Recta,
Mkuu unachoshindwa kuelewa ni kitu kimoja tu.. Kwamba kwa kutumia katiba hiyo hiyo mtu anaweza kukiuka sheria kwa kutumia sera za chama. Kwa mfano Hitler na ubaya wake wote ule alitumia katiba ya nchi yake kufanya yote aloyafanya akilindwa na sera za NAZIs..Mugabe kwa ushenzi wake anatumia katiba ya nchi yake akilindwa na sera za Chama..
Mkapa pia ameyafanya yote aloyafanya kwa kutumia Katiba lakini akilindwa na sera za chama chake CCM..
Azimio la Zanzibar ni moja ya sera za CCM ambazo zilimwezesha kiongozi kuanzisha mradi wake ama kuingia biashara..hakuna chama wala wananchi waliohusishwa na azimio hilo. hata hivyo wakati sera hii ikijengwa hakuna hata kifungu kimoja kinachomruhusu ama kumpa nguvu kingozi wa serikali kujiuzia mradi wa serikali ama kuweka sheria ya kuuza hizo mali za Umma kwa viongozi..Alichofanya Mkapa na sera na Ubinafsishaji ni kinyume cha miiko/ maadili ya Uongozi sawa na dalali kujiuzia yeye mwenyewe mali aliyopewa dhamana ya kuiuza sokoni...
Kwa hiyo tunapozungumzia swala la sheria na katiba ya nchi halihusu maamuzi ya sera au Maazimio ya chama CCM wala mipango endelevu/ bomoa ya kiongozi aliyeshika maradaka...Hata huyo Bush aliposhughulikia swala la magaidi na kufungua kwa jela ya Guatanamo Bay limezua utata kutokana na hatua zilizofuatia namna ya ku deal na hao magaidi..Ni makosa yanayomwangukia Bush kukubali baadhi ya torture zitumike lakini hakuna kifungu ndani ya katiba ya Marekani inayoruhusu mateso hayo..
Obama amekusudia kuifunga jela hiyo na Wamarekani wanaweza kabisa kumsimamisha Bush kwa makosa yaliyofanyika ambayo katumia cheo chake kuhalalisha mateso..Kosa la Mkapa halikuwa Ubinafsishaji kama navyoweza kusema kosa la Bush halikuwa kufungua gereza la Guatanamo Bay isipokuwa kosa la Mkapa ni kutumia vibaya madaraka ndani ya katiba kwa kukiuka miiko ya Uongozi bora kama Bush ambavyo amekiuka miiko ya Uongozi bora pale alipotumia torture kinyume cha Uongozi bora..
Mkuu unachoshindwa kuelewa ni kitu kimoja tu.. Kwamba kwa kutumia katiba hiyo hiyo mtu anaweza kukiuka sheria kwa kutumia sera za chama. Kwa mfano Hitler na ubaya wake wote ule alitumia katiba ya nchi yake kufanya yote aloyafanya akilindwa na sera za NAZIs..Mugabe kwa ushenzi wake anatumia katiba ya nchi yake akilindwa na sera za Chama..
Mkapa pia ameyafanya yote aloyafanya kwa kutumia Katiba lakini akilindwa na sera za chama chake CCM..
Azimio la Zanzibar ni moja ya sera za CCM ambazo zilimwezesha kiongozi kuanzisha mradi wake ama kuingia biashara..hakuna chama wala wananchi waliohusishwa na azimio hilo. hata hivyo wakati sera hii ikijengwa hakuna hata kifungu kimoja kinachomruhusu ama kumpa nguvu kingozi wa serikali kujiuzia mradi wa serikali ama kuweka sheria ya kuuza hizo mali za Umma kwa viongozi..Alichofanya Mkapa na sera na Ubinafsishaji ni kinyume cha miiko/ maadili ya Uongozi sawa na dalali kujiuzia yeye mwenyewe mali aliyopewa dhamana ya kuiuza sokoni...
Kwa hiyo tunapozungumzia swala la sheria na katiba ya nchi halihusu maamuzi ya sera au Maazimio ya chama CCM wala mipango endelevu/ bomoa ya kiongozi aliyeshika maradaka...Hata huyo Bush aliposhughulikia swala la magaidi na kufungua kwa jela ya Guatanamo Bay limezua utata kutokana na hatua zilizofuatia namna ya ku deal na hao magaidi..Ni makosa yanayomwangukia Bush kukubali baadhi ya torture zitumike lakini hakuna kifungu ndani ya katiba ya Marekani inayoruhusu mateso hayo..
Obama amekusudia kuifunga jela hiyo na Wamarekani wanaweza kabisa kumsimamisha Bush kwa makosa yaliyofanyika ambayo katumia cheo chake kuhalalisha mateso..Kosa la Mkapa halikuwa Ubinafsishaji kama navyoweza kusema kosa la Bush halikuwa kufungua gereza la Guatanamo Bay isipokuwa kosa la Mkapa ni kutumia vibaya madaraka ndani ya katiba kwa kukiuka miiko ya Uongozi bora kama Bush ambavyo amekiuka miiko ya Uongozi bora pale alipotumia torture kinyume cha Uongozi bora..