mwakatojofu
JF-Expert Member
- Dec 17, 2008
- 326
- 227
Mkuu FMES,
HIvi mzee Mkapa akiwekwea Ndani wewe utafaidika na nini?
sio suala la mtu binafsi kufaidika. kama ni kufaidika ni kwetu sote - watanzania. na hii itakuwa faida ya leo na kesho.
kama atafikishwa mahakamani na kupatikana na makosa, say ya kujiuzia 'mali' kwa bei poa au rushwa etc inamaana kuwa utakuwa utaratibu wetu kwa siku zijazo kuwachukulia hatua za kisheria marais wetu wa kifanya makosa. kwa atakae fuata halitokuwa jambo jipya.
na yeye atakuwa madarakani akijua akiharibu kifuatacho ni kisutu.
nina uhakika kama kuna makosa ben aliyafanya hakutegemea kama angeweza tinga kisutu. alijua anakinga ya wakat ule na ujao - akishastaafu.
watu wengi hatufanyi makosa/dhambi/uhalifu kwa sababu ama tunamuogopa mungu au taratibu/miiko au sheria za nchi au vyote. mwingine anaweza asiogope viwili vya mwanzo lakin akaogopa cha mwisho ambacho ni sheria. na siku hiz ndicho hasa kinachoogopwa. sasa gembe hujaona faida hapo bado?
1. viongoz wetu/watu wote watakuwa chini ya sheria
2. tutakuwa tumekubali kuwa binadamu ni binadamu tu hata kama ana akili kama 'einstein' na mkubwa kama 'goliati'
3. binadamu ana udhaifu wake kama binadamu na hivyo anaweza tenda baya au zuri
4. binadamu amezungukwa na binadamu wenzie - wabaya kwa wazur na wote hao wanamuinfluence kwa namna moja au ingine
5. mali za 'taifa' zinakuwa 'salama' zaidi maana awaye yeyote hata kama atazitamani kias gani atakuwa anaogopa 'kujimilikisha'
6. rushwa itapungua kwa kuogopa kutinga mahakamani baadae
7. kwa kuwa uraisi wa nchi ni ngazi ya 'mwisho' ya 'mafanikio' ya binadamu kutinga mahakamani ukishatoka uraisini itakuwa aibu. hivyo mtu atajitahidi kutenda yaliyo sawa aibu isije mkuta
8. etc.
kuna haja gani ya watu wenye heshima mbele ya jamii kuanza kushtakiwa>?
mambo yote ya maana au ya ovyo popote pale yana buniwa, kuanzishwa, kusimamiwa na watu wenye heshima katika jamii.
mara ingine mabovu yanafanywa ilihali wanajua kuwa ni mabovu. kwanini wasihukumiwe kama wamekosea? lingekuwa kosa moja au la kwanza tungesema bahat mbaya.
hebu angalia ujerumani kipindi cha hitler na marafiki wake. cheki pale rwanda na majirani zao burundi. chungulia zimbabwe. angalia mtafaruku wa kenya. vurugu au mauaji au vyote vilianzishwa na kusimamiwa na watu wenye heshima katika jamii.
au unataka kuniambia hitler alikuwa haheshimiwi?