WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 970
Siku zote huwa nina some sympathy na hii rule ya kuuza baadhi ya nyumba za serikali kusaidia viongozi, kwa mfano ninaelewa kuwa kiongozi kama Adam Sapi, na Bob Makani wamenufaika sana na hiki kitendo wka sababu hawakuwa na nyumba za kwenda baada ya kutoka serikalini,
Ninaamini kuwa nia ya sheria ilikuwa njema, lakini in the process wametokea vibaka na kuharibu the whole good intent ya serikali na hasa wabunge katika kuipitisha hii rule, sasa kama kuna cha kufanyika iundwe kamati ya bunge na kuamua publicily kama nani ana meet the creteria za kuuziwa hizo nyumba na wasiozi-meet, zirudishwe mara moja.
Naona tunatoka nje ya mada ila unapoongelea utendaji wa magufuli huwezi kukwepa KUONGELEA hili suala la uuzaji nyumba za serikali.
KUMBUKA..Adam Sapi alikuwa anaangukia katika lile kundi la wateule wa kunufaika na mafao ya viongozi wa juu serikalini( rais, PM, CJ, Speaker n.k) ..Makani naye sidhani ni wa kuonewa huruma kiasi hicho maana alikuwa wakili na halafu mwanasiasa. Kumbuka watu kama Marehemu Lawi Nangwana Sijaona, watu kama kina Timothy Apiyo n.k ambao baada ya kustaafu walienda kuishi maisha ya kimasikini sana vijijini! Na bado wako wengi sana kama wangeorodheshwa hapa na madhila yaliyowapata basi ingekuwa ni huruma tupu. Ukija kuangalia ni nani hasa wameuziwa hizo nyumba..ni maajabu maana nyingi ya hizo nyumba zimebomolewa na kujengwa majumba ya kutisha. Je? ni kweli sababu za kuwauzia nyumba ni kwa vile kama watumishi wa umma hawana kipato? je? hizo pesa walizojengea baada ya kuuziwa na kubomoa wametoa wapi? je? isingekuwa vema zaidi kuwatafutia viwanja wakajenga badala ya kuwauzia hizo nyumba kwa bei ya sawa na bure? je? kwanini basi hawakuuziwa kwa bei ya soko wakapewa hata mikopo iwawezeshe?