za watoto wake huko majuu, bongo tuna viongozi wezi wa mchana kina Mkapa na wa usiku kina Kaduma, Muuugwana ameingia akiwa masikini hana kitu, sasa na yeye tumemsubiria tu, so far bado! Na mzee Mkapa posho na mikopo ilianza pale tu Mwalimu alipofariki, akiwa hai Mkapa hakupata mikopo wala posho, zilisubiri mpaka Mwalimu alipofariki!
 
Mzee Es,
AFTER landing a highly controversial $500,000 loan from the National Bank
of Commerce Limited in 2002, the company owned by former president
Benjamin Mkapa and first lady Anna Mkapa bought the building housing the
upcoming Bank M (Tanzania) Limited in Dar es Salaam for the same amount,
it has been confirmed

Kwa maelezo hayo mafupi tu 500,000 ni gharama ya nyumba ya vyumba sita choo cha mchuchumio nje Kariakoo! mitaa ya Livingstone, Congo na Kidongo chekundu!...
Hapa bado hatujazungumzia maghorofa ya Ilala Quoters ambayo mojawapo mkewe kakodisha mtu kuweka hotel ya Lamada!..
Tumekwishaaaa!
 
Mzee Bob,

Mimi sina nguvu tena, hivi unajua what it takes kwa hiyo bank kukupa mkopo wa dola $ 500,000? Wewe washikaji kina Mike Kida, alikuwa akidaiwa hela ndogo tu na tayari walishataka kumnyang'anya jengo lake kwa kudaiwa hela mbuzi tu ambazo hata hazifiki dola $ 20,000, kwa sababu wazungu walidai kuwa hana mali au mitaji ya kuwahakikishia kuwa atawalipa hela zao,

Sasa huyu rais wa zamani ameonyesha nini kuwahakikishia kuwa atawalipa hizo dola $ 500, 000? Nasikia kizungu zungu!
 
Mkapa was corrupt and he is corrupt . The never felt the plight of Tanzanian yeye mali mbele. CCM ndiyo aina ya viongozi inao wataka na tungojee ya awamu ya 4 , maana hata watoto wanafukuzwa mashuleni na wananchi wanawekwa ndani na kunyimwa dhamani kisa wawekezaji. CCM mnatumaliza .
 
Dhamana ya ccm kwenye hili iliiisha pale tu Azimio lilipovunjwa, sasa ni tatizo la taifa na hasa bunge ndio maana viongozi wote wa taifa wanatakiwa kusema mali zao kwa bunge na sio ccm,

hili mzee ni tataizo letu wote as taifa sio ccm!
 
Uuzaji nyumba za serikali kilio nchi nzima

*Watumishi wa umma wahangaika huku na kule
*Ukerewe sasa waanza kukimbiwa na wafanyakazi
*Baadhi ya wamiliki wazigeuza nyumba za wageni
*Waziri Chenge ajinoa kupamaba na maswali bungeni


Na Waandishi Wetu

ZOEZI la uuzwaji nyumba za serikali lililofanywa na Serikali ya Awamu ya Tatu, limeendelea kuibua mambo mazito na mateso kwa watumishi wa umma na kuwakatisha tamaa katika majukumu yao.

Katika uchunguzi wake katika maeneo mbalimbali nchini, Mwananchi limebaini malalamiko mengi kutoka kwa watumishi wa umma wanaosema kuwa mbali na kukosa makazi, kuuzwa kwa nyumba hizo kumeilazimisha serikali kupanga nyumba ilizouza.

“Suala la uuzaji wa nyumba za serikali katika wilaya yetu ya Ukerewe ni pigo kutokana na wilaya hii kubakiwa na nyumba mbili tu za serikali, huku ikikosa ardhi nyingine kwa ajili ya ujenzi wa nyumba nyingine,” anasema Peter Toima, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe.

Wakati mkuu huyo wa Wilaya akisema hayo, gazeti hili limebaini pia kuwepo kwa matumizi kinyume na taratibu za uuzwaji wa nyumba hizo, hali inayobainisha kuwa nyumba hizo ziliuzwa bila kufanya tathmini ya kina.

Kuna baadhi ya nyumba zilizogeuzwa matumizi na moja iko mkoani Morogoro ambayo imebadilishwa kutoka makazi ya watu na kuwa nyumba ya wageni.

Miongoni mwa masharti ya kumiliki nyumba ambazo awali zilikuwa za serikali ni kuwa nyumba hizo ziendelee kuwa sehemu ya makazi ya watu na zisitumike kibiashara.

Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge, aliliambia gazeti hili kuwa, suala la uuzwaji wa nyumba hizo kwa sasa ni tata na hana taarifa rasmi kuhusu namna ya kuweza kulitazama upya.

Utata huu anaouzungumza Chenge unatokana na ushahidi kuwa, uuzwaji huo wa nyumba ulipitishwa na Baraza la Mawaziri la awamu ya tatu na wengi waliokuwemo humo na kunufaika na zoezi hili sasa wapo katika ngazi za juu katika serikali ya awamu ya nne.

Chenge aliendelea kusema kuwa, suala hili kwa sasa lipo mikononi mwa rais mwenyewe.

"Suala hili la kutazama zoezi la uuzwaji wa nyumba za serikali lilitangazwa na mheshimiwa rais mwenyewe, ameunda task force, nafikiri ndiyo itatoa majibu," alisema Chenge na kuongeza:

"Mimi pia siwezi kusema tu kwamba suala hili liko chini ya kamati maalum ya rais, nitapaswa kutafuta taarifa ya wapi limefikia," alisema huku akibainisha kuwa hoja hii inaweza kuzua mjadala mpya katika kikao cha nane cha bunge kitakachoanza mwezi ujao.

Hata hivyo, siku moja baada ya kutangazwa kuwania urais kupitia CCM mwaka 2005, Rais Jakaya Kikwete, alieleza kuwa hana mpango wa kurejesha nyumba za serikali, na kwamba hata yeye alikuwa amenunua nyumba mojawapo iliyopo Mtaa wa Ursino jijini Dar es Salaam.

Hali iliyopo sasa ni kuwa, kuna watumishi kadhaa wa serikali ambao wanastahili kupatiwa nyumba za kuishi lakini hazipo. Hali hii imewafanya kuhangaika kupata makazi, huku pia kukiwa na taarifa kuhusu baadhi ya waliouziwa nyumba za serikali kutozitumia kwa makazi.

Kuna taarifa zinazoeleza kuwa, baadhi ya vigogo waliouziwa nyumba hizo nao wameziuza kwa watu wengine ikiwa ni kinyume na masharti ya umiliki wa nyumba hizo.

Wananchi mbalimbali kwa vipindi kadhaa wamekuwa wakilalamikia zoezi hilo na kuitaka serikali ya awamu ya nne kulitazama upya.

Waliozungumzia uamuzi huo wa serikali wa kuuza nyumba za serikali kwa watumishi walisema kuwa, uamuzi huo haukuwa umefanyiwa utafiti wa kina kwani serikali inaingia gharama zaidi kwa kuwaweka watumishi wake hotelini kwa kipindi kirefu na pia kulazimika kujenga nyumba nyingine za serikali nchini kote.

Inaelezwa kwamba baada ya kuuza nyumba hizo, mahitaji yake yameongezeka maradufu kutokana na ongezeko la ajira katika idara na taasisi mbalimbali za serikali.

Afisa mmoja mwandamizi mkoani Morogoro, ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema kuwa utaratibu wa uuzaji wa nyumba za serikali haukuwa mzuri na haukuangalia athari ambazo zinaweza kutokea baadaye. Soma makala maalum za madhara ya uuzaji wa nyumba za serikali ndani ya gazeti hili.
 
Serikali irejeshe nyumba zilizouzwa

Na Dismas Lyassa

Tanzania ni mojawapo ya nchi duni sana duniani ingawa tunao wajanja wachache wanaoishi maisha bora na ya kifahari kama waishivyo wakazi wengi wa nchi za Ulaya.

Kulingana na ripoti za mashirika tofauti ikiwemo Benki ya Dunia, umaskini Tanzania ni wa hali ya juu, huku thamani ya fedha nayo ikiendelea kuporomoka.

Wastani wa pato la Mtanzania ni chini ya sh1000 kwa siku, wakati thamani ya fedha ya Tanzania ni zaidi ya Sh1,269 kwa dola moja ya Marekani.

Huenda Tanzania ikawa ni mojawapo ya nchi inayoongozwa kwa kupewa ahadi nzuri za kuboreshewa maisha, lakini ukweli ni tofauti, hali ya uchumi inaendelea kuwa mbaya, watu wengi wanaonekana kukata tamaa.

Wanaoongea ukweli kama huu ninaoueleza hapa wanaonekana wabaya machoni mwa watu wanaoishi kifahari katika nchi hii iliyo na utitiri wa maskini.

Katika hali duni ya maisha iliyopo nchini, uko umuhimu wa Serikali kuangalia njia tofauti za kuimarisha uchumi ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji wa shughuli zake.

Sehemu mojawapo muhimu ya kupunguza matumizi ni kuhakikisha nchi inakuwa na nyumba za kutosha kwa ajili ya watumishi wake.

Inashangaza na kutia kichefuchefu kuona nchi inahitaji nyumba zaidi ya 300,000 kwa ajili ya watumishi, lakini zilizopo chache zinauzwa.

Tayari nyumba 7700 zimeuzwa na 1800 zimesalia baada ya zoezi hilo kusitishwa. Ni lini nyumba 300,000 zitajengwa ili kukidhi mahitaji ya nyumba za watumishi nchini? Ni swali lisilo na jibu.

Tunauza nyumba ili watumishi waishi wapi? Hilo nalo ni swali ambalo naamini hakuna mwenye uwezo wa kulijibu kwa ufasaha.

Ninachokiona mimi mpango wa kuuza nyumba za Serikali umeanzishwa sio tu kwamba pengine haukufanyiwa uchambuzi wa kina, lakini inawezekana ni wajanja wachache wametamani kupora nyumba hizo.
Naamini hivyo kwa sababu kama kweli lengo lilikuwa kusaidia maisha bora ya mtumishi, kungekuwa na mradi maalum wa kujenga nyumba za kuziuza, lakini sio kuuza zilizopo ambazo ni chache.

Ni suala linalowezekana kwa Serikali kuanzisha mradi wa namna hiyo, kwa mfano inaweza kuingia katika mji fulani na kujenga nyumba kisha wakawa wanalipa kidogo kidogo.

Athari za kuuza nyumba hizi zimeshaonekana, kwani baadhi ya viongozi hadi sasa inadaiwa wanaishi hotelini kutokana na kukosa nyumba.

Pia kuna baadhi ya watumishi kwa sababu ya uzito wa nyadhifa zao inakuwa vigumu kuwapangishia nyumba katika mazingira ya ajabu-ajabu, matokeo yake wanalazimika kukaa hotelini kwa muda mrefu huku wakitafutiwa sehemu nzuri za kuishi.

Matokeo ya hali hii, ni kwa nchi kutumia fedha nyingi kuendesha Serikali badala ya shughuli za maendeleo.

Hivi karibuni Serikali ilitoa kauli ya kusitishwa zoezi zima la kuuza nyumba, taarifa hii ni nzuri, lakini ni vema ikafikiria kuzirejesha nyumba zote zilizouzwa.

Wale waliozinunua nyumba hizo warudishiwe fedha zao.Suala hili halihitaji mjadala, bali linapaswa kutekelezwa mara moja.

Nifahamu waliozinunua nyumba hizi wanajua wamefanya dhambi, sio tu kwa sababu wamezinunua, lakini kwa sababu wamenunua kwa bei ndogo ukilinganisha na thamani halisi ya majengo.

Kwa mfano taarifa za vyombo vya habari zinasema katika Halmashauri ya Rungwe, mkoani Mbeya, zipo nyumba za Serikali ambazo zimeuzwa hadi Sh1.6milioni.

Hata Jijini Dar es Salaam ambako thamani ya nyumba inaongezeka kadri miaka inavyokwenda mbele, zipo nyumba zilizouzwa hadi Sh10milioni, bei ambayo ni ndogo.

Inakuwaje nyumba yenye nyumba vitatu au zaidi iuzwe bei ndogo kama hiyo wakati gharama za ujenzi ni za juu sana, kiasi kwamba ujenzi wa chumba kimoja pekee hadi kinakamilika unaweza kugharimu Sh2milioni.

Kwanini zinauzwa bei chee kiasi hiki kama njugu? Mimi sina jibu.Nina hakika ukichukua fedha ya mauzo ya nyumba iliyouzwa na kwenda kutafuta nyumba kama hiyo ya kununua huwezi kupata.

Nina imani kuuzwa kwa nyumba hizo ni mipango michafu ya wachache kutaka kujichukulia mali za umma, wakitumia kigezo kuwa inaziuza kwa watumishi ili kuboresha maisha yao.

Wengi wa watumishi walionunua nyumba hizo ambao nao hawajamalizia malipo kwa sababu wanahojia watanyang’anywa, ni wale wenye uwezo wa kujenga kutoka na mishahara mikubwa wanayopata.

Je kuna Polisi gani wa kawaida anayelipwa mshahara wa Sh100,000 au chini ya hapo, aliyeuziwa nyumba hizo kama sio vigogo wanaolipwa mishahara minono na ambao wana uwezo wa kujenga majumba kibao kwa mwezi mmoja tu? Je, ni walimu wangapi wa shule ya msingi waliouziwa nyumba hizo? Wafagizi na wapika chai wangapi wanaofanya kazi ofisi za Serikali waliouziwa nyumba hizo?

Nina maswali mengi ya kuuliza ambayo naamini nikiorodhesha yote ukurasa huu pengine ukawa hautoshi.

Ushauri wangu ni kwa Serikali kuachana na mipango ya kuuza nyumba, na pia kuzirudisha nyumba zote zilizouzwa.

Kutokana na ukweli kuwa wengi wa wale waliouziwa nyumba hizi ni watumishi wenye uwezo kifedha, ni vema wakaziacha nyumba hizi na kujenga zao waishi kwa amani.

Nina hakika hata kama sasa Serikali haitazirudisha nyumba hizi, lakini ipo siku Mungu atatupatia Rais ambaye atazirudisha, iwe kwa fidia au bila fidia.

Kama ambavyo chama kilichotawala Kenya kwa muda mrefu Kenya (KANU) kiliweza kuondolewa madarakani bila ulimwengu kuamini kilichokuwa kikitokea, inawezekana pia kwa chama fulani ndani ya Tanzania kikawa imara au kudhoofika. Yote yanawezekana!!!

Waulize machinga ‘leo ukitokea uchaguzi mkuu utampigia kura nani’, nina hakika jibu halitafanana na lile ambalo angekupa wakati wa kampeni za kunadi sera za ‘maisha bora kwa kila Mtanzania’.

Ninachotaka kusisitiza hapa ni kuwa Serikali irejeshe majumba yaliyouzwa, badala yake ianzishe mradi wa kujenga nyumba na kuziuza kwa mkopo kama kweli lengo ni kuboresha maisha kwa jamii Tanzania, sio kuuza zilizopo.


Dismas Lyassa ni mwandishi wa makala gazeti Mwananchi, 0754 498972
 
BAK,
Hii issue ya nyumba za serikali ni usanii just like anything else... siwezi ku-imagine waziri mmoja aliyenunua nyumba ya serikali na kuivunja na kujenga ingine ya mamilioni akilielewa hili; labda CCM ife
 
Burglars snatch THISDAY laptop, sensitive documents

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam


A LAPTOP computer and several documents belonging to Media Solutions Limited, publishers of THISDAY and KULIKONI newspapers, were stolen on Wednesday night in a burglary on a personal car owned by a senior journalist with the newspapers in Dar es Salaam.

The incident occurred outside the Millennium Towers building situated along New Bagamoyo Road in the city’s Kijitonyama suburb.

The vehicle, a Toyota RAV4 owned by THISDAY news editor Fumbuka Ng’wanakilala, was raided while parked in the building’s external car park, right in front of armed police officers guarding the CRDB bank branch offices situated inside the building.

On the opposite side of the road from the building is a taxi stand where several cabs are normally parked awaiting customers at any given time.

The journalist was not hurt in the raid, which took place while he was somewhere inside the building.

The burglar(s) broke the back passenger window on the right hand side of the vehicle to force their way in and grab the laptop and documents, which were all inside a black leather bag.

Other items on the back seat of the vehicle next to the laptop bag, including a plastic bag containing two new shirts and colognes, were left untouched.

’’I came out of the building without suspecting a thing...as I was driving towards home, I felt the wind blowing in through the side window. That’s when I noticed part of the window had been smashed open and the laptop was missing,’’ he narrated.

The theft was immediately reported at the Oysterbay Police Station, where the journalist gave a written statement to the police. A case file numbered OB/RB/8987/2007 was opened and the incident classified as ’’Theft From Vehicle.’’

The laptop - a Dell Inspiron 2200 - and many of the documents inside it were the property of Media Solutions Limited.

According to the journalist, the stolen computer and documents contained some information for a series of investigative reports published by THISDAY and KULIKONI newspapers over the past few weeks.

He noted that since the car has very dark tinted windows, it was next to impossible for anyone on the outside to see what was inside.

’’It is therefore quite obvious that whoever carried out the burglary must have known exactly what they were targeting,’’ said the journalist.
 
Mkapa company shows the way: $0.5m bank loan was cleared so fast

-That NBC Ltd even charged ANBEM Ltd with $600 fine as ’early redemption penalty’!


THISDAY REPORTERS
Dar es Salaam


THE company owned by former president Benjamin Mkapa and first lady Anna Mkapa cleared a $500,000 loan it took from NBC Limited in such quick time that the bank itself had to impose a charge for early repayment, it has been learnt.

Our sources now say that ANBEM Limited had by July last year repaid in full the controversial loan issued by the country’s oldest and most well-established bank, long before its maturity date.

It has been established that ANBEM Ltd, with Mr and Mrs Mkapa as sole directors, was granted loans amounting to over 750m/- from both NBC Ltd and CRDB Bank between July and December 2002, while the couple was still at State House.

The first loan of $500,000 was issued by the newly privatised NBC Ltd in July 2002, followed by another huge credit-line in the form of 250m/- extended by CRDB Bank in December of the same year.

According to the 2005 annual report of ANBEM Ltd, the company had total registered debts amounting to some 750m/- by the time the accounts were filed.

’’Total amount of indebtedness of the company in respect of all mortgages and charges of the kind which are required to be registered with the registrar of companies under the Companies Ordinance (is) 750,000,000/-,’’ says the report signed by Mr Mkapa himself on July 31, 2005 - when he was still the sitting president.

Although THISDAY has not been able to peruse the company’s subsequent returns from that date, latest findings by this newspaper now confirm that the NBC Ltd loan was settled within a very short time span of December 2005 to July last year.

Mr and Mrs Mkapa departed State House in December 2005, at the end of his second and final term as president.

Our sources say because the repayment of the hefty loan was way ahead of schedule, ANBEM Ltd was obliged to pay an acceleration charge to NBC Ltd amounting to about $600.

The sources also strongly hinted that the speedy repayment of the debt was done with all intention of ensuring the former State House couple stayed free from debt in their retirement.

’’ANBEM Ltd cleared the loan over a very short span of six or seven months, between December 2005 and July 2006. It appears the Mkapa family was seeking to rid themselves of any future indebtedness as they sought to move from State House into a life of comfortable retirement,’’ a reliable source told THISDAY.

According to our investigations, a current key source of income for ANBEM Ltd is the monthly rent paid by tenants of a two-storey office building on Plot No. 8 Ocean Road in the city, that the company bought with the NBC bank loan in 2002.

THISDAY has learnt that before leasing the building to the present tenants ? the soon-to-be-launched Bank M (Tanzania) Limited ? ANBEM Limited collected rent from a couple of other companies occupying the property.

According to our sources, these were Cowi Tanzania Consulting Engineering and Axios Healthcare Development, who together paid rent to ANBEM Limited totaling around $226,930 in the period between 2002 and 2005, when they had office space within the building.

’’Using the rent accrued from the building as well as some other sources, the company managed to repay the NBC loan even before its due date,’’ said one source.

The source further explained that for settling the loan way ahead of schedule, NBC Ltd actually charged ANBEM Limited ’’what is called an early redemption penalty of around $600’’ in July last year.

It is understood that after landing the half-a-million dollar credit line from NBC Ltd, ANBEM Limited completed its purchase of the building currently housing Bank M (Tanzania) Limited in Dar es Salaam for the same amount.

Although the company - in which Mr and Mrs Mkapa are sole directors - used the same building on Plot No. 8 Ocean Road in the city’s Sea View area as collateral for the loan, records show that a legal mortgage for the loan was dated May 14, 2002.

This was some two months before the company actually gained legal ownership of the building, which is situated right next to Mr and Mrs Mkapa’s official residence after retirement.

Records show that the building was bought from a local company called Tanzania Building Works Limited.

The NBC Ltd loan to ANBEM Limited was granted at a time of heated national debate over the privatization process surrounding the once state-owned bank, which was taken over by South Africa’s ABSA Group in April 2000.

ANBEM Limited was officially registered with Mr and Mrs Mkapa named as sole directors and shareholders on June 22, 1999, while the couple were still at State House.

In the legal documents for setting up the company, Mr and Mrs Mkapa described themselves as ’’entrepreneurs.’’

THISDAY has sent written questions to Mr Mkapa’s office in Dar es Salaam regarding the nature of the business transactions conducted by himself and Mrs Mkapa while at Ikulu. No response has been forthcoming so far.
 
Its a bit strange,hili gazeti halina waandishi wa habari? news zake karibuni zote zinaandikwa na THIS DAY REPORTER au kwa kiswahii, NA MWAANDISHI WETU
 
DrWHO,
Mie wala sishangai kuhusu u-wizi,it was inevitable trust me.
Hivi vitu vina fanywa every day kwenye issue kama hizi na hao so called 'Usalama wa Taifa'.Hapo kuna kitu kinaitwa 'kuchafuana' sasa jamaa kila upande una watu wake,upande mmoja unavujisha skendo na mwingine unajaribu ku-retain the information to prevent more harm na wewe ngojea nini kitatokea baada ya hiyo laptop kupotea.
kama upande mwengine utajua jamaa hawana ushaidi wa ziada may be hawa kusave kwenye disc watawaburuza mahakamani ili kujisafisha.
Na kama hii issue nzima sio danganya toto ili msaahau mambo ya 'Kaive' basi hao THISday wamelikoroga au wapate another copy kutoka kwa hiyo source wao.ambayo kwa a simple mathematic unaweza ku-guess.....!
Na kwanini anafanya hivyo kuna mambo mengi on the pile.
 
Jamani habari za uchunguzi hufanywa na timu ya waandishi pengine kwa uongozi wa mmoja, lakini pia kuandika jina la mwandishi bado kwa Tanzania si salama sana
 
Tumeshaona kuwa PCB ni jumuia ya CCM kama ilivyo UVCCM na UWT (bado muda kidogo mkurugenzi wa PCB atapaswa kuwa mjumbe wa NEC na CC za CCM) na kuwa hawawezi kufanya kitu kwa waajiri wao mafisadi. Jee haiwezekani jamani majizi ya rasilimali zetu wakashtakiwa huko nje? kama akina Pinocheti? maana huu sasa ujinga,na kulalama sasa imetosha. Hamkusikia JK kule Mwanza issue ile ya Mbunge kihiyo kauli yake? ''kelele za mlango hazimnyimi usingizi mwenyenyumba'' Sasa? hata kelele za hapa JF ziweje, wao usingizi burudaaaani.
 
turudishe MIIKO JAMANI ..kama leo tunamuongelea mkapa ..vijana wetu watamuonelea kikwete na lowassa ..mungu akipenda tukishuhudia...na wajukuu zetu watasema "rais" mstaafu nchimbi miaka hiyo..kajengea machangudoa wote nyumba{kiddin]...sasa tuanzie hapa BUNGE LIPELEKE UPYA SHERIA YA MIIKO YA VIONGOZI..Hivi ile tume ya tabia za viongozi alikuwapo jaji meena ipo?...wanasiasa hawataki kuishi kwa maadili kwa nini....majaji ..maafisa wa jeshi ..wote wanazingatia maadili...ndio maanna siku hizi wanasiasa tunagimbea nao rose garden na kwingine wote tukiwa na makaputula yetu tunaumwa mbu...kina jk wanaita kujichanganya ...wamegundua huku uswahilini kwetu ndio kuna mambo...mabinti zetu ,samahani ..wake zetu ..yes hawawezi kuwa na uwezo wa kufika gymkhana au obay..MIIIKO..MIIKO ..MIIKO..MAADILI

Well said,

Solution ni kuwa na miiko ya uongozi na maadili haya mengine ni porojo za kufurahisha baraza tu, mintaarafu Mkapa hajavunja sheria yeyote.
 
Kuna hoja kwamna upo uwezekano wa kumshitaki Mkapa kwa jinai na kwa madai. Wapo wanasheria wanaosema kwamba katiba ya Tanzania inatoa kinga kwa Rais anapokua katika kazi zake za URAIS. Sasa kama mtu anapatikana na tuhuma zinazohusu kula rushwa, kuua mtu kwa ugomvi nyumbani kwake, kufanya uhalifu wowote usiohusiana na kazi za URAIS, a nakua hana kinga yoyote. Hapo kuna kila sababu sasa wanasheria wakaweka wazi kama kuna rushwa ama jinai kumhusu Mkapa, basi hakutakua na sababu ya kutomshitaki.

Kuhusu jinai ikiwa wananchi wataona kwamba Mkapa ama yeyote alichukua mali za umma, wanna haki ya kufungua kesi ya jinai mahakamani na kutaka mali hizo zirudishwe mikononi mwa umma zikalipie elimu na hospitali kwa wasio na uwezo.
 
hapa werevu wameshabaini ... hii ni siasa ,yes tujadili ya mkapa tusahau mengine....kuna upupu mwingi tu unaendelea leo nashangaa watu wanahangaika kukanyaga MAVI YA N"GOMBE........WATANZANIA tubadilike jamani kuopa sio dhambi!!!!!!!!!! najua kuna tatizo kupata mikopo lakini kama mtu kakopa na amelipa TATIZO LIPO WAPI????? Hata mkimchafua mkapa kwa mavi ....yatakua maarashi...kila mara nasema yule si malaika ...ILA NANI HAPA ANAKATAA UTENDAJI WA MKAPA ULIKUA MZURI KIUCHUMI????? Utafananisha na huu usanii....msilete mambo ya mwaka jana bwana ..fanyeni kazi nanyie tuwaone ....ya mkapa tumeyaona ..na ya kwenu je,..watu sio watoto hapa wanajua kuna propaganda za aina nyingi hasa pale mtu anaposhindwa kudeliver baadhi ya watu wanafikiri kuhamishia FIKRA za watu kusahau matatizo ya leo na kuanza kutaka kumlaumu mkapa kwa njaa ya leo...kitaalamu utafanikiwa kubadili mawazo ya watu kwa muda tu...lakini baada ya muda mfupi watachoka kumuongelea mkapa na kutaka uwape chakula .wakijua kumbe wewe ndio mpishi...na bahati mbaya [mungu pishia mbali]wakati huo TAIFA stars labda imeshafungwa na senegal...hutakuwa na jambo lingine la kuteka fikra cheap za wadanganyika ...teh labda utamuomba amina alete hoja ya kutaja wauza bangi au tuzushe tena kafumaniwa safari hii sijui itakuwa na nani tena.....

anyway tufanye kazi tuache ujanja ujanja na usanii ...na wala hakuna dhambi yoyote mtu kumiliki mali yoyote kihalali ..kama hakuna mwenye ushahidi wa mali kupatikana kwa wizi basi tuamue tu kuwa tunajifurahisha hapa PASS TIME???!!! Hoja ya bei ya nyumba upanga almost miaka kumi iliyopita kuwa $500,000 ni sawa that was a market price ten years ago...ilikuwa inarange hadi $ 750,000 kwa nyumba ile....msichanganye na bei ya soko ya leo...bei ya nyumba upanga imepanda maradufu baada ya watu kama richmond towers kuleta stlye ya kujenga apartment za hadi ghorofa 15 ,...upanga kabla ilikuwa watu hawajengi majumba makubwa saana .....sasa hivi bei ya ile nyumba ya mkapa itakuwa imefika hadi $ 1,250,000 tena hapo mtu anaibomoa anapiga ghorofa 15 zenye apartment

200 ambapo wahindi wengi wanagombea kupanga kwa dola 1,200 hadi 2,000 kwa mwezi ..capital return ya nyumba upanga ni kubwa kwa sababu maofisi pia yanahama posta to upanga ...kumbukeni miaka kumi nyuma nyumba nyingi upanga walikuwa wanakaa retired officers au wafanyakazi ..leo nyingi wamenunua devolopers wanafanya maajabu..pale mtaa wa magore mwaka 1999 kuna mtu alikuwa anauza ghorofa milioni 300 tu..aliuziwa kama mfanyakazi wa kampuni iliyofilisika leo hii kama anevumilia ile nymba angekula milioni si chini ya 800....nyumba pia za upanga zinapanda chati kwa sababu za masaki wanakopenda wazungu ...maji ni shida ..tofauti na upanga...rate ya kupanuka kwa soko la nyumba ni kubwa although pia rate ya kupanda inashuka bei simply kwa sababu ya supply kubwa inayotokana nautayari wa watu wengi kuwekeza kujenga kuliko kuweka investment kwenye areas nyingine ..they feel safe in real estate....
 
Phillemon Mikael,

anyway tufanye kazi tuache ujanja ujanja na usanii ...na wala hakuna dhambi yoyote mtu kumiliki mali yoyote kihalali ..kama hakuna mwenye ushahidi wa mali kupatikana kwa wizi basi tuamue tu kuwa tunajifurahisha hapa PASS TIME???!!! Hoja ya bei ya nyumba upanga almost miaka kumi iliyopita kuwa $500,000 ni sawa that was a market price ten years ago...ilikuwa inarange hadi $ 750,000 kwa nyumba ile....msichanganye na bei ya soko ya leo...bei ya nyumba upanga imepanda maradufu baada ya watu kama richmond towers kuleta stlye ya kujenga apartment za hadi ghorofa 15 ,...upanga kabla ilikuwa watu hawajengi majumba makubwa saana .....sasa hivi bei ya ile nyumba ya mkapa itakuwa imefika hadi $ 1,250,000 tena hapo mtu anaibomoa anapiga ghorofa 15 zenye apartment

Toka Mkapa aondoke madarakani haijapita miaka KUMI, Usitake kupindisha vitu hapa!
Mkapa hakuwa na uwezo wa kuchukua mali hizo awamu yake ya kwanza.. yote haya yametokea miaka mitano ya mwisho!...baada ya Mwl. Nyerere kufa huo ndio ukweli.

Sasa unapozungumzia Upanga 2003 rafiki yangu kauza nyumba yake sikukuu, Kariakoo mwaka 2003 kwa laki 250 tena kalijenga kwa nguvu zake mwenyewe...Leo unazungumzia majumba ya Upanga sehemu ambayo ni barabara kuu karibu na beach/Hospital?
Huyo wa Magole kauziwa na kina nani?.....sii ndio mpango tunaouzungumzia huo! na sii ajabu jina lake tu ndilo linatumika hali jumba ni la Mkapa &co - who knows!
Swali kubwa tunalouliza ni nani aliyeweka sheria hiyo ya kuuza nyumba hizo?...Mkapa! na kwa nini yeye kawa mtu wa kwanza kutumia nafasi hiyo kununua majengo mengi mjini, yeye pamoja na mkewe kwa bei walizopanga wafanya kazi wake?
Mbona hakuna ruksa kwa raia wa kawaida kuuziwa nyumba za NHC ama msajili ila kwa wale wenye fedha. masharti yanayotakiwa leo hayakumkuta Mkapa, mbona yeye hakubomoa hilo jengo na kujenga lenye ghorofa tano sijui kumi kama wanavyotakiwa watu wengine!...
 
Back
Top Bottom