Mkuu FM ES heshima,
kweli kuna sympath kwa hawa wazee. Lakini Mkuu ukiangalia sana kuna wazee ambao nao tunatakiwa kuwaonea pia huruma, kuna watu maisha yao yote yamekuwa ni wakulima, wafugaji, wafanyabiashara nk. Nadhani nao wana haki ya kupata hizi nyumba pia. Kwangu mimi hata hili zoezi lingeendeshwa kwa kufuata utaratibu halali, kuwauzia tu wafanyakazi wa serikali hizi nyumba hilo ni kosa, hizi nyumba hazikujengwakwa kodi wanazotoa wafanyakazi tu, bali ni kodi za watanzania wote. Hivyo haikuwa na haja ya kuuza nyumba, then utumie kodi ya wananchi kujenga nyumba tena nje ya mji (kama walivyotoa mifano wachangiaji waliopita). Ukumbuke unapokaa nje ya mji,mbali na ofisi kwa wale wanaohudumiwa na magari ya serikali pia huongeza gharama za mafuta. Wakuu hapa jamaa walichemsha kuziuza hizi nyumba.